TANZIA Gardner G Habash mtangazaji wa Clouds Media afariki dunia

TANZIA Gardner G Habash mtangazaji wa Clouds Media afariki dunia

Mtangazaji Mahiri wa Clouds FM, Gadner G. Habash (50) amefariki Dunia Leo April 20, 2024.

Gadner maarufu kama ‘Captain’ aliejizolea Umaarufu Mkubwa kupitia Kipindi cha Jahazi, alikua amelazwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Jijini Dar es Salaam kutokana na kusumbuliwa na Pressure (Shinikizo la Damu).

Wasafi Media Tunatoa Pole kwa Familia , Clouds Media Group , Ndugu Jamaa na Marafiki . Mungu ailaze Roho yake Mahali Pema Peponi Amein

Wasafi Media

View attachment 2968923

Pia soma
- Mtangazaji Captain G. Habash alazwa JKCI kwa tatizo la Shinikizo la Damu
Rip
 
Huyo mlevi na chapombe ulevi umeigharimu afya yake

Endeleeni kunywa na kujishindilia mi bia na miAlcohol kupitiliza kwa makusudi muue figo na maini

Mjifariji kwa kusema Kufa ni kufa

Mnamuona Dr Janabi ni Punguani hajui starehe anapowapa ushauri
 
Rip, much respects!
IMG_20240420_100746_626.jpg
 
Sasa inakuwaje kuna watu life style yao ni nzuri, hawatumii vileo, anasa zozote ila wamekufa vijana tu na kuna mwamba hapo juu kasema babu yake anakunywa gongo na ana 98 years?

Kifo ni fumbo mjomba, siku ile unazaliwa amini ulizaliwa na destiny yako, duniani hakuna kuishi kwa kubahatisha au ku dictate ufe lini ndugu.
Wewe endelea kufanya rationalisation tuu, kifo ni lazima lakini biblia inaongea miaka 70 angalau. Wewe unaua viungo vyako kama moyo, figo, ini na mapafu kwa pombe na sigara unakuja ku justify eti kifo ni kifo tuu. Kufa kizembe na miaka 30- 40 unajua ni hasara gani unaacha kwa wategemezi wako. Nyie mliokata tamaa na maisha msitafute wafuasi.

Huo mfano unaotumia wa mtu 1 sio realistic nenda kafanye tafiti expose watu 10 kwenye gongo kwa miaka 10 ndio uje utoe majibu ya tafiti yako kuwa ni wangapi wamebaki bila madhara.
 
Mungu atupe mwisho Mwema! Sote tutakufa
Lavit njalas Miss_Mariaah machiaveli granitized OscarkambonaJr Lethergo magnifico min -me
Sikuwahi kumuona live baba wa watu nimeropoka tu, sijui kama alikua anakunywa au hapana
nipuuzieni..!
Bila sisi kunywa nchi itapitia kipindi kigumu sana , pombe haijawahi kuua mtu ila maamuzi ya mtu kuelekea pombe ndio yanaua .

yani ni kama kisu tu uamue kukatia mboga au kujichinja nacho , apo tatzo ni kisu au ni huyo mtu alie amua kutumia kisu vibaya?
 
Back
Top Bottom