Full Text: Ripoti ya PAC Bungeni kuhusu Tegeta Escrow Account

Full Text: Ripoti ya PAC Bungeni kuhusu Tegeta Escrow Account

Huyu singasinga akamatwe fasta mpuuz sana huyu maana kina kova walikuwa wanakula na kunywa nae sijui kama wataweza kumtia nguvuni na unaweza kukuta kashapotea tutaambiwaanatafutwa na interpol
 
Nadhan sasa hata atakaeteuliwa kuwa waziri wa nishati atawaza mara mbili mbili
 
Kumekucha jamani, tamthiliya ya eskroo Ni episodi nyingine Leo, lakini Kuna jambo tofauti nafikria, sawa Zito na Deo wanastahili kupongezwa kwa niaba ya kamati ya PAC!, Lakini mbona sifa zinazidi kwao Tu wakati Wao Ni waleta chakula(kitoweo) mezani. Mbona muwindaji mahiri kwenye pori hatari(Kafurira a.k.a kaka WA taifa) tunamsahau!?.
Jamani kakoswakoswa na Na mengi huyu.
Jamani katukanwa Sana huyu(tumbili).
Jamani taifa zima lilikuwa linaimba katiba mpya, lkn yeye aliamua kufikria nje ya box.
Jamani kawpiga knock out watu wenye mamlaka ya kidola kwenye lips 👄 zao,
Sasa linapokuja suala la sifa mbona tunaishia kuwasifu wahudumu wa mezani kwa utumishi uliotukuka lakini muwindaji/mpishi tunamchukulia poa!?.
Jamani mwenzenu hili linanikereketa.
Tutende haki kwa kaka WA Taifa. Nawasilisha.
 
Kumekucha jamani, tamthiliya ya eskroo Ni episodi nyingine Leo, lakini Kuna jambo tofauti nafikria, sawa Zito na Deo wanastahili kupongezwa kwa niaba ya kamati ya PAC!, Lakini mbona sifa zinazidi kwao Tu wakati Wao Ni waleta chakula(kitoweo) mezani. Mbona muwindaji mahiri kwenye pori hatari(Kafurira a.k.a kaka WA taifa) tunamsahau!?.
Jamani kakoswakoswa na Na mengi huyu.
Jamani katukanwa Sana huyu(tumbili).
Jamani taifa zima lilikuwa linaimba katiba mpya, lkn yeye aliamua kufikria nje ya box.
Jamani kawpiga knock out watu wenye mamlaka ya kidola kwenye lips í-½í±„ zao,
Sasa linapokuja suala la sifa mbona tunaishia kuwasifu wahudumu wa mezani kwa utumishi uliotukuka lakini muwindaji/mpishi tunamchukulia poa!?.
Jamani mwenzenu hili linanikereketa.
Tutende haki kwa kaka WA Taifa. Nawasilisha.

Ndio maana kuna mgawanyo wa kazi. Nadhani nafasi yake ipo palepale kama mtu aliyeibua kashfa hii ya Escrow.
 
Ndio maana kuna mgawanyo wa kazi. Nadhani nafasi yake ipo palepale kama mtu aliyeibua kashfa hii ya Escrow.

Sawa nakubaliana na unaloniambia, lakini hebu tizama hii imekaa vp? Kuna hoja zimewasilishwa humu za kui please Chadema kumsamehe Zitto, kwa sababu tu ya kusoma ripoti, hpo ndio naona hz sifa hazitendewi haki. Kwa mtizamo wa wangu.
 
Mingoi, mpaka sasa naiona ni drama na fitna lakini sijaona haswa sheria iliyovunjwa. Usisikie zile porojo za Zitto. Ngoja kesho.

Kosa kubwa nililobaini ni kwamba SingaSinga alikuwa na hati ya mauziano ya Iptl ila hati ya umiliki hakuwa nayo. Kwa maana hiyo aliuziwa kampuni hewa kwasababu hakupewa hati ya umiliki wa kampuni.

Rugemalira hakuwa na kosa lolote kuuza hisa zake. Hapo ndo kamati haikuweka sawa mambo siasa ikapigwa zaidi. Kilichomgarimu ni kuwa mali yake alimuuzia mwizi aliyekwapua sehemu ya fedha za umma. Kama umeuza mali yako kwa mwizi huoni kama fedha aliyokupa itakuweka matatani?
 
Duuu hadi viongozi wa dini kwenye mgao?
Afu kesho wanakaa madhabauni ooh waumini tuwaombee viongozi wetu tuachane na wizi
mxxyuuuuuu!!! zao loh!
 
Kosa kubwa nililobaini ni kwamba SingaSinga alikuwa na hati ya mauziano ya Iptl ila hati ya umiliki hakuwa nayo. Kwa maana hiyo aliuziwa kampuni hewa kwasababu hakupewa hati ya umiliki wa kampuni.

Rugemalira hakuwa na kosa lolote kuuza hisa zake. Hapo ndo kamati haikuweka sawa mambo siasa ikapigwa zaidi. Kilichomgarimu ni kuwa mali yake alimuuzia mwizi aliyekwapua sehemu ya fedha za umma. Kama umeuza mali yako kwa mwizi huoni kama fedha aliyokupa itakuweka matatani?

Zitto alikosa hoja, hati ya mauziano ni tosha kabisa kuwa wewe ni mmiliki, si lazima kuwe na share certificates immediately.

Hata Mahakimu walilikubali na kutoa ruksa ya kuwa PAP ndiye sasa mmiliki wa IPTL kwa hizo hizo hati za mauziano.

Katika mlolongo wa hoja ya Zitto kuna mengi sana hakuyasema na kuna mengi kaya dramatize, moja wapo ni hili la hati za umiliki wa shares.
 
Zitto alikosa hoja, hati ya mauziano ni tosha kabisa kuwa wewe ni mmiliki, si lazima kuwe na share certificates immediately.

Hata Mahakimu walilikubali na kutoa ruksa ya kuwa PAP ndiye sasa mmiliki wa IPTL kwa hizo hizo hati za mauziano.

Katika mlolongo wa hoja ya Zitto kuna mengi sana hakuyasema na kuna mengi kaya dramatize, moja wapo ni hili la hati za umiliki wa shares.

Labda nikupe mfano halisi. Kuna mama alitaka kuniuzia kiwanja kwa hati ya mauziano ya serikali ya mtaa. Siku ya mauziano pale serikali ya mtaa nikadai ofa ile hati ya umiliki, mama akasema hati ya umiliki hana bali anayo hati ya mauziano baina yake na yule wa muuzaji wa awali na ameishi pale zaidi ya miaka 12 wala hakuwahi kubughudhiwa na serikali ikakiri kumtambua. Hati ya umiliki nikapewa jibu kuwa aliipoteza kwenye mafuriko ya jangwani.

Maelezo yake yakanipumbaza nikafanya malipo na kupewa hati ya mauziano ya serikali ya mtaa mbele ya mwenyekiti na ile ya awali waliouziana na mmiliki wa kwanza.

Kizaazaa kilikuja pale nilipoenda wizarani kuangalia namba ya kiwanja mmiliki wake ni nani. Nilikuta jina la mtu mwingine tofauti kabisa na haya majina mawili ya wamiliki waliotangulia. Kuna mtu toka 1996 ameandikwa ardhi kama mmiliki na huyo ndo anatambulika kama mwenye hati miliki. Kwahiyo huo ndo ulikua mwanzo wa kujua kama nilipigwa changa la macho.. na wale wamama mpaka leo wanajitetea kuwa ile ilikuwa ni sehemu yao ya halali. kibaya zaidi huyo anayesomeka wizarani kama mmiliki kila ninakouliza kuanzia wale wamama, serikali za mtaa na majirani kila mtu anadai kutokumfahamu huyo mtu na wala hawajawahi kumuona. Kwa maana hiyo inawezekana alijimilikisha kiwanja kile kwa njia zisizo sahihi lakini mkienda kwenye sheria yeye ndo atatambulika kama mmiliki halali kwani ndo mwenye hati miliki. Mpaka leo nimeogopa kujenga pale zaidi ya kuacha kajumba kadogo nilikonunuliana na kiwanja chake.

KUWA NA HATI YA MAUZIANO SHERIA HAIKUTAMBUI KAMA MMILIKI HALALI. HATI MILIKI NDIO KILA KITU.

Hapo ndio singasinga kapigwa changa la macho na Iptl. Labda nikuibie siri ya kufikirika. Inawezekana hati miliki mpaka sasa inamilikiwa na bank iptl alikochukua mkopo.
 
mimi bado napata wakati mgumu sn kuielewa hii report! Kutokana na maelezo ya report ya PAC wanadai pesa zilizokuwa kwenye ESCROW ACCOUNT ni za umma kwa mantiki kwamba ndani ya zile pesa kulikuwa na kodi iliyotakiwa kulipwa kwa serikali. Kwa maana hiyo basi ktk pesa ile kuna pesa za umma na zile za IPTL.

Nilitegemea kamati itatuainishia fedha halali ya umma ni kiasi gani na ile ya IPTL ni kiasi gani! Kwan kwa mujibu wa maelezo yao nidhahiri kuwa sio kweli pesa yote bilion 306 ni mali ya umma!!

Pia silioni kosa la SING SETH kwan TRA walipaswa kuujua mtaji halisi wa huyu jamaa ili alipe kodi kulingana na mtaji wake! Ni uzembe wa TRA kutokujua mtaji wa huyu jamaa na kujikuta akilipa kodi kidogo ukilinganisha na mtaji wake! Uzembe wao ulimpa fursa jamaa ya kupiga pesa.

Waziri mkuu hana hoja ya kujitetea coz kutokana na kauli zake za hapo nyuma juu ya sakata hili na isitoshe yeye ndio mtendaji mkuu wa serikali, mimi namuomba tu ajihudhuru in good faith hata km boss wake hataki.

TUNATAKA KUJUA KIASI CHA PESA ZA UMMA ZILIZOIBIWA KWA UZEMBE WA TRA.
 
Wakuu mimi napenda nipate list ya majina ya waliopokea mgawa kupitia Stanbic bank. Nasikia ni ndefu sana.
 
huyu singasinga akamatwe fasta mpuuz sana huyu maana kina kova walikuwa wanakula na kunywa nae sijui kama wataweza kumtia nguvuni na unaweza kukuta kashapotea tutaambiwaanatafutwa na interpol

hakamatwi ng'oo ujawajua matezi dume au unawaskia
 
CHENGE ANA ROHO MBAYA SANA ! PAMOJA na KUPIGA HELA NYINGI TENA ZA MARA KWA MARA LAKINI SIJAWAHI KUSIKIA AMECHANGIA KANISA , MSIKITI WALA SACCOS ! USIFANYE HIVYO BHANA .
 
Hata Yeye walimgusa, dua za watanzania zitamwepushia lolote juu yake, hata Mwakyembe alituasa kumwombea na akapona
 
Back
Top Bottom