Gaudensia Kabaka Mwenyekiti wa UWT?

Gaudensia Kabaka Mwenyekiti wa UWT?

"Na zaidi ni kuwa safari ya kwanza ya Mwalimu Nyerere ya kwenda UNO 05/03/1955 , Kanisa Katoliki lilitoa msaada kwa chama cha TANU wa tiketi ya ndege ya kwenda na kurudi, lilifanya hivyo kupitia shirika lake la Maryknoll Sisters la New York Marekani,

Si hivyo tu bali katika moja ya utani wa Mwalimu wenye ukweli ndani yake aliwahi kusema kuwa Kasisi Art Wille wa Shirika la Maryknoll ni boss wake, akikumbuka malipo ya shilingi 600 angali ameacha kazi ya ualimu akiwa kijijini Butiama."

Hili lililetwa na wanajukwaa utalikataa ila yako unataka tuyaamini na kwa Kejeli unasema tuna lipi tujualo.. Mitihani kweli
Jones...
Mimi naijua historia ya safari ya Mwalimu Nyerere UNO 1955.

Fedha za safari mkusanyaji alikuwa Iddi Faiz Mafungo Mweka Hazina wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika na pia Mweka Hazina wa TANU.

Hafla ya kumuaga Nyerere ilifanyika jengo la Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika Mtaa wa Stanley na New Street.

Safari hii hakukuwa na msaada wa Maryknoll.

Msaada huo wa tiketi unaosema wewe ni safari ya pili 1957.

Naomba niazime msemo wako, "Mitihani kweli kweli."
 
Tatizo lako Mohamed unajinasibisha Na historia ya Tanzania kwa Ujumla wakati so kila kitu unakijua japo nakupongeza kwa kujua angalau 30% ya history lakini so 100% hivo wenye mawazo mbadala usuwabeze
Brit...
Ndugu yangu mimi ni sehemu ya historia hii.

Hawa waliounda African Association na TANU na kumpokea Nyerere alipokuja Dar es Salaam mwaka wa 1952 ni wazee wangu.

Sijayajua haya kwa kusoma kitabu.
 
Alivunja misikiti kwa vigezo gani? Hana mamlaka wala nguvu hizo. Nchi hii inaongozwa na sheria na taratibu. Ukijenga msikiti katikati ya barabara utamlaumu nani greda likiuvunja, kwa mfano?
Kufukuza watukutu 11 sio sawa na kufukuza waislamu 11. hebu eleza kwa kina nani, na kwanini walifukuzwa? Hii mada yako imejaa uchochezi na chuki kubwa. Hailitakii mema Taifa letu. Unachotaka ni kuonyesha waislamu wananyanyaswa wakati si kweli
 
Jones...
Mimi naijua historia ya safari ya Mwalimu Nyerere UNO 1955.

Fedha za safari mkusanyaji alikuwa Iddi Faiz Mafungo Mweka Hazina wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika na pia Mweka Hazina wa TANU.

Hafla ya kumuaga Nyerere ilifanyika jengo la Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika Mtaa wa Stanley na New Street.

Safari hii hakukuwa na msaada wa Maryknoll.

Msaada huo wa tiketi unaosema wewe ni safari ya pili 1957.

Naomba niazime msemo wako, "Mitihani kweli kweli."
Huu ubabaishaji wako wanausikiliza watu wanaotaka kujifurahisha nafsi...unapindisha ukweli makusudi
 
Jones...
Mimi naijua historia ya safari ya Mwalimu Nyerere UNO 1955.

Fedha za safari mkusanyaji alikuwa Iddi Faiz Mafungo Mweka Hazina wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika na pia Mweka Hazina wa TANU.

Hafla ya kumuaga Nyerere ilifanyika jengo la Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika Mtaa wa Stanley na New Street.

Safari hii hakukuwa na msaada wa Maryknoll.

Msaada huo wa tiketi unaosema wewe ni safari ya pili 1957.

Naomba niazime msemo wako, "Mitihani kweli kweli."
Mzee wangu Mohamed nimesoma maandiko yako mengi ila sijapata kubahatika kuona ukisema/kuandika kuwa Maryknoll ilitoa msaada wa ticket kwa Nyerere mwaka 1957 Kwenda UNO kama ipo basi nifahamishe la hamna huna haja ya kukwepa hoja za wanaosema wewe ni mdini kweli kweli.
 
1. Udini hautakufanya uonewe huruma.
2. Issue ya Udom hujui chochote, bora ukae kimya tu.
3. Funga bakuli lako, historia ya ukombozi wa TZ tunaijua pia.
 
Jones...
Huyajui.
Mimi nikwepe swali gani kwako?
Una kipi ukijuacho?

Chuki niitoe wapi?

Huwasomi wenye chuki humu wanaotoa matusi na kejeli?

Mimi niko hapa kusomesha yale wengi msiyoyajua.

Je, ulijuankuwa sababu ya serikali kuivunja EAMWS ni mradi wake wa kujenga Chuo Kikuu?

Je, unajua kuwa uliletwa mradi mwingine na Organisation of Islamic Conference (OIC) wa kujenga Chuo Kikuu serikali ikakataa kutoa kibali?

Nikiwa mimi mtu wa chuki nitapata wapi utulivu kusomesha haya?

Masikini ya Mungu ulikuwa kizani unajitolea maneno yasiyo na ithibati.

Sasa unajua na aliyekufunza ni Mohamed Said.
Mr. Mohamed Said kama unachonifunza nakitilia shaka inabidi ujitathimini kama mafunzo yako yanakidhi vigezo. We will question everything na kila hoja ijibiwe kwa hoja na kwa ukamilifu wake mengi unayojinasibu kuyajua yeyote anaweza kuyajua hoja ni je? Yana ukweli uso shaka?

Viongozi wote wakubwa wa kiislam serikalini kwa kipindi hicho hawakuyaona hayo unayosema ni dhuluma umekuja kuyaona wewe?? Mzee hutufunzi ila unatuchanganya ukakasi ni mwingi kuliko uhalisia.
 
Mohamed Said, hebu twende taratbu...

1. Bibi Titi Mohamed anafahamika katika historia ya Tanzania kama kiongozi wa Waislamu katika kada yoyote, au anatambulika kama mwana-siasa aliyepigania uhuru wa Tanganyika na Mwenyekiti wa UWT?

2. Huyo Gaudensia Kabaka alikuwepo kwenye sherere za kumuenzi Bibi Titi akiwa na kofia ya Utawa au akiwa na kofia ya Uenyekiti wa UWT?

3. Wale walioenda kumuona mtoto wa Bibi Titi, walikuwa ni viongozi wa Kiislamu au CCM?

4. Paliwahi kuwa na tuhuma kwamba Mwalimu Nyerere alifanya sahihi kumtia korokoroni Bibi Ti

5. Kwamba:-
Huyu Mama hastahili kuongoza wala kunasibishwa na umoja huu ulioasisiwa na mama zetu akina Bi. Titi, Bi. Hawa bint Maftah, Bi. Zarula bint Abdulrahman kwa kuwataja wachache.
Ni umoja upi huo ambao uliasisiwa na mama zenu?! Umoja wa Wanawake wa Kiislamu Tanzania, au Umoja wa Wanawake Tanzania?!

6. BInafsi, labda kwa kutokuwa na uelewa, sijapata kusikia Bibi Titi kuasisi Umoja wa Wanawake wa Kiislamu Tanzania bali nimesoma mara kadhaa kuhusu yeye na wenzake kuasisi Umoja wa Wanawake Tanzania! Sasa kama unazungumzia UWT, hivi hujisikii aibu kutoa kauli kama hiyo hapo juu?

Niwe mkweli Mzee Mohamed Said... nakuheshimu kutokana na umri wako na pia kutokana na maarifa yako lakini ukweli ni kwamba UNABOA!!!

Hivi unajisikiaje kila mada kuhusisha na udini?!

Ajabu yako sasa... mtoto wa Bibi Titi mwenyewe kafurahia ugeni lakini unakuja kuumia wewe na kuingiza udini! Ina maana unataka kusema wewe unamfahamu sana Bibi Titi, na una mahaba nae sana kuliko mtoto wake wa kumzaa?!

Badala ya mara kwa mara kuleta mada zinazoakisi udini, Hivi kama kweli una uchungu na imani yako, kwanini usitumie muda wako kuelimisha
Angalieni picha hiyo ya kwanza hapo chini pcha iliyopigwa na Mohamed Shebe ya mkutano wa TANU 1955 wakati wazee wetu wanautafuta uhuru wa Tanganyika.

Angalia huo umma Viwanja Vya Mnazi Mmoja na tazama hiyo sehemu nyeusi.

Hayo ni mabaibui ya bibi. mama, na shangazi zetu wamekuja kuujaza uwanja na kumtia nguvu Mwalimu Nyerere.

Mama zetu wameitika mwito wa "kuno kuno."
Wazee wenu wewe na akina nani?

Mama zenu wewe na akina nani?

Kama hiyo "mama zetu" unamaanisha "mama wa Waislamu", tafadhali stop generalizing kwa sababu sio Waislamu wote wanapendezwa na huu ujinga wa mambo ya udini!!
Hapo ndipo walipokuwa wakiimba nyimbo za lelemama kuhamsisha wakiimba."

Muheshimiwa nakupenda sana....Insha Allah Mungu yupo Tanganyika tutajitawala.''

Tujitawale halafu iwe nini?
Nilidhani ungesema hapo ndipo walipokuwa wakiimba qaswida, kusoma quran na maulidi kumuomba Mwenyezi Mungu!! Kumbe walikuwa wakiimba nyimbo za hamasa katika kupigania uhuru?!

Itoshe tu kusema kwamba, tumia elimu na maarifa yako kuhubiri umoja badala ya kuhubiri umimi na udini!! Sisi, na wengine miongoni mwetu ni Waislamu, tunamfahamu Bibi Titi kama miongoni mwa wapigani uhuru wa taifa hili!!

Tumefundishwa Bibi Titi alikuwa mwanamke shupavu katika harakati za kupigania uhuru, lakini HAKUNA popote tulipofundishwa alikuwa Mwanamke wa Kiislamu Shupavu katika kupigania Uislamu!!

And FYI, hata Madrasa nimesoma, tena Kurasini Dar es salam... mwendo mfupi tu kutoka Kariakoo lakini HATA SIKU MOJA hatukuwahi kufundishwa habari za Bibi Titi!!!

ACHA UDINI....
 
Kwa hiyo hafai kuwa Mwenyekiti wa UWT kwa sababu alikataa msikiti usijengwe?,..hmm kuna siku mtataka misikiti ijengwe jwenye kambi za jeshi.
 
Vyovyote vile naamini kuna mapungufu mengi sana katika uandishi wa historia ya nchi ya Tanganyika na baadae Tanzania, mfano mwingine mzuri, shujaa wa mapinduzi ya Zanzibar ni yule Mganda Okello lakini leo historia imejaa na kumtukuza Mzee Karume!
Hizo sia Anga za Moh@med Said
 
Kwa hiyo hafai kuwa Mwenyekiti wa UWT kwa sababu alikataa msikiti usijengwe?,..hmm kuna siku mtataka misikiti ijengwe jwenye kambi za jeshi.
Na Upande wa pili was maisha ya Bibi Titi ,Kama unamwita Muislam ni kuinajisi dini
 
Alivunja misikiti kwa vigezo gani? Hana mamlaka wala nguvu hizo. Nchi hii inaongozwa na sheria na taratibu. Ukijenga msikiti katikati ya barabara utamlaumu nani greda likiuvunja, kwa mfano?
Kufukuza watukutu 11 sio sawa na kufukuza waislamu 11. hebu eleza kwa kina nani, na kwanini walifukuzwa? Hii mada yako imejaa uchochezi na chuki kubwa. Hailitakii mema Taifa letu. Unachotaka ni kuonyesha waislamu wananyanyaswa wakati si kweli
Tangawizi,
Sikushangai kusema hivyo.

Wala sishangai kwa lugha hii yako ya ''watukutu.''

Wala sistaajabu kwa hii lugha ya ''uchochezi.''

Ila nafarajika kuwa majibu yanatoka kwako na si kwa serikali.

In Shaa Allah iko siku serikali yetu itatupa jibu.
 
Hizo sia Anga za Moh@med Said
Lombo,
Mimi nilikuwa Research Assistant wa Dr. Harith Ghassany wakati anatafiti kitabu chake maarufu, ''Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru,'' kuhusu Mapinduzi ya Zanzibar.

Ndugu yangu wewe hunijui kabisa.

Mimi nakukaribisha kuniuliza jambo kabla ya kuwa unajisemea chochote kinachokuja akilini kwako.

Hiyo picha hapo chini niko fukwe ya Kipumbwi, Tanga ambako majahazi ya kuwavusha Wamakonde wakata mkonge shamba la Sakura walipokuwa wakivushwa kupelekwa Zanzibar kushiriki katika upigaji wa kura uchaguzi wa 1961 na kushiriki katika mapinduzi 1964.

Hii ni picha ya mwaka wa 2008 na iko ndani ya kitabu.

1635193055881.png
 
Huu ubabaishaji wako wanausikiliza watu wanaotaka kujifurahisha nafsi...unapindisha ukweli makusudi
Tangawizi,
Ukumbi huu wote wa Historia kwangu ni darasa.

Ninapoandika sikuangalii wewe jicho langu lnakwenda kwa picha kubwa na naisomesha historia hii kama niijuavyo kwa hao wengine.

Ikiwa wewe huamini niandikayo hakuna neno lakini elewa kuna watu wananufaika sana na elimu hii ninayoitoa hapa.
 
Mzee wangu Mohamed nimesoma maandiko yako mengi ila sijapata kubahatika kuona ukisema/kuandika kuwa Maryknoll ilitoa msaada wa ticket kwa Nyerere mwaka 1957 Kwenda UNO kama ipo basi nifahamishe la hamna huna haja ya kukwepa hoja za wanaosema wewe ni mdini kweli kweli.
Jones...
Ikiwa tutakwenda kwa hoja ya chembelecho "udini," hutofika mbali na mimi nitakuwa nishakushinda.

Nitakuuliza wale watafiti waliowafuta Waislam kwenye historia ya TANU na ukitazama nyuma utakuta majina yao hawakusukumwa na udini kufanya hivyo?

Wale waliovunja EAMWS wakati wanajenga Chuo Kikuu hawakusukumwa na dini nk. nk.

Maryknoll kuwa walitoa tiketi sina taarifa hiyo lakini kwa kuwa wewe umesema nikakwambia itakuwa safari ya 1957 na nimesema hayo kwa ustaarabu kwa kuamini utakuwa unasema kweli.
 
Mohamed Said, hebu twende taratbu...

1. Bibi Titi Mohamed anafahamika katika historia ya Tanzania kama kiongozi wa Waislamu katika kada yoyote, au anatambulika kama mwana-siasa aliyepigania uhuru wa Tanganyika na Mwenyekiti wa UWT?

2. Huyo Gaudensia Kabaka alikuwepo kwenye sherere za kumuenzi Bibi Titi akiwa na kofia ya Utawa au akiwa na kofia ya Uenyekiti wa UWT?

3. Wale walioenda kumuona mtoto wa Bibi Titi, walikuwa ni viongozi wa Kiislamu au CCM?

4. Paliwahi kuwa na tuhuma kwamba Mwalimu Nyerere alifanya sahihi kumtia korokoroni Bibi Ti

5. Kwamba:-

Ni umoja upi huo ambao uliasisiwa na mama zenu?! Umoja wa Wanawake wa Kiislamu Tanzania, au Umoja wa Wanawake Tanzania?!

6. BInafsi, labda kwa kutokuwa na uelewa, sijapata kusikia Bibi Titi kuasisi Umoja wa Wanawake wa Kiislamu Tanzania bali nimesoma mara kadhaa kuhusu yeye na wenzake kuasisi Umoja wa Wanawake Tanzania! Sasa kama unazungumzia UWT, hivi hujisikii aibu kutoa kauli kama hiyo hapo juu?

Niwe mkweli Mzee Mohamed Said... nakuheshimu kutokana na umri wako na pia kutokana na maarifa yako lakini ukweli ni kwamba UNABOA!!!

Hivi unajisikiaje kila mada kuhusisha na udini?!

Ajabu yako sasa... mtoto wa Bibi Titi mwenyewe kafurahia ugeni lakini unakuja kuumia wewe na kuingiza udini! Ina maana unataka kusema wewe unamfahamu sana Bibi Titi, na una mahaba nae sana kuliko mtoto wake wa kumzaa?!

Badala ya mara kwa mara kuleta mada zinazoakisi udini, Hivi kama kweli una uchungu na imani yako, kwanini usitumie muda wako kuelimisha

Wazee wenu wewe na akina nani?

Mama zenu wewe na akina nani?

Kama hiyo "mama zetu" unamaanisha "mama wa Waislamu", tafadhali stop generalizing kwa sababu sio Waislamu wote wanapendezwa na huu ujinga wa mambo ya udini!!

Nilidhani ungesema hapo ndipo walipokuwa wakiimba qaswida, kusoma quran na maulidi kumuomba Mwenyezi Mungu!! Kumbe walikuwa wakiimba nyimbo za hamasa katika kupigania uhuru?!

Itoshe tu kusema kwamba, tumia elimu na maarifa yako kuhubiri umoja badala ya kuhubiri umimi na udini!! Sisi, na wengine miongoni mwetu ni Waislamu, tunamfahamu Bibi Titi kama miongoni mwa wapigani uhuru wa taifa hili!!

Tumefundishwa Bibi Titi alikuwa mwanamke shupavu katika harakati za kupigania uhuru, lakini HAKUNA popote tulipofundishwa alikuwa Mwanamke wa Kiislamu Shupavu katika kupigania Uislamu!!

And FYI, hata Madrasa nimesoma, tena Kurasini Dar es salam... mwendo mfupi tu kutoka Kariakoo lakini HATA SIKU MOJA hatukuwahi kufundishwa habari za Bibi Titi!!!

ACHA UDINI....
Chige,
Unataka twende taratibu.
Nami nakuitikia kuwa hakika twende taratibu,

Unasema niache udini.
Jibu langu na nachukua hapo juu jibu nililompa msomaji wangu mmoja # 191:

''Jones...
Ikiwa tutakwenda kwa hoja ya chembelecho "udini," hutofika mbali na mimi nitakuwa nishakushinda.

Nitakuuliza wale watafiti waliowafuta Waislam kwenye historia ya TANU na ukitazama nyuma utakuta majina yao hawakusukumwa na udini kufanya hivyo?

Wale waliovunja EAMWS na kuunda BAKWATA bila ya ridhaa ya Waislam wakati wanajenga Chuo Kikuu hawakusukumwa na udini nk. nk.''

Umesema twende taratibu unaniuliza ni wazee wangu gani waliopigania uhuru wa Tanganyika?

Nakuwekea hapo chini historia ya babu yangu Salum Abdallah ingia kwenye link hizo hapo chini:


Tusimame hapa kwa kuwa umesema twende taratibu.

Hiyo picha hapo chini kulia ni Kassanga Tumbo na anefuata ni Salum Abdallah viongozi waasisi wa Tanganyika Railways African Union (TRAU) 1955 na chama hiki kilipigania uhuru wa Tanganyika bega kwa bega na TANU.

Mengine hayana maana kwa hiyo nimeyanyamazia.

1635195267528.png
 
Upuuzi kama huu unaandika kwa sababu top yote ni dini yako.
Sasa kama 20:80 kwa nn usimshauri Mama awaweke 100 kabisa tuone mtafanya nn zaidi ya kuifanya nchi kama Somalia.
Wewe mzee ni mtu wa hovyo sana na kizazi chetu hiki cha sasa hakipaswi kuwa na mbegu yoyote ya aina yako..
Kaka unapaswa ukaishi Somalia maana nahisi una chembechembe za huko.
Huko utaishi vyema kabisa na hautapata kichefuchefu cha mgalatia hata mmoja.
Nchi yetu ni ya amani na upendo,
Familia zetu zina mchanganyiko wa watu wenye imani tofauti tofauti,
Hizi chuki zako zilizojaa pomoni unazipeleka wapi?
Peleka ushauri juu ili majina ya mawaziri,manaibu wao,wakuu wa mikoa na wilaya wote uwapendekeze wewe ili hicho kijiriba chako cha chuki kikuishe kaka.
Au ndivyo mnavyofundishwa Madrasa?
Maujinga kama haya usingeandika kipindi kilichopita na moja ya vitu ambavyo Magu hakuchekelea ni upuuzi upuuzi na uchochezi kama huu.
Unataka kumharibia Mama Kabaka ili iweje?
Chuki chuki chuki, Udini Udini hupofusha akili
 
Hili andiko limejaa chuki, unafiki na uchonganishi.

Huyu Ndugu muda wote yeye ni kuwazia dini yake tu.

Tumshukuru sana Mungu kumleta Mwalimu Nchi hii ingeangukia kwenye mikono ya hii familia hakika ingekuwa ni majuto.
😂
😂
 
Ni ushambuliaji binafsi, udini, na chuki vimeonyeshwa hapa. Alisimamisha vipi wakati UDOM wana uongozi wao na wanaamua mambo yao wenyewe. Shake well before use.
 
Upuuzi kama huu unaandika kwa sababu top yote ni dini yako.
Sasa kama 20:80 kwa nn usimshauri Mama awaweke 100 kabisa tuone mtafanya nn zaidi ya kuifanya nchi kama Somalia.
Wewe mzee ni mtu wa hovyo sana na kizazi chetu hiki cha sasa hakipaswi kuwa na mbegu yoyote ya aina yako..
Kaka unapaswa ukaishi Somalia maana nahisi una chembechembe za huko.
Huko utaishi vyema kabisa na hautapata kichefuchefu cha mgalatia hata mmoja.
Nchi yetu ni ya amani na upendo,
Familia zetu zina mchanganyiko wa watu wenye imani tofauti tofauti,
Hizi chuki zako zilizojaa pomoni unazipeleka wapi?
Peleka ushauri juu ili majina ya mawaziri,manaibu wao,wakuu wa mikoa na wilaya wote uwapendekeze wewe ili hicho kijiriba chako cha chuki kikuishe kaka.
Au ndivyo mnavyofundishwa Madrasa?
Maujinga kama haya usingeandika kipindi kilichopita na moja ya vitu ambavyo Magu hakuchekelea ni upuuzi upuuzi na uchochezi kama huu.
Unataka kumharibia Mama Kabaka ili iweje?
Chuki chuki chuki, Udini Udini hupofusha akili
Kipuyo,
Unaandika umeghadhibika.
Ghadhabu hukimbiza fikra za kutafakari.

Matokeo yake ndiyo haya.
 
Back
Top Bottom