Freeman Mbowe, Mnyika na Viongozi CHADEMA wakutana na Rais Samia na Viongozi wa CCM Ikulu ya Chamwino - Dodoma leo 20/5/2022

Lete sababu za msingi kwanini alikuwa na kesi ya kujibu na ghafla kesi inafutwa lakini anatoka na kuunganisha Ikulu kwa mtesi wake, em jibu hili suali japo points 2 tu.
Kesi ilikua ya mchongo, ushahidi wa kuunga unga! Serikali walijua utetezi watapangua kesi, wakaweka mpira kwapani. Mmekuwa mkisema CHADEMA wanafanya siasa za fujo, sasa Mbowe anatafuta muafaka mnaleta maneno ya usaliti! Nyie msiotaka mazungumzo, anzisheni Umoja Party!
 
Wamesha anzisha hao ila pia wamekwama kabla ya kuanza Kwa kuendeleza mrengo uliowagawa watanzania na kuwaudhi pakubwa🚶
 
kwanini alienda Ikulu break ya kwanza? walizungumza nini hasa na mama lakini hivi naandika pia alitoka tena ikulu juzi ajenda ni nini hasa na Rais ambaye ni mtesi wake?

Kina msigwa kwanini hawaongei chochote? heche? kwanini kama Mbowe ametupiwa paka wa uso peke yake, tundu lissu aliulizwa akasema atajibu mwenyewe mbowe kwanini na yeye kila kitu kikitokea anajifanywa mwanasheria kutoa fatwa? kwanini hili la mbowe Ikulu mara kwa mara hasemi kitu? mnawafanya watanzania wajinga kiasi hichi, kwanini mwenyekiti wenu anatumiliwa na ccm mchana kweupe?
 
Hatua ya sasa ya kwenda ikulu, ameenda na viongozi kadhaa, ikifikia wakati wa umma kufahamishwa mazungumzo hayo, taarifa itatolewa! Lakini kinacho kuwasha hapa, siyo CHADEMA kununuliwa na ccm, ni kwa sababu mh. Samia anaenda kinyume na mungumfu wenu!
 
Kuna wakati Mungu hushindwa na kuweka wasikuwa wa mipango yake eee
 
Hatua ya sasa ya kwenda ikulu, ameenda na viongozi kadhaa, ikifikia wakati wa umma kufahamishwa mazungumzo hayo, taarifa itatolewa! Lakini kinacho kuwasha hapa, siyo CHADEMA kununuliwa na ccm, ni kwa sababu mh. Samia anaenda kinyume na mungumfu wenu!
Ndio mana Mbowe amesema ataifumua na kuipanga upya chadema ili wanaotaka kwenda na kasi ya manunuzi ya chama hicho waende kina Piter Msingwa, Heche na wenzake ambao wanaamini chadema ile ya zamani wasioamini kwenye udalali wao watapuumzishwa
 
Simple logic. Rais wa Tanzania hahitaji kubembeleza mtu au kikundi cha watu ili atawale bila mikwaruzo. Uongozi wa CHADEMA haujaalikwa Ikulu kwa kubahatisha. Kete yao ni ipi?

Crack your head, nini kilichofanya maRais wa awamu ya 4, 5 na 6 kuhangaika na CHADEMA kiasi cha kukiuka katiba, sheria na utu wazi wazi ili kupunguza harakati za chama hicho hasa katika chaguzi zote?

Peoples power! Hilo ndilo jibu.

Demokrasia ya kweli ikiruhusiwa kufanya kazi nchini, 2025 CHADEMA inasepa na kijiji (zaidi ya asilimia 90 ya wapiga kura wote). CCM wanajua hili vizuri sana.

Rais wa awamu ya 5 aliamini au aliaminishwa kuwa CHADEMA inaweza kutoweshwa kwa “Final Solution”: kununua na/au kuua viongozi wake, kutengeneza kesi ya ugaidi kisha kufutilia mbali usajili wa chama hicho. The aftermath is history.

Mrithi wake kaelimika kuwa ilikuwa ni kujidanganya. Upinzani ni nafsi, huwezi kuuua. CHADEMA ni chombo tu lakini madhubuti. Sasa yeye kaja na kete yake ya “maridhiano”. Ukweli utadhihirika punde.
 
Hivi tukikumbuka yaliyo tokea Uchaguzi Zanzibar 2020 ,Machafuko na kupotea kwa watu Mbali Mbali kwa sababu za kisiasa.

Kupigwa na kuteswa kwa Wanasiasa mbali mbali kama Kina Tundu Lissu.

Kukimbia Nchi kwa Wanasiasa mbali mbali kama kina Lema kwa sababu za kisiasa.

Hivi Watanzania tujifunze nini kuhusu SIASA ZA TANZANIA?
 
Hivi tukikumbuka yaliyo tokea Uchaguzi Zanzibar 2020 ,Machafuko na kupotea kwa watu Mbali Mbali kwa sababu za kisiasa...
Chadema wanatufundisha mazuzu ya Lumumba na nduli alliyeko kusiko julikana kuwa siasa sio uadui, kutekana kuuana na kusingiziana kesi za urongo Bali siasa ni kushindanisha sera kwa wananchi na bado mkabakia mnaheshimiana na kushirikiana japo mna itikadi tofauti.
 
kwani mpaka ukasirike ndio uonekane unatetea hoja una mawazo ya kijinga sana
 
Ndio mana Mbowe amesema ataifumua na kuipanga upya chadema ili wanaotaka kwenda na kasi ya manunuzi ya chama hicho waende kina Piter Msingwa, Heche na wenzake ambao wanaamini chadema ile ya zamani wasioamini kwenye udalali wao watapuumzishwa
Huna lolote wewe sukumagang, na mtakufa tu nyie Warundi!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…