Fursa za Nje ya Nchi: Scholarship (kusoma), Ajira/kujiajirina Biashara/kuwekeza

Unachokisema ni kweli. Lakini bafo inawezekana .. ni wewe tu na jinsi gani unchat na muhusika wako , kuna wayu akili hazijakuwa anachata na mchuchu anamuomba hela sasa utaachaje kuonekana tapeli hahahahaha
west african wametuharibia sana. Waafrica hatuaminiki kwa sababu ya tabia zao za kishenzi
 
Mkuu, Vibali gani inahitajika kuwa na vyo ili uweze ku export bidhaa nje?

Namna gani unaweza kupata masoko/wateja nchi za nje?
 
Kuna vigezo vingi wanaangalia hiyo ya experience ni kigezo kimoja wapo kisha wanacalculate credits.
Baadhi ya vigezo ni;
Education level
Experience
Age
Language profficiency(English/French)
Uko sawa kabisa mkuu! Canada wanacaluclate marks ukikidhi hivi vigezo unakuwa kwenye nafasi nzuri zaidi
 
oi ma bro naombeni mnisaidie kutengeneza cv
Yes ni jambo zuri sana maana kampuni nyinine za nje hziz cv zetu format yake hawazielewi kabisa ..
Mtu anaorodhesjha hadi primary school wakati ana level nyingj kubwa tu za elimu na skills..

Marital status , dini..

Kiufupi zjnakuwa n information nyingi ambazo haya makampuni hayaiziitaji kabla hawajakupatia kazi
 
Asante kwa tag, naomba mwenye taarifa ya namna ya kuingia Canada au mchongo wa wazi anijuze l...nasema wa wazi mfano kupitia scholarship etc. maana siku hizi kupigwa kwingi
 
Asante kwa tag, naomba mwenye taarifa ya namna ya kuingia Canada au mchongo wa wazi anijuze l...nasema wa wazi mfano kupitia scholarship etc. maana siku hizi kupigwa kwingi
Level ya Masters/phd ?
 
mtamba b
 
Kikwazo ni IELTS mkuu ni gharama sana.
 
Kikwazo ni IELTS mkuu ni gharama sana.
Ni kweli Mkuu. Ila kuna mitihani ya umahiri wa lugha ya kiingereza (English Proficiency Tests) inayotolewa na UDSM ambayo gharama zake ni chini zaidi. Ila lazima pia uangalie kama mitihani na cheti utakachopata vinatambuliwa na chuo au fursa utakazotuma maombi.

Vilevile, kipindi hiki cha janga la UVIKO, kuna baadhi ya nchi na vyuo vimeondoa uthibitisho wa umahiri wa lugha kama shahada ya kwanza ulisomea kwa lugha ya kiingereza.

Usikate tamaa mkuu.
 
oi ma bro naombeni mnisaidie kutengeneza cv
Inategemea unataka CV ya aina gani na kwa matumizi gani:

1. Kama ni ya kawaida tumia Microsoft Word au hata LinkedIn zinakupa muongozo wa kinachohitajika kuandaa CV. Ukimaliza inakutengenezea hapo hapo.
Kama unataka CV zenye madoido na nakshi za kileo: Hizi ni programu mahiri za kuandaa:
Best CV builders in 2021
  • Resume.com.
  • ResumUP.
  • CakeResume.
  • Reed.co.uk.
  • Novoresume.
  • ResumeHelp.
  • CVmaker.
  • VisualCV.

2. CV zozote unaandaa kutokana na matumizi. Kama unaomba kazi hakikisha unaweka taarifa itakayohitajika na ofisi au kazi unayoiombea. Usitumie CV moja kuomba kila aina ya kazi.

3. Hakikisha CV yako ni rahisi kuelewa bila kuweka vifupi au maneno magumu, isipokuwa kama unauhakika atakayeisoma ataelewa. CV zenye taarifa nyingi zinashauriwa kwa watu wanaowasilisha kwaajili ya consultancy. Kama ni maombi ya kazi, usiweke CV ndefu sana, kurasa mbili zinatosha kabisa.
 
Ni kweli kwasasa baadhi ya byuo wanaangalia kama ulisoma bachelor na lugha iliyotumika kufundishia ni kiingereza basi unakuwa unakidhi vigezo
 
Asante kwa tag, naomba mwenye taarifa ya namna ya kuingia Canada au mchongo wa wazi anijuze l...nasema wa wazi mfano kupitia scholarship etc. maana siku hizi kupigwa kwingi
Canada: Scholarships for Non-Canadians

Ni rahisi kuhakiki taarifa yoyote kuhusu fursa katika nchi nyingine kupitia balozi zao. Siku zote kama una mashaka na fursa tuma email kwa ubalozi wao nchini au ubalozi wenye uwakilishi wa hiyo nchi na watakuhakikia. Ni moja ya jukumu lao pia.
 
Mm natamani nipate permit ya resident na work permit huko canada
Yaani nipate ili nikiona nikiomba iwe rahis kupata kwasababu nina kibali cha makaz na cha kufanya kazi
Hii inawekana wakuu?
 
Mm natamani nipate permit ya resident na work permit huko canada
Yaani nipate ili nikiona nikiomba iwe rahis kupata kwasababu nina kibali cha makaz na cha kufanya kazi
Hii inawekana wakuu?
Binafsi, mimi sijakuelewa mkuu... andika tena pole pole
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…