Fahamu kuhusu kuanzisha biashara ya Mobile Money (M-Pesa, Tigopesa)

Fahamu kuhusu kuanzisha biashara ya Mobile Money (M-Pesa, Tigopesa)

Nadhani ni kama asilimia 3 hivi. Huwa najaribu kupiga mahesabu ya kiwango nilichotumia kutoa huduma na commission niliyopata inakuja around hiyo percent.
 
Wakuu naomba kujua namna kuweka pesa ya mtaji kwenye line ya MPESA!! Je ni lazima uende Bank? na kama una deposit bank, ni details gani zinahitajika ili kufanikisha zoezi hili? Natanguliza shukurani
 
mimi nafanya sana hizi biashara ngao za kufanikiwa ni tatu, LOCATION, MTAJI NA MFANYAKAZI MWENYE IQ na MWAMINIFU
 
JAMANI LAINI YA MPESA NA TIGO PESA KWA MKOANI MFANO KILIMANJARO NI SHILINGI NGAPI KWA SASA MAANA HAPA DSM HAWATOI TENA
tAFADHALI ANAYEJUA ANIJUZE
 
Line ukiwa na tin no na leseni una apply kwenye makampuni ya simu husika.Au unaweza kununua kwa mtu unakuja kufanya mchakato wa kubadili majina yasome jina lalo.Faida wanatoa kwa commission
 
ukitaka line m-pesa unatakiwa kuwa na tin namba ,mtaji wa kutosha kama laki tano na leseni ya biashara unaenda ofisi za voda gharama zake haizidi 20000 faida inaipata kutokana na miala unayofanya .
 
..hayo maelezoo apo ju nayaunga mkono 100%,ila kama ukiitaji pia kutumia line za watu wengine ambao wameacha hiyo biashara na baaa ya kubanwa au kupata fursa kubwa zaidi pia inawezekana alafu baadae ukishajipanga zaidi unachange majina utakayokuwa unatumia yasome majina yako..na gharama za kuchange majina si kubwa kivile na pia hizo doc's kama TIN NO.LESENI YA BIASHARA na copy ya kitambulisho chako..cha kura,Leseni ya udereva.Pasport au ID ya Taifa...
 
Nilipeleka photocopy ya leseni kitambulisho tin namba kwa dealer mmoja Kahama mwaka jana hadi sasa niongeapo sijapata line ya M Pesa!Wao wananishauri nitoe laki na nusu nitumie line ya mtu mwingine.Nimeona ni wababaishaji nikafanya kitu kingine

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Line kwa watu zinarange laki sita mpaka nane kwa zote mbili mimi juzi nimenunua tigo&voda kwa laki saba kama unahitaji nipm nikupeleke kwa mdau kkoo
 
Line kwa watu zinarange laki sita mpaka nane kwa zote mbili mimi juzi nimenunua tigo&voda kwa laki saba kama unahitaji nipm nikupeleke kwa mdau kkoo

sijakupata unasema zina range la saba adi nane kwa moja au mbili mm nina laki nne adi tano kwa zote mbili tigo na voda
 
Mkuu mimi nimefungua m-pesa na nimetumia gharama kama ifuatavyo
Simu mbili = 70,000
Laini mbili = 300,000 (nilinunua lain za mtu)
Pesa ya kuanzia yani ile ya kuweka kwenye mzunguko = 1,500,000.
NB: Hiyo ni m-pesa tu. Na ukitaka kufaidi zaidi inatakiwa uwe na mtaji mkubwa kidogo. Mtaji ukiwa mdogo utaishia kuwa unarudisha wateja tu kwa kuishiwa pesa.
 
Mitandao inaruhusu kuuziana line? Kama ndio, je watahtaj tena upeleke lesen ya biashara na docs zngne?
 
Naombeni msaada wakuu,nahitaji kuanzisha biashara ya mpesa na tigo pesa.Mwenye uzoefu na biashara hii naombeni anijuze yafuatayo
1.Jinsi ya kupata line hizo
2.Je ni mtaji at least wa shs ngapi nikianza nao nitaweza kuendesha biashara kiufasaha bila kusuasua
3.Vitu gani niwe navyo vinavohitajika mf leseni,tin no
4.Faida inavohesabiwa kwa mwezi naamisha calculation zao wanafanyaje?
Asanteni hope nitapata ushirikiano wakuu
 
Mi ninavyo jua. ili kupata till lain ya mpesa, tigo, aitel.
1.uwe na tin namba
2.leseni ya biashara
3.kitambulisho
4.barua toka m/kiti
nenda navyo tigo,voda,airtel umasajiliwa line zako nazani kusajiri ni bule, pia uwe na mtaji ktk line zako. utapewa line mbili mbili ambapo moja ni kwa huduma na nyingine ni kwa mshahara pia inaikontrol na kukagua ile ya huduma.
 
Mimi naifanya biashara hii hapa Dsm, mahitaji ya kupata laini za kazi TIN NO, LESENI YA BIASHARA NA ENEO LA KUFANYIA HIYO BIASGARA pamoja na mtaji.Ili uweze kufanya kazi bila kurudisha wateja wengi kwa kutokuwa na salio unanatakiwa uwe na mtaji usiopungua milioni mbili, na hapa mzunguko wa hela utauona na utaweza kupata kamisheni kubwa.

Mfano kama unafanyia kazi eneo kama kimara mwisho au mbezi mwisho au eneo lingine lenye mzunguko mkubwa wa watu hukosi kamisheni kuanzia laki nne hadi nane kwa mwezi. ANGALIZO, UNATAKIWA UFANYE MIAMALA MINGI ILE KAMISHENI IWE KUBWA KIUJUMLA.

CHANGAMOTO KUBWA KWA SASA Ni kupata line ktk haya makampuni mawili yaani tigo na voda, nakuhakikishia utapeleka document zako pale utasubiri hata mwaka na laini bado hujapata, sanasana utaambiwa utoe laki tatu hadi tano na vishoka wa kule akakutafutie laini zile ambazo wanazifungia kwa mawakala wanaoshindwa kazi

Mimi nina laini moja ya MPESA NAIUZA SH350,000/= Kama unahitaji.

Biashara ni nzuri sana, Faida mojawapo ni urahisi katika uendeshaji usiokuwa na ‘longolongo’ nyingi kwa mfano, biashara hii hata kama unamuachia majukumu msaidizi ama mfanyakazi, huumii sana kichwa kwani hesabu zake zinajulikana na isitoshe,
miamala yote hurekodiwa kiteknolojia na kampuni husika ambapo huwa rahisi
mwisho wa mwezi au kipindi cha biashara kuja kupewa kamisheni ya miamala iliyofanyika.

Hakuibii mtu hapa. Uzuri mwingine wa biashara hii ya uwakala wa makampuni ya simu ni kwamba, jioni baada ya kufunga kazi mjasiriamali unafahamu mara moja faida
uliyopata katika siku husika kulingana na idadi ya watu na kiasi cha miamala
waliyofanya. Husumbuani na mteja kwenye bei kwani bei zinakuwa zimeshapangwa tayari na makampuni, na hamna shida ya wateja kwani mahitaji ya huduma za kipesa ni mengi na mawakala bado ni wachache nchini.

Kuna vikwazo pia katika biashara hii, na kubwa likiwa ni suala zima la usalama. Ili
kuanzisha biashara hii mahali fulani yafaa kwanza suala la usalama wa pesa na
wewe utakayekaa hapo litiliwe kipaumbele cha kwanza kabisa. Ikiwa ni duka au kibanda basi ni sharti uhakikishe, unajengea ‘gril’kuzunguka dirisha na milango ili kuhakikisha hapawi kivutio kwa wezi na majambazi wenye silaha.
 
Nami nitoe tu angalizo kwa wateja wote mnaohitaji kununua hizo till. Itakapotokea wakala umekutana na changamoto halafu ukaambiwa uende tigo/v-shop ndipo utakapopata usumbufu. Tafuta till ya jina lako, kwani hata mtu akigundua unatumia till ya jina lake anaweza kuifungia kwa kuwasiliana na kampuni husika halafu wewe ukose pa kulalamika.
 
Nami nitoe tu angalizo kwa wateja wote mnaohitaji kununua hizo till. Itakapotokea wakala umekutana na changamoto halafu ukaambiwa uende tigo/v-shop ndipo utakapopata usumbufu. Tafuta till ya jina lako, kwani hata mtu akigundua unatumia till ya jina lake anaweza kuifungia kwa kuwasiliana na kampuni husika halafu wewe ukose pa kulalamika.

Umenena mkuu.kuna jamaa yangu alinunua till kwa mtu baada ya mda jamaa akaenda voda na nyaraka zote akasema till yake imepotea jamaa akafanyiwa swap na till zikarudi tena kwake na huyo jamaa angu alikua na commission yake humo na laki mbili ya mtaji!!kwahyo wawe makini na watu wanaowauzia.
 
me nlikuwa napita tu na nmejfunza kitu kikubwa mno congraturation kwa mtoa elimu
 
Habarini wanamaendeleo wenzangu.

Nina laki 7 cash nahitaji kuiwekeza katika mradi tajwa juu.

Naomba unieleze hatua za kufuata na kila hatua na gharama zake.

NB.
Nimepiga Huduma kwa Wateja wakaniambia niende voda shop lakini nipo kijijini sana.

Ukiwa na namba za wakala Mkuu wa Mwanza au Shinyanga ni pm pia.

Mbarikiwe sana.

Tunataka amani Oct 25!
 
Back
Top Bottom