Familia inateseka sana. Nisaidieni natafuta Kazi, Kibarua

Familia inateseka sana. Nisaidieni natafuta Kazi, Kibarua

Hata mimi pia nishawahi tapeliwa mtandaoni,naelewa sana worry yako!Hakuna sehem nimeandika kuwa asubuhi niliamkia kuendesha baiskeli baada ya kulala njaa,japo pia naona ni kitu kinawezekana! Baada ya muda mrefu leo ndio nimetoka na baiskeli kwenda Miyuji nilikokuwa nalangua maziwa kucheck upatikanaji wa maziwa,kuna wadau wamenishauri na wanataka nisapoti niendeleze hyo business!
Kwa sasa nakuachia upumue ili nikubane kwa data zako katika uzi huu.
 
Habari wana JF,

Mie kijana wa kiume, naishi Dodoma! Nina mke na mtoto mchanga wa miezi 4. Kitaalum ni muhitimu wa Bachelor ya Computer Science, na nilikuwa nimeajiriwa sehem lkn tulipunguzwa kipindi kile janga la corona limepamba moto.

Sina kazi maalum kwa muda sasa, naunga unga tu kiukweli, nikibahatisha kupata kazi ya mtu binafsi mfano kutengeneza website au la kidogo imekuwa ikinibeba hasa kulipia kodi, lkn sijapata hizo kazi kitambo sasa! nimejaribu sana na bado naendelea kutuma maombi lkn sijafanikiwa, hali imekuwa ngumu kweli kweli kwetu! Nafanya vibarua sometimes hadi vya kubeba zege japo tu familia ipate mlo hasa mke anaenyonyesha!

Lakini saa nane kasoro hii usiku naandika hapa, tumelala njaa, leo nimejaribu vibarua bila mafanikio, hatuna hata sh. mia hapa ndani, imeniuma sana ndio maana nimekuja kwenu kuomba kazi, kibarua chochote halali hata cha kipato kidogo tu!

Mtoto wa miezi minne imebidi tu aanze kunywa uji maana mlo wetu mmoja kwa siku mama anakosa maziwa ya kutosha!

Mwenye chumba kanivumilia hadi kachoka kaniambia nikabidhi tu chumba, japo hii laptop naitumia kwa kazi zangu, lakn kama kuna mteja wana JF naiuza laki3, au kama kuna mtu anakopesha niiweke bond, atunusuru tafadhalini tunatolewa kwenye hii nyumba!

Nipo tayari kuja popote kufanya kazi/kibarua chochote halali! Naombeni sapoti nateseka sana, hasa huyu mzazi kulala njaa hivi inanipa stress sana!

Kwa mawasiliano, namba zangu 0767 960 255 au 0629 531 358.

Natanguliza Shukrani na Mungu atubariki!
Hujatuambia lolote kuhusu Shemeji? Yeye shuhuli zake zinaendaje?
 
Afadhali umepata mwanamke mvumilivu, angekuwa mwingine tayari ungekuta kisha leta nguo za mabwana zake wahamie kwako.

Ukipata hela usije ukamsahau mkeo
Hayo maneno atakayokuwa anatamkiwa akipata hela lazima amwache. Mwanaume Gani? Ulioa ya nini, Bora Fulani angenioa. Najuta kukubalia. Hivi hata nikitongozwa nakataaaje kwa hali hii
 
Kwa sasa nakuachia upumue ili nikubane kwa data zako katika uzi huu.
Seems kama unafurahi struggle za kijana mwenzio!!Napambana na life unataka tena nianze pambana na wewe ndugu?ushaamua kuwa negative kwangu,lkn sina TONE la utapel,na hutakuja kuona huo utapeli unadhani upo kwangu!
 
Seems kama unafurahi struggle za kijana mwenzio!!Napambana na life unataka tena nianze pambana na wewe ndugu?ushaamua kuwa negative kwangu,lkn sina TONE la utapel,na hutakuja kuona huo utapeli unadhani upo kwangu!
Hapa najaribu kuonesha kuwa wewe si muhitaji kama unavyoonesha. Mtaka cha uvunguni .... Ukiona mtu anaomba na bado yupo jeuri jua kuwa ni tapeli tu. Kwa vile dodoma kuna watu kama Madame B tunaweza thibitisha
 
Kakwambia alioa bila Kazi? Si kakwambia alifukuzwa?
Soma uangalie hii Sub-topic imeanzaje na nimejibu hivo kwamantiki gani, jibu langu halihusiani na mtoa mada bali kimada kilichozuka Happ nimetoa View yangu...kama unasoma kabla kujibu.
 
Hujatuambia lolote kuhusu Shemeji? Yeye shuhuli zake zinaendaje?
Shem yupo hapa,kitaalum yeye aliishia form four,japo alifaulu lkn naye ana story ndefu,matatizo ya kifamily huko Mwanza akaishia hapo,akaja Dodoma kwa kaka ake kutafuta maisha,badae akajifunza issue za secretarial services,akawa anafanya kazi stationary!alipopata ujauzito akapoteza hicho kibarua, kipindi hicho nilimsapoti akawa anakopesha vitenge ila hii business ilimshinda kudai,sijui mpole sana!ila ni mpambanaji akaanza tengeneza bites,karanga,kuuza matunda, uji wa ulezi gengeni kwetuu hapa Iringa Road Dodoma karibu na kanisa la Roma,kajifunza kutengeneza cakes,kiufupi ni mjasiriamali mzuri!Badae akalazwa General Hosp.na kufanyiwa Operation,manake alisimama business yake hiyo,nikabaki mie napambana na issue ya maziwa!ilitakiwa apumzike miezi sita, sabu ya Operation yake lkn kaniomba nimsapoti arudi kengeni kwake, jana kafikisha miez 4 tangu ajifungue kwa OP.
 
Hapa najaribu kuonesha kuwa wewe si muhitaji kama unavyoonesha. Mtaka cha uvunguni .... Ukiona mtu anaomba na bado yupo jeuri jua kuwa ni tapeli tu. Kwa vile dodoma kuna watu kama Madame B tunaweza thibitisha
Umlete tu huyu Madame,naweza hata umconnect na wife akaongea naye kama wadhani mie ni tapeli,tena uzuri naishi karibu kabisa na kituo Kikuu cha Police Dom,kama anaijua shule ya Msingi amani au kanisa la Roma tuko maeneo hayo,na Asubuhi retired OCD alikuwa hapa kituoni kanipigia ameona hii post yangu na nimemuelekeza nilipo kasema anapajua vzuri kabisa,mlete huyo MadaeB kama wadhani mie ni Tapeli kaka!
 
Mkuu pole kwa unayopitia.
Ni mapito na kila kitu huwa kina sababu aminj nakuambia
Hebu fuatilia zabibu kule mpunguzi na mbabala ujue kilo wanauzaje huko mashambani naweza nikatoa hela ukawa unanitumia hapa mwanza ,kwa namna iyo unaweza ukapata kibarua Cha kufanya.
Kuna muda nilikuwa nazifuata dodoma nauzia pale karibia na yenu bar ubungo opposite na tanesco.
Watu tuliosoma nao hawakuaniamini wakajua mie ni double agent.
Kama soko liko vizuri tunaweza tukawa tunazipeleka Kenya kule Bei ni nzuri.
Mie nitakaaa kule afu wewe unazituma.
Pia unaweza ukawa na mtu mwenye akaunti ya crdb nikutumie kitu afu atatoa kwa atm makato ni 1200 huko Kuna unafuu namie kimakato.
Pia namie natuma bure crdb to crdb Kuna unafuu wa kunitumia mtu pesa.
Tafuta akaunti ya crdb ninacho kidogo nifanye ibada Mana sio lazima nipeleke kwa gwajima lusekelo ama kakobe ambao wanafuja zaka zetu
 
Mkuu pole kwa unayopitia.
Ni mapito na kila kitu huwa kina sababu aminj nakuambia
Hebu fuatilia zabibu kule mpunguzi na mbabala ujue kilo wanauzaje huko mashambani naweza nikatoa hela ukawa unanitumia hapa mwanza ,kwa namna iyo unaweza ukapata kibarua Cha kufanya.
Kuna muda nilikuwa nazifuata dodoma nauzia pale karibia na yenu bar ubungo opposite na tanesco.
Watu tuliosoma nao hawakuaniamini wakajua mie ni double agent.
Kama soko liko vizuri tunaweza tukawa tunazipeleka Kenya kule Bei ni nzuri.
Mie nitakaaa kule afu wewe unazituma.
Pia unaweza ukawa na mtu mwenye akaunti ya crdb nikutumie kitu afu atatoa kwa atm makato ni 1200 huko Kuna unafuu namie kimakato.
Pia namie natuma bure crdb to crdb Kuna unafuu wa kunitumia mtu pesa.
Tafuta akaunti ya crdb ninacho kidogo nifanye ibada Mana sio lazima nipeleke kwa gwajima lusekelo ama kakobe ambao wanafuja zaka zetu
Asante ndugu kwa wazo hilo zuri,nitaenda kweli Mpunguzi,nina wadau niliwahi jaribu fanya nao biashara ya nyanya wapo kule,Jirani hapa ana account ya ya CRDB ila yupo kazini kwa sasa,na je mfano nikikupa namba ya wakala wa CRDB inafaa au?alafu kama unapeleka nchi jirani,jaribu pia kucheki na Rwanda,niliwahi kukaa kule wananunua sana matunda,mchele,karanga na bidhaa nyingi toka huku,japo issue ya Corona imeingilia kati,kesho asubuhi naomba niamkie Mpunguzi!
 
Umlete tu huyu Madame,naweza hata umconnect na wife akaongea naye kama wadhani mie ni tapeli,tena uzuri naishi karibu kabisa na kituo Kikuu cha Police Dom,kama anaijua shule ya Msingi amani au kanisa la Roma tuko maeneo hayo,na Asubuhi retired OCD alikuwa hapa kituoni kanipigia ameona hii post yangu na nimemuelekeza nilipo kasema anapajua vzuri kabisa,mlete huyo MadaeB kama wadhani mie ni Tapeli kaka!
Usipoteze muda na wajinga ambao hawatakuja kukusaidia. Hii nchi ina wapumbavu na wenye roho mbaya wengi sana. Achana na huyo mjinga
 
Back
Top Bottom