Fahamu kuhusu bakteria wa H.Pylori; Athari na tiba yake

Fahamu kuhusu bakteria wa H.Pylori; Athari na tiba yake

Nenda duka la dawa tafuta dawa inaitwa heligo kit tumia then ikiisha endelea na omeprrazole kwa siku 21...tatzo lako litabak kua historia ndugu
 
Sasa wakuu mngeweka hapa hizo info ili na wengine pia wapate msaada ndo maana nzima ya jamiiforum.. Mkipeana taarifa kimya kimya sio poa.. Nawasihi na kuwaomba kiungwana tu muweke ufumbuzi wa hilo tatizo hapa ili na wengine wapone...
Kweli mi pia ninatatizo hilo asee
 
Nenda duka la dawa tafuta dawa inaitwa heligo kit tumia then ikiisha endelea na omeprrazole kwa siku 21...tatzo lako litabak kua historia ndugu
Mkuu umeshawahi kutumia, na ikabaki historia
 
Hiyo ni full dose kwa helicobacter pylori...usiwe na waswas rumia kama nilivyokuelekeza ..
Nishawahi kutumia, ndio maana nakuuliza hivyo. Je kuna masharti wakati unatumia, unaweza kunieleza
 
Na si kuumwa tu chembe ya moyo na tumbo unaweza hata kujifikiria una ukimwi maana dalili zake ni nyingi vidonda mdomoni maumivu ya mwili hata unaweza kufikiri ni typhoid au malaria mgongo na kiuno kuuma miguu uchomvu mwilini kichwa kuuma miguu kuwanga nk
Kweli kabisa!
Hapa tatizo hasa huwa ni lipi?
Maana ukienda hospitali ukiwaelezea dalili ya unavyosumbuliwa na tumbo suspect yao ya kwanza huwa ni vidonda vya tumbo!

Nilishawahi kupimwa hispitalini wakaniambia nina vidonda vya tumbo wakanipa dawa za kutuliza vidonda vya tumbo na wakaniambia nisile baadhi ya vyakula lakini dawa hiyo haikunisaidia sana.

Ikabidi nibadilishe hospitali nikaenda kukutana na specialist wa masuala ya tumbo yeye baada ya vipimo akaniambia sina vidonda vya tumbo ila nina fungus tumboni hivyo nile vyakula vyote nilivyokuwa nimezuiliwa mara ya kwanza akanipa dawa ya kutibu fungus. Nimetumia dawa hiyo ikanipunguzia maumivu kwa kiasi kikubwa sana na nikaona ahueni.

Tumbo kuuma kwa dalili zilizokuwepo mwanzoni ziliisha yaani kuuma pale unapohisi njaa badala yake lilianza kuuma kivingine likawa linauma juu kwenye ubavu au chini ya kitovu yaani maumivu yanakuwa yanahama! Nikaenda tena hospitali nyingine nikapima wakaniambia bandama ina shida sikuwaelewa ikabidi niende sehemu nyingine wakanipima wakaniambia sina tatizo hilo lakini wakasema kuna dalili za vidonda vya tumbo tu kuna mikwaruzo kwa mbaaaali! Wakanipa dawa nikatumia nikapata ahueni tena mpaka sasa ni afadhali kwa upande wa tumbo.

Kuna shida zingine kama uchovu wa mwili, kukosa appetite ya chakula, kutokuongezeka uzito(nimekuwa na uzito ule ule zaidi ya miaka minne pamoja na kuwa nimeimprove kidogo level ya maisha na sina majukumu makubwa yanayonikabili kwa wakati huu) nk bado hizi zinakuwa zinajirudia.

Dawa ambazo nimekwishatumia ninazokumbuka ni Rabeprazole, Esomeprazole. Kwa jinsi majibu ya hospitalini yanavyokuwa yanakinzana huwa nashindwa kujua tatizo linalonisumbua hasa ni lipi ninachoweza kuelezea tu ni jinsi ninavyoumwa ila tatizo lenyewe sijui hasa ni lipi!

Sijawahi kuumwa seriously kuweza kuacha kutekeleza majukumu yangu ya kila siku!

Hebu naomba kwa experience ambavyo mnafahamu mnisaidie. Tatizo hasa ni nini?
Dawa yake ni ipi?
 
tebweta,
Mkuu ukipata suluhisho unikumbuke na mimi kwenye ufalme maana nami dalili kama zako huwa nazi-experience!
 
mwasita,
Mimi mwenyewe nimepima vipimo vyote nimeambiwa sina vidonda vya tumbo, ila nina hao bacteria wanaosababisha vidonda vya tumbo. Cha ajabu kiungulia na kifua kuwaka moto ndio tatizo kubwa nililo nalo.
 
Nilienda hospital ya Regency wakanipa heligo kit na dawa nyingine mbili mwaka jana nikazitumia ipasavyo mpaka tembe ya mwisho. Mpaka sasa sijaumwa tena na nilienda kupima tena sikukuta huo ugonjwa.
 
Nilienda hospital ya Regency wakanipa heligo kit na dawa nyingine mbili mwaka jana nikazitumia ipasavyo mpaka tembe ya mwisho. Mpaka sasa sijaumwa tena na nilienda kupima tena sikukuta huo ugonjwa.
Je kifua kilikuwa kinawaka moto au ni dalili tofauti na hizo
 
H. Pylori ndio ansababisha vidonda mpaka upate dalili hizo ni tayari una vidonda hivyo basi nenda wakufanyie endoscopy kubaini hivyo vidonda, huyo bakteria mara nyingi ana tabia ya kurudi ukitumia dawa anaisha baada ya muda anarudi, prof mmoja aliniambia kati ya watu 10, nane wanao huyo kitu na hadi daliki zijitokeze umeshaishi nae si chini ya miaka 10 huwa anamwaga acid kwenye utumbo ambayo husababisha vidonda na kukausha yale majimaji yayofanya choo kiwe laini matokeo yake kupata choo kigumu
 
H. Pylori ndio ansababisha vidonda mpaka upate dalili hizo ni tayari una vidonda hivyo basi nenda wakufanyie endoscopy kubaini hivyo vidonda, huyo bakteria mara nyingi ana tabia ya kurudi ukitumia dawa anaisha baada ya muda anarudi, prof mmoja aliniambia kati ya watu 10, nane wanao huyo kitu na hadi daliki zijitokeze umeshaishi nae si chini ya miaka 10 huwa anamwaga acid kwenye utumbo ambayo husababisha vidonda na kukausha yale majimaji yayofanya choo kiwe laini matokeo yake kupata choo kigumu
Dalili ninazo, na nimefanya endoscopy sina vidonda ila bacteria ninao, je hapo suluhisho ni lipi
 
Tumia kwanza helicokit kwa wk 2 hadi 3 wakati unatumia hiyo tumia na amoxicillin 2 bd kwa siku 14 utanipa majibu
 
Asante umempa jibu ni 2 kutwa mara 2 inakuwa mara 2 kwa sababu kule kwenye kit kuna antibiotic nyingine hivyo zinachanganywa ili umuue ukimaliza hii dose kapime tena choo kikubwa na damu,ndani ya kit kuna flagyl hivyo usishangae mdomo kuwa mchungu na kujisikia vibaya fulani hivi siipendi flagyl ila ni dawa inatibu vizuri, mimi leo nipo nusu ya kit ya pili niliandikiwa kule regency
 
Nakuonea huruma maana najua jinsi hiki kitu kinatesa mimi aliondoka juzi nimempima tena karudi baada ya kuwa niliumwa sana
 
Kuna dawa aina tatu katika kutibu vidonda vya Tumbo
Antibiotic hii ni ya kuua bakteria hpylori
Dawa ya pili ni ile ya kupunguza tindikali
Na dawa ya tatu ni ile ya kutengeneza ute ndani ya kuta za tumbo
Wakati unatumia heligo kit unashauriwa usitumie tena dawa nyingine ya antibiotic zaidi ya kutumia dawa za kupunguza tindikali Omeprazole au jamii ya dawa za kupunguza tindikali
Kwa wale wanaotaka kujalibu kutumia dozi ya heligo kit tafadhari someni kwanza maelezo yake..
 
Kuna dawa aina tatu katika kutibu vidonda vya Tumbo
Antibiotic hii ni ya kuua bakteria hpylori
Dawa ya pili ni ile ya kupunguza tindikali
Na dawa ya tatu ni ile ya kutengeneza ute ndani ya kuta za tumbo
Wakati unatumia heligo kit unashauriwa usitumie tena dawa nyingine ya antibiotic zaidi ya kutumia dawa za kupunguza tindikali Omeprazole au jamii ya dawa za kupunguza tindikali
Kwa wale wanaotaka kujalibu kutumia dozi ya heligo kit tafadhari someni kwanza maelezo yake..
Heligo kit ina dawa tatu, mbili zikiwa ni antibiotics yaani Clarithromycin na Tinidazole na ya tatu ni ile yakupunguza tindikali(proton pump inhibitor) Lansoprazole. Dose ni vidonge 3 kila baada ya masaa 12 (mara mbili kwa siku) kwa siku 7, jumla ni vidonge 42. Baada ya hapo utaendelea na Lansoprazole pekee kwa wiki 4.
 
Huu ugonjwa unatesa sana jamani, yaani kuna siku nilikuwa mahali nje ya mji na kulikuwa hakuna chakula tulienda msibani na huko chakula kilipikwa cha wafiwa wakati wa kurudi nikanunua muhindi wa kuchoma nikanywa na soda ya Novida, Mungu wangu maumivu niliyoyapata ile siku na wiki nzima baadae sita sahau kabisa ni maumivu makali mno ya tumbo na kichwa., huu ugonjwa Mungu tu atushushie dawa ya uhakika tupone.
 
Back
Top Bottom