For Political Survival, Halima Mdee na wenzake wahamie ACT Wazalendo

For Political Survival, Halima Mdee na wenzake wahamie ACT Wazalendo

Hapa nadhani watakimbilia Mahakamani kama alivyofanya Zitto miaka ileeeee!! Wakienda Mahakamani wanazuia maamuzi ya Baraza Kuu kutekelezwa na wanafungua kesi ya kupinga mchakato wa kuwafukuza. Wanarudi Bungeni kuendelea na Ubunge wao, kedi inaendeshwa miaka 3 hivyo wanamaliza miaka 5!! Ngoma sasa ni kwa chama, watachukua ruzuku ama la??
Kwani hapo kabla walikuwa wanachukua ruzuku?
 
Kazi ya mwanasiasa ni kufanya siasa.

Maamuzi ya mwisho ya kuwavua uwanachama wa CHADEMA wabunge Halima Mdee na wenzake 18 baada ya rufaa yao kukataliwa, huenda yakawatoa rasmi kwenye siasa za vyama, hivyo kulazimika kutetea ubunge wao mahakamani kwa ajili ya kusogeza siku mbele kuelekea 2025.

Labda wengi wanajiuliza au wengine wanadhani huu ndio mwisho wa kisiasa kwa wanasiasa hawa wazoefu na machachari. Kisiasa, hesabu nzuri zaidi ni wanawake hawa kuhamia chama cha ACT ili wapate jukwaa halali la kuendelea kuwa relevant kwenye siasa za upinzani na uwakilishi hapa nchini.

Jambo la muhimu zaidi, maamuzi ya CHADEMA yaheshimiwe.
Ila hawataweza kuaminika tena
 
Chadema haina shida na Ubunge wao, Cha msingi ni kwamba imewakataa na kwa Sasa chadema Ina mwakilishi mmoja bungeni pekee yake.
Ni kweli na nawasifu Sana Chadema kutomgusa AIDA KENANI Kwa kuheshimu maamuzi ya wananchi wa Nkasi waliopiga Kura zào na kuzilinda mbali ya mabomu ya machozi waliyopigwa siku nzima lakini hawakuondoka uwanja wa Sabasaba walikojikisanya kusubiri matokeo karibu na ofisi za Halmashauri ya Nkasi. Wananchi walioamua kuwapa Udiwani Madiwani zaidi ya 5 mbali ya dhuluma zilizofanyika kwenye Kata nyingine.

Sent from my M2003J15SC using JamiiForums mobile app
 
Jamani Zito alienda Mahakamani kutetea Ubunge wake enzi zile hata Magu hakuwa Rais bado, sijui kwanini binadamu tunasahau haraka, au mna shida gani na hayati Magufuli, muacheni mzee wa watu apumzike kwa amanii
Anazungumziwa Mwendazake kwa vile yeye ndio chanzo cha matokeo ya akina Halima Mdee, Bulaya na wenzao 17 wa CHADEMA, Mwendazake ametuharibia sana Bunge bora na siasa safi kwa maslahi yake binafsi na sio ya Taifa.
 
Kazi ya mwanasiasa ni kufanya siasa.

Maamuzi ya mwisho ya kuwavua uwanachama wa CHADEMA wabunge Halima Mdee na wenzake 18 baada ya rufaa yao kukataliwa, huenda yakawatoa rasmi kwenye siasa za vyama, hivyo kulazimika kutetea ubunge wao mahakamani kwa ajili ya kusogeza siku mbele kuelekea 2025.

Labda wengi wanajiuliza au wengine wanadhani huu ndio mwisho wa kisiasa kwa wanasiasa hawa wazoefu na machachari. Kisiasa, hesabu nzuri zaidi ni wanawake hawa kuhamia chama cha ACT ili wapate jukwaa halali la kuendelea kuwa relevant kwenye siasa za upinzani na uwakilishi hapa nchini.

Jambo la muhimu zaidi, maamuzi ya CHADEMA yaheshimiwe.
Halafu waliotajwa kuwa wahuni wataenda kutoa ushahidi mahakamani?
Mimi nitafurahi waende mahakamani ili ikadhihirike waliowasaidia kufoji nyaraka
 
Naunga mkono hoja wahamie ACT. Hawa ni wanawake smart sana na CHADEMA inaenda kufa mara moja.
 
Yule ni mzee Halima na umri wa kujiunga ktk hyo jumuiya ya chama chakavu umeshapita

images (2).jpg
 
Rufaa imeshasikilizwa na baraza kuu ndio chombo Cha mwisho. Halafu wale kwa Sasa hawana chama na pia kuhusu kuondoka bungeni hilo ni juu ya spika. Ila chadema kwa Sasa Ina mbunge mmoja tu kenan wa nkasi.
Kama chama kinamtambua kenan Basi wanehalalisha uchaguzi 2020 hivyo wapeleke majina hakuna namna.

Sent from my TECNO KD6 using JamiiForums mobile app
 
Ndicho nilichokisema. Mbinu ya kukimbilia mahakamani ndio short term goal sahihi itakayowasaidia kwa lengo la ku-buy time. Zitto bila shaka atatumia fursa hii vizuri kurudisha ubest wake wa nguvu na pacha wake wa kitambo Halima Mdee na kukiimarisha zaidi chama chake.
Watakuwa wapumbavu kujiunga na chama cha zitto , kwa kuwa hicho chama ni mfu zaidi ya mfu
 
Hapa nadhani watakimbilia Mahakamani kama alivyofanya Zitto miaka ileeeee!! Wakienda Mahakamani wanazuia maamuzi ya Baraza Kuu kutekelezwa na wanafungua kesi ya kupinga mchakato wa kuwafukuza. Wanarudi Bungeni kuendelea na Ubunge wao, kedi inaendeshwa miaka 3 hivyo wanamaliza miaka 5!! Ngoma sasa ni kwa chama, watachukua ruzuku ama la??
Je na wao wakifunguliwa kesi ya kugushi?
 
Hapa nadhani watakimbilia Mahakamani kama alivyofanya Zitto miaka ileeeee!! Wakienda Mahakamani wanazuia maamuzi ya Baraza Kuu kutekelezwa na wanafungua kesi ya kupinga mchakato wa kuwafukuza. Wanarudi Bungeni kuendelea na Ubunge wao, kedi inaendeshwa miaka 3 hivyo wanamaliza miaka 5!! Ngoma sasa ni kwa chama, watachukua ruzuku ama la??
Huu ndiyo ukweli. Na kwenye kikao walienda tu ili wawe vizuri kwenye rufaa yao. Nashangaa watu wanavyojenga matuamaini eti wametimuliwa.
 
Back
Top Bottom