Fursa/ kazi watu wanapiga pesa ndefu na hazijastukiwa na wengi

Fursa/ kazi watu wanapiga pesa ndefu na hazijastukiwa na wengi

Binafsi me ni msomi na Kwa Sasa nimejiajiri katika kilimo.
Kama kawaida kilimo Kuna kipindi tunapata Kuna kipindi hali inakuwa mbaya mno

Kuna fursa au taaluma zinalipa Kwa vijana, Ile kijana kusomea kupasua miamba, sijui doctor wa ubongo, sijui ualimu wa physics umalize ukose kazi au ulipwe laki 5 huo ni upumbavu

Baadhi ya fursa
1. Upishi/ chef
Hawa wapishi unaweza kijiajiri au kuajiriwa na ukapiga pesa ambayo hata polisi, mwalimu, doctor, mhasibu hawezi pata
Wapishi wanaofanya caterings wanalipwa mkwanja ukiambiwa hutakubali
Akihudumia harusi, majibu, au tukio malipo ni million 10+
Kuna watu wanafanya bakery 🥯 🧁 wanapiga hela, hata walimu wanaotoa tamko wanaipata siku 1
Jitahidi kumiliki hata bakery ndogo tu mtaani, ukiuza mikate 100 , keki, mandazi ni pesa ndefu
Kuna chefs wameajiriwa Zanzibar na Migodini na mahoteli makubwa wanalipwa million 10 ambayo hakuna mtumishi wa umma anapata

2. Mapambo
Hawa wapambaji wanapiga pesa ndefu
Hapa kikubwa uwe na vifaa vyote
Uzuri wa mapambo shughuliza harusi, misiba, mikutano n.k Huwa haziishi

3 mechanics/ garage
Hapa ni ufundi na uaminifu
Vyombo vya moto kama magari na pikipiki ni nyingi na Zina magonjwa yasiyoisha
Ukijitega vizuri ukawa fundi mzuri na ukawa na duka la spear utapiga pesa wakukimbie hata mtumishi wa umma hawezi pata pamoja na kuchomokea mashati na kuweka pen mfuko wa shati

4. Urembo wa magari
Hawa watu wa stika, taa, rangi na seat covers wanapiga pesa kirahisi mno

5. Ufundi simu
Kuna dogo langu yupo kariakoo ni fundi simu alinipa code kuwa Kwa siku ana uweZo Kwa kukunja 200k na hiyo ni uhakika.
Akiuzwa vio, betri na k solve matatizo madogo ya simu
Kama mtaji upo kuagiza simu Zanzibar na kuuza uku unapiga pesa ndefu

6 MC wa harusi
Hapa inahitaji kipaji na kupiga Domo haswaa, ukiwezea utapiga pesa hadi wakuroge

7. Usafirishaji
Hapa kupiga bolt au Uber
Kuna jamaa angu alinunua Raum yake million 8 alinambia kuwa anapata si chini ya laki 2 Kwa siku, hapa tatizo ni gari kupata magonjwa na Huwa inachukua pesa
Jaribu kununua gari zima utapiga pesa hadi ushangae
Sijagusia bajaji na bodaboda
Usafiri Kwa Sasa ni hitaji la muhimu sana

8 ulinzi
Kama una uweZo wa kumiliki kampuni ya ulinzi
Watu wanahitaji usalama, hapa utapiga pesa

9.Ushonaji
Hapa ukiwa fundi mkubwa na ukawa na vitambaa, utapiga pesa sana
Kuna marafiki zangu huko Dar es salaam ni mafundi wa cherehani lakini wanapiga pesa ambayo watumishi wa umma na mikopo Yao hawawafikii

10. Biashara ya mazao/nafaka
Mazao hayaozi kama matunda
Yanapanda bei Toka mavuno
Hapa ni msuli wa kuhifadhi tu

Vile vile Biashara ya viazi vya Chips
Kuna mchizi wangu nilisoma nae pale SAUT ndo harakati zake
Yeye Huwa anafuata mzigo huko Mbeya na anapeleka Dar alinambia kuwa hii biashara haijawahi kumtupa yaani akifikisha mzigo sokoni hatumii madalali Bali watu wanakimbilia wenyewe

Wale wasomi wenzangu tuweke vyeti pembeni tukomae na mtaa
Wale walimu wasio na ajira wanaoandamana ili kupata kazi ya kulipwa laki 5
Fursa hizo nimepeni bure
Na wale WA barabarani sinza/kinondonj
wanaingixa 50000-100000 per day
Omba KIBALI
Mwaka WA kumiliki na KUTAWALA
Kujiongeza
 
Mkuuu KUNA Mdada ma best SIJAWAHI trmbra nae na ana befriend

NAmhifadhia helà zake nikikwambia pesa anayonipa siku nyingine nimhifadhie n mshahara WA mtu serikalini mkuu

Mpaka namtaniaga umempiga mhindi nn...YAAN min n 60000...
 
Back
Top Bottom