Finland tayari wamekatiwa gesi na umeme na Russia

Finland tayari wamekatiwa gesi na umeme na Russia

Wewe unafikiri Finland itakufa njaa? Mnafurahia ufara wa fara fulani ambaye ameamua kuvamia nchi huru kibabe tu. Halafu nchi hiyo inapojitetea mnaumia. Misimamo mingine ni ya kishetani kabisa. Kama Idd Amin alivyovamia Kagera 1978, ulitaka Nyerere afanyeje kama siyo kutetea ardhi ya Tanzania?
Libya siyo nchi huru?
Syria siyo nchi huru?
Afghanistan vp?
Somalia nako?

Upimbi uache
 
Na hii factor ya utegemezi wa hiyo 10% tu hawa Pro Russia wanajifanya hawaioni,hawathubutu kuiweka hapa wazi,wanatuletea propaganda zao za Kikomunist za kuondoa ukweli unabakiza yale unayotaka watu wayasikie na kujifurahisha moyo.
Hiko kipengele cha asilimia 10 wanakiruka kabisa.
 
Ni sawa na Uganda waikatie umeme Tanzania. Sehemu ndogo tu za mpakani kagera huko. Finland wameendelea kuliko Russia wana Umeme wa kila aina. Gas watachukua Norway.
Finland nishat wanayotumia toka russia ni 10% tu.
 
Hata hawakumbuki tena,siku zote huwa wanarukia ajenda inayokuwa mbele yao
Poland sasa hivi ananunua gesi kutoka Ujerumani iliyo nunuliwa kutoka Urusi tena kwa bei kubwa zaidi ya awali ,tuache ushabiki gesi ya Urusi ni muhimu kwa uchumi wa Ulaya.

Najua chuki yenu dhidi ya Urusi ni kubwa lakini hilo haliwezi kubadili ukweli ya kuwa Urusi ni taifa muhimu dunia linapo kuja suala la nishati na hilo halitabadirika kamwe.

Marekani kapiga marufuku uagizaji wa mafuta ya Urusi lakini ukiangalia kwenye rekodi za usafirishaji wa mafuta bado Marekani ananunua mafuta ya mamilioni ya $ kutoka Urusi, kwa maana hiyo marufuku iko kwenye makatatasi tu lakini kiuhalisia umeshindikana.

Qtaar na Ujerumani wametiana saini ya kusambaza gesi lakini mchakato wa kusambaza gesi utaanza mwaka 2024 na penyewe hawataweza kuziba pengo la Urusi bali watakuwa na uwezo kuziba gepu la asilimia 10 tu.
Nishati ya Urusi ni muhimu kwa uchumi wa dunia hilo halina mjadara hata tukibishana miaka kumi.
 
Tutafakar upande wa pili, yaani finland. Wao hawakujua kuwa watakatiwa umeme na gas? Ni ushabiki tu usio na maana haya mataifa yanayomzingua russia yanaonekana tayari yalishajiandaa kwa muda mrefu. Kama hiyo gas na umeme ndo vingekuwa ni maisha yao, wala wasingethubutu kupeleka hayo maombi NATO, ila mpaka wanapeleka maana yake kuna namna wamejiandaa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ndezi kazini!!!
😂😂😂😂
 
Kwani mpaka ufoke?Jifunze arts ya kuzungumza...ungeweza kunielezea kawaida tu ningeelewa jebu punguza mihemuko...tatizo hamtaki kusikia ukweli
Tena huyo anayefoka ni mtoto wa kiume, ndo maana wanatutia aibu kaka zao ktk mahusiano, kila siku wanaachika.
 
Libya siyo nchi huru?
Syria siyo nchi huru?
Afghanistan vp?
Somalia nako?

Upimbi uache
Wew kemea hiyo nchi iliyozivamia hizo nchi ulizotaja na sio uhalalishe uvamizi wa Russia huko Ukraine kwa makosa ya wengine. Eti " kwa nini umemuuwa huyu kijana"? Unajibu "nimemuuwa sababu amemgonga mwanangu na pkpk akamuuwa" UTAFUNGWA MKUU
 
Poland sasa hivi ananunua gesi kutoka Ujerumani iliyo nunuliwa kutoka Urusi tena kwa bei kubwa zaidi ya awali ,tuache ushabiki gesi ya Urusi ni muhimu kwa uchumi wa Ulaya.

Najua chuki yenu dhidi ya Urusi ni kubwa lakini hilo haliwezi kubadili ukweli ya kuwa Urusi ni taifa muhimu dunia linapo kuja suala la nishati na hilo halitabadirika kamwe.

Marekani kapiga marufuku uagizaji wa mafuta ya Urusi lakini ukiangalia kwenye rekodi za usafirishaji wa mafuta bado Marekani ananunua mafuta ya mamilioni ya $ kutoka Urusi, kwa maana hiyo marufuku iko kwenye makatatasi tu lakini kiuhalisia umeshindikana.

Qtaar na Ujerumani wametiana saini ya kusambaza gesi lakini mchakato wa kusambaza gesi utaanza mwaka 2024 na penyewe hawataweza kuziba pengo la Urusi bali watakuwa na uwezo kuziba gepu la asilimia 10 tu.
Nishati ya Urusi ni muhimu kwa uchumi wa dunia hilo halina mjadara hata tukibishana miaka kumi.
Huyo Russia angekuwa na umuhimu huo uusemao basi angekuwa Taifa lenye uchumi wenye nguvu barani Ulaya.Wewe unakuja na assumptions zako kichwani za Poland wananunua Germany ambayo inanunua Russia just to make you feel good baada ya kuona Poland pamoja na kukatiwa hiyo gesi wameendelea kupeta tu.

Finland na Sweden hawatishiki na wataendelea na mchakato wa kujiunga NATO kama kawaida,huyo mwenye gesi yake akate tu abakie nayo tuone kama yeye atakula hiyo gesi na uchumi wake wa kuunga unga kwa sasa.
 
Kweli kaka, ni nchi ndogo sana Finland yenye strategic plan kubwa na za muda mrefu.Pia moja kati ya Nchi zinangoza kwa kujali raia wake. Kuna kukurupuka kwenye kutoa mada
Ni nchi yenye watu wenye akili, wana pesa. Na bado wanaweza wakapata backup pia, sio rahisi kukurupuka kujiunga NATO. Na finland anategemea nishat ya Russia kwa 10% tu.
 
Ni nchi yenye watu wenye akili, wana pesa. Na bado wanaweza wakapata backup pia, sio rahisi kukurupuka kujiunga NATO. Na finland anategemea nishat ya Russia kwa 10% tu.
Kabisa, nchi inatoa elimu bure mpaka chuo na huduma za afya bure, na kama hauna kazi unalipwa
 
Huwezi shindana na mwenye pesa, russia ni masikini kulinganisha na mataifa ya ulaya.
Hiyo Ufini, Uswidi, Latvia, Estonia, Poland, Bulgaria, Romania, Moldova, Norway, Austria, Croatia, Czech, Serbia, Ugiriki, Cyprus, Hungary, Slovakia[emoji38][emoji38][emoji38][emoji38]

Kuna vinchi vingi masikini kule Ulaya ambavyo havitaweza kuhimili hii economic shock inayoletwa na Mrusi.

Unapoiongelea Ulaya usiziwaze tu Ujerumani, Ufaransa, Uingereza au Italy pekee
 
Huyo Russia angekuwa na umuhimu huo uusemao basi angekuwa Taifa lenye uchumi wenye nguvu barani Ulaya.Wewe unakuja na assumptions zako kichwani za Poland wananunua Germany ambayo inanunua Russia just to make you feel good baada ya kuona Poland pamoja na kukatiwa hiyo gesi wameendelea kupeta tu.

Finland na Sweden hawatishiki na wataendelea na mchakato wa kujiunga NATO kama kawaida,huyo mwenye gesi yake akate tu abakie nayo tuone kama yeye atakula hiyo gesi na uchumi wake wa kuunga unga kwa sasa.
Ndio maana nimekuambia mnatanguliza sana ushabiki badala ya uharisia.

Haya niambie kwann Marekani anaendelea kununua mafuta ya Urusi kwa mlango wa nyuma wakati ameyapiga marufuku?

Kwanza kuhusu Poland ni Ujerumani yenyewe ilitangaza kuwa ita isambazia gesi Poland baada ya Urusi kusitisha usambazaji sasa sijui tukusikilize ww au viongozi wa Ujerumani.

Kuhusu Uchumi Urusi ni moja wapo ya taifa lenye nguvu za kiuchumi barani ulaya na ni taifa la 5 kwa Uchumi mkubwa barani ulaya kati ya nchi zaidi ya therathini na kitu.

Alafu kila taifa duniani lina Umuhimu katika nafasi yake na kutokana na ilicho nacho.
Mfano kwenye sekta ya viwanda nchi kama Japan, China, Marekani,na Ujerumani ni mataifa muhimu sana.

Kwenye sekta ya nishati mataifa kama Urusi, Qtaar, Saudia,UAE,Iran na Venezuela ni mataifa muhimu sana.

Kwenye sekta ya kilimo na usambazaji wa chakula duniani mataifa kama Urusi, Ukraine,India, Thailand na Pakistan ni mataifa muhimu sana.
Kila taifa lina Umuhimu wake.


Ulaya kamwe haotakuja kuacha kutumia nishati ya Urusi ni kuomba mungu atupe uhai tu,watajifanya wamepiga marufuku lakini wanaenda kuinunua kwa mlango wa nyuma.
Hata kwenye suala la Rubo kwenye vyombo vyao vya habari wanakataa lakini nyuma ya pazia wameruhusu makampuni yao kununua kwa Rubo.
 
Kwa kitendo Chao cha kupeleka maombi kutaka kujiunga na nato ,mzee Putin amefunga koki za kupeleka gesi na tayari amewakatia umeme Sasa ngoma inogire raia wa finland
Mzungu sio mswahili wa mbagala hayo ya umeme na gesi Finland wanajua zaidi na alternatives kibao kama zilivyofanya nchi za Ujerumani na nchi nyengine za ulaya., bora uendelee kumlaumu putin kwanini Finland wamefanikiwa kupeleka maombi ya kujiunga na NATO na hakuwasha ata nuclear moja ambayo aliahidi atapiga katika kitovu cha nchi za ulaya.
 
Jifunze kusoma na kuelewaView attachment 2232702
Kwamba hujui tofauti ya USSR na Russia au makusudi tu. Sisi tunazungumzia current Russian Federation wewe unaleta Soviet Union. Basi kama ni hivyo turudi ukouko Soviet era, USSR iliivamia Finland mwaka 1938. Si umeuliza lini Russia imeitishia Finland, basi ni kwamba iliwahi ivamia kwahiyo acha Finland ijiunge NATO
 
Sasa hiyo gas atakuwa anakunywa mwenyewe? Wananchi wake atawafungia ndani? Ubabe nao kazi sasa!
 
Back
Top Bottom