Gaudensia Kabaka Mwenyekiti wa UWT?

Gaudensia Kabaka Mwenyekiti wa UWT?

mtu yeyeto anayeipenda Tanzania lazima atagadhabika na uchochezi unaoufanya
Sajo...
Mimi naipenda nchi yangu na naithamini historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika.

Naipenda historia hii kwa sababu kubwa moja kuwa ni historia ya wazee wazee wangu walivyosimama kupambana na ukoloni hadi wakashinda na uhuru ukapatikana tarehe 9 Desemba 1961.

Nimeghadhibishwa kuja kuona kuna watu wameifuta historia hii na kuweka ya kwao.
Huu si uchochezi.

Kitabu kilipotoka kilishtusha wanahistoria wakubwa wataalamu katika African History na wakafanya pitio la kitabu changu.

John Iliffe, James Brennan na Jonathon Glassman walikipitia kitabu na wote wakachapwa na Cambridge Journal of Africa History.

Hakuna hata mmoja wao aliyesema hiki kitabu ni uchochezi.
 
Reginald...
Bei ni Shs: 10,000.00.
Kipo cha Kiingereza na cha Kiswahili.

Nunua ukisome hiki kitabu kina mengi sana ambayo wengi hawakuwa wanayajua katika hitoria ya TANU na uhuru wa Tanganyika.

Nakushauri ununue cha Kiswahili kwa kuwa baada ya kutoka kitabu 1998 kabla Mzee Tewa Said Tewa hajafa aliniita nyumbani kwake akanipa faili.

Nilikuwa nimezungumza mengi na Mzee Tewa lakini alikuwa mengine hakuniambia.

Kilipotoka kitabu alibadili fikra akaamua kunipa hilo faili ili nisome yale ambayo yeye alifanya siri kwa wakati ule.

Hakuchukua muda baada ya kunipa lile faili Mzee Tewa akafariki dunia.

Mwaka wa 2002 ikachapwa tafsiri ya Kiswahili na humo ndimo nilipoandika haya niliyotoa katika faili la Mzee Tewa.



View attachment 1991500
Nashukuru sana kwa maelezo yako mazuri.

Kwa sasa nipo Kanda Ya Ziwa hapa Mwanza, Utaratibu wa kukipata ukoje?
 
GAUDENSIA KABAKA MWENYEKITI WA UWT?

Mwenyekiti wa UWT Gaudensia Kabaka ndiye aliyehusika kuwafukuza Waislam 11 Chuo Kikuu cha Dodoma na kusimamisha ujenzi wa msikiti hapo chuoni ambao ujenzi wake ulishaidhinishwa.

Leo yupo katika sherehe za kumuenzi Bi. Titi Mohamed.

Huyu ndiye kiongozi aliyewafukuza wajukuu wa Bi. Titi hapo chuoni na kuzuia ujenzi wa msikiti.

Kwa yale aliyopigania Bi. Titi Mohamed na wanawake wote katika TANU ya enzi zile huu ni msiba mkubwa.

Huyu Mama hastahili kuongoza wala kunasibishwa na umoja huu ulioasisiwa na mama zetu akina Bi. Titi, Bi. Hawa bint Maftah, Bi. Zarula bint Abdulrahman kwa kuwataja wachache.

Angalieni picha hiyo ya kwanza hapo chini pcha iliyopigwa na Mohamed Shebe ya mkutano wa TANU 1955 wakati wazee wetu wanautafuta uhuru wa Tanganyika.

Angalia huo umma Viwanja Vya Mnazi Mmoja na tazama hiyo sehemu nyeusi.

Hayo ni mabaibui ya bibi. mama, na shangazi zetu wamekuja kuujaza uwanja na kumtia nguvu Mwalimu Nyerere.

Mama zetu wameitika mwito wa "kuno kuno."

Hapo ndipo walipokuwa wakiimba nyimbo za lelemama kuhamsisha wakiimba."

Muheshimiwa nakupenda sana....Insha Allah Mungu yupo Tanganyika tutajitawala.''

Tujitawale halafu iwe nini?

Gaudensia anyanyase Waislam, Gaudensia avunje misikiti yetu?

Gaudensia awafukuze chuoni wajukuu wa hawa wanawake unaowaona hapo chini kwenye picha?

Picha ya pili hao wote mbele hapo wanaongoza maandamano ya akina mama mimi mama zangu.

Hao ndiyo msingi wa UWT.

Yupo Bi. Mwamvua bint Mrisho (Mama Daisy), Bi. Titi Mohamed na Bi. Zainab Tewa.

Baraza la Mitihani Tanzania (Necta), limemtaja mwanafunzi aliyehitimu shule ya msingi St Anne Marie iliyopo mkoani Dar es Salaam, Eluleki Evaristo Haule kuwa ndiye aliyeibuka kinara katika matokeo ya mtihani ya Darasa la Saba 2021.

Akitangaza matokeo hayo leo Jumamosi Oktoba 30, 2021 Katibu Mtendaji wa Necta, Dk Charles Msonde amesema watahiniwa bora kitaifa ni wale ambao wamepata alama nyingi zaidi kuliko wenzao kwenye masomo sita waliyotahiniwa.

Alimtaja aliyeshika nafasi ya pili kuwa ni Happy Joseph Deus kutoka shule ya msingi Twibhoki ya Mkoa wa Mara na nafasi ya tatu ikienda kwa John Chacha Charles kutoka Twibhoki.

Aliyeshika nafasi ya nne ni Joshua Mahende Jacob kutoka shule ya msingi Twibhoki iliyopo Mara pia, Eva Sebastian Chengula kutoka shule ya msingi Fountain of Joy ya Dar es Salaam ameshika nafasi ya tano, Joctan Samwel Matara kutoka Twibhoki ameshika nafasi ya sita.

[emoji835]️ Kwa UPDATES zote, Download GLOBAL APP:
[emoji835]️ ANDROID:Global App - Apps on Google Play
[emoji835]️ iOS:‎Global Publishers

Mudi akiona hivi ndo anaita udini.we mzee utakufa kihoro!
Screenshot_20211030-164252_Instagram.jpg
 
Baraza la Mitihani Tanzania (Necta), limemtaja mwanafunzi aliyehitimu shule ya msingi St Anne Marie iliyopo mkoani Dar es Salaam, Eluleki Evaristo Haule kuwa ndiye aliyeibuka kinara katika matokeo ya mtihani ya Darasa la Saba 2021.

Akitangaza matokeo hayo leo Jumamosi Oktoba 30, 2021 Katibu Mtendaji wa Necta, Dk Charles Msonde amesema watahiniwa bora kitaifa ni wale ambao wamepata alama nyingi zaidi kuliko wenzao kwenye masomo sita waliyotahiniwa.

Alimtaja aliyeshika nafasi ya pili kuwa ni Happy Joseph Deus kutoka shule ya msingi Twibhoki ya Mkoa wa Mara na nafasi ya tatu ikienda kwa John Chacha Charles kutoka Twibhoki.

Aliyeshika nafasi ya nne ni Joshua Mahende Jacob kutoka shule ya msingi Twibhoki iliyopo Mara pia, Eva Sebastian Chengula kutoka shule ya msingi Fountain of Joy ya Dar es Salaam ameshika nafasi ya tano, Joctan Samwel Matara kutoka Twibhoki ameshika nafasi ya sita.

[emoji835]️ Kwa UPDATES zote, Download GLOBAL APP:
[emoji835]️ ANDROID:Global App - Apps on Google Play
[emoji835]️ iOS:‎Global Publishers

Mudi akiona hivi ndo anaita udini.we mzee utakufa kihoro!View attachment 1992226
Luku...
Unanidhania kuwa mimi mjinga hapana.
Ninayoandika si mambo ya kipuuzi hata kidogo.

Yote yana ushahidi usio na shaka.
Zipo taarifa za yaliyokuwa yakifanyika Wizara ya Elimu na NECTA.
 
Tk...
Hakika soma mchango wa masheikh waliokuwa mstari wa mbele katika kupigania uhuru wa Tanganyika utajifunza mengi.

Sina sababu ya kujificha.
Jina langu liko hapa.

Uliyejificha ni wewe.
Nini kinakutisha?
Kwa hiyo lengo la kuleta Udini ni nini? Hizi ni dalili za akili mufilisi
 
Luku...
Unanidhania kuwa mimi mjinga hapana.
Ninayoandika si mambo ya kipuuzi hata kidogo.

Yote yana ushahidi usio na shaka.
Zipo taarifa za yaliyokuwa yakifanyika Wizara ya Elimu na NECTA.
Naona unaanza kurekebisha Uandishi wako....👆 Eti,yaliyokuwa yakifanyika...utanyooka tu kwa huu upotoshaji unaufanya!
 
Kwa hiyo lengo la kuleta Udini ni nini? Hizi ni dalili za akili mufilisi
Ghichi...
Hili suala la udini nimelijibu sana na inarejea tena na tena.
Udini ni kutumia imani yako kukandamiza wale wasiokuwa wa imani yako.

Mimi nieandika historia ya mchango wa Waislam katika uhuru wa Tanganyika.
Sababu ya kufanya utafiti huu na kuandika kitabu ni kuwa historia ya uhuru iliwafuta Waislam.

Ikiwa unanisoma utaona mengi ambayo hukuwa unayajua.

Ningekuwa muflisi nisngekuwa napata mialiko kuzungumza kwenye radio na televisheni nyingi hapa nyumbani wala vitabu nilivyoandika visingekuwa maarufu.

Angalia watu wangapi wanafuatilia huu uzi utaujua ukweli.
 
Kwako Mwwnyekiti wa UWT Taifa.
Hata kwetu tusio wanachama wa CCM.

Taasisi unayoiongoza ni kubwa na imebeba sehemu historia ya Tanzania

Hivi karibuni kuna kuna mwandishi aliandika shutuma kubwa dhidi yako kuwa eti hustahili kuwa Mwenyekiti wa UWT, kwa kuwa wewe ulishiriki kuwakandamiza Waislam pale Chuo Kikuu cha Dodoma kwa kuzuia kujengwa msikiti na hatimaye kuwafukuza Watumishi 11 Waislam

Mwandishi amebainisha kuwa wewe hustahili kuongoza Jumuia iliyoaasisiwa na Waislam kina Bibi Titi Mohamed na Leo unawanyanyasa Waislam.

Mama hizi shutuma ni nzito sana kwako kukaa kimya bila kusema lolote haina afya kwako wala chama chako.

Tafadhali jibu shutuma hizi Waislam wajue pumba na mchele,
kinyume chake Umma wa Waislam hautakuelewa.

Andiko hili lipo JamiiForums tangu Oktoba 23 2021
 
Kumekucha Vema Asubuhi Hii Naona Atakuja Kukujibu Soon
 
Kuna baadhi ya watu chuki dhidi ya dhehebu au dini nyingine wanadhani ni sehemu ya ibada na kumpendezesha Mungu wakidhani wao ndio wako sahihi katika kumuabudu Mungu na wengine ndio wakosaji na wafuasi wa shetani.

Na hufanya kila jitihada kukwamisha ibada na maendeleo yao wakidhani wanapata wokovu au thawabu! Bahati mbaya kwao wasichofahamu kuwa Mungu ndie anayejua usahihi wa matendo yetu!

Shutuma hizi anapaswa azijibu.
 
Wakawaulize TISS ,huyo mama wanamwonea,nasikia wao waislam walianza kujitwalia nasafi nyeti serikali iliposhtuka wakamwondoa mkuu wa chuo,alieletwa mpya wakamfanyizia navyosikia,hapo unataka wachukue hatua gani zaidi yakusambalatisha hako kakikundi
 
Wakawaulize TISS ,huyo mama wanamwonea,nasikia wao waislam walianza kujitwalia nasafi nyeti serikali iliposhtuka wakamwondoa mkuu wa chuo,alieletwa mpya wakamfanyizia navyosikia,hapo unataka wachukue hatua gani zaidi yakusambalatisha hako kakikundi
Aise wasingeingilia UDOM kilikuwa kinakuwa a Muslim University. Walianza hadi kuwakamata mabinti wanaovaa nguo fupi!
 
Mimi ni mwislamu,na huyo mama namjua sana toka akiwa mkuu wa chuo cha ualimu butimba mwanza,ni mama ambae anahitsji huruma ya watu,kwani alibahatika kupata watoto 2 tu, mmoja wa kike na mmoja wa kiume na wote walikufa wakiwa watu wazima,tumhurumie mama huyu,haya maneno ya nini jamani
 
Back
Top Bottom