Faida ya kuishi duniani ni ipi kama tulizaliwa ili tufe?

Faida ya kuishi duniani ni ipi kama tulizaliwa ili tufe?

Habari zenu,

Natumaini wote wazima.

Huwa najiuliza swali hili kila siku. Na jibu sijawahi kupata, sasa kuna umuhimu gani wa kuishi duniani hali ya kuwa utakufa?

Biblia inasema kuwa Adamu na Hawa walikula tunda pale edeni eti ndo sababu tunakufa. Ina maana kuwa kifo hakikuwa kabla ya kula lile tunda na hata sijui nitunda gani hilo, biblia imetuficha kutupa ukweli.

Sasa kifo na tunda linahusiana na nini? kama MUNGU hakutaka Adam na Hawa wale lile tunda yanini aliliweka kwenye bustani ya edeni? majaribio mengine bana.

Hilo tunda lina ubaya gani? Kitu umekiumba kwanini ukataze kisiliwe? Biblia imetudanganya hapo.

Jamani hata kwa akili ya kawaida kweli upande mazao yako shambani halafu ukataze familia yako kula kweli inakuja? Biblia imeficha ukweli.

Hivi kweli uzae watoto wako alafu uje kuwauwa kisa hawajakutii au hawajafanya utakacho??

Kama tuliumbwa ili tufe ina faida gani kuishi duniani. MUNGU angetuuliza kila mmoja kama utakubali kuishi ili uje kufa baadae kuliko kutufanyia umafia kama huu.

Mtu unahangaika kutafuta maisha kwa kila hali hata mda mwingine hupati milo yako vizuri ili kujibana upate maisha manzuri, sasa unafanya yote ya nini wakati utakufa?

Mambo haya yanachanganya kichwa sana.
Faida si hiyo ya kufa.
 
Ni hivi kijana Mungu alimuumba binadamu na lengo la Mungu ni kwamba binadamu asife ,kifo kilikuja baada ya binadamu kutenda dhambi ya kula lile tunda ambalo lilikuwa la kutambua mema Na mabaya Na kabla ya kula tunda binadamu alikua haujui ubaya wowote so kula tunda kulifanya binadamu aondoke kwenye lengo la Mungu Kwa kuujua ubaya,na ubaya ndio uliozaa mauti so mauti ilikuja baada ya binadamu kuujua ubaya automatically kifo kikatokea
Hivi kweli Mungu hakujua ya kwamba viumbe aliowaumba yeye watakuja kula tunda walilokatazwa?
Kama Mungu anajua future zetu iweje hakutambua hilo?
 
Ni hivi kijana Mungu alimuumba binadamu na lengo la Mungu ni kwamba binadamu asife ,kifo kilikuja baada ya binadamu kutenda dhambi ya kula lile tunda ambalo lilikuwa la kutambua mema Na mabaya Na kabla ya kula tunda binadamu alikua haujui ubaya wowote so kula tunda kulifanya binadamu aondoke kwenye lengo la Mungu Kwa kuujua ubaya,na ubaya ndio uliozaa mauti so mauti ilikuja baada ya binadamu kuujua ubaya automatically kifo kikatokea
[emoji120]
 
Unajua kuna vitu huvielewi I used to be like u but elimu ya mambo ya kiroho ni elimu pana sana na inahitaji imani kuielewa Kuna for nutshell mambo ya rohoni yanaongozwa Kwa kanuni binadamu tuliumbwa Kwa mfano wa Mungu so tuna uwezo mkubwa sana ndani yetu nafsi yako inauwezo wa kufanya maamuzi binafsi rejea kwenye mfano wa ibrahim wakati Mungu anampa mtihani wa kumpima imani Kwa kumtoa sadaka mwanawe so kama Mungu angekua anajua ya kwamba ibrahimu hawezi Kwa nn Mungu alimjaribu ibrahimu so Kuna nguvu flani Au nafsi flani binadamu kapewa ambayo Mungu hawezi kuijua
Kwamba kuna vitu sivielewi then wewe unavielewa.....!?

Hv unaelewa nkikwambi kuwa bible ni kitabu cha hadithi!?
Tena ukiwa unaanza kusimulia inabidi uanze kwa kisema "hadith hadithi..."
Ili watu tuitikie
"hadithi njoo uongo njoo utamu kolea.."

Wewe unaleta hadithi za Ibrahimu hapa, hizo ni hadithi za kutungwa tu, unautafuta ukweli kwenye hadithi.

Na kukuonesha kwamba hujui kitu, ni kwamba wewe hujui hata hizo hadithi zimepitia mambo gani!? Zimeandikwa na akina nani...!?
Zimerekebishwa na kuongezewa content mara ngapi..!?
Na umeanza kuamini bila kujua hata chembe ya hiko kitabu.

Hayo maajabu mbona hayatokei siku hizi!?

Huyo Mungu wa waisrael aliyekuwa nao kuwaokoa kutoka Babylon na misri, alishindwa vipi kuwapaisha tena kipind kile cha mtaalam Adolf hittler akawaua mamillion (zaid ya 5 million waliuawa).
Unadhan isingekuwa kabla ya usasa wangeshindwa kuandika hadithi hapo ya Musa part 2!?

Huyo Mungu muweza wa yote mjuzi wa yote na mwenye upendo wote hayupo.
Wala hata hawezekani kuwepo.
Mungu mwenye hizo sifa asingeweza kumjaribu Ibrahimu.
Kitendo cha kumjaribu Ibrahimu kinaonesha kuwa si mjuzi wa yote.
Unaelewa hilo!?
 
Okay let's assume walikatazwa kusex
1. Nyoka kafanyaje Sasa kala tunda la Eva ndo Adam Akala au Eva kala tunda la nyoka afu akampa Adam? Usitoke nje ya Biblia ni jibu accord to logic na verses.
2. Wamekatazwa kulana ehe watoto wanatoka wapi ambao wameambiwa wajaze dunia.
3. In short the analogy ya tunda kuwa bikra falls apart completely hii story sio valid coz it's impossible scientifically haiwi supported historically geologically na pia logically. It's not historical na imeigwa from older cultures so ni myth story tu.
Sasa kama ilikuwa ni sex,
Nikisema kuwa huyu Mungu alikuwa hajitambui ntakuwa nakosea!?

Yani aliumba uume na uke halafu akawakataza wasisex??

Kwanini aliwaumba na hzo organs..!?

Mimi nimewaambia watu, hyo project ya eden haikuwa na specific objectives, naweza sema kuwa Mungu alikurupuka tu hakujiandaa.

Inakuwaje akaumba wanaume na magovi halafu baadae aje awaambie watahiri!?
 
Ye si mjua yote? We unaweza ukaweka bomb chumbani afu ukawaambia watoto wako chezeni huko ila msiguse bomb? Hizi ni story za mababu katika kujaribu kujua shida zimetokea wapi ndo maana wamemtunga Eva Kama mwenye kosa coz ni mwanamke
Mimi huwa sipend hata nkiskia mtu anarejelea mwanamke kama chanzo cha shida na mabaya yote anayopitia.

Huwa nateseka sana moyoni.

Maisha yakikupiga, mwanamke hahusiki.
Mungu mwenye upendo wote hawezi akahukumu kizazi chote kwa kosa la mtu mmoja.
Huyo Mungu wa design hyo anamatatizo makubwa sana kwa tafsiri ya chini kabisa ya kibinadamu.

Hiyo ni dhana ya zama za giza, mwanamke alikuwa hathaminiwi.
 
Kwa hiyo faida za kufa huzioni??

JIULIZE
1. Kama ingekuwa hakuna kufa, watu wote toka enzi hizo Hadi sasa, hivi idadi ya watu ingekuwaje??
2. Ikiwa watu wanakufa na idadi ya watu baadhi ya nchi na Miji mfano Dsm Ina watu wengi kupitiliza, ingekuwa watu hawafi hali ingekuwaje??

3. Unadhani dunia ingetosha kusupport maisha ya watu wote??

4. Umewahi kuchinja mbuzi, kuku, bata, ng'ombe??

Wenyewe wanaona dhiki na tabu kuchinjwa na kuukiwa lakini wewe unachinja tu bila kuwaonea huruma, ndio hivyo hivyo Mungu anaona kawaida na kitu chepesi tu kufa kwako.
Sasa Mungu muweza wa yote na mwenue ujuzi wote angeshindwa kuumba ulimwengu ambao watu hawafi na idadi haiongezeki!?

Unataka kunambia Mungu muweza wa yote na mjuzi wa yote angeshindwa kuumba dunia ya watu immortal na ikatosha kusupport maisha ya watu wote??
 
Hatukuumbwa tufe ila kutokana na kutotii maagizo ndio maana ikatolewa adhabu hiyo, mfano rahisi ni huu je wewe baba yako akikwambia usifanye hiki halafu we ukakaidi kipi kitakukuta??

Pamoja na hayo na kupewa kutokufa, lakini binadamu alipaswa kutii maagizo ili awe hai mfano Adamu alitakiwa aishi kama binadamu ili aendelee kubaki hai mfano. Isingetegemewa apande juu ya mti mrefu halafu ajitupe chini asijeruhiwe hapana vyote vilipaswa kuzingatiwa


By the way, maisha ni matamu sababu tunakufa sipati picha leo hii bado tungekuwa na kina kingunge, Yuda eskarioti, plato etc sasa si dunia ingekuwa inaboa sana, we unakutana na watu wamezaliwa enzi za nuhu😁😁
Sasa Mungu muweza wa yote mjuzi wa yote na mwenye upendo wote alishindwa kuumba ulimwengu ambao watu wasingewezekana kuja kufa!?

Yaani hakujua kuwa hao watu wa kwanza wanacharacter ya ukaidi na wangekuja kutokumtii maagizo yake?
 
Sasa kama ilikuwa ni sex,
Nikisema kuwa huyu Mungu alikuwa hajitambui ntakuwa nakosea!?

Yani aliumba uume na uke halafu akawakataza wasisex??

Kwanini aliwaumba na hzo organs..!?

Mimi nimewaambia watu, hyo project ya eden haikuwa na specific objectives, naweza sema kuwa Mungu alikurupuka tu hakujiandaa.

Inakuwaje akaumba wanaume na magovi halafu baadae aje awaambie watahiri!?
🤣Story yenyewe imeibwa Gilgamesh
 
Mimi huwa sipend hata nkiskia mtu anarejelea mwanamke kama chanzo cha shida na mabaya yote anayopitia.

Huwa nateseka sana moyoni.

Maisha yakikupiga, mwanamke hahusiki.
Mungu mwenye upendo wote hawezi akahukumu kizazi chote kwa kosa la mtu mmoja.
Huyo Mungu wa design hyo anamatatizo makubwa sana kwa tafsiri ya chini kabisa ya kibinadamu.

Hiyo ni dhana ya zama za giza, mwanamke alikuwa hathaminiwi.
🤣Ni coz story zimeanzishwa na wanaume
 
Ebwanaee, kuna utata sana apo kuhusu suala la kufa ndo maana wanasemaga usijudge sana kuhusu mungu unaweza ukakufuru ikala kwako....ila kwamfano maandiko yamesema mshahara wa dhambi ni mauti, jee kwann watenda mema nao wanakufa? na kama wakifa hao watenda dhambi kwanini wafufuliwe afu wauwawe tena au kuteswa kwenye jehanum
Jehanamu ni Israel, ni sehemu walikuwa wanachomea maiti zamani.
Maarufu kama bonde la hinnom ama Gehenna.
Kwahyo Moto wa Jehanam ni kama metaphor kurejelea hapo.

Usiteswe na hadithi za watu wa israel 🇮🇱
 
🤣Story yenyewe imeibwa Gilgamesh
Watu hawaelewi haya,
Hawajui kuwa Miungu wa Babylon kule Mungu Enlil na Enki walikuwa wanapiga story wanaambizana "na tumuumbe mtu kwa mfano wetu"
Halafu mwandishi wa bible akasahau kurekebisha hapo ili awe Mungu mmoja. Huyo Muweza wa yote mjuzi wa yote.

Watu hawajui kuwa Mungu wa maji na hekima, Mungu Enki alimwambia Atrahasis ajenge safina ili aokoe kizazi kwani angeshusha gharika.

Haya yote hawajui kuwa ni hadithi.

Sasa wao wamesoma kwa mhusika Nuhu pekee,
Ilikuwa ngumu kwangu kukubali Penguin 🐧 alitoka America akaenda mashariki ya kati kutafuta safina.
 
Tafuta biblia zilizo halali utajua maana ya Tunda, achana na hizo nakala za kihuni walizotafsiri VATICAN kwa kuficha ficha mambo kwa maslahi yao.

Mtu wa kwanza hakuitwa Adam wala mkewe hakuitwa eve maana hawakuwa na asili ya Uzungu, pili hawakuishi huko walikotuaminisha hawa wachungaji na wanasayansi uchwara.

Tatu Tunda maana yake ilikuwa ni maarifa/Neno la ujuzi wa kutambua mambo fulani hapa dunian, na Mti ulito toa hayo matunda ni Malaika ambao waliishi dunian na walikuwa na mission zao hapa hapa dunian.

Mtu wa kwanza alipewa ONYO asiwasiliane na hao malaika wala kuwaomba wampe/wamwambie Habari za maarifa waliyonayo ambayo walukatazwa kuyajua maana yalikuwa nje ya uelewa wao(Tunda).

Baada ya kuumbwa kwa mwanamke ambaye biblia za uongo zinamuita eva/hawa huyu hakuumbwa kwa udongo kama Adam bali aliumbwa kutokana na Imagination+mawazo ya Adamu kuhusu uwepo wa kiumbe kitakachofanana nayeye kitakachomtoa upweke hivyo eva aliumbwa kwa staili hii.

Kwakuwa Eva hakuwa na Uelewa sawa ama nguvu sawa na adamu bali alishawishika na kiumbe ambacho biblia zenu zinasema ni nyoka(Dragon) ambaye ndiye alimshawishi eva na eva ndiye wa kwanza kuyasikiliza maarifa ya wale malaika walioambiwa wasiyasikie na baadae akamueleza Adam, hapa ndipo chanzo cha maovu kilipoanza.

Adam hakufa kama tunavyodanganywa bali alipewa laana kwa wazawa wake na hata eva hakufa tafuta ktk biblia yako hutoona maala wanaeleza hili jambo zaid ya kudanganya kuwa adam alikufa na umri wa miaka fulan which is nonsense.

Unatakiwa ujuwe kuwa Adam mission yake aliyoletwa dunian ilikuwa ni kuongeza idadi ya malaika waliosaliti ambao idadi yao ilitakiwa kuwa replaced na wana wa adam atakao wazaa na mkewe maana Adamu nae kabla ya kuumbiwa mwili alikuwa ni sehemu ya malaika, baada ya anguko la shetan na wenzie ndipo ikaja sababu ya adamu kushushwa dunian na akafanyiwa mwili ili aweze kuendeleza uumbaji wa malaika wapya(wanadamu).

Idadi inayotakiwa kwa wana wa adamu kureplace idadi ya malaika waliosaliti mbingu inajulikana na huenda ikatimia muda ukifika.

Shida za dunia hazitokwisha na hizo raha mnazotamani hazitopatikana maana huyo kiumbe anaeitwa shetan hataki idadi ya wana wa adamu itimie maana ikitimia na ule mwisho utafika na hukumu kwa shetan na wafuasi wake itafika.

Shetan si mjinga kuwapotosha watu na kuwafanya wamsaliti Muumba ili tu idadi isifikie na malengo ya shetani kuutawala ulimwengu yaendelee uku idadi ya wana wa adamu ikiendelea kudhorota na anguko la wengi liwepo.

Tutafute elimu nje ya box, Hilo kanisa la kizungu la Katolic wakishirikiana na madhehebu yote na dini zote hawa ndio wahuni nambari moja waliopotosha Biblia ya kweli kwa kufuta baadhi ya vitabu na vingine kuvipotosha kwa kuedit na kuweka uongo mwingi maana hawa wote wako chini ya shetan kuhakikisha wana wa Adamu hatuijui kweli na hatuifikii ile idadi inayotakiwa kureplace jeshi la shetani.

Tuendeleeni kushabikia mamipira, maushenzi ya kubishiana dini ya nani ndio sahihi, kuuwana sisi kwa sisi, kujadiri uwepo wa Mungu na ujinga mwingne tunajichelewesha sisi wenyewe
excellent!!! iyo biblia unayo utume humu
 
mungu alitaka kujua je mtamuamini yeye? na je makatazo yake uliyazingatia ? na je unamuabudu yeye au una mungu wako uliyemshirikisha? baada ya kufa ndio utayakuta uliyoyatenda
1. Jibu la mtoa mada kuhusu kwanini mti uliokataliwa ulikuwepo bustanini lipo hapo. Yale yote yalifanyika ili tu kujua IMANI (msimamo) wa Adam na mkewe yaani lilikuwa ni JARIBU

Kwenye majaribu ndipo wengi wanapomsaliti Mungu. Na ukishinda kwenye jaribu hapo ndipo Mungu anakukubali. Unajifunza nini kutoka kwa...

-Abrahamu kumtoa sadaka mwanae wa pekee Isaka? je angekataa ingekuwaje na baada ya kukubali ilikuwaje?
-Meshack, shedraka na Abednego kama wangekataa kuchomwa moto ingekuwaje?

2. Jibu la mtoa mada kuhusu kufa lipo hapa, kwanza kabisa ndani ya mwili wa binadamu kuna Roho ambayo shauku yake ni kumwona Baba yake (MUNGU) na kuketi pamoja naye.
-Mungu hana mwili yaani ni Roho naye huketi katika ule ulimwengu wa Roho. Ukitaka kwenda kumwona Mungu sharti mwili uuache kwanza ndipo roho yako itaenda kumwona Mungu.
- Ni kama tu ilivyo kwa wanafunzi ukitaka kwenda shuleni lazima manguo yako uyaache kwanza nyumbani then unavaa sare na kwenda shuleni.

Nitakuja kuendelea...
 
Kufa kwa Adam sio kwamba Mungu ndo alimuua, bali ni matokeo ya uchaguzi wake. Yaani, kuchagua tofauti na Mungu alivopendekeza ndio mauti yenyewe.
Mfano. Baba anaweza mshauri mwanawe kwamba ukigusa moto hakika utaungua; mtoto akikaidi na kugusa moto ule ataungua kweli, na hatuwezi kusema Baba kamuunguza, hapana. Kadhali Mungu hakumuua Adam bali hiyo ilikuwa ni matokea ya kutokutii maelekezo.
Mungu muweza wa yote mjuzi wa yote na mwenye upendo wote aliweza vipi kuweka machaguo mabaya kama hayo?

Wewe mwanao aliye mchanga na nidhaifu unaempenda utamfungia chumbani halafu uweke sumu peupe!?
Kulikuwa na ulazima gani wa kuweka option mbaya kama hiyo!?
Sasa mtu anakwambia huyo Mungu anaupendo wote?
 
Jibu la mtoa mada kuhusu kwanini mti uliokataliwa ulikuwepo bustanini lipo hapo. Yale yote yalifanyika ili tu kujua IMANI (msimamo) wa Adam na mkewe yaani lilikuwa ni JARIBU

Kwenye majaribu ndipo wengi wanapomsaliti Mungu. Na ukishinda kwenye jaribu hapo ndipo Mungu anakukubali. Unajifunza nini kutoka kwa..
Hapo tyari umesema Mungu si mjuzi wa yote.
Na wala hana upendo.

Ukitaka kwenda kumwona Mungu sharti mwili uuache kwanza ndipo roho yako itaenda kumwona Mungu.
Yale yale ya MacKenzie.

Mkuu usije tuondolea nguvu kazi ya taifa.
 
Tafuta biblia zilizo halali utajua maana ya Tunda, achana na hizo nakala za kihuni walizotafsiri VATICAN kwa kuficha ficha mambo kwa maslahi yao.

Mtu wa kwanza hakuitwa Adam wala mkewe hakuitwa eve maana hawakuwa na asili ya Uzungu, pili hawakuishi huko walikotuaminisha hawa wachungaji na wanasayansi uchwara.

Tatu Tunda maana yake ilikuwa ni maarifa/Neno la ujuzi wa kutambua mambo fulani hapa dunian, na Mti ulito toa hayo matunda ni Malaika ambao waliishi dunian na walikuwa na mission zao hapa hapa dunian.

Mtu wa kwanza alipewa ONYO asiwasiliane na hao malaika wala kuwaomba wampe/wamwambie Habari za maarifa waliyonayo ambayo walukatazwa kuyajua maana yalikuwa nje ya uelewa wao(Tunda).

Baada ya kuumbwa kwa mwanamke ambaye biblia za uongo zinamuita eva/hawa huyu hakuumbwa kwa udongo kama Adam bali aliumbwa kutokana na Imagination+mawazo ya Adamu kuhusu uwepo wa kiumbe kitakachofanana nayeye kitakachomtoa upweke hivyo eva aliumbwa kwa staili hii.

Kwakuwa Eva hakuwa na Uelewa sawa ama nguvu sawa na adamu bali alishawishika na kiumbe ambacho biblia zenu zinasema ni nyoka(Dragon) ambaye ndiye alimshawishi eva na eva ndiye wa kwanza kuyasikiliza maarifa ya wale malaika walioambiwa wasiyasikie na baadae akamueleza Adam, hapa ndipo chanzo cha maovu kilipoanza.

Adam hakufa kama tunavyodanganywa bali alipewa laana kwa wazawa wake na hata eva hakufa tafuta ktk biblia yako hutoona maala wanaeleza hili jambo zaid ya kudanganya kuwa adam alikufa na umri wa miaka fulan which is nonsense.

Unatakiwa ujuwe kuwa Adam mission yake aliyoletwa dunian ilikuwa ni kuongeza idadi ya malaika waliosaliti ambao idadi yao ilitakiwa kuwa replaced na wana wa adam atakao wazaa na mkewe maana Adamu nae kabla ya kuumbiwa mwili alikuwa ni sehemu ya malaika, baada ya anguko la shetan na wenzie ndipo ikaja sababu ya adamu kushushwa dunian na akafanyiwa mwili ili aweze kuendeleza uumbaji wa malaika wapya(wanadamu).

Idadi inayotakiwa kwa wana wa adamu kureplace idadi ya malaika waliosaliti mbingu inajulikana na huenda ikatimia muda ukifika.

Shida za dunia hazitokwisha na hizo raha mnazotamani hazitopatikana maana huyo kiumbe anaeitwa shetan hataki idadi ya wana wa adamu itimie maana ikitimia na ule mwisho utafika na hukumu kwa shetan na wafuasi wake itafika.

Shetan si mjinga kuwapotosha watu na kuwafanya wamsaliti Muumba ili tu idadi isifikie na malengo ya shetani kuutawala ulimwengu yaendelee uku idadi ya wana wa adamu ikiendelea kudhorota na anguko la wengi liwepo.

Tutafute elimu nje ya box, Hilo kanisa la kizungu la Katolic wakishirikiana na madhehebu yote na dini zote hawa ndio wahuni nambari moja waliopotosha Biblia ya kweli kwa kufuta baadhi ya vitabu na vingine kuvipotosha kwa kuedit na kuweka uongo mwingi maana hawa wote wako chini ya shetan kuhakikisha wana wa Adamu hatuijui kweli na hatuifikii ile idadi inayotakiwa kureplace jeshi la shetani.

Tuendeleeni kushabikia mamipira, maushenzi ya kubishiana dini ya nani ndio sahihi, kuuwana sisi kwa sisi, kujadiri uwepo wa Mungu na ujinga mwingne tunajichelewesha sisi wenyewe
Sasa kama tunakufa idadi inayotakiwa itafikiwa kwa style gani?
 
Habari zenu,

Natumaini wote wazima.

Huwa najiuliza swali hili kila siku. Na jibu sijawahi kupata, sasa kuna umuhimu gani wa kuishi duniani hali ya kuwa utakufa?

Biblia inasema kuwa Adamu na Hawa walikula tunda pale edeni eti ndo sababu tunakufa. Ina maana kuwa kifo hakikuwa kabla ya kula lile tunda na hata sijui nitunda gani hilo, biblia imetuficha kutupa ukweli.

Sasa kifo na tunda linahusiana na nini? kama MUNGU hakutaka Adam na Hawa wale lile tunda yanini aliliweka kwenye bustani ya edeni? majaribio mengine bana.

Hilo tunda lina ubaya gani? Kitu umekiumba kwanini ukataze kisiliwe? Biblia imetudanganya hapo.

Jamani hata kwa akili ya kawaida kweli upande mazao yako shambani halafu ukataze familia yako kula kweli inakuja? Biblia imeficha ukweli.

Hivi kweli uzae watoto wako alafu uje kuwauwa kisa hawajakutii au hawajafanya utakacho??

Kama tuliumbwa ili tufe ina faida gani kuishi duniani. MUNGU angetuuliza kila mmoja kama utakubali kuishi ili uje kufa baadae kuliko kutufanyia umafia kama huu.

Mtu unahangaika kutafuta maisha kwa kila hali hata mda mwingine hupati milo yako vizuri ili kujibana upate maisha manzuri, sasa unafanya yote ya nini wakati utakufa?

Mambo haya yanachanganya kichwa sana.
Maisha mazuri na sio manzuri
 
Back
Top Bottom