Fei Toto ni mchezaji wa kigeni, Yanga ilifuata kanuni?

Fei Toto ni mchezaji wa kigeni, Yanga ilifuata kanuni?

Ungeanza kwanza kwa kuwa na uelewa mpana juu ya hali ya uanachama wa Zanzibar katika shirikisho la soka Africa ndipo ungekuja na hii mada. Sasa tunajadili nini wakati hujui hata kwanini Zanzibar timu yao ya taifa haishiriki kombe la dunia wala AFCON. Unashindwa kwanini Feitoto huyo huyo yupo kwenye timu ya taifa inayosimamiwa na TFF badala ya ZFA
Wewe umesoma kiupandupande. Najua hayo mambo na najua kuwa ZFA iliomba tena kwa bidii kuwa mwanachama wa FIFA na ikakataliwa kwa kigezo kwamba si nchi inayotambulika kimataifa kwa kuwa na mipaka yake.

Zanzibar inatambuliwa CAF kama mwanachama mshirika na ingawa haina sifa kama Tanzania (kwa Timu za Taifa) lakini ligi yake ya vilabu ina sifa kama Ligi ya vilabu ya Tanganyika. Kwa ivo linapokuja suala la Ligi ya vilabu, Zanzibar inajitegemea.

Kujitegemea kwake ndiyo maana zile nafasi mbili za Klabu Bingwa (Simba na Yanga ) na zile mbili za Shirikisho (Azam na Geita Gold FC), haziwahusu Zanzibar bali zinazihusu timu za Tanganyika Pekee. Leo KMKM ikiongeza nafasi zitakuwa ni za Zanzibar peke yake, Tanganyika haitahusika.

Yanga ilifuata Kanuni?
 
Leo KMKM ya nchi ya Zanzibar ilikuwa inacheza na timu ya Al Ahli Tripoli kwenye Mashindano sawa na Simba na Yanga. Kimantiki Zanzibar ina hadhi sawa na TFF kwenye mashindano haya ya CAF na uanachama wa CAF.

Kwa ivo Ligi iliyoitoa KMKM ndiyo ligi aliyokuwa anacheza Feisal Salum, kwa CAF, Ligi ya Tanganyika na Zanzibar ni Ligi mbili tofauti.

Jee Yanga ilifuata Kanuni za kuhamisha wachezaji wa kimataifa?
Tuanze na TFF, kwanini kwenye zile kanuni za wachezaji 12 wa kigeni haziwahesabu wachezaji wa zanzibar kama ni wa kigeni?
 
Sina uelewa na timu za taifa. Ila kwa vilabu mchezaji ni lazima anapotoka Ligi ya nchi moja kwenda nchi nyingine ni lazima afanyiwe uhamisho wa kimataifa.

Hivi Zanzibar hawana timu ya Taifa na huwa inashiriki mashindano gani? Nilishawahi kuona Timu ya Zanzibar inacheza na timu ya Tanganyika. Ikicheza Tanganyika na Zanzibar Fei toto anaweza kucheza Tanganyika?
Tuanze kuuliza, je hiyo timu ya Taifa ya Zanzibar ipo? Kama haipo ni kwanini?
 
Wewe umesoma kiupandupande. Najua hayo mambo na najua kuwa ZFA iliomba tena kwa bidii kuwa mwanachama wa FIFA na ikakataliwa kwa kigezo kwamba si nchi inayotambulika kimataifa kwa kuwa na mipaka yake.

Zanzibar inatambuliwa CAF kama mwanachama mshirika na ingawa haina sifa kama Tanzania (kwa Timu za Taifa) lakini ligi yake ya vilabu ina sifa kama Ligi ya vilabu ya Tanganyika. Kwa ivo linapokuja suala la Ligi ya vilabu, Zanzibar inajitegemea.

Kujitegemea kwake ndiyo maana zile nafasi mbili za Klabu Bingwa (Simba na Yanga ) na zile mbili za Shirikisho (Azam na Geita Gold FC), haziwahusu Zanzibar bali zinazihusu timu za Tanganyika Pekee. Leo KMKM ikiongeza nafasi zitakuwa ni za Zanzibar peke yake, Tanganyika haitahusika.

Yanga ilifuata Kanuni?
Ifuate kanuni ipi mbona unajichanganya? Feitoto ni raia wa nchi gani?
 
Ifuate kanuni ipi mbona unajichanganya? Feitoto ni raia wa nchi gani?
Najichanganyaje? Wewe hujui kwamba kwenye mashindano haya inayoshiriki Simba na Yanga Zanzibar Mwakilishi wake ni KMKM. KMKM inashiriki ligi ya Tanganyika?

Klabu hazihamishi uraia zinahamisha uchezaji wa mtu. Chama alipotoka Simba kwenda Al ahly ya Misri, kibali chake cha uhamisho kilitolewa na chama cha soka Zambia au Tanzania?

Mambo ya Uraia hayapo kwenye uhamisho wa wachezaji. Yaani CR7 anatoka Juve kwenda Man U anaulizwa Uraia ama alikuwa anacheza ligi ipi? Yaani kwa kuwa ni Mreno basi uhamisho utoke Ureno!!

Leo hii itokee Mwamnyeto asajiliwe na Mamelod Sundown na kama hajamaliza mkataba wake akitaka kurudi Tanzania hata kama yeye ni mtanzania, ni lazima apate kibali cha Uhamisho toka chama cha soka cha Afrika ya Kusini.

Naandika ninachokijua siyo ninachokihisi,

Yanga ilifuata utaratibu wa kumhamisha Fei Toto??
 
Feisal Salum Mchezaji wa Yanga leo nimegundua kumbe alikuwa anacheza kwenye Ligi ya Nchi ya Zanzibar ambayo pia ni mwanachama wa CAF. Kwa mujibu wa Kanuni za CAF mchezaji anapotoka Ligi ya nchi moja kwenda ligi ya nchi nyingine, hutakiwa kuwa na uhamisho wa Kamataifa kwa mchezaji kama huyo.

Jee Yanga ilimhamisha Feisal Salum kimataifa na kuijulisha CAF kwamba mchezaji huyo alikuwa anacheza kwenye Ligi ya nchi ya Zanzibar?
Kwanini fei Toto kwanini ujauliza kuhusu Ninja, Kanavaro, Banka na wengine kibao ambao walishapita yanga miaka na miaka!!
 
Kwanini fei Toto kwanini ujauliza kuhusu Ninja, Kanavaro, Banka na wengine kibao ambao walishapita yanga miaka na miaka!!
Ndugu yangu kila jambo na wakati wake. Halafu hata mahakamani huwezi kusema kwa nini ushitakiwe wewe mwenye msokoto mmoja wakati unawajua walimaji wa bangi hawajashitakiwa. Hao kina Ninja na wenzake nilikuwa bado sijatanabahi kwamba kumbe Zanzibar wana Ligi yao inayojitegemea.
 
Tuanze na TFF, kwanini kwenye zile kanuni za wachezaji 12 wa kigeni haziwahesabu wachezaji wa zanzibar kama ni wa kigeni?
Hoja hapa siyo uraia, bali ni kucheza kwenye Ligi ya nchi nyingine. Kichuya ni Mtanzania lakini Simba ilipotaka kumrejesha toka Pharco ya Misri haikufanya hivyo kienyeji tu eti kwa kuwa yeye ni mtanzania.

Feisali alikuwa anacheza Kwenye Ligi ya Zanzibar isiyosimamiwa na TFF, sasa anapotaka kuja kwenye Ligi inayosimamiwa na TFF haitaji uhamisho wa Kimataifa?
 
Feisal Salum Mchezaji wa Yanga leo nimegundua kumbe alikuwa anacheza kwenye Ligi ya Nchi ya Zanzibar ambayo pia ni mwanachama wa CAF. Kwa mujibu wa Kanuni za CAF mchezaji anapotoka Ligi ya nchi moja kwenda ligi ya nchi nyingine, hutakiwa kuwa na uhamisho wa Kamataifa kwa mchezaji kama huyo.

Jee Yanga ilimhamisha Feisal Salum kimataifa na kuijulisha CAF kwamba mchezaji huyo alikuwa anacheza kwenye Ligi ya nchi ya Zanzibar?
Itakuwa vyema kama pia utapewa majibu kama Simba S.C nao wamekamilisha uhamisho wa kimataifa kwa goalkeeper Ally Salim maana nae pia ni raia wa nchi ya Zanzibar
 
Feisal Salum Mchezaji wa Yanga leo nimegundua kumbe alikuwa anacheza kwenye Ligi ya Nchi ya Zanzibar ambayo pia ni mwanachama wa CAF. Kwa mujibu wa Kanuni za CAF mchezaji anapotoka Ligi ya nchi moja kwenda ligi ya nchi nyingine, hutakiwa kuwa na uhamisho wa Kamataifa kwa mchezaji kama huyo.

Jee Yanga ilimhamisha Feisal Salum kimataifa na kuijulisha CAF kwamba mchezaji huyo alikuwa anacheza kwenye Ligi ya nchi ya Zanzibar?
Ligi ya Zanzibar inaitwaje mdau?
 
Hoja hapa siyo uraia, bali ni kucheza kwenye Ligi ya nchi nyingine. Kichuya ni Mtanzania lakini Simba ilipotaka kumrejesha toka Pharco ya Misri haikufanya hivyo kienyeji tu eti kwa kuwa yeye ni mtanzania.

Feisali alikuwa anacheza Kwenye Ligi ya Zanzibar isiyosimamiwa na TFF, sasa anapotaka kuja kwenye Ligi inayosimamiwa na TFF haitaji uhamisho wa Kimataifa?
Kwahiyo Zanzibar ni nchi?
 
Najichanganyaje? Wewe hujui kwamba kwenye mashindano haya inayoshiriki Simba na Yanga Zanzibar Mwakilishi wake ni KMKM. KMKM inashiriki ligi ya Tanganyika?

Klabu hazihamishi uraia zinahamisha uchezaji wa mtu. Chama alipotoka Simba kwenda Al ahly ya Misri, kibali chake cha uhamisho kilitolewa na chama cha soka Zambia au Tanzania?

Mambo ya Uraia hayapo kwenye uhamisho wa wachezaji. Yaani CR7 anatoka Juve kwenda Man U anaulizwa Uraia ama alikuwa anacheza ligi ipi? Yaani kwa kuwa ni Mreno basi uhamisho utoke Ureno!!

Leo hii itokee Mwamnyeto asajiliwe na Mamelod Sundown na kama hajamaliza mkataba wake akitaka kurudi Tanzania hata kama yeye ni mtanzania, ni lazima apate kibali cha Uhamisho toka chama cha soka cha Afrika ya Kusini.

Naandika ninachokijua siyo ninachokihisi,

Yanga ilifuata utaratibu wa kumhamisha Fei Toto??
Zanzibar ni nchi?
 
Nyerere alituachia haya mazingaombwe yanayoitwa Muungano. Hata ukijaribu kuwaelekeza CAF wataona unawachanganya tu. Hakuna anayeelewa haya makitu.
 
Nimeupenda huu mjadala ila pia naomba nielekezwe kwa ajili ya afya ya uelewe wangu, kwan TFF ni mamlaka ya nchi gani?
 
Feisal Salum Mchezaji wa Yanga leo nimegundua kumbe alikuwa anacheza kwenye Ligi ya Nchi ya Zanzibar ambayo pia ni mwanachama wa CAF. Kwa mujibu wa Kanuni za CAF mchezaji anapotoka Ligi ya nchi moja kwenda ligi ya nchi nyingine, hutakiwa kuwa na uhamisho wa Kamataifa kwa mchezaji kama huyo.

Jee Yanga ilimhamisha Feisal Salum kimataifa na kuijulisha CAF kwamba mchezaji huyo alikuwa anacheza kwenye Ligi ya nchi ya Zanzibar?
Hili nalo CAF walitazame ngoja tuanze kukoleza [emoji91]

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom