Fatma Karume: Tatizo Watanganyika hawajitambui utaifa wao, sisi Zanzibar hatuwezi kufuta utaifa wetu

Fatma Karume: Tatizo Watanganyika hawajitambui utaifa wao, sisi Zanzibar hatuwezi kufuta utaifa wetu

Zanzibar ndo hawajitambui ndo maana tumewafanya ni koloni letu
Kati ya Zanzibar na Tanganyika nani koloni la mwenzake. Zanzibar mTanganyika hauwezi kumiliki ardhi wala leseni yako ya kuendesha gari haitambuliki. Hadi miaka ya 2000 Zanzibar ulikuwa unaenda kwa passport ila wao Wanzanzibar siku zote wanakuja huku wanamiliki ardhi, leseni zao zinakubalika. Wakija huku ni kama wanakuja tu shambani
 
Naipenda nchi yangu Jamhuri ya Tanganyika
 

Attachments

  • FB_IMG_1702085740919.jpg
    FB_IMG_1702085740919.jpg
    1.6 KB · Views: 3
Wazanzibari always wako proud kuitwa Wazanzibari, sijui kwanini sisi Watanganyika tukiitwa Watanganyika huwa tunakasirika na kuona kama tunabaguliwa?
Ila wapemba ukiwaita wapemba wanakasirika mno!
 
Wakili msomi Fatma Karume anasema kuwa viongozi waTanganyika ndiyo tatizo.


View: https://m.youtube.com/watch?v=upbVqLpdVmk

Viongozi wa Zanzibar na wananchi wa Zanzibar wanajitambulisha kama wazanzibari katika muungano wa nchi mbili kisha inafuata uTanzania.

Lakini viongozi wa kutoka upande wa bara hasa hawa wa CCM na serikali yake wanaona haya na kulazimisha kuufuta utanganyika wa asili raia taifa lao Tanganyika.

Upande wa Zanzibar utambulisho ni Mzanzibari kwanza, halafu mbili kutoka Tanzania.

Hapo ndipo kunapotokea zogo lakini kiuhalisia huwezi kufuta uasili wa kitaifa wa mtu katika Muungano anasisitiza wakili Fatma Karume kwa viongozi wa CCM bara na walio katika serikali yake.

Jamhuri ya muungano wa Tanzania ni wa nchi mbili Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar.

Jina la kwanza lilitambulika kama nchi ya Jamhuri za Tanganyika na ya Watu wa Zanzibar April 26, 1964.

Ilichukua miezi kadhaa baada ya muungano jina hilo la kwanza refu hadi kubadilishwa kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwezi Oktoba 1964

Historia ya nchi ya Tanganyika iliyopata uhuru mwezi December 1961 na nchi ya Zanzibar iliyopata uhuru wake mwaka 1963 mwezi December pamoja na vizazi vya nchi hizo vilivyofuatia haviwezi kufutwa na viongozi wachache wa CCM kwa kuwa utaifa ni asili.

Wenye akili bila ego tunashauri tuwe na nchi moja
 
Wakili msomi Fatma Karume anasema kuwa viongozi waTanganyika ndiyo tatizo.


View: https://m.youtube.com/watch?v=upbVqLpdVmk

Viongozi wa Zanzibar na wananchi wa Zanzibar wanajitambulisha kama wazanzibari katika muungano wa nchi mbili kisha inafuata uTanzania.

Lakini viongozi wa kutoka upande wa bara hasa hawa wa CCM na serikali yake wanaona haya na kulazimisha kuufuta utanganyika wa asili raia taifa lao Tanganyika.

Upande wa Zanzibar utambulisho ni Mzanzibari kwanza, halafu mbili kutoka Tanzania.

Hapo ndipo kunapotokea zogo lakini kiuhalisia huwezi kufuta uasili wa kitaifa wa mtu katika Muungano anasisitiza wakili Fatma Karume kwa viongozi wa CCM bara na walio katika serikali yake.

Jamhuri ya muungano wa Tanzania ni wa nchi mbili Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar.

Jina la kwanza lilitambulika kama nchi ya Jamhuri za Tanganyika na ya Watu wa Zanzibar April 26, 1964.

Ilichukua miezi kadhaa baada ya muungano jina hilo la kwanza refu hadi kubadilishwa kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwezi Oktoba 1964

Historia ya nchi ya Tanganyika iliyopata uhuru mwezi December 1961 na nchi ya Zanzibar iliyopata uhuru wake mwaka 1963 mwezi December pamoja na vizazi vya nchi hizo vilivyofuatia haviwezi kufutwa na viongozi wachache wa CCM kwa kuwa utaifa ni asili.

Kinachonishangazi ni serikali ya Zanzibar, ila hakuna serikali ya Tanganyika. Mtikila aliliona hilo ila akatangulia mbele ya haki.
 
Kati ya Zanzibar na Tanganyika nani koloni la mwenzake. Zanzibar mTanganyika hauwezi kumiliki ardhi wala leseni yako ya kuendesha gari haitambuliki. Hadi miaka ya 2000 Zanzibar ulikuwa unaenda kwa passport ila wao Wanzanzibar wao wanakuna huku wanamiliki ardhi, leseni zao zinakubalika. Wakija huku ni kama wanakuja tu shambani
Maana yake Tanganyika ni giant hivyo ni vitu vidogo sana bro.
 
Kuweni na akili timamu basi pale watu tunapotaka kuujua ukweli hapa sio MMU au Chit-chat.
Moderator waonyeni watu kama Hawa niliowa quote hapa. Yaani kuna watu wa hovyo sana humu hata kwenye mijadala yenye afya kwa ustawi wa Taifa letu.
 
Ila kusema ukweli Watanganyika tunajitia aibu sana ebu fikiria siku ya kumbukumbu ya uhuru wetu tarehe 9,Disemba mgeni rasmi na ndiye anayesimama kama kiongozi wetu ni Mzanzibar! Bora angekuwa Dr Mpango au Kassim Majaliwa.
Kuna haja ya kuwa na serikali tatu kwa kweli.
 
Kuweni na akili timamu basi pale watu tunapotaka kuujua ukweli hapa sio MMU au Chit-chat.
Moderator waonyeni watu kama Hawa niliowa quote hapa. Yaani kuna watu wa hovyo sana humu hata kwenye mijadala yenye afya kwa ustawi wa Taifa letu.
Hao moderator ungewambia bila kushoboka kuni-quote ujumbe usingefika!
 
Fatuma Karume kaonge maneno mazito, yatawauma Watanganyika lakini ni ukwel.

1. Tanganyika imevaa koti la Muungano, ni ukweli! kila kitu cha Tanganyika ni cha Muungano. Balozi Amina anataka '' Formula '' ya kugawana rasilimali za Muungano yaani za Tanganyika ( hajasema kuchangia ni kugawana tu).

Gharama za Muungano zinabebwa na Tanganyika kwa jina la koti la Tanzania; Bajeti ya Zanzibar, madeni ya mikopo ya Zanzibar hata bili za majumbani kwao

Rais SSH alipokabdihiwa madaraka akachukua deni la Bilioni 60 za Umeme akalifanya la Muungano(Tanzania).
Ni haki alichofanya Rais SSH kwasababu tumebeba koti, kama kuna chawa na kunguni hiyo ni juu yetu.

2. Fatma kasema kinachotakiwa ni uwepo wa Serikali ya Tanganyika.
Hili nalo ni la kweli kwasababui Rais wa Koti la Muungano anapatikana tu bila kujadili anatoka wapi.

Fatma anasema Uzalendo kwa maneno ya Uzanzibar yanawafanya wajivunie Uzanzibar, sasa huyu anayejivunia Uzanzibar anauchungu gani na Tanganyika?

Lakini muhimu alichosema ni kwamba Serikali ya Tanganyika itasimamia na kulinda masilahi yake.
Fatma anona wazi Masilahi ya Tanganyika hayana mwangalizi, ni ukweli mchungu lakini ni ukweli.

3. Fatma anasema Wazanzibar wanajivunia Uzanzibar kwanza kabla ya Utanzania.
Ni kweli, na Watanganyika wanapaswa kujivunia Utanganyika kwanza ili wanaohitaji Muungano wauheshimu.

Nakubaliana na Fatma , Wazanzibar hawana uchungu na Muungano kwasababu ya ''free ride'

Mtamsema Fatma lakini ukweli unabaki pale pale, tunahitaji Tanganyika tusimamie masilahi yetu na watu wetu.

CCM wanaotetea huu Muungano ni wanaufaika wa mfumo, mwananchi wa kawaida wa Kadewele, Kidogo Basi, Magoroto , zaidi ya kuumia kwa gharama za kubeba Muungano na Zanzibar anafaidikaje na Muungano!

Wasichotakaueleza Wazanzibar , Tanganyika inanufaika na nini na huu Muungano au kuvaa koti la Muungano?

Hili ndilo akina Fatma hawasemi wanajificha kwamba Wananchi wa pande zote wanataka Muungano!
No! Mwananchi wa Tanganyika haihitaji Muungano , kama anahitaji ni kwa faida gani?


PakiJinja Pascal Mayalla Mag3
 
Back
Top Bottom