EX wako unamuombea maombi gani na kwanini?

EX wako unamuombea maombi gani na kwanini?

Maex wangu wote karibia 50 hakuna niliyegombana nae serious mpaka kufikia kutoongea.

Maex wangu wote nawaambia mimi ni mzima na nawasalimu sana , ujumbe waheshimu mahusiano yao ya sasa tukikutana wasiniweke kwenye mitego ya kula tunda tena maana huwa nategeka haswa.
Waanzishie whatsApp group hao Maex wako... Na uwaombe whatsApp wenyewe wakupe uadmin ambao mtu akitaka kuleft awe hawezi baada ya wewe kumu-add hadi hapo utakapomuondoa wewe mwenyewe kundini
 
Ndugu yangu angenifata na kunipasulia ukweli like "Man safari iishie hapa kwasababu kadha wa kadha" hata nisingem mind ila for type of action she took. namuandalia maumivu nitamdunga virusi vya covid nimeshaanza kuandaa team ya umafia na umafia nauweza na ulokole nauweza pia. ngoja nipite alikotaka nipite ili mama akiniuliza fulani hajambo sikuhizi amenisusa nimpe jibu alishakufa.
Kwenye maisha yangu sipendagi kukaribisha roho ya kisasi kama.

Hebu achana nae ndugu yangu unaweza fanya tukio ukajikuta mnabadilishana majengo ya serikali maisha yakaishia hapo.sikushauri aiseh
 
Mungu ambariki EX wangu (first lover wangu)
huyu tuliachana kwa amani tuliitana mezani tukafanya analysis tukaona hakuna mwendo tukavunja mahusiano .
asubuhi ya leo amenipigia anasema angependa kuja nilipo kuifanya Master research yake i was like njoo na nitakuandikia research report yako buree.

anyway kuna mbwa iliniacha December au January baada ya kumkabidhi maisha yangu for 6 or 7 years yule mbwa ni bora angenichoma tu moto ndani ya Nyumba, sina cha kumuombea one day i will find her in a corner that i will have a chance to burn her to death MF
Mkuu punguza jazba, na usitembee na bastola pengine mnaweza mkakutana njiani ukaleta mabalaa kama vijana wa sinza [emoji38]

Sent from my SM-J730F using JamiiForums mobile app
 
Maskini 😌😌😌🥺🥺🥺 nimepata huzuni aiseh

Tuendelee kumsubiri amalize kufua ndugu yangu
Usihudhunike I did that for love, nilitaka kumfungulia dunia ili awe anachotaka kabla sijamaliza kumfungulia dunia vizuri akaamua kufua.

Nitakwenda kumsaidia kuanika, hajui tu huko alipo najua mpaka aina ya kitanda anacholalia, alijitoa tu akili ila anajua kuwa alikua anadate mtu mwenye akili nyingi haahaahahaa
 
Wangu nilimuombea mabaya mno,sikutamani kumuona akifanikiwa wala akiwa na furaha kabisa,ilinichukua zaidi ya miaka mitatu au minne na zaidi.Nilianza kusali,lakini sala zangu zilikuwa ni za uchungu na laana juu yake nilikuwa nalia mno[emoji3064][emoji3064]nilikuwa najiona nasali kumbe kiuhalisia nilikuwa nanung’unika(kwa tafsiri nyingine ni kwamba nilikuwa namwambia Mungu amwangamize)

Nilikuwa nakwenda kwenye maombi sana kanisa la KKKT Korogwe,au Kwenye mikutano ya Mwalimu Mwakasege kipindi hicho ilikuwa ni viwanja vya mlimani kabla hajaamia Tanganyika Packers.kupindi chote nilikuwa nasali kwa kunung’unika tu.

Siku ya mwisho wa mkutano Tanganyika packers wa mwakasege ndo siku ambayo nilifunguliwa ufahamu kwa yale maombi ya miaka yote niliyokuwa nayaomba.sikuwa sahihi hata kidogo.nilijipa muda wa kumtafakari Mwamba kwa kina sana nikagundua kuwa ninadhambi ya kutubu ya kumuombea masta mabaya.mwamba alikuwa baba,mama,kaka,dada,mshkaji wangu,mwalimu wangu alikuwa kila kitu kwa kipindi hicho.

Ilinibidi nianze upya kusali kuomba toba iliyothabiti.nakumbuka nilifunga siku 80 kama sio 100 kwa ajili ya kuomba msamaha kwa Mungu kwa maombi ya laana niliyokuwa nikumuombea.niliahidi kufunga hata siku elfu moja mpka pale nitakaposhusha mzigo niliokuwa nimemuwekea mwamba siku nitakayopata Amani na nikawa sina kinyongo tena basi ndipo siku nitakayoacha kufunga(wachache mno watanielewa nikisema kushusha mzigo na kuitafuta amani ya moyo)

Moyo wangu ni mweupe kwake kama theluji.ninauhakika alitumwa na Mungu kwenye maisha yangu kwa asilimia [emoji817].yapo mengi sana ya kumshukuru Mungu kwa ajili ya huyu kiumbe.
Na nikisikiaga mke wake anamsumbua natamani nikamzibue huyo mwanamke vibao 20 mfululizo astuke usingizini.

Mpka sasa sijapata mtu siriazi mwenye tabia kama zake. alinifundisha usela flani Hivi.imagine tulikuwa tukitaka kupelekeana moto utamsikia “mwanangu tukapige basi game”or”twende tukakulane basi”tulikuwa tukipika pamoja..huku vitunguu vinaungua jikoni sisi tu napiga game[emoji16][emoji16]jamani..yani tulikuwa kama watoto vile.

Mjinga yule alijua kunifundisha maisha namshukuru mno. Sijui nisingekutana nae kwenye maisha haya ningekuwa na maisha gani.nazidi kumtukuza Mungu kwa ajili yake aiseh.

Niliahidi kumchukua yatima mmoja awe mtoto wangu niwe mzazi wake hii yote ni kusema asante kwa Mungu na Mwamba kwa waliponitoa.hili ni lazima nilitekeleze hatotokea wa kuubadilisha huu msimamo.

Mungu wa majeshi azidi kumtunza huyu baba.amuepusha na kila hila ya muovu shetani.Amen
Mshikaji ulimpenda aisee, ila ndio hivo we plan but God decides. Pole sana

Sent from my SM-J730F using JamiiForums mobile app
 
Maskini pole..
Bwana akupe wa kushikamana nae asije kukupiga chini
Daktar wa saikolojia alishanihakikishia tatzo langu haliwez kutibika itabidi nikubali kuwa naachwa tu.
Yan hili tatzo la WIVU!!! usiombe likupate. bora uwe na kibamia utavumiliwa. huu ugonjwa nampataga mpenz nampa kila mwanamke anapenda kwa mwanaume lakin nakaba hadi ananikimbia!
mtaalam alinitest kuwa ninunue callgirl, lakin nilipomaliza kuhudumiwa nikalipa pale pale nikaanza mashart asiuzie mwingine nikajicommit kuwa nampa wastan wa posho, ndo Dr akasema nimeshashindikana kupona!
ndo hivyo nikashauriwa na nisioe kabsa. sijui nikizeeka nani atanifunga pampers na kunipeleka juan!
 
Back
Top Bottom