Familia zina siri kubwa, mwanasheria msibani: Mwanasheria kazua gunzo msibani akisoma mirathi, watu tulishangaa sana

Familia zina siri kubwa, mwanasheria msibani: Mwanasheria kazua gunzo msibani akisoma mirathi, watu tulishangaa sana

Kuna jirani yangu mmoja hapa alifariki mwaka jana.
Yeye na mkewe wa ndoa wanawatoto 3. Mtaani tulikuwa tunajua wote hawa ni watoto wake wa kuwazaa kabisa. Hata marafiki zake walikuwa wanajua hivyo kabisa na watu wanaofanya kazi moja.
Na ndugu wa mkewe na ndugu wa mume. Wote walikuwa wanajua watoto watatu kwenye ndoa hio ni wao kabisa.

Sasa msibani, mwanasheria alipewa nafasi ya kusoma mirathi, ni mwanasheria wake kabisa anayefahamika hata na familia kabisa. Alisoma mengi sana ila sasa kwenye utambulisho alisema kwamba,
Marehemu mtu flani alikuwa na mke mmoja wa ndoa na watoto 2 (nasio 3) wa kuwazaa. Watu tulishituka kidogo hata mkewe na watoto 3 wale.

Baadae akawataja majina, alimtaja mototo wa kwanza na wamwisho (tena alitaja kwa majina yao). Wa pili hakumtaja mwanasheria yule.

Kitu kile watu tulishangaa sana japo kichinichini. Hata ndugu nao walipata mshangao kidogo.

Walisafilisha maiti baadae.
Sasa watu tulijiuliza inamaana mama alichepuka akazaa na mtu mwingine?.

Baada ya kurudi kutoka kuzika nilisikia tuu kwamba yule mwanasheria aliongea jinsi marehemu alivyomwambia nini aseme kwa hio mengine hayo yeye hajui.

-Hivi ungekuwa wewe kama ni mke ungefanyaje na ungefikili watoto wanakufikiliaje mama yao???
-Au pengine wewe ni mtoto ambae hujatajwa pale ungejisikiaje, na mama yako ungemfikilije na mwishowe ungefanya nini?
-Na kama wewe ndo mtoto ambae umetajwa mwenzenu asiye Tajwa mungemuonaje na mngemfikilia nini mama yenu??

haya ni maswali nimejiuliza endapo ningekuwa mmoja wao pale sijui ingekuwaje

Hao watoto ni wa kubwa tuu wa mwisho kama anaumri wa miaka 27 hivi.
Karibuni jamani.
Watanzania tunapenda umbea.

Wewe kama nani kwenye hiyo familia mpaka ualikwe inapofunguliwa mirathi yao?

Nijuavyo hayo ni mambo private
 
Kuna jamaa mtoto wao wa kwanza alikuwa sio wake lakini waliitunza siri hiyo hata ndugu ni wachache tu ndio walijua na mtoto hakujua kabisa na jamaa hakumbagua hata kidogo na kwa bahati nzuri wakati jamaa anaumwa yule mtoto ndiye aliyekuwa akijitoa sana akiamini anamuhudumia baba yake lakini alipofariki katika wosia wa marehemu uliosomwa ndio ulibainisha kwamba yule mtoto sio wa marehemu,kwakweli mtoto aligalagala kwa kilio kikali na kumlaumu sana mama yake kwanini hakumwambia ukweli huo miaka yote.
Mwishoni mwa uhai wake jamaa baada ya kuona huyo mtoto ambaye sio mwanawe anamsaidia kuliko hao wanawe alijaribu kutaka kumjumuisha kwenye mirathi lakini ilishindikana kwa sababu ule wosia wa mahakamani ulibaki kama ulivyo hivyo kumaanisha wenyewe ndio wosia halisi na maelezo yaliotolewa kienyeji nyumbani hayakuzingatiwa.
 
Kuna jirani yangu mmoja hapa alifariki mwaka jana.
Yeye na mkewe wa ndoa wanawatoto 3. Mtaani tulikuwa tunajua wote hawa ni watoto wake wa kuwazaa kabisa. Hata marafiki zake walikuwa wanajua hivyo kabisa na watu wanaofanya kazi moja.
Na ndugu wa mkewe na ndugu wa mume. Wote walikuwa wanajua watoto watatu kwenye ndoa hio ni wao kabisa.

Sasa msibani, mwanasheria alipewa nafasi ya kusoma mirathi, ni mwanasheria wake kabisa anayefahamika hata na familia kabisa. Alisoma mengi sana ila sasa kwenye utambulisho alisema kwamba,
Marehemu mtu flani alikuwa na mke mmoja wa ndoa na watoto 2 (nasio 3) wa kuwazaa. Watu tulishituka kidogo hata mkewe na watoto 3 wale.

Baadae akawataja majina, alimtaja mototo wa kwanza na wamwisho (tena alitaja kwa majina yao). Wa pili hakumtaja mwanasheria yule.

Kitu kile watu tulishangaa sana japo kichinichini. Hata ndugu nao walipata mshangao kidogo.

Walisafilisha maiti baadae.
Sasa watu tulijiuliza inamaana mama alichepuka akazaa na mtu mwingine?.

Baada ya kurudi kutoka kuzika nilisikia tuu kwamba yule mwanasheria aliongea jinsi marehemu alivyomwambia nini aseme kwa hio mengine hayo yeye hajui.

-Hivi ungekuwa wewe kama ni mke ungefanyaje na ungefikili watoto wanakufikiliaje mama yao???
-Au pengine wewe ni mtoto ambae hujatajwa pale ungejisikiaje, na mama yako ungemfikilije na mwishowe ungefanya nini?
-Na kama wewe ndo mtoto ambae umetajwa mwenzenu asiye Tajwa mungemuonaje na mngemfikilia nini mama yenu??

haya ni maswali nimejiuliza endapo ningekuwa mmoja wao pale sijui ingekuwaje

Hao watoto ni wa kubwa tuu wa mwisho kama anaumri wa miaka 27 hivi.
Karibuni jamani.
Kikulacho kinguoni mwako
 
Back
Top Bottom