Gaudensia Kabaka Mwenyekiti wa UWT?

Gaudensia Kabaka Mwenyekiti wa UWT?

Ujuaji mwingi kumbe ni kolo. Mimi nipo serikalini, nimejaza history sheet ya mkataba wa ajira. Wewe ndio bado unaomba kazi tutaelewana? Subiri upate ajira kwanza halafu uje ubishe.
Uongo Tena mkubwa.Weka hiyo sheet plain tuoone hayo mambo Hakuna .Huyo aliyekujazisha ni wa ofisi ipi.Weka wazi ni kitu serious hayo mambo hayapo. weka jina la taasisi hapa.
 
Ila udom ilizidi udini enzi hizo, hafu hizi mambo za dini mbona akiingia Rais mwislamu ndio zinaanza chokochoko, maana waja wamsagia kunguni mama wa watu, pia taasisi za umma why ujenge nyumba ya ibada ya aina moja tu wakati hyo ni taasisi ya umma ka si ujinga nini
Kwa bahati mbaya baadhi ya wenzetu hawa akili zao hazina tofauti na za Wataliban wa Afghanistan wanatamani sana Tanzania iwe Islamic Republic - Watanzania wote wa jinsia ya kike wavae hijabu, wanaume wasinyoe ndevu,wavae mapajama,kanzu na vilemba kichwani - ajabu sana!!

Tungetegemea wenzetu wazungumzie masuala ya maendeleo ya madhehebu yao ya kidini, mfano: ujenzi wa mashule na vyuo vya ufundi na vyuo vikuu, Hospitali, vitega uchumi nk at least wajaribu kuiga wenzao wa madhehebu ya kikristo kuliko baadhi yao wenye itikadi kali kupoteza muda wakilalama ovyo kwa kutunga madai yasiyo kuwa na kichwa wala miguu masaa yote kuangalia wangapi wamepewa nyadhifa Serikalini, mbona wakati wa utawala wa Nyerere, Mwinyi na Mkapa nambo ya udini haukuwepo kabisa na kama ulikuwa unajitokeza ulidhitiwa vilivyo bila utani.

Tujaribu kuangalia madai haya yanayo husu mama Kabaka, lengo lenu ni nini hasa, je, mlitaka muhusika hasichukuliwe hatuwa kali kwa tabia iliyo kuwa imejengeka chuo kikuu cha UDOM bila aibu, jamaa alikuwa anajifanyia apendalo kwa kupalilia upendeleo wa wazi wazi.
 
Ila udom ilizidi udini enzi hizo, hafu hizi mambo za dini mbona akiingia Rais mwislamu ndio zinaanza chokochoko, maana waja wamsagia kunguni mama wa watu, pia taasisi za umma why ujenge nyumba ya ibada ya aina moja tu wakati hyo ni taasisi ya umma ka si ujinga nini
Kwhy Hayati mwendamjini hakufanya teuzi za kikanda ,kikabila na kidini ...ujinga Ni ujinga tu
 
Hapa ndio utajua kwanini maRais wakiwa waislam, magereza huwa yanajaa sana waislam kwa makosa kama ugaidi.

Maana hawa watu hakuna kitu utafanya wataridhika.

Wana mapepo ya vurugu na chokochoko muda wote.

Mtu anakwambia kuna 20:80 kwamba wanafunzi wa kiislam wanafelishwa na NECTA.

Mara analeta stori za BAKWATA na EAMW ya enzi za ukoloni sasa hivi ni ilimradi fujo tu.

Mara Ndalichako alikuwa anawafelisha waislamu, Kikwete akamtoa bado wanalalamika eti kwanini wameweka walewale yaani mkristo Charles Msonde.

Wakati wa Kikwete hawa watu walimsumbua sana.

Mkapa mpaka alichukua eneo la TANESCO akawapa wakajrnga chuo cha MUM Morogoro cha kushngaza maprofesa happ wamekuwa kina Sheikh Ponda ni mihadhra mwanzo mwisho.

Samia akianza kuwachekea hawa wajinga watamshika mpaka Mboni ya jicho.
Ni kweli hawa Wana tatizo kubwa vichwani wao daily tu ndio huonewa, Sasa kama watoto hawatii juhudi kusoma wakifeli wanasingiziwa NECTA tutafika kweli?
Rais tu kuwasamehe wale mashekhe wa uhamisho Sasa wameanza kuleta chokochoko za kidini kila corner.
Mama awadhibiti mapema Hawa watu
 
Kwhy Hayati mwendamjini hakufanya teuzi za kikanda ,kikabila na kidini ...ujinga Ni ujinga tu
Ubaguzi au upendeleo n mbaya hata Kama umefanywa na Mungu!
Huwezi kuhalalisha kujisaidia barabarani kwa kuwa eti ulimuona na jirani yako akifanya hivyo!
 
Serikalini na Taasisi zake zote hakuna form ya hivyo religion na Tribe havipo kabisa kwenye form labda huko sekta binafsi lakini serikalini na Taasisi zake Hakuna hivyo vipengele kuanzia unapoomba kazi Hadi kujaza form ya mkataba havipo
Huna ujualo Mungu akusamehe. Kwa hiyo ni wakati gani serikali ilijua:-
1. Nyerere Mkristu
2. Mwinyi muislam
3. Mkapa mkristu.
4. Kikwete Muislam
5. Magufuli Mkristu.
6. Samia Muislam.

Au kusema serikali mpaka leo haitambui dini za watu hao? Au inajuaje?
 
Hili ni kweli Madam Aziza yule albino mzenj alianza hadi kuwa anawawinda mabinti mpaka town yani anawawinda hadi nje ya chuo akiwakamata wanafukuzwa.
What the hell was that! unatumia sheria za kidini kwenye chuo ambacho hakifungamani na dini yoyote.......na kwa nini hilo lilifikia hapo?
 
What the hell was that! unatumia sheria za kidini kwenye chuo ambacho hakifungamani na dini yoyote.......na kwa nini hilo lilifikia hapo?
Hiki ndicho kilikuwa kinatokea. Ukionewa huruma anakupa adhabu ya kupanda miti. Uongozi ulikuwa unajua wengine wanasema pembeni lakini hakuna aliyekuwa anathubutu kumzuia. Alikuwa anajifunga ushungi anapanda hadi daladala aangalie ni binti gani kavaa sijui suruali au nguo flani. Mabinti walipokuwa wakikutana naye hata town wanakimbia kama wehu.
Alikuwa anatumia suma jkt kuwafukuza na kuwakamata wanafunzi hasa wa kiume.
 
Huna ujualo Mungu akusamehe. Kwa hiyo ni wakati gani serikali ilijua:-
1. Nyerere Mkristu
2. Mwinyi muislam
3. Mkapa mkristu.
4. Kikwete Muislam
5. Magufuli Mkristu.
6. Samia Muislam.

Au kusema serikali mpaka leo haitambui dini za watu hao? Au inajuaje?
Katiba inatamka wazi kuwa serikali haina dini ukiwa Raisi unageuka huna Dini ndio maana Raisi hukusanya Kodi kutoka kwenye bia na maduka ya kitimoto hata Kama ni muislamu

Ukiweka hata mkurugenzi mkuu wa shirika la ndege au la reli au wizara ya biashara moja ya kazi zake ni kusimamia bia ziingie kwenye ndege na treni na Kama Yuko wizara ya biashara moja ya kazi zake ni kusimamia biashara ya pombe kuanzia viwanda Hadi lesen

Serikali kutamkwa haina dini ilikuwa kuwasaidia Wenye dini kuwa ukikubali ajira au cheo it is at your own risk

Walipaji Kodi wakubwa nchi hi ni walevi magari na misafara ya Mama Samia sehemu kubwa inagharimiwa na Kodi za pombe sababu Ndio biggest taxpayers.

Mfano Muislamu akiajiriwa TRA moja ya kazi zake ni kuhakisha wauza pombe wanalipa Kodi stahiki

Kifupi ukijiunga na serikali ujue dini yako umeiweka rehani uchague mawili pepo au dini ukitaka pepo achana na vyeo vya serikali au Bunge au mahakama.Bunge hupitisha sheria za vileo na mahakama husimamia sheria zikiwemo za Chapombe

Ukiwa mkuu wa taasisi au serikali mfano mojawapo ya kazi zako ni kusimamia bajeti za taasisi au serikali ambayo mojawapo ya vipengele ni kusimamia bajeti za vileo vya sherehe ya taasisi kuipitisha na kusimamia

Ushauri wangu Kama wewe ni mtu wa dini epuka vyeo vya serikali ,Bunge na mahakama fanya tu biashara au kilimo utaiona pepo huko kwingine Jehanamu inakuhusu
 
Katiba inatamka wazi kuwa serikali haina dini ukiwa Raisi unageuka huna Dini ndio maana Raisi hukusanya Kodi kutoka kwenye bia na maduka ya kitimoto hata Kama ni muislamu

Ukiweka hata mkurugenzi mkuu wa shirika la ndege au la reli au wizara ya biashara moja ya kazi zake ni kusimamia bia ziingie kwenye ndege na treni na Kama Yuko wizara ya biashara moja ya kazi zake ni kusimamia biashara ya pombe kuanzia viwanda Hadi lesen

Serikali kutamkwa haina dini ilikuwa kuwasaidia Wenye dini kuwa ukikubali ajira au cheo it is at your own risk

Walipaji Kodi wakubwa nchi hi ni walevi magari na misafara ya Mama Samia sehemu kubwa inagharimiwa na Kodi za pombe sababu Ndio biggest taxpayers.

Mfano Muislamu akiajiriwa TRA moja ya kazi zake ni kuhakisha wauza pombe wanalipa Kodi stahiki

Kifupi ukijiunga na serikali ujue dini yako umeiweka rehani uchague mawili pepo au dini ukitaka pepo achana na vyeo vya serikali au Bunge au mahakama.Bunge hupitisha sheria za vileo na mahakama husimamia sheria zikiwemo za Chapombe

Ukiwa mkuu wa taasisi au serikali mfano mojawapo ya kazi zako ni kusimamia bajeti za taasisi au serikali ambayo mojawapo ya vipengele ni kusimamia bajeti za vileo vya sherehe ya taasisi kuipitisha na kusimamia

Ushauri wangu Kama wewe ni mtu wa dini epuka vyeo vya serikali ,Bunge na mahakama fanya tu biashara au kilimo utaiona pepo huko kwingine Jehanamu inakuhusu
Kumbe wewe ni mzembe kiasi hiki? Unaulizwa kingine unatoa majibu mengine.
 
GAUDENSIA KABAKA MWENYEKITI WA UWT?

Mwenyekiti wa UWT Gaudensia Kabaka ndiye aliyehusika kuwafukuza Waislam 11 Chuo Kikuu cha Dodoma na kusimamisha ujenzi wa msikiti hapo chuoni ambao ujenzi wake ulishaidhinishwa.

Leo yupo katika sherehe za kumuenzi Bi. Titi Mohamed.

Huyu ndiye kiongozi aliyewafukuza wajukuu wa Bi. Titi hapo chuoni na kuzuia ujenzi wa msikiti.

Kwa yale aliyopigania Bi. Titi Mohamed na wanawake wote katika TANU ya enzi zile huu ni msiba mkubwa.

Huyu Mama hastahili kuongoza wala kunasibishwa na umoja huu ulioasisiwa na mama zetu akina Bi. Titi, Bi. Hawa bint Maftah, Bi. Zarula bint Abdulrahman kwa kuwataja wachache.

Angalieni picha hiyo ya kwanza hapo chini pcha iliyopigwa na Mohamed Shebe ya mkutano wa TANU 1955 wakati wazee wetu wanautafuta uhuru wa Tanganyika.

Angalia huo umma Viwanja Vya Mnazi Mmoja na tazama hiyo sehemu nyeusi.

Hayo ni mabaibui ya bibi. mama, na shangazi zetu wamekuja kuujaza uwanja na kumtia nguvu Mwalimu Nyerere.

Mama zetu wameitika mwito wa "kuno kuno."

Hapo ndipo walipokuwa wakiimba nyimbo za lelemama kuhamsisha wakiimba."

Muheshimiwa nakupenda sana....Insha Allah Mungu yupo Tanganyika tutajitawala.''

Tujitawale halafu iwe nini?

Gaudensia anyanyase Waislam, Gaudensia avunje misikiti yetu?

Gaudensia awafukuze chuoni wajukuu wa hawa wanawake unaowaona hapo chini kwenye picha?

Picha ya pili hao wote mbele hapo wanaongoza maandamano ya akina mama mimi mama zangu.

Hao ndiyo msingi wa UWT.

Yupo Bi. Mwamvua bint Mrisho (Mama Daisy), Bi. Titi Mohamed na Bi. Zainab Tewa.

Chuo kilikuwa na Waislamu 11 tu?
Kama ujenzi uliidhinishwa kimakosa alikuwa sahihi. Misikiti na Makanisa yakajengwe sehemu zake.

Ioneshwe wapi alivunja sheria.otherwise ni muendelezo wa malalamiko yasiyokoma ya kutojiamini na roho za ulalamishi siku zote.
 
Jiwe...
Utaelezaje 20:80.

Mjadala huu unahitaji ujuzi vinginevyo utabakia kwenye ghadhabu.

Serikali katika hili hawana la kusema.

Serikali ndiyo ya kutoa majibu si wewe.
Serikali ingekuwa inajibu kila ujinga nadhani ingekuwa ngumu sana kufanya mambo ya maendeleo. Mi nadhani Dodoma kuna viwanja vingi sana Waislmu wajenge tu misikiti kadri wawezavyo waache kulia lia kipuuzi. Gaudensi hajazuia kujengwa misikiti ijengwe mingi sana ...nashauri yanunuliwe maeneo mengi misikiti ijengwe mingi sana. Waislamu wamche mola wao.... Wakati wote.
 
Saint...
Ahsante hii ni data nitamrushia sahib yangu nisikilize atasema nini.
Hakika kuishi kwingi ni kuona mengi.

Nina miaka 69 nakimbilia 70 In Sha Allah February 2022''

Naomba ufafanuzi kidogo Mzee wangu kama hutojali.Kuna picha moja umepost ukiwa wewe na kina Sykes umesema ilikuwa ni 1968 na katika hiyo picha ukasema Sykes alikuwa na miaka 20 na wewe ukiwa na miaka 18.Sasa tuchukulie hayo maelezo ya hiyo picha yalikuwa sahihi maana yake umezaliwa mwaka 1950.Lakini kwa maelezo hayo niliyoku quote unasema 2022 utakuwa na miaka 70.Tushike lipi kati ya haya mawili? Umezaliwa mwaka 1950 au 1952?
 
Naomba ufafanuzi kidogo Mzee wangu kama hutojali.Kuna picha moja umepost ukiwa wewe na kina Sykes umesema ilikuwa ni 1968 na katika hiyo picha ukasema Sykes alikuwa na miaka 20 na wewe ukiwa na miaka 18.Sasa tuchukulie hayo maelezo ya hiyo picha yalikuwa sahihi maana yake umezaliwa mwaka 1950.Lakini kwa maelezo hayo niliyoku quote unasema 2022 utakuwa na miaka 70.Tushike lipi kati ya haya mawili? Umezaliwa mwaka 1950 au 1952?
Nyamizi,
Hiyo picha haikuwa ya kina Sykes.

Hiyo picha ni group yetu tukijiita Scorpions.

Katika caption nimesema Kleist alikuwa na miaka 20 na mimi miaka 18.

Kleist kazaliwa 1950 na mimi 1952.
 
Nyamizi,
Hiyo picha haikuwa ya kina Sykes.

Hiyo picha ni group yetu tukijiita Scorpions.

Katika caption nimesema Kleist alikuwa na miaka 20 na mimi miaka 18.

Kleist kazaliwa 1950 na mimi 1952.

Ahsante sana Mzee wangu,basi maelezo ya picha yatakuwa na kasoro maana umesema kwa hiyo picha ni mwaka 1968.Kwa maelezo haya maana yake hiyo picha imepigwa 1970.
 
Nyamizi,
Hiyo picha haikuwa ya kina Sykes.

Hiyo picha ni group yetu tukijiita Scorpions.

Katika caption nimesema Kleist alikuwa na miaka 20 na mimi miaka 18.

Kleist kazaliwa 1950 na mimi 1952.

IMG_2977.png
 
May Day,
Hivi unajua Nyerere kaja Dar es Salaam hana ndugu wala jamaa?

Unawajua waliompokea?

Unadhani endapo wazee wetu wamgekuwa wabaguzi wa dini au kabila Nyerere angefika hapo alipofika?

Wewe unaridhishwa na hii hali ya leo katika mgawanyo wa fursa 20:80?
Here we go again, he goes "Mgawano wa fulsa" how do you mean? Kwani fulsa zinagawanwa au inategemea na akili za MTU kuchangamkia fulsa - wakati mwingine mnashangaza sana sana

Labda nikuhoji swali dogo: Hivi Tanzania kuna sect ngapi za kidini? Za kikristo na zaidi ya kumi,dini za kihindi sijui ngapi, wapagani nk - mbina hao wote hawsjseshi kulalama kwamba: sijui wanaonewa au kusahurika au hawapewi fulsa sawa - lawama mwanzo mwisho na kibaya zaidi mnapandikiza chuki zenu mpaka kwa watoto kwenye madrassa, badala ya kuwafundisha masuala ya dini mnapoteza muda mwingi kuwaharibu kisaikolojia kujenga dhana kwamba Waislaam hawatendewi haki katika taifa letu as if hakuna madhehebu mengine nchini zaidi yenu, hapa nataka nieleweke vizuri, mimi sina tatizo na Waaslamu kwa jumla, ninacho kemea ni hawa baadhi yenu wenye itikadi za ajabu ambao masaa yote wanayapoteza wakilalama kwamba hawatendewi haki, hawapewi vyeo Serikalini na kwenye mashirika ya UMMA, mambo gani haya kama siyo agenda za chini chini za kutaka Taifa letu lianze kuvurugika kwa misingi ya kidini, yaani baadhi ya hawa wenye itikadi za ajabu ajabu wanatamani masahibu yanayo ikumba Nigeria ya kasikazini na Msumbiji ya Kasikazini yahamie Tanzania.
 
May Day,
Hivi unajua Nyerere kaja Dar es Salaam hana ndugu wala jamaa?

Unawajua waliompokea?

Unadhani endapo wazee wetu wamgekuwa wabaguzi wa dini au kabila Nyerere angefika hapo alipofika?

Wewe unaridhishwa na hii hali ya leo katika mgawanyo wa fursa 20:80?
Moh, look: Nyerere alikuja Dar kama Mwalimu was shule ya Sekondari ya Pugu
 
Back
Top Bottom