Fahamu kinachojiri kuhusiana na kirusi cha Corona (Coronavirus)

Wakuu,

Nimekuwa nikitafakari, idadi ya vifo Marekani ni kubwa mno, nadhani kwa sasa kila kifo wanasema ni Corona ndio maana namba iko juu sana.

Ukiangalia nchi zilizopata maambukizi mengi sana na ya ghafla kama Spain na Italy vifo havikuwa vingi kiasi hicho. Hata China yenyewe watu hawakufa wengi kiasi hicho ingawa kwao mlipuko ulikuwa mkubwa sana na kwa muda mfupi.
 
Mambo niaje?
Naona kama nimebakinyuma kwasababu kumbukumbu zinanilazimisha na kuninyima nguvu nisisonge mbele na kuwa sambamba na Watanzania wengine au hata Waafrika penginepo. Akili,fikra,tahadhari,juhudi na maarifa vya watu walio wengi, wengi sana vyote vimeelekezwa kwenye mapambano dhidi ya Corona.binafsi nashindwa kuelewa ilikuaje tukaidharau Mvua ambayo licha ya kuuwa inatesa,inanyanyasa,inadhalilisha,inadumaza na kutusababisha adha za kila aina!? Au ni kwasababu Corona ilivamia kwa mtindo wa nguvu ya Soda Ndio ikawateka!? Kwangu Mimi mvua isiyo na kikomo kama hii inayoendelea ni hatari zaidi ya Corona. Corona litatokomea zake kusipo julikana Ila Mvua itaendelea kutuadabisha daima dumu ikiwa tu tutaendelea kuichukulia poa, binafsi nipo karantini kwasababu ya Mvua na si Corona.
 
 
ADHABU ILIYOSHUKA ITALIA INATOSHA. WATU SASA WAPUMUE WAKIWA NA ANGALAU KHOFU JAPO KIDOGO
 
Ulaya< Marekani, Uarabuni na mashariki ya kati wote hawana dawa maalumu ya korona na wanakufa vibaya vibaya, siye kama watumwa wa akili eti tunasubiri wao watupe dawa na kuwaamini zaidi kuliko tunavyojiamini kama tuliofutwa akili. Tunasikiliza kila wanachosema kutufanya wajinga wanaojua waliyofundishwa na wazungu tu.

Ni wakati wa waafrika kuonyesha wanaelimu ya sasa na ya jadi, wachina wanatumia dawa za asili kutibu korona na mengi, bila WHO kuthibitisha dawa hizo, na wanapona na kupambana na Korona kikamilifu, kwa nini siye tusifanye hivyo?

Huoni aibu kusubiri wazungu wakupe kila kitu kama wewe huna akili? Au ndiyo zimefutwa kama tunavyojua?
 
Effect of colonialism

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huwa nasema mtu kuwa na ngozi nyeusi sio shida, shida ni pale akili yako inapofanana na rangi ya ngozi yako.
Nashangaa sana Waafrika wanapoipinga dawa ya Madagascar kisa eti WHO hawajathibitisha.Lakini ukweli ni kuwa wanaipinga kisa haijatengenezwa na Mzungu.
Juzi Mbunge wa Lushoto alisema amepata dawa ya korona na imekabidhiwa maabara kwa uchunguzi.Sasa watu badala ya kusubiri majibu wanaanza kumtukana huyo Mbunge eti ni muongo na tapeli,kwanini? kwasababu ndani ya akili zao wanaamini mtu mweusi hawezi kupata tiba ya janga kubwa kama hili.
Ndio maana huwa nasema Waafrika wengi(hasa weusi) hawahitaji kiongozi wanahitaji Mtawala atakayewatawala kwa mkono wa chuma na mijeledi mpaka ujinga uishe vichwani mwao ndiposa wapewe kiongozi.
 
Ndio maana huwa nasema Waafrika wengi(hasa weusi) hawahitaji kiongozi wanahitaji Mtawala atakayewatawala kwa mkono wa chuma na mijeledi mpaka ujinga uishe vichwani mwao ndiposa wapewe kiongozi.

Kuna waafrica wasio weusi.?
 
Vifo vilivyotokana na Corona katika mataifa ya Amerika na Palestina mpaka kufikia leo hii 09/May/2020, kama ifuatavyo.

MAREKANI:
Confirmed 1, 325, 519
Dead 78,762
Recovered 223,930


PALESTINA:
Confirmed 275
Dead 2
Recovered 228


ISRAEL:
Confirmed 16,444
Dead 245
Recovered 11,313


Inshaallah nitaendelea kuwaletea Updates
 
Duuh: Naona miaka 5 nyuma kulikuwa na mataifa yanaongoza kwa Vita hasa Vita vya kuletewa, mwaka 2020 naona mambo yamebadikika, NATO ndo wameshika usukani
 
Mkuu madereva teksi na basi Newyork wengi ni Waislam wakufa wengi sana. Acha ushabiki
 
Kwajinsi ugongwa huu ambavyo unawapelekesha watu bado kuna watu wanasema ugongwa huu Auui dah masikhara tuache jamani Gonjwa hili ni baya kupita maelezo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…