Fei Toto ni mchezaji wa kigeni, Yanga ilifuata kanuni?

Fei Toto ni mchezaji wa kigeni, Yanga ilifuata kanuni?

Sawa ila una uhakika Zanzibar ni mwanachama wa CAF?

Maana inafikirisha kwa upande wa vilabu kupewa nafasi ya kushiriki michuano inayosimamiwa na CAF huku timu yao ya Taifa ikinyimwa nafasi
Ni mwanachama wa CAF ila sio mwanachama kamili
 
Hili swali lina mantiki ila majibu yake huwezi kuyapata kwasababu yataambatana na siasa ambazo kimsingi zina mauza uza mengi sana kwenye huu muungano.
 
Aisee!! Hii nayo kumbe ni Kero??

Zanzibar wana ligi yao na Tanganyika wana ligi yao. Ligi ya kule mwiko kudhaminiwa na makampuni ya pombe huku kwetu TBL ilishawahi kuwa mdhamini mkuu wa Ligi ya Tanganyika. Kwa ivo Yanga ilifuata Kanuni?
Kwani Ligi ya Tanganyika inaitwaje?
 
Hoja aina mashiko inamaana wascotch hawachezi London?
 
Hoja aina mashiko inamaana wascotch hawachezi London?
Haina mashiko kwa mfano wa uskochi? Unajua kwamba ligi zetu zote mbili siyo "Professional" bali ni "Amature"? Wewe unazungumzia ligi zisizofanana kabisa.
 
Moja na mwaka huu ni KMKM inashiriki!!
Basi lile ni tawi la Tanganyika, wangetoa timu mbili moja klabu bingwa na nyingine ni shirikisho basi tungejua CAF wanaitambua kama ina mamlaka kamili hivyo Zanzibar ipo chini ya mwamvuli Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
Basi lile ni tawi la Tanganyika, wangetoa timu mbili moja klabu bingwa na nyingine ni shirikisho basi tungejua CAF wanaitambua kama ina mamlaka kamili hivyo Zanzibar ipo chini ya mwamvuli Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Hapana, kwenye Shirikisho ipo Kipanga.
 
Haya ni maelezo yashawahi kutolewa na Rais wa CAF kipindi hicho 2017 pale Zanzibar alipopewa uanachama na kunyang'anywa baada ya miezi 4

Zanzibar has had its membership of the Confederation of African Football (Caf) rescinded just four months after the island was accepted as a member.

Caf president Ahmad said Zanzibar, which is part of Tanzania, should never have been admitted as the body's 55th member in March.

"They were admitted without properly looking into the statutes which are crystal clear," said Ahmad.

"Caf cannot admit two different associations from one country."

"The definition of a country comes from the African Union and the United Nations," added the Malagasy at Caf's Extraordinary Congress in Morocco.

Fifa refused to admit Zanzibar after Caf, under Ahmad's predecessor Issa Hayatou, allowed the East African island into its ranks.

Zanzibar is part of Tanzania but has operated independently as a footballing entity in regional completion.
 
Haya ni maelezo yashawahi kutolewa na Rais wa CAF kipindi hicho 2017 pale Zanzibar alipopewa uanachama na kunyang'anywa baada ya miezi 4

Zanzibar has had its membership of the Confederation of African Football (Caf) rescinded just four months after the island was accepted as a member.
Uhalisia ni upi? KMKM iinashiriki mashindano ya Klabu Bingwa Afrika ama haishiriki? Jee Kipanga inashiriki Mashindano ya Kombe la shirikisho Afrika ama haishiriki?
 
Uhalisia ni upi? KMKM iinashiriki mashindano ya Klabu Bingwa Afrika ama haishiriki? Jee Kipanga inashiriki Mashindano ya Kombe la shirikisho Afrika ama haishiriki?
Nafasi hizo wamepata ni kama. Upendeleo tu
 
Kuna mambo yaki muungano hayapo sawa na tatizo halipo kwa Yanga bali tatizo linaanzia kwenye katiba yetu kisha inakuja mpaka kwa TFF.

  • mtu kutoka Zanzibar ni ruksa kuja Tanzania kufanya kazi ya aina yoyote ile bila kibali
  • Ni ruksa kumiliki ardhi bila ya kuwa sharti lolote
  • Ni ruksa kuwa raia wa Tanzania bara ili mradi tu upo Tanzania bara.
Ni ruksa ruksa tu,

Wakati upande wa Zanzibar wametuwekea sheria kali watu wa Tanzania bara a.k.a machogo.

Hili ni kosa la kikatiba, na sio Yanga tu bali ni timu zote zinazoshiriki ligi kuu Tanzania bara hakuna mchezaji wa Zanzibar aliyekatiwa kibali. Simba wana Ally Salim pia, shida ni mfumo wetu wa katiba imewachukulia kama wazanzibar kama ni sehemu yetu japo wao wazanzibar hilo ujinga kwa nchini kwao hawataki kuusikia.

TFF nao ikaja kuchukua mfumo huo huo wa mapungufu ya kikatiba hivyo imebariki huo muingiliano wa wachezaji kutoka Zanzibar kutokana na hali ile ile iliyokuwepo kikatiba.
Thread closed
 
Back
Top Bottom