From the book 'I am the State' (Mimi ni Dola)

From the book 'I am the State' (Mimi ni Dola)

Kiukweli nilitokea kumchukia sana hayati Magufuli hasa kwa mambo 'binafsi' hata kabla hajawa rais!

Ila pamoja na yote Magufuli alikua ana afadhali ukimlinganisha na Kikwete au Samia tuongee tu kwa kumtendea haki.

Ni nani hakupapendelea kwao nchi hii?

Nyerere na Mara? Nyerere na akina Butiku?

Mwinyi na Zanzibar/Mkuranga?

Mkapa na kusini?

JK?

Pili kuna haja gani ya kutumia rasilimali kubwa hivyo kuchapisha kitabu chenye maudhui yasiyo na msaada? Lengo ni kujifunza? Kama ni kujifunza si tunayo historia ya Gbadolite huko Zaire sasa DRC? Nani ana fadhili hayo na kwa maslahi gani?

Magufuli ni lost case kwa sasa haya hayatusaidii.

Mwisho tuwe makini sana na waandishi uchwara maana huu ni ulaji unatafutwa kwa mtu na ni njia ya kututoa kwenye reli.
Hey, Magufuli is not a lost case..!!

Magufuli is a living being though his body is under six feets down the soil..

Nawapongeza sana hawa waandishi Kwa sababu sasa matendo na maspamuzi yake wakati wa uongozi wako yako documented Kwa ajili kizazi kijacho kujifunza..
 
waacheni watanzania wajue kila jambo kumhusu huyu jamaa, hii ndiyo njia pekee ya kujua nyayo zake - vpi na ule mzigo ulioenda China wameuandikamo? 😀
Jamaa wamepeleka China mzigo wao halafu wanamsingizia mwendazake,
 

Yaliyojificha uwekezaji wa Hayati Dk Magufuli Chato yawekwa vitabuni​

Ijumaa, Aprili 14, 2023
magufuli-pic.jpg



Dar es Salaam. Ikiwa ni miaka miwili tangu aliyekuwa Rais wa Tanzania, Dk John Magufuli kupoteza maisha Machi 17, 2021 akiwa madarakani, waandishi wakongwe wanne wamezindua kitabu kinachoonyesha sura ya kiongozi huyo na uwekezaji mkubwa alioupeleka wilayani Chato.

Absalom Kibanda, Ansbert Ngurumo, Neville Meena na Jesse Kwayu ndio waandishi walioandika kitabu hicho chenye jina 'I am the State' ikiwa na maana Mimi ndio Dola.

Kitabu hicho linaonyesha hali ilivyo sasa wilayani Chato alipozaliwa kiongozi huyo mkuu wa nchi baada ya miradi mikubwa ya maendeleo
Miongoni mwa mambo yaliyoangaziwa katika kitabu hicho ni wanyama waliopelekwa Chato enzi ya utawala wa Rais Dk Magufuli, ujenzi wa kiwanja cha ndege, uboreshaji mkubwa wa miundombinu, wananchi kukimbilia kununua viwanja, ujenzi wa masoko na miradi mingineyo.

Pia kitabu hicho kimeangazia fedha zilizopelekwa wilayani huko zitarejeshwaje, mpango wa wilaya hiyo kuandaliwa kuwa mkoa uko uliishia wapi.

Kabla ya uzinduzi wa kitabu hicho Ansbert Ngurumo amesema jina la kitabu limetokana na hofu iliyoshuhudiwa baada ya utawala wa hayati Dk Magufuli tangu mwaka 2015-2021 kuelekeza miradi mingi eneo alikozaliwa bila kuwepo mtu aliyehoji.

Amesema kilichofanyika ndani ya utawala wa Dk Magufuli ilikuwa ni historia ya kipekee kwani awamu zote za viongozi waliopita hapa nchini hakukuwa na kiongozi aliyefanya uwekezaji mkubwa eneo alilotoka.

Mbali na uwekezaji walioutaja kuwa na dalili zote za ubinafsi alioufanya kiongozi huyo, amesema upo ukandamizaji mkubwa alioufanya kwenye jamii na kutoa kauli zenye vitisho kuonyesha hakuna aliye juu yake.

"Kama mnafikiri mpo huru kiasi hicho watch it,"Kauli hayati Dk Magufuli enzi ya uhai wake ambaye imeleta tafsiri kwenye kitabu hicho namna ambavyo uongozi wake haukutetereshwa na kitu chochote.

Akizindua kitabu hicho Askofu wa Jimbo la Karagwe mkoani Kagera, Dk Benson Bagonza amesema uandishi wa kitabu hicho uwe chachu kwa viongozi wastaafu na walio madarakani kuandikiwa vitabu kulingana na mazuri na mabaya yao.

Amesema kitabu cha I am the State kinaonyesha namna fedha za umma zilivyotumika nje ya bajeti ya bajeti ya serikali.

"Mambo yaliyotajwa katika kitabu hiki yalitendeka nchi ikiwa gizani na watu walinyamazishwa na haya yaliyoandikwa ni sehemu ndogo ya yaliyotendeka nchi ikiwa gizani"amesema.
Ila Tanzania tutaendelea kuwa masikini daima kwa huu ujinga kwani huko chato wao hawastahili maendeleo au chato sio tanzania
 
Hawajaandika wachaga walivyojipendelea raslimali za Taifa wakajipelekea kwao Mana wao ndio watangulizi kwa kusoma so walikuwa na ubinfasi wa hali ya juu. Yaani mchaga tu kununu duka ambalo sio la mchaga mwenzake sahau. Sema vyasaka wao wananunua kwao
Kabisa wachaga wabinafsi sana na sio wa kupapa nchi hata second
 
View attachment 2587865

Waandishi nguli wa habari nchini Tanzania wamezindua kitabu 'I am the State' (Mimi ni Dola) chenye kuonyesha maendeleo ya miradi ya uwekezaji yaliyofanyika wilayani Chato mkoani Geita na ukiukwaji wa sheria uliofanyika ndani ya utawala wa hayati Rais Dk John Magufuli wakati wa utekelezaji wa miradi hiyo.

Akizindua kitabu hicho Askofu wa Jimbo la Karagwe mkoani Kagera, Dk Benson Bagonza amesema uandishi wa kitabu hicho uwe chachu kwa viongozi wastaafu na walio madarakani kuandikiwa vitabu kulingana na mazuri na mabaya yao.

Amesema kitabu cha I am the State kinaonyesha namna fedha za umma zilivyotumika nje ya bajeti ya bajeti ya serikali.

"Mambo yaliyotajwa katika kitabu hiki yalitendeka nchi ikiwa gizani na watu walinyamazishwa na haya yaliyoandikwa ni sehemu ndogo ya yaliyotendeka nchi ikiwa gizani"amesema.
Hilo li askofu nalo linawaumini kabisa kuna watu wanasali kwake kiongozi wa dini mwenye chuki?
 
Hey, Magufuli is not a lost case..!!

Magufuli is a living being though his body is under six feets down the soil..

Nawapongeza sana hawa waandishi Kwa sababu sasa matendo na maspamuzi yake wakati wa uongozi wako yako documented Kwa ajili kizazi kijacho kujifunza..
Hao wenye utamaduni wa kusoma vitabu ni akina nani?
 
Hivi kuna anayemsifia bwana joni mwendazake! Kuna mtu anataka kulinganisha butiama na chato? Mkuranga na chato? Lupaso na chato? msoga na chato?
tuwe tu serious jamani! watanzania hatuna umakini wowote kwenye uchaguzi wa viongozi!
Huyu aliyeuza nyumba za serikali binafsi akiwa waziri na kugawia michepuko yake?
Huyu aliyediriki kuchepusha barabara ipitie nyumbani kwake chato akiwa waziri?
Tukubali kujifunza kwa maandiko haya tusije kujisahau tena
Tukachagua U4- Uthubutu - Ushupavu - Ubinafsi - Ukabila. Tuwachunguze watu tunaowapeleka ikulu!
Tulipigwa kiboko baada ya kutojali ule ubinafsi aliouonyesha akiwa waziri.
Nilikuwepo kwenye mojawapo ya kampeni zake sehemu ya biharamulo ambao aliwanyima barabara iliyokuwa ipitie kwao! walipomlalamikia aliwaambia hivi- "kunyeni mavi mubandike barabarani iwe lami"
Huko Kigamboni aliwaambiaje kuhusu kushusha bei ya nauli ya pantoni? "kama hamna hiyo hela pigeni mbizi"
Lugha za uhuni/ukibaka na akathibitisha kwenye uongozi wake kwa kutuwekea mavibaka kama kina Sabaya, Makonda nk.
Ansbert andikeni kitabu kingine kuhusu umuhimu wa hekima katika uongozi.
😅😅😅
 
Chuki kumzidi Magufuli ambaye alikiri kutokupeleka maendeleo majimbo ya wapinzani-akasema yakikosa koneksheni?
Kwani chato ipo nchi gani wewe zwazwa au chato ipo kenya na hizo flyover na hizo barabara alizojenga huko dar napo alipapendelea nyie machizi.
Alafu kiongozi wa dini utakiwi kujihusisha na siasa moja kwa moja na kuwa upande fulan coz unapokea waumini wenye itikadi tofauti ndio maaana YESU alisema ya kaisali muachieni kaisali na ya MUNGU muachieni MUNGU lakini ilo liaskofu lenu linachuki kama lilichukuliwa mke kama ndio wewe mwenyewe au chawa wake kamwambie afanye kazi yake.HAKUNA MKAMILIFU CHINI YA JUA
 
Kwani chato ipo nchi gani wewe zwazwa au chato ipo kenya na hizo flyover na hizo barabara alizojenga huko dar napo alipapendelea nyie machizi.
Umekaza magego kuitaja Chato, wapi nimetaja Chato hapo. Nimeuliza Chuki kumzidi Magufuli ambaye alikiri kutokupeleka maendeleo majimbo ya wapinzani
 
Umekaza magego kuitaja Chato, wapi nimetaja Chato hapo. Nimeuliza Chuki kumzidi Magufuli ambaye alikiri kutokupeleka maendeleo majimbo ya wapinzani
Nitajie jimbo ambalo magufuli hakupeleka maendeleo yaani hakuna mradi wowote uliofanyika wewe zwazwa
 
Watanzania siyo wajinga kiasi hicho kwa sasa.
Hata mkiandika vitabu zaidi ya 60,000,000 vya kumchafua JPM, nawaambia hamtaweza hata kidogo.

JPM ni habari nyingine, ule ulikuwa ni mtambo wa NYUKLIA. Ona mnavyopata taabu sasa. JPM anaishi mioyoni mwa Watanzania wazalendo zaidi ya 91%.
Nenda mitaani humo, iwe Mjini au vijijini, watu wa rika zote wanamkumbuka JPM.
Kamwe kamwe kamwe kamwe hamtaweza kumchafua JPM.
Hawa waandishi ni wa kuwashitaki

Defamation
MediaNewspaper Act
i) Section 35(1) “any matter which, if published, is likely to injure the reputation of any person by exposing him to hatred, contempt or ridicule, or likely to damage any person in his profession or trade by an injury to his reputation, is defamatory matter”.

ii) Section 35(2) “The matter referred to under subsection one (1) shall qualify to be a defamatory matter even when it is published against a deceased person.”

iii) Section 36 (1) A person shall be deemed to make publication of a libel if that person causes the print, writing, painting, effigy, or other means by which the defamatory matter is conveyed, to be dealt with, either by exhibition, reading, recitation, description, delivery or otherwise, in a way that the defamatory meaning thereof becomes known or is likely to be known to either the person defamed or any other person.

iv) Section 38(3) “Nothing in this section shall exempt any person from any liability of a civil or criminal nature under any other Part of this Act or under any other written law if the publication of a matter alleged to be absolutely privileged is prohibited or the relief to a person injured is available under the Constitution of the United Republic.”

Mwenye privilege na vitendo hivyo hapo juu ni Rais, Serikali, Bunge, Spika labda hao waandishi waliidhinishwa na mamlaka tajwa hapo juu.
DPP atang'olewa kisha mashitaka dhidi yao yatarindima
 
Back
Top Bottom