Fundisho la Utatu haliingii akilini kabisa, mnaoamini mmetoa wapi mbona Biblia iko wazi kabisa?

Fundisho la Utatu haliingii akilini kabisa, mnaoamini mmetoa wapi mbona Biblia iko wazi kabisa?

Kwani mtu mmoja hawezi kuwa na sifa au kufanya Kazi zaidi ya moja,
Kuwa na sifa au Kazi tendaji zaidi ya moja hakuondoi sifa ya kuwa wewe. John ni Mwalimu, ni mfanyabiashara, ni fundi na pia ni mkulima je hapa kuna John wangapi. Kwani kwenye Jamii hatuna watu wenye taaluma mbalimbali
 
Nasikitika sana kuona mtu anatetea fundisho la Utatu jambo ambalo ndani ya biblia halipo.

Upo ushahidi mwingi wa maandiko unaotofautisha Mungu, Yesu Kristo na Roho Takatifu ambayo waamini wa Utatu wanaita Roho Mtakatifu kama vile ni mtu. Je, Mungu anaonekana? Yesu alionekana, hakuna aliemuona Mungu hata Musa mwenyewe.

~ Andiko la Yoh 17:3 lina maana gani? Ikiwa Yesu ni Mungu?

~ Methali 8:30 ina maanisha nini?

~ Mwanzo 1:26 Mungu alikuwa akizungumza na nani?

Ningependa kupata majibu ya maandiko, jibu hoja kwa andiko ili tuamini unachosema. Maandiko yapo mengi sana yanayo tifautisha Mungu, Yesu na roho/nguvu ya Mungu ya utendaji.
Wewe bana ungetuacha tu na imani yetu.

Kama tumeweza kuamini kua huyu muigizaji hapa chini ndio mfano wa Yesu hivyo tukamchonga kwenye sanamu na kumuweka madhabahuni basi lisikusumbue sana swala la utatu.

Linapokuja swala la imani sisi hua tunawapa akili zetu wakuu wetu wa dini wafikirie kwa Niaba yetu, halafu watakachoamua wao basi sisi hufuata bila kuuliza.
FB_IMG_16718383153941311.jpg
 
BIBLIA INAFUNDISHA NINI JUU YA UTATU?
JIBU.

Mungu ni mkubwa kuliko sisi na tusitarajie kumuelewa katika kila jambo. Utatu ni jambo gumu kulieleza kwa kina. Hakuna mwanadamu anayeweza kulielewa kwa undani zaidi. Biblia inafundisha kuwa Baba ni Mungu, ya kuwa Yesu ni Mungu na pia Roho mtakatifu ni Mungu. Biblia pia inafundisha kuna Mungu mmoja tu. Ijapokuwa tunaweza kufahamu uhusiano tofauti tofauti wa sehemu za utatu huu ni vigumu kuelewa kwa akili ya kibinadamu. Hii haimaanishi kuwa si kweli au si maagizo ya Biblia.

Utatu ni Mungu mmoja katika nafsi tatu. Aya za biblia zifuatazo zitatumika kufafanua neno hili.

1) Kuna Mungu mmoja: kumbukumbu la torati 6:4; wakorintho wa kwanza 8:4; wagalatia 3:20; Timotheo wa kwanza 2:5.

2) utatu una nafsi tatu: mwanzo 1:1; 1:26; 3:22; 11:7 Isaya 6:8; 48:16; 61:1; Mathayo 3:16-17; Mathayo 28:19; wakorintho wa pili 13;14. Katika mwanzo 1:1 neno la wingi “Elohim” linatumika. Katika mwanzo 1:26; 3:22; 11:7 na Isaya 6:8, neno la wingi “sisi” limetumika. Kwa hivyo neno “Elohim’ na “sisi” kumaanisha zaidi ya mmoja halina pingamizi.

Katika Isaya 48:16 na 61:1, Mwana azungumza huku akihusisha Baba na Roho Mtakatifu. Fananisha Isaya 61:1na Luka 4:14-19 kuona Mwana akizungumza. Mathayo 3:16-17 inaelezea ubatizo wa Yesu. Anayeonekana hapa ni Mungu Roho mtakatifu akimshukia Mungu Mwanahuku Mungu Baba akitangaza furaha yake katika Mwana. Mathayo 28:19 na wakorintho wa pili 13:14 ni mifano ya nafsi tatu katika Mungu mmoja.

3) Nafsi hizi tatu zinatambulika katika maandiko. Katika agano la kale “ BWANA” linatofautishwa na “Bwana” (mwanzo 19:24; Hosea 1:4). “BWANA” ana “Mwana” (zaburi 2:7, 12; Methali 30:2-4). Roho anatofautishwa na “BWANA” (hesabu 27:18) na pia kutoka “Mungu” (zaburi 51:10-12). Mungu mwana atofautishwa na Mungu Baba (zaburi 45:6-7; waebrania1:8-9). Katika agano jipya, Yohana 14:16-17 ndipo Yesu anazungumza na Baba juu ya kuleta Msaidizi, Roho mtakatifu. Hii ina maana ya kuwa Yesu hakujichukulia yeye mwenyewe kuwa Baba wala Roho Mtakatifu. Katika kila mahali ndani ya agano jipya Yesu alipozungumza na Mungu Baba alikuwa akizungumza na nafsi moja wapo ya Utatu – Baba.

4) kila nafsi katika utatu huu ni Mungu: Baba ni Mungu: Yohana 6:27; warumi 1:7; petro wa kwanza 1:2. Mwana ni Mungu: Yohana 1:1, 14; warumi 9:5; wakolosai 2:9; waebrania 1:8; Yohana wa kwanza 5:20. Roho mtakatifu ni Mungu: Matendo ya mitume 5:3-4; wakorintho wa kwanza 3:16 (anayedumu ndani ni Roho mtakatifu –warumi 8:9; Yohana 14:16 –17; Matendo ya mitume 2:1—4).

5) Katika mpangilio ndani ya utatu huu: maandiko yanaonyesha kuwa Roho Mtakatifu humtumikia Baba na Mwana na Mwana humtumikia Baba. Huu ni uhusiano wa ushirika wao wala hupunguzi uungu wa nafsi yoyote ile. Kuhusu Mwana tazama: luka 22:42; Yohana 5:36; Yohana 20:21; Yohana wa kwanza 4:14. kuhusu Roho Mtakatifu tazama Yohana 14:16; 14:26; 15:26; 16:7 na hasa Yohana 16:13-14.

6) Majukumu ya kila nafsi katika utatu: Baba ndiye aliyesababisha kuwako kwa 1) ulimwengu (wakorintho wa kwanza 8:6; Ufunuo wa Yohana 4:11), 2) ufunuo wa kimungu (Ufunuo wa Yohana 1:1) 3)wokovu (Yohana 3:16-17); Matendo ya kibinadamu ya Yesu ( Yohana 5:17; 14:10). Baba anaonekana kwanza katika haya yote.

Mwana ni wakala ambaye Baba humtumia kufanyia haya: 1) Kuumba na kustawisha ulimwengu (wakorintho wa kwanza 8:6; Yohana 1:3; wakolosai 1:16-17); 2) ufunuo wa kimungu (Yohana 1:1; Mathayo 11:27; Yohana 16:12-15; Ufunuo wa Yohana 1:1); na 3) wokovu ( wakorintho wa pili 5:19; Mathayo 1:21; Yohana 4:42). Baba alifanya mambo haya yote kupitia Mwana anayetenda kazi kama mwakilishi wake.

Roho Mtakatifu ndiye anayetumiwa na Baba kufanya haya: 1) uumbaji na ustawishaji wa ulimwengu (mwanzo 1:2; Ayubu 26:13; zaburi 104: 30); 2) ufunuo wa kimungu (Yohana 16:12-15; waefeso 3:5; petro wa pili 1:21); 3) wokovu (Yohana 3:6; Tito 3:5; petro wa kwanza 1;2); na 4) matendo ya Yesu ( Isaya 61:1; Matendo ya mitume 10;38). Haya yote Baba ayatenda kupitia Roho Mtakatifu.

Baba, Mwana na Roho si vipande vya Mungu bali kila nafsi ni Mungu. Mungu asiyeonekana na macho hawezi kuelezwa kwa usahihi na mwenye kuona na macho ya kibinadamu akaeleweka. Lakini katika hali zote tazama Mungu kama nafsi tatu zisizogawanyika kuwa Miungu mitatu bali Mungu mmoja tu. “jinsi zilivyo kuu utajiri wa hekima na maarifa ya Mungu! Hukumu zake hazichunguziki, wala njia zake hazitafutikani! Maana ni nani aliyeijua nia ya Bwana?” 9 warumi 11:33-34)
 
Wewe bana ungetuacha tu na imani yetu.

Kama tumeweza kuamini kua huyu muigizaji hapa chini ndio mfano wa Yesu hivyo tukamchonga kwenye sanamu na kumuweka madhabahuni basi lisikusumbue sana swala la utatu.

Linapokuja swala la imani sisi hua tunawapa akili zetu wakuu wetu wa dini wafikirie kwa Niaba yetu, halafu watakachoamua wao basi sisi hufuata bila kuuliza.
View attachment 2456633
Nani kakuambia huyu Brian Decon raia wa UK toka lini akawa ndie Yesu
 
Ndio nimemaliza, mpangilio huu wa ulimwengu lazima una mwanzo, au mbunifu aliyefanya hiyo kazi, bila shaka ni Mungu hakuna anayeweza kufanya aliyofanya

Hoja yako ya kwamba mpangilio huu lazima una mwanzo, na bila shaka mwanzo huo ni Mungu ina mapungufu mengi.

Kwanza umelazimisha kwa kuweka "bila shaka" bila kuelezea kwa nini iwe "bila shaka".

Una hakika gani chanzo cha ulimwengu huu ni Mungu?

Ulimwengu kulazimika kuwa na chanzo haina maana kwamba chanzo ni lazima kiwe Mungu.

Yani ni hivi, wewe muafrika kulazimika kuwa na baba, kwamba haiwezekani uwepo bila kuwa na baba mzazi, haimaanishi automatically baba yako ni Donald Trump aliyekuwa rais wa Marekani, mzungu.

Hoja uliyoitoa hapo ni sawa na kusema kwamba wewe muafrika, baba yako mzazi ni Donald Trump, mzungu. Kwa sababu wewe ni lazima uwe na baba.

Hata kama ni lazima uwe na baba, hilo halithibitishi baba yako ni Donald Trump. Thibitisha baba yako ni Donald Trump.

Hata kama ulimwengu ni lazima uwe na mwanzo, hilo halimaanishi mwanzo wake ni lazima uwe Mungu. Thibitisha mwanzo wake ni Mungu, usilazimishe hili kwa nguvu tu.

Hili la kwanza.

La pili,

Ukisema kitu chochote chenye mpangilio/complexity ni lazima kiwe na muumbaji, kimsingi unajiwekea mtego wa kuulizwa na Mungu naye ni complex, hivyo naye lazima atakuwa na muumbaji, na muumbaji wake naye ana muumbaji, na muumbaji wake ana muumbaji, ad infinitum, ad nauseam.

Yani ukishasema kila kilicho na mpangilio na complexity kinahitaji muumba, umeshakubali hakuna Mungu. Kwa sababu kila Mungu utakayemuweka atahitaji kuwa ameumbwa na Mungu/ kitu kingine, na akishaumbwa na Mungu au kitu kingine tu, anakuwa si Mungu.

Kwa hivyo, hii hoja ya kusema kwamba mpangilio wa dunia unathibitisha kuna Mungu, ni hoja ambayo inaweza kuonekana ya maana kwa mtu asiyefikiri kwa kina tu.

Kwa mtu anayefikiri kwa kina hii si hoja ya kutetea uwepo wa Mungu.

Kwa mtu anayefikiri kwa kina, hii hoja inaonesha Mungu muumba vyote hawezi kuwapo.
 
Inaoneka haujui utatu mtakatifu(MUNGU)
MUNGU ni kama raisi . U-Raisi umetengenezwa na vyeo vitatu raisi mwenyewe , makamu raisi na waziri mkuu
MUNGU imetengenezwa na vyeo vitatu
I - JEHOVAH (MUNGU Baba) yeye huwa haonekani
II - Yesu / Masihi ( MUNGU Mwana ) yeye ndiye kiumbe cha kwanza kuumbwa , ndo mana anajulikana kama kaka wa kila kilicho umbwa na ndiye yeye pia alishiriki katika uumbaji wa mbingu(malaika) na dunia(wanadamu)
III Roho Mtakatifu (MUNGU Roho) - Roho ya Mungu ina act kama kiumbe. Huja kwa maumbo mbalimbali - kama nguvu , kama mwanadamu , kama njiwa
kati ya Yehova na Yesu aliye muumba mwenzake nani?
Na kati ya Yehova na Roho mtakatifu anaye tumwa na mwenzake nani?
 
MUNGU ni kama raisi . U-Raisi umetengenezwa na vyeo vitatu raisi mwenyewe , makamu raisi na waziri mkuu
MUNGU imetengenezwa na vyeo vitatu
I - JEHOVAH (MUNGU Baba / MUNGU Mwenyewe) yeye huwa haonekani
II - Yesu / Masihi ( MUNGU Mwana ) yeye ndiye kiumbe cha kwanza kuumbwa , ndo mana anajulikana kama kaka wa kila kilicho umbwa na ndiye yeye pia alishiriki katika uumbaji wa mbingu(malaika) na dunia(wanadamu)
III - Roho Mtakatifu (MUNGU Roho) - Roho ya Mungu ina act kama kiumbe. Huja kwa maumbo mbalimbali - kama nguvu , kama mwanadamu , kama njiwa

Kwa maelezo yako ya mafano wako inamaana
JEHOVA ni kama RAISI
Yesu/masiha ni Kama MAKAMU WA RAISI
Roho mtakatifu ni Kama WAZIRI MKUU
 
kati ya Yehova na Yesu aliye muumba mwenzake nani?
Na kati ya Yehova na Roho mtakatifu anaye tumwa na mwenzake nani?
Yehova ni Baba - ndiye aliyemuumba Yesu
Roho Mtakatifu yupo chini ya Yesu , ni nafsi ya tatu ya MUNGU

Yehova(MUNGU Baba) huukaa katika kiti cha enzi , hutoa maagizo kwa Yesu na Yesu hutoa maagizo kwa Roho Mtakatifu
 
Kuna majamaa walijenga mnara kumfuata Mungu wakadondoshwa, wangekuwepo wangekupa majibu sahihi!
Mimi nina SIMULIZI ya jamaa aliyefanya kila aina ya miujiza kumtafuta MUNGU akihusisha UCHAWI wa aina wote ulopata kuhusikia hapa DUNIANI
alifika kila pembe ya DUNIA
kumtafuta MUNGU
alifika mpk katika SAYARI zingine kuonana na VIUMBE walopata kuishi kabla ya ADAM
 
Yehova ni Baba - ndiye aliyemuumba Yesu
Roho Mtakatifu yupo chini ya Yesu , ni nafsi ya tatu ya MUNGU

Yehova(MUNGU Baba) huukaa katika kiti cha enzi , hutoa maagizo kwa Yesu na Yesu hutoa maagizo kwa Roho Mtakatifu
Kwa hiyo ni kitu/mtu mmoja au tofauti ?
 
Nasikitika sana kuona mtu anatetea fundisho la Utatu jambo ambalo ndani ya biblia halipo.

Upo ushahidi mwingi wa maandiko unaotofautisha Mungu, Yesu Kristo na Roho Takatifu ambayo waamini wa Utatu wanaita Roho Mtakatifu kama vile ni mtu. Je, Mungu anaonekana? Yesu alionekana, hakuna aliemuona Mungu hata Musa mwenyewe.

~ Andiko la Yoh 17:3 lina maana gani? Ikiwa Yesu ni Mungu?

~ Methali 8:30 ina maanisha nini?

~ Mwanzo 1:26 Mungu alikuwa akizungumza na nani?

Ningependa kupata majibu ya maandiko, jibu hoja kwa andiko ili tuamini unachosema. Maandiko yapo mengi sana yanayo tifautisha Mungu, Yesu na roho/nguvu ya Mungu ya utendaji.
The fourth looks like a son of a living God Almighty

Daniel 3:19-27
 
Nasikitika sana kuona mtu anatetea fundisho la Utatu jambo ambalo ndani ya biblia halipo.

Upo ushahidi mwingi wa maandiko unaotofautisha Mungu, Yesu Kristo na Roho Takatifu ambayo waamini wa Utatu wanaita Roho Mtakatifu kama vile ni mtu. Je, Mungu anaonekana? Yesu alionekana, hakuna aliemuona Mungu hata Musa mwenyewe.

~ Andiko la Yoh 17:3 lina maana gani? Ikiwa Yesu ni Mungu?

~ Methali 8:30 ina maanisha nini?

~ Mwanzo 1:26 Mungu alikuwa akizungumza na nani?

Ningependa kupata majibu ya maandiko, jibu hoja kwa andiko ili tuamini unachosema. Maandiko yapo mengi sana yanayo tifautisha Mungu, Yesu na roho/nguvu ya Mungu ya utendaji.
Kumbe fundisho haliingii akilini!
Soma hapa liingie Akilini kabla hujafa!
[emoji116][emoji116]
2.NAFSI TATU ZA MUNGU KATIKA BIBLIA

Katika MWANZO 1:1, tunaona hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi. Neno hili kwa kiebrania linaitwa ELOHIM Mwenye nguvu. Neno hili linatajwa katika Agano la kale pekee yake mara elfu mbili mia saba ( 2700 ).Sasa tuaangalia mifano ya matumizi ya dhahiri yanayoonyesha wingi katika UMOJAwa Mungu. MWANZO 1:26; MWANZO 3:22; MWANZO 11:5-7, wingi huo unaojitokeza pia katika kila kitabu cha Agano Jipya

IFUATAYO NI MISTERI AMBAYO MAHALI PAMOJA WAMETAJWA, BABA, MWANA, ROHO MTAKATIFU, IKIONYESHA WAZI KUWA NI NAFSI TATU TOFAUTI.

( MATHAYO 3:16-17; MATHAYO 28:19; YOHANA 14:16-17; MARKO 1:10-11; LUKA 1:32-35; LUKA 24:49; MATENDO 1:7-8; MATENDO 7:55-56; MATENDO 10:38-40; WAEFESO 3:14-17; 1WATHESALONIKE 1:1-5; 1PETRO 1:2-3; 1YOHANA 5:7-8; YUDA 1:20-21; UFUNUO 1:4-6 ).

Ifuatayo tena ni mistari ambayo mahali pamoja wametajwa Baba na Mwana au

Baba na Roho Mtakatifu au Mwana na Roho Mtakatifu ikionyesha wazi kuwa ni nafsi tatu tofauti. ( MARKO 13:32; YOHANA 1:18; YOHANA 5:17, 19-23; 1 WAKORINTHO 1:4; 1 WAKORINTHO 2:10; 1WAKORINTHO 1:2-3; WAGALATIA 1:1-4; WAFILIPI 1:1-3; WAFILIPI 1:2; WAFILIPI 2:9-11; WAKOLOSAI 1:2-3; WAKOLOSAI 3:1; 1WATHESALONIKE 3:13; 2WATHESALONIKE 1:1-2; 2WATHESALONIKE 2:16; 1TIMOTHEO 1:2; 2TIMOTHEO 1:2; 2TIMOTHEO 4:1; TITO 1:4; WAFILIPI 1:3; WAEBRANIA 1:5; WAEBRANIA 13:20; YAKOBO 1:1; 2YOHANA 1:3; UFUNUO 2:7; UFUNUO 21:22-23; UFUNUO 22:1-3 ).
 
Kumbe fundisho haliingii akilini!
Soma hapa liingie Akilini kabla hujafa!
[emoji116][emoji116]
2.NAFSI TATU ZA MUNGU KATIKA BIBLIA

Katika MWANZO 1:1, tunaona hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi. Neno hili kwa kiebrania linaitwa ELOHIM Mwenye nguvu. Neno hili linatajwa katika Agano la kale pekee yake mara elfu mbili mia saba ( 2700 ).Sasa tuaangalia mifano ya matumizi ya dhahiri yanayoonyesha wingi katika UMOJAwa Mungu. MWANZO 1:26; MWANZO 3:22; MWANZO 11:5-7, wingi huo unaojitokeza pia katika kila kitabu cha Agano Jipya

IFUATAYO NI MISTERI AMBAYO MAHALI PAMOJA WAMETAJWA, BABA, MWANA, ROHO MTAKATIFU, IKIONYESHA WAZI KUWA NI NAFSI TATU TOFAUTI.

( MATHAYO 3:16-17; MATHAYO 28:19; YOHANA 14:16-17; MARKO 1:10-11; LUKA 1:32-35; LUKA 24:49; MATENDO 1:7-8; MATENDO 7:55-56; MATENDO 10:38-40; WAEFESO 3:14-17; 1WATHESALONIKE 1:1-5; 1PETRO 1:2-3; 1YOHANA 5:7-8; YUDA 1:20-21; UFUNUO 1:4-6 ).

Ifuatayo tena ni mistari ambayo mahali pamoja wametajwa Baba na Mwana au

Baba na Roho Mtakatifu au Mwana na Roho Mtakatifu ikionyesha wazi kuwa ni nafsi tatu tofauti. ( MARKO 13:32; YOHANA 1:18; YOHANA 5:17, 19-23; 1 WAKORINTHO 1:4; 1 WAKORINTHO 2:10; 1WAKORINTHO 1:2-3; WAGALATIA 1:1-4; WAFILIPI 1:1-3; WAFILIPI 1:2; WAFILIPI 2:9-11; WAKOLOSAI 1:2-3; WAKOLOSAI 3:1; 1WATHESALONIKE 3:13; 2WATHESALONIKE 1:1-2; 2WATHESALONIKE 2:16; 1TIMOTHEO 1:2; 2TIMOTHEO 1:2; 2TIMOTHEO 4:1; TITO 1:4; WAFILIPI 1:3; WAEBRANIA 1:5; WAEBRANIA 13:20; YAKOBO 1:1; 2YOHANA 1:3; UFUNUO 2:7; UFUNUO 21:22-23; UFUNUO 22:1-3 ).
Endelea kutubariki na Nondo makini kama hizi.


Kuna mabwege wanaamini same sex marriage at the same time wanasherekea Christmas.

Ina akisi confusion 100%+.

Baadhi yetu tunao-amini kwenye haya maandiko inatufaa mno.
 
Back
Top Bottom