Full Time: Yanga SC 1 - 3 Tabora United | NBC Premier League | Azam Complex | November 7,024

1. Sindano FC
2. Kinyesi FC
3. Manyani FC
4. Utopolo FC
5. Kandambili FC
6. Mihogo FC
7. Yebo yebo FC
8. Vidimbwi FC
9. Vyura FC
10. Vitenge FC

Baadaye..
 
Grahams sumbai mtoto kautaka agizeni Gahawa kwa Aaliyyah ntawalipia nyie wazee
Walikuwa wanataka majibu Kwa swali lao kwamba "Yanga hii itafungwaje"

Sasa majibu wameyapata kupitia vichapo vya 1-0 vs Azam FC

Na 3-1 vs Walina asali wa Tabora (Tabora United)

Kwa taarifa za ndaaani kabisa, wamepanga kumfukuza Gamondi wao kabla ya Christmas hii 🙌
 
Leo hawajachomwa sindano.Baada ya kushtukiwa kuhusu sindano za kuongeza nguvu hii ndio nguvu yao ya asili.Huu ni mwanzo tu.Na kufuru zenu za Ali Kamwe eti labda mfungwe na Mwenyezi Mungu.
Kama kuna MTU anaamini injinia amewekeza kwenye vipaji na ubora basi huyo MTU hayuko makini. Wakati anaongea na chombo kimoja cha habari kuhusiana na Chama alisema amemwambia aje Yanga Kule walikuwa wanamu overwork nini maana yake, Yanga iwe na wachezaji wazuri au wabaya ushindi ni lazima hakuna haja ya kutumia NGUVU kupata matokeo. Tumeanza kuyaona😂😂
 
Hahaha Mungu akuponye we mzee ila mpunguze mdomo...
 
Utopolo walizidiwa kila mahali, hata kwenye nyuzi! wameanzishiwa na mashabiki wa Simba.
cc; Vincenzo Jr , kiwatengu
 
Unapigwa Chuma 3 na Tabora vipi ukikutana na TP Mazembe!
Yao Yao Kwasi majeruhi
Bocca majeruhi
Baka ana nyekundu

Mabeki hao wote wameenda bench sasa Yanga imebakia haina mabeki kule nyuma amebakia Mwamnyeto tu

Kingine Yanga hawatulii uwanjani sijui kuna tatizo Diara magoli yanaingia hata haruki lile goli la kwanza limeingia hajaruka kaacha tu liingie angeruka hata angepangua lingekua sio goli na goli la pili pia hivyo hivyo na goli la tatu hakua anafuata mpira karibu magoli yote kwa hio Diarra bila mabeki hakuna kitu Yanga itaishia kufungwa tu Aucho amejitahidi sana kumsaidia Mwamnyeto pale ila haikuwezekana sababu Tabora walikua wanarudi wote nyuma kuziba goli ila Yanga wanawaachia Aucho na Mwamnyeto huku nyuma wengine hawarudi nyuma kwa hio Tabora wanakuja wengi wanajifungia tu

Kingine Pacome Aziz Ki Mudathir Mzize Chama Maxi Nzengeli Dube wakifika karibu na goli nje ya 18 wajaribu kutia mashuti walenge goli km alivyokua anafanya Sureboy alilenga mara 2 ila alikua anatoa nje hayakua yanalenga goli yale mashuti kwani nani aliewafundisha wakafungie ndani ya goli ndani ya 18 nani anawaambi wapasiane mpaka ndani ya 18 yaan wakafungie mbele ya kipa ndani ya 18 Gamond ndio anawalazimisha wafanye hivyo?

Mimi sikuelewa yaan wanakazana wakafungie ndani ya 18 kwanini wasifunge nje ya 18 wangepiga mashuti mengi nje ya 18 Tabora ingefungwa Yanga walikua na nafasi nyingi za kufunga ila mbinu waliyoitumia ndio imewafelisha Mwalimu kwanini anawalazimisha wakafungie ndani ya 18? Kwanini wasitie mashuti nje ya 18 pale kufunga kupo tu

Kingine Yanga wachezaji wakifika karibu na goli hawatulii kabisa yaan sijui niseme hawajiamini au namna gani ila hawatulii wakifika golini kufunga km wanashikwa na kitete sio Aziz Ki sio Pacome sio Dube sio Maxi yaan almost wote wakifika golini kufunga wanakua km wanakosa kujiamini hivi sasa sielewi hawa wachezaji wa Yanga wana matatizo gani?

Kidogo niliemuona Kibabage alikua anajituma sana na confidence za kutosha na Sureboy, Chama na Mzize nae kwa mbali walikua wametulia tatizo lilikua ni wakifika goli la Tabora Tabora wote wanajaa golini wote wanaziba goli wote ila kwa Yanga mpira ukifika golini kwa Yanga anaekuepo kuzuia ni Mwamnyeto na Aucho tu wengine wote hawarudi golini kuzuia wasifungwe hapo lazima mfungwe na Tabora walipoona hilo wakawa wanatumia mwanya huo huo kwenda kufunga na wanaenda wengi kule goli la Yanga yupo Aucho na Mwamnyeto tu ndio wanalinda goli kwanini msifungwe wakati mpo out numbered?

Wachezaji wa Yanga hawapo sawa kabisa kocha inabidi abadiri kikosi Aziz Ki Pacome Maxi hawa wasianze dakika 45 za kwanza inabidi watokee bench Chama Mzize na Dube inabidi waanze dakika 45 za kwanza Aziz Andambwile sijamuona jana Baleke aingizwe dakika za mwishoni zimebaki 20, 10 au 15 ndio aingizwe Nickson Kibabage Khalid Aucho ni bunduki za Yanga

Watu kwenye bandaumiza walikua wanasema Yanga pale nyuma haina beki mpaka nikasogelea TV nimtafute Mwamnyeto ndio nikamuona Bakari Nondo nikajiuliza hamna beki au hamna Mabeki?
 
Hahaha Mungu akuponye we mzee ila mpunguze mdomo...
Sasa tukipunguza midomo tutakula, kunywa na kuzungumza kwa kutumia nini bila kuwa na midomo yetu? Mdomo ni kitu cha muhimu sana katika maisha ya kila kiumbe; hata wewe una mdomo na huwezi kuupunguza. Tonge la ugali linalopita mdomoni mwangu haliwezi kupita kwenye midomo ya watu wengine.
 
Na bado golikipa namba moja WA Tabora aliumia akatoka wao wamekazania bacca, bacca😂 wakubali Jana ilikuwa siku mbaya kazini Tu🤓🤓
 
Na bado golikipa namba moja WA Tabora aliumia akatoka wao wamekazania bacca, bacca😂 wakubali Jana ilikuwa siku mbaya kazini Tu🤓🤓
Tatizo Yanga wanataka wakafunge ndani ya 18 siku ile Pacome alifunga nje ya 18 ndio wanatakiwa wafunge magoli ya vile haya magoli ya pasi pasi mpaka ndani ya 18 ni kupoteza muda tu nje ya 18 pale achia dongoooooo usilembeeeee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…