Feisal Salumu: Nimeondoka Yanga kutokana na manyanyaso, nilizungumza na Rais wa Yanga kwa saa 6, nikamwambia nataka kuondoka

Feisal Salumu: Nimeondoka Yanga kutokana na manyanyaso, nilizungumza na Rais wa Yanga kwa saa 6, nikamwambia nataka kuondoka

Kwanini hua mnawaza haya mambo? kuna vitu ni aibu hata kuviandika tu,ukiona mtu ana andika vitu kama hivi tena bila wasiwasi with full confidence basi tambua kua huyo mtu huenda ndio michezo yake hiyo.
[emoji1][emoji1][emoji2][emoji2][emoji4]niwie radhi kaka ila hizo kashfa yanga zipo sana
 
Uto siipendi Ila dogo Fei anapuyanga Sana. Hivi hata habari za huko nje za wachezaji wenzao hawafuatilii? Sadio Mane alikuwa hana furaha pale Liverpool kutokana na kulipwa kidogo Kuliko akina Milner lakini alikuwa anapiga kazi kama kawaida na akasubiri mkataba wake ukaisha akasepa.

Sio kwamba hakujua kama kaongezewa mwaka bali kwa wakati huo aliona inafaida kwake, hakuangalia wakati na alileta ushabiki badala ya kazi.
Sadio mane mkataba haukuisha, aliomba aachiwe kuondoka Bayern wakaja na 20m akasepa
 
Kama unaweza kuwasiliana nae ebu msaidieni huyu dogo anapotea kakubari kua tambara la deki. Club imesha sema kwa maandishi kua kama anaondoka club zifike mezani ziweke bids basi hawawezi kataa offa zitakazo kuja.
Amesema hana team inayomtaka, ndo maana yeye aliamua binafsi kuvunja mkataba kupitia ktk kifungu kinacho dai hivyo. Sasa hayo ya team inayomtaka iende kuzungumza na yanga unaitoa wapiii??
 
Nawaambia kuna kitu kizito Fei anakificha kukisema nadhani ni cha aibu na hakina uthibitisho....so ngoja tuone kuna siku mambo yatakua hadharani.
Na kitakua wazii tyuuh hata ichelewee.
 
Labda unijuze,Baba yake Messi ana elimu gani na Mama yake Feisal ana elimu gani? na unatakiwa kua na elimu gani ili umuongoze mwanao?

Pia comment niliyoiquote haikulenga elimu bali ililenga kwa kusema "Kuhusu mtoto kusimamiwa maamuzi na Mama yake"
Kwa taarifa yako Baba yake Messi ni Mwanasheria usidhani wanafanya mambo kama ngo'mbe
 
Kwa hiyo miaka3 alikubaliana nayo na sio aliwekewa bila kujua kama alivosema. Akae zake kitaa mpaka 2024. Na ile milioni 100 alio rudishiwa haitoshi kwenda cas au fatma karume kaimaliza yote.
Haya maswali unayouliza yote kayajibu. Na hiyo m100 baadhi imetoka kwa watu wa huko huko Yanga ili aachane na Hersi na baada ya kukataliwa ameshairudisha kwa wenyewe. Na hao watu wapo tayari kumchangia tena ila akaona ngoja aje kwanza kwa watanzania lisiwe jambo la wachache. Pia ikiwa Hersi atasema ni kiasi gani kilipwe kama faini atarudi kuwaomba watu hao hao ambao wengine wapo na Hersi huko Yanga. Tatizo Hersi hataki kumwacha na pesa kutoka kwa Fei hataki anataka timu inayomtaka ije ilihali Fei anasema hakuna timu inayomtaka, na sasa hivi ndo kabisa, hakuna timu inayotaka mchezaji mwenye mgogoro wa kimkataba.

Mwishoni mwandishi alisema ukitaka kutoa judgement sahihi, achana na mapenzi na timu. Mtazame Fei na Hersi kama individuals.
 
[emoji117]Nimenyanyaswa sana nikiwa Yanga,nimeambiwa nauza mechi na viongozi.

[emoji117]Nimekaa na Hersi na Makamu wake masaa 6 nikamwambia yanayonisibu dhidi yake akaniomba radhi akasema tusameheane nikamwambia nimekusamehe lakini nataka kuondoka.

Akasema sisi bado tunakuhitaji, nikamwambia mimi siwezi tena kuendelea na Yanga, naomba niondoke.

Akasisitiza nibaki nikamwambia basi wanipe siku 3 niongee na familia yangu.

[emoji117]Mkataba huu nilio nao wakati nasaini mama aliniambia nitasaini mkataba wa miaka 2 lakini Hersi akaniongezea ikawa 3 bila mimi kujua.

[emoji117]Mkataba uliandikwa Kingereza na mimi Kingereza sijui na nilikuwa pekeyangu. Wao walikuwa Saimon, Hersi, Arafat na Mdhamini.

[emoji117]Mama yangu ni mpenzi mkubwa sana wa Yanga na yeye ndiye aliyenipambania wakati Yanga mambo yakiwa mabaya alikuwa ananipa pesa yake mwenyewe.

[emoji117]Nimekula Ugali na Sukari wakati Yanga ikiwa na hali mbaya sio sasahivi.

[emoji117]Wanamtukana na kunyanayasa pepo yangu, mama yangu ndiyo pepo yangu mimi halafu anafananishwa na andazi kweli?

[emoji117]Nawapenda sana mashabiki wa Yanga na najua wananipenda pia, hawajui niliyopitia wanaambiwa uongo wanamtukana mama yangu na mimi mwenyewe.

[emoji117] Simkimbii Hersi nimkimbie ili iweje Kwani Mimi nimeua? Nimekaa nae yeye na Makamu wake masaa 6

My Take
Msimamo wangu ni kwamba Yanga sio club ya kwenda mtu makini. Imejaa uhuni na wahuni
Mchezaji anaefuata Kwa kuzuiliwa kuondoka na kunyanyasika ni Mayele. Yanga Kuna uswahili mwingi. Pole sana Fei Toto.
 
Heeee...[emoji3064][emoji3064][emoji849][emoji849][emoji849][emoji849][emoji849]makubwaaa hayaaa kaah
Wala sio siri, hujawahi ona picha yake ya mahaba na Takadini?? Sio kwa pozi lile.
Hata bumbuli aliwahi sema hili.
 
Inawezekana.
Yaani honestly kipo kinafichwa kikubwa tu kustiri utu wa hao wawili ila twende tu ..tutajua tuu kwani Yana muda baasi!!!
Si rahisi kukataa kurudi yanga na fei sikutegemea km ataondoka Yanga miongoni mwa wachezaji wenye mapenzi na Yanga ni naweza sema anaongoza..
Na mzanzibar akisema noooo....amemaanisha NOOO Tena kubwaa
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
"Baada ya kuwasumbua sana ndio wakaniongezea Million 20 zingine baaae."

Mazungumzo yalikua nilipwe signing fees million 100 Kwa mkupuo, baada ya kusaini wananiambia kua mkataba unasema nitalipwa Kwa mafungu. Mkataba ni wa Kingereza na mi sikijui".
Fei aongee na nafsi yake vizuri kilichopo mbele yake siyo kizuri saaaaana
 
Sasa mbna Fei bado anabakizwaa tyuh na mshahara analipwa km kawaaa [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Ndio najikuliza kama umemuajiri mtu na hatimizi majukumu uliyompa, ww kama mwajiri kwanini usivunje mkataba nae, na akulipe kufidia hasara aliyokuletea.
 
Kipanya amemwambia Fei kuna jambo halisemi ili kumsitiri kiongozi wa Yanga. Msimamo wa Fei ni mkubwa mno kwa manyanyaso ya kawaida. Kama hakuna timu inamtaka basi kuna jambo Fei kaamua kutokulisema maana kapelekwa hadi kwa mashekhe, kapewa ofa ya m30 ila kagoma. Wakili wake anasema hakuna timu inataka mchezaji mwenye mgogoro hivyo Fei anajua kashikilia makali lakini kaamua kuyashika hivyo hivyo.
Timu inakunyanyasa wakati huo huo inakupa offer ya million 30 hivi mbona nyie watu hamtumii akili?
 
Mchezaji anaefuata Kwa kuzuiliwa kuondoka na kunyanyasika ni Mayele. Yanga Kuna uswahili mwingi. Pole sana Fei Toto.
Unajua maana ya mkataba ?? Nianzie hapo kwanza. Unajua maana ya kunyanyaswa? Una elimu gani?
 
Back
Top Bottom