Pre GE2025 Freeman Mbowe kuona ni kuamini, achana na siasa za mkia wa mbuzi, jeuri na kiburi sio mtaji kuelekea uchaguzi 2024/2025

Pre GE2025 Freeman Mbowe kuona ni kuamini, achana na siasa za mkia wa mbuzi, jeuri na kiburi sio mtaji kuelekea uchaguzi 2024/2025

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Yapi ya Samia na Mbowe? Sijui maana yake, niambie.
Kumbe hujui hata maana ya maridhiano!!! Nenda shule kwanza ndio uje tujadiliane. Wewe utakuwa kunguni wa Mbowe.
 
Kumbe hujui hata maana ya maridhiano!!! Nenda shule kwanza ndio uje tujadiliane. Wewe utakuwa kunguni wa Mbowe.
Wala sipo huko kwa CDM wala CCM. Nipo kwa maslahi ya Tanzania. Usilazimishe Watanzania wote kuwa chawa watumwa kama wewe wa binadamu, chama fulani badala ya kujali maslahi ya taifa kwanza.
 
Tunawajua wazee wa kususa. Watanzania wamechoshwa na wasusaji. Kama wanawake wajawazito
Ni vile tu wapinzani nchini hawana umoja, hawana misimamo, wengi wao ni vigeugeu, wachumia tumbo na pia wanafiki. Na ndiyo maana mara zote mmekuwa mkiwachezea mpendavyo.

Ila ukweli nyinyi Ma ccm, hamjawahi kutanguliza maslahi ya Taifa kwenye jambo lolote lile. Siku zote kila mnachofanya, huwa mnatanguliza maslahi yenu kwanza.
 
Ni kumpaMbowe 150 mn za kanisa na ruzuku CDM na ACT watulie kama ulivyosema hapo juu na kwa upeo wako unapoishia.
Nimekuuliza swali unayajua maslahi ya Tanzania? Kama unayajua yataje.
 
Ni vile tu wapinzani nchini hawana umoja, hawana misimamo, wengi wao ni vigeugeu, wachumia tumbo na pia wanafiki. Na ndiyo maana mara zote mmekuwa mkiwachezea mpendavyo.

Ila ukweli nyinyi Ma ccm, hamjawahi kutanguliza maslahi ya Taifa kwenye jambo lolote lile. Siku zote kila mnachofanya, huwa mnatanguliza maslahi yenu kwanza.
Kwahiyo unakubali kuwa Mbowe ni kigeugeu, Mchumia tumbo na pia ni mnafiki?
 
Warioba alipita nchi nzima kukusanya maoni kwa maslahi ya Taifa. Kama kuna nia ya dhati tungeanzia hapo.
Nimekuuliza unayajua maslahi ya Taifa. Kama hujui sema.
 
Na;
Hamis Abeid Baruani
UDASA, UDSM.

Kwa masikitiko makubwa leo Mbowe ameushangaza umma kwa kuongea mambo mawili ambayo hadi sasa yamepingwa kila kona ya nchi.

1. Katangaza kususia maridhiano
2. Kaitisha anayoyaita maandamano ya amani.

a) Mhe. Mbowe kabla ya kususia MARIDHIANO unakumbuka lakini majuzi tu 31.12.2023 pale Hai wakati unaongoza Harambee ya kumalizia ujenzi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT) Usharika wa NSHARA MACHAME, Rais Dkt. Samia alichangia Tsh Milioni 150, haya yakiwa ni matunda ya MARIDHIANO ya kisiasa hapa nchini.

b) Mnakumbuka CDM mlikuwa na ziara pamoja na mikutano mikoa mbalimbali na mkafanya kwa amani hakuna mtu alienyooshewa kidole hata mmoja inamaana mmesahau kama hayo ni matunda ya MARIDHIANO

c) Maridhiano haya unayotaka kuyakataa hukumbuki kuwa ndio yamefanya viongozi wa CDM waliokuwa nje ya nchi kurejea nchini kufanya siasa kwa amani bila wasiwasi

d) Hujiulizi hata tukio la leo limefanyika vizuri kwa amani na umepewa ushirikiano wa namna zote kwenye vyombo vya habari kwasababu ya matunda ya MARIDHIANO yaliyoletwa na Rais Dkt. Samia

e) Hata umuhimu wa RUZUKU ambao pengine umepelekea kuhamisha Ofisi toka Kinondoni kwenda Mikocheni nao huoni kama ni matunda ya MARIDHIANO

Tujifunze kuwa waungwana tunapofanyiwa uungwana.

Wakati unafikiria kuandamanisha watu kumbuka wananchi wa sasa sio wa miaka ile, wananchi wanaona mambo makubwa yanayofanywa na Serikali yao, wanaona jitihada za Rais Samia kuwapigania. Ngoja niwakumbushe kidogo:-

1. Januari za miaka ya nyuma Wazazi walikuwa wanateseka kwa michango ya ujenzi wa madarasa na kununua madawati ila sasahivi hakuna mzazi hata mmoja nchini anaesumbuliwa na michango hii, Rais Samia kajenga madarasa mengi nchi nzima lakini pia Serikali kila mwezi inatoa takribani Bilioni 33.3 kugharamia elimu kwa wanafunzi wa ngazi ya awali, msingi na sekondari.

2. Rais Samia amesambaza Vifaa vya Afya Majimbo yote nchini kama ifuatavyo kwa ujumla
a) Vitanda vya wagonjwa 3080
b) Vitanda vya kujifungulia 1000
c) Magodoro 5500
d) Mashuka 36,808
e) Meza za Vitanda 306
f) Pia kasambaza magari ya kubebea wagonjwa (Ambulance) kila kona

Hii inaonesha namna gani ana huruma na wananchi na anajali afya zetu.

3. Takribani asilimia 95% ya Madai ya Watumishi yamefanyiwa kazi ndani ya muda mfupi. (Ulipaji madeni, Ongezeko la Posho, Mikataba ya hali bora, Ajira mpya, Mazingira bora ya Kazi).

4. Wakati wananchi wanajiuliza michango yao mliochangisha CDM kuipeleka Hanang haijulikani imeenda wapi na hakuna jibu kuwa mlikusanya shilingi ngapi,

Rais Samia ametenga ekari 100 kwaajili ya makazi mapya ya wahanga wa Hanang, lakini Serikali itawajengea nyumba 101 ambazo kila moja itakuwa na vyumba vitatu na eneo litawekewa huduma zote za kijamii.

5. Kwa muda mfupi mno wa Rais Samia kuwa madarakani sasahivi kati ya Vijiji 10, Vijiji 9 vina umeme, hii ni hatua kubwa mno.

Hawa wana vijiji huwezi ukawaambia habari za kuandamana wakakuelewa.

6. Ndani ya muda mfupi tu Waalimu takribani 227,263 wamepandishwa madaraja na wanaendelea kuchapa kazi, hawa wataandamana kushukuru na kumpongeza Rais Dkt. Samia.

7. Kwenye kuongeza mapato makubwa hivi karibuni Serikali inatatajia kuanza kuchimba MAKAA YA MAWE katika mradi wa MCHUCHUMA, Tani karibia 315,000 zitachimbwa.

8. Wakulima wanafurahia Ruzuku kwenye Pembejeo za Kilimo ambazo zimefanya hali ya kilimo kuwa vizuri.

9. Ndani ya muda mfupi fedha za kigeni zimeongezeka baada ya kuongeza biashara nje ya nchi.

Mauzo ya bidhaa na huduma nje ya nchi yameongezeka kwa asilimia 17.8
  • Novemba 2022 tuliuza Trilioni 29.8
  • Novemba 2023 tuliuza Trilioni 35.1

Mfano; Desemba 2022 hadi Desemba 2023 tumeuza NYAMA Tani 20,500 nje ya nchi, takribani mara mbili ya mauzo ya mwaka uliopita.

Hii inaonyesha ni namna gani Serikali inapambana kuleta maendeleo.

10. Miradi ya Maji nchi nzima inaendelea ili lengo la kumtua Mama Ndoo Kichwani litimie, mfano kwa Wilaya ya Ubungo kuna Miradi mikubwa miwili a) Tegeta A na b) Mshikamano
Ambayo itamaliza kabisa tatizo la maji.

Hawa wananchi hawahitaji maandamano bali wanahitaji kutoa pongezi kwa kazi kubwa inayofanywa.

Ni mengi yaliyofanyika na yote yana lengo la kumfaidisha Mwananchi ili aendelee kuwa na imani na Serikali yake.

Tusikubali kuyumbishwa na SIASA ZA MKIA WA MBUZI.

Kila Chama kijipange tukutane kwenye DEBE muda ukifika.

Ahsanteni.
Chawa kama chawa.
Acheni ubinafsi.
Alichokisema Mbowe ni Sauti ya wananchi wengi.
Endeleeni kuumiza watu, siku moja mtapata kinachowastahili
 
Na;
Hamis Abeid Baruani
UDASA, UDSM.

Kwa masikitiko makubwa leo Mbowe ameushangaza umma kwa kuongea mambo mawili ambayo hadi sasa yamepingwa kila kona ya nchi.

1. Katangaza kususia maridhiano
2. Kaitisha anayoyaita maandamano ya amani.

a) Mhe. Mbowe kabla ya kususia MARIDHIANO unakumbuka lakini majuzi tu 31.12.2023 pale Hai wakati unaongoza Harambee ya kumalizia ujenzi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT) Usharika wa NSHARA MACHAME, Rais Dkt. Samia alichangia Tsh Milioni 150, haya yakiwa ni matunda ya MARIDHIANO ya kisiasa hapa nchini.

b) Mnakumbuka CDM mlikuwa na ziara pamoja na mikutano mikoa mbalimbali na mkafanya kwa amani hakuna mtu alienyooshewa kidole hata mmoja inamaana mmesahau kama hayo ni matunda ya MARIDHIANO

c) Maridhiano haya unayotaka kuyakataa hukumbuki kuwa ndio yamefanya viongozi wa CDM waliokuwa nje ya nchi kurejea nchini kufanya siasa kwa amani bila wasiwasi

d) Hujiulizi hata tukio la leo limefanyika vizuri kwa amani na umepewa ushirikiano wa namna zote kwenye vyombo vya habari kwasababu ya matunda ya MARIDHIANO yaliyoletwa na Rais Dkt. Samia

e) Hata umuhimu wa RUZUKU ambao pengine umepelekea kuhamisha Ofisi toka Kinondoni kwenda Mikocheni nao huoni kama ni matunda ya MARIDHIANO

Tujifunze kuwa waungwana tunapofanyiwa uungwana.

Wakati unafikiria kuandamanisha watu kumbuka wananchi wa sasa sio wa miaka ile, wananchi wanaona mambo makubwa yanayofanywa na Serikali yao, wanaona jitihada za Rais Samia kuwapigania. Ngoja niwakumbushe kidogo:-

1. Januari za miaka ya nyuma Wazazi walikuwa wanateseka kwa michango ya ujenzi wa madarasa na kununua madawati ila sasahivi hakuna mzazi hata mmoja nchini anaesumbuliwa na michango hii, Rais Samia kajenga madarasa mengi nchi nzima lakini pia Serikali kila mwezi inatoa takribani Bilioni 33.3 kugharamia elimu kwa wanafunzi wa ngazi ya awali, msingi na sekondari.

2. Rais Samia amesambaza Vifaa vya Afya Majimbo yote nchini kama ifuatavyo kwa ujumla
a) Vitanda vya wagonjwa 3080
b) Vitanda vya kujifungulia 1000
c) Magodoro 5500
d) Mashuka 36,808
e) Meza za Vitanda 306
f) Pia kasambaza magari ya kubebea wagonjwa (Ambulance) kila kona

Hii inaonesha namna gani ana huruma na wananchi na anajali afya zetu.

3. Takribani asilimia 95% ya Madai ya Watumishi yamefanyiwa kazi ndani ya muda mfupi. (Ulipaji madeni, Ongezeko la Posho, Mikataba ya hali bora, Ajira mpya, Mazingira bora ya Kazi).

4. Wakati wananchi wanajiuliza michango yao mliochangisha CDM kuipeleka Hanang haijulikani imeenda wapi na hakuna jibu kuwa mlikusanya shilingi ngapi,

Rais Samia ametenga ekari 100 kwaajili ya makazi mapya ya wahanga wa Hanang, lakini Serikali itawajengea nyumba 101 ambazo kila moja itakuwa na vyumba vitatu na eneo litawekewa huduma zote za kijamii.

5. Kwa muda mfupi mno wa Rais Samia kuwa madarakani sasahivi kati ya Vijiji 10, Vijiji 9 vina umeme, hii ni hatua kubwa mno.

Hawa wana vijiji huwezi ukawaambia habari za kuandamana wakakuelewa.

6. Ndani ya muda mfupi tu Waalimu takribani 227,263 wamepandishwa madaraja na wanaendelea kuchapa kazi, hawa wataandamana kushukuru na kumpongeza Rais Dkt. Samia.

7. Kwenye kuongeza mapato makubwa hivi karibuni Serikali inatatajia kuanza kuchimba MAKAA YA MAWE katika mradi wa MCHUCHUMA, Tani karibia 315,000 zitachimbwa.

8. Wakulima wanafurahia Ruzuku kwenye Pembejeo za Kilimo ambazo zimefanya hali ya kilimo kuwa vizuri.

9. Ndani ya muda mfupi fedha za kigeni zimeongezeka baada ya kuongeza biashara nje ya nchi.

Mauzo ya bidhaa na huduma nje ya nchi yameongezeka kwa asilimia 17.8
  • Novemba 2022 tuliuza Trilioni 29.8
  • Novemba 2023 tuliuza Trilioni 35.1

Mfano; Desemba 2022 hadi Desemba 2023 tumeuza NYAMA Tani 20,500 nje ya nchi, takribani mara mbili ya mauzo ya mwaka uliopita.

Hii inaonyesha ni namna gani Serikali inapambana kuleta maendeleo.

10. Miradi ya Maji nchi nzima inaendelea ili lengo la kumtua Mama Ndoo Kichwani litimie, mfano kwa Wilaya ya Ubungo kuna Miradi mikubwa miwili a) Tegeta A na b) Mshikamano
Ambayo itamaliza kabisa tatizo la maji.

Hawa wananchi hawahitaji maandamano bali wanahitaji kutoa pongezi kwa kazi kubwa inayofanywa.

Ni mengi yaliyofanyika na yote yana lengo la kumfaidisha Mwananchi ili aendelee kuwa na imani na Serikali yake.

Tusikubali kuyumbishwa na SIASA ZA MKIA WA MBUZI.

Kila Chama kijipange tukutane kwenye DEBE muda ukifika.

Ahsanteni.
Hizi hoja kama zimetolewa na mhudumu wa ofisi ya UDASA, atakuwa amejitahidi, ila kama ni lecturer, basi huyu naye atakuwa ni lecturer takataka.

Argument zake zimekaa kilayman hasa. Hana utofauti na wale wajinga ambao huwa wanasema kuwa mapato ya Serikali yameongezeka saba katika miaka hii saba, kwa sababu miaka saba iliyopita makusanyo yalikuwa trillion 1 na sasa ni shilingi trillion 3.

Yaani mtu anabwabwaja bila ya kufikiria depreciation ya shilling against hard currencies, na depreciation ya hard currencies pia. Hafikirii juu ya ongezeko la watu pia. Anataka ajisifu kuna ongezeko la makusanyo kwa kulinganisha makusanyo wajati watu wakiwa 40m na pale ambapo wapo 60m. Kama angekuwa msomi anayejitambua angetoa takwimu ya ongezeko la kodi in real terms.

Mtu hajui kuwa shilling imekuwa ikishuka thamani.
Sarafu nyingine kubwa kama dollar, euro na pauni nazo zimekuwa zikishuka thamani. Hajui kuwa hard currencies on average zina-depreciate by 25% after every 7 years.

Yawezekana kabisa makusanyo ya shilingi trilion 1.5 ya miaka 7 iliyopita ni makubwa kuliko makusanyo ya shilingi trilioni 2 ya leo. Unatakiwa ubadilishe trilioni yako 1.5 kwa rate ya dola miaka 7 iliyopita. Halafu shilingi trilioni 2 ya leo. Halafu depreciate hii ya sasa kwa 25%, uone itakuwa ni dollar ngapi, linganisha na hiyo ya miaka 7 iliyopita.

Mtu hajui kuwa dollar 100 ya mwaka 1960 ni kubwa kuliko dollar 1,000 ya leo.

$100 in 1960 is equivalent in purchasing power to about $1,036.30 today, an increase of $936.30 over 64 years. The dollar had an average inflation rate of 3.72% per year between 1960 and today, producing a cumulative price increase of 936.30%

Kama dolar ina-depreciate kwa 3.72%; jiulize shilingi ina-depreciate kwa asilimia ngapi?
 
Tangu 1995 Mbowe anaiongoza CDM hivi hakuna wenye akili wengine ndani ya CDM?
Ccm inavyolazimisha kukaa madarakani kwa shuruti muda wote huu, kwani hakuna chama kingine chenye uwezo huo wa kuongoza?
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Ccm inavyolazimisha kukaa madarakani kwa shuruti muda wote huu, kwani hakuna chama kingine chenye uwezo huo wa kuongoza?
Hakuna chama kisicholazimisha kukaa madarakani.
 
Maandano hufanywa na primitive people.

Uchawa hufanywa na punguani. Maandamano ya amani hufanywa na watu wanaojitambua ikiwa ni njia shirikishi zaidi ya kufikisha maoni yao kwa watawala. Maandamano hupima ni watu wengi kiasi gani wanaguswa na suala husika. Ndiyo maana kwa nchi zilizostaarabika, kama maandamano ni ya amani, watawala huweza kujitokeza mbele ya waandamanaji na kutoa majibu ya yale yaliyowafanya waandamane.
 
Wakae madarakani kwa ridhaa ya wananchi, sio kwa kubaka uchaguzi.
CHADEMA chama cha familia. Wananchi gani walimruhusu Mbowe kukaa kwenye uenyekiti zaidi ya miaka 20?
 
Back
Top Bottom