Gazeti la The Economist: Rais Magufuli na CCM kuendelea kushika madaraka baada ya Uchaguzi Mkuu

Gazeti la The Economist: Rais Magufuli na CCM kuendelea kushika madaraka baada ya Uchaguzi Mkuu

CCM ya 2015 ilikuwa imedhoofika ndio maana ilibidi Halmashauri Kuu umuagize Katibu Mkuu afanye ziara nchi zima ili kuimarisha.

CCM ya 2015 ilikuwa na wanachama ambao hata kuvaa sare zao za chama waliogopa!

CCM ya 2015 ilianza kukosa uungwaji mkono kwenye kundi la wananchi wa kipato cha chini kutokana na utendaji wa serikali yake.

CCM ya wakati wa sasa ni tofauti sana na kwa msingi huu, wapinzani wana wakati mgumu sana katika Uchaguzi Mkuu.

Ngoja mruhusu mikutano ya siasa ndio mtashangaa,

Wana ccm wengi wanajidanganya kwa kuhisi wanainchi wote wanahangaika na ndege, au madaraja, wakati hali haiko hivyo
 
Wangesema Jamaa ni Dikteta ungetokwa jasho hadi kwenye meno
Nadhani huu utafiti na angalizo la hili gazeti umewafanya viongozi wetu wa upinzani kuingiwa na hofu/wasiwasi na kuanza kutafuta nguvu za kisiasa na kiuchumi kutoka nje ya mipaka ya nchi!

Hii sentesi ya INTELLIGENCE UNIT isemayo, ‘’Under the leadership of John Magufuli, the long-standing ruling party, the CCM, will retain a firm grip on power’’, imetoa ujumbe ambao vyama vya upinzani kama havitajipanga vizuri kuna uwezekano wa kujikuta bunge lina idadi ndogo sana ya wabunge wa upinzani na pia halmashauri za miji na Majiji zikiangukia kwenye mikono ya CCM!

Sio ajabu kuona kwa sasa viongozi wetu wa upinzani wanashindana kwenda nje ya nchi kutafuta msaada wa kisiasa na kifedha!

Kitochi Original
 
Hilo gazeti lilichokifanya pamoja na kuwa halimpendi Magufuli LINALENGA kuwaonya wafadhili wa nchi zao kuwa wasiingie mkenge kuwachangia pesa upinzani walioanza kujipitisha pitisha huko nje ya nchi kwenye nchi zao kuwa ni matapeli wala hawana nia ya kushinda wanawinda pesa tu dakika hizi za majeruhi wazitafune kuelekea uchaguzi mkuu

LInatoa warning signals
Likewise linatoa signal kwa mabeberu wanaotaka kuwekeza bongo kwamba CCM ipo sana tu, kama hawakubaliani na sera zake sasa, then wasitarajie mabadiliko baada ya uchaguzi....Kwa hivyo wawe makini wasipoteze pesa zao...

Hii ina maana FDI zitazidi kupungua na ajira kuota mbawa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
INTELLIGENCE UNIT ni sehemu ya kitengo ndani ya Gazeti la The Economist ambacho hufanya uchunguzi na utafiti wa kisiasa na kiuchumi kwa nchi mbali mbali duniani na kutoa matokeo au matarajio.

Kitengo hiki cha kiuchunguzi kina wafanyakazi wabobezi zaidi ya 100 duniani ambao hutoa tafiti na utabiri baada ya uchunguzi kuhusu masuala ya kiuchumi kwa nchi mbali mbali kila mwanzo wa mwaka kulingana na mazingira halisi.

Ikumbukwe kuwa gazeti la The Economist limekuwa mwiba mkali hasa kwa Rais Magufuli kwa sababu linaamini sera za kisiasa na kiuchumi za Rais Magufuli zinaenda kinyume na mtazamo/msimamo wa kisiasa na kiuchumi wa gazeti hili.

Kwenye suala la kiuchumi, The Economist linaamini katika Ubinafsishaji na kuachia uchumi huru bila ya serikali kuingilia kati. Kwenye suala la kijamii, The Economist linaamini katika ndoa za jinsia moja na kuhalalisha utumiaji wa baadhi ya madawa ya kulevya kama bangi.

Ukitaka kujua msimamo wa Gazeti la The Economist kuhusu masuala ya kisiasa na kiuchumi;
GONGA LINK HII>>>Is The Economist Left or Right Wing

Hata hivyo linapofika suala la uchambuzi na utafiti, gazeti la The Economist hutoa matokeo ya tafiti na utabiri kama ambavyo jopo la wachunguzi wake limeona na kufikia hitimisho.

Kwenye masuala ya kisiasa nchini, jopo la wachunguzi wa INTELLIGENCE UNIT limesema baada ya Uchaguzi Mkuu, Rais Magufuli na CCM wataendelea sio kutawala tu bali pia watahodhi kwa kiwango kikubwa madaraka ya nchi.

Kwenye masuala ya kiuchumi limesema pamoja na kwamba serikali ya Rais Magufuli imeonesha mipango na nia ya kuboresha uwajibikaji katika sekta za umma na kuboresha maisha ya wananchi lakini inakabiliwa na uwezo mdogo kifedha.

INTELLIGENCE UNIT imebainisha kuwa, kutokuwa na utungaji sera ulioeleweka nchini kutawafanya wawekezaji kuogopa kuwekeza nchini, hata hivyo matarajio kwa nusu ya mwaka yanaonekana kuwa imara kutokana na kukua kwa sekta ya utoaji huduma nchini na uwekezaji kwenye miundombinu kitaifa.

Ukitaka kusoma repoti yote;
GONGA LINK HII>>>ENTELLIGENCE UNIT: Tanzania political and economic forecast

Maghufuli atakuwa amekubali kusaini ule mkataba wa EPA unaozihusisha nchi 6 za Africa.
 
Nisilo elewa mimi na hii elimu yangu mangungu ni kuwa inakuwaje kwenye uhakika huo wa ushindi bado ccm inakosa confidence?
Haitaki kutoa nafasi sawa za kufanya siasa, imewaamuru Polisi kuwadhibiti wapinzani kila kona, haitaki Tume huru ya uchaguzi na mengineyo ya aina hiyo? Unauhakika wa ushindi inakuwaje uwahonge na kuwatisha marefa?
Nadhani hata hao wabobezi wa Economist wameliona hilo kuwa kwa vile hali ni hiyo basi hakuna namna lazima wajitangaze ushindi

Sent using Jamii Forums mobile app
Chama makini hakiwezi kubweteka eti kwa sababu kinajua kitashinda Uchaguzi Mkuu.

Huwezi kukuta eti timu kama Liverpool FC eti hawafanyi mazoezi na haijiandai kupambana na timu iliyoko kwenye nafasi ya mwisho katika league eti kwa sababu wanajua watashinda mchezo. Kama kujiandaa kwa CCM katika Uchaguzi Mkuu ni kukosa confidence basi acha waendelee kukosa confidence!

Sio kazi ya CCM kutoa nafasi sawa za kufanya siasa au kuwaamuru polisi kuwadhibiti wapinzani bali hiyo ni kazi ya serikali kama unachokisema kipo. Sijaona wapinzani wakitakazwa kufanya siasa au polisi kuwadhibiti wapinzani.
 
T

The economist hawa wanafiki tu!
Sasa ndo wanajifanya kuanza kubalance story sio?
Too late, tulishawastukia siku nyingi sana. Maleongo yao na wanayemtumikia tunayajua hata mkijifanya leo mnakuwa neutral na kuanza kuuona ukweli.
Mkuu;
Wao wametoa ukweli kwa kile wanachokiona kwa sababu hawawezi kupingana na ukweli ulio njiani kuwafikia baada ya Uchaguzi Mkuu!
 
Likewise linatoa signal kwa mabeberu wanaotaka kuwekeza bongo kwamba CCM ipo sana tu, kama hawakubaliani na sera zake sasa, then wasitarajie mabadiliko baada ya uchaguzi....Kwa hivyo wawe makini wasipoteze pesa zao...

Hii ina maana FDI zitazidi kupungua na ajira kuota mbawa

Sent using Jamii Forums mobile app
Haina shida CIA wanajifanya wako highly informed swali dogo tu kwao Zitto Kabwe,Mbowe na Seif Shariff Hammad Ni wapinzani na viongozi wa upinzani Tanzania? Sihitaji wajibu humu watajijua who cares in Tanzania?
Current CIA are stupid .The best CIA was in the 1960s !!! The current CIA they are crap and stupid to hell with them .
 
Maghufuli atakuwa amekubali kusaini ule mkataba wa EPA unaozihusisha nchi 6 za Africa.
Tatizo la CIA wanajifanya much knowlegge kumbe wajinga tu 2015 nilikuwa Zanzibar nikakutana na CIA operative kisichana kidogo kililewa kikasema Zanzibar CCM haishindi nikakiuliza why kikasema ooh Mimi mjerumani wa Namibia mtalii Lakini taarifa za CIA Marekani zinasema serikali ya Zanzibar lazima ichukuliwe na CUF na lazima Seif Shariff Hamad awe Raisi na Raisi Wa Tanzania awe Lowasa mlutheri
Likewise linatoa signal kwa mabeberu wanaotaka kuwekeza bongo kwamba CCM ipo sana tu, kama hawakubaliani na sera zake sasa, then wasitarajie mabadiliko baada ya uchaguzi....Kwa hivyo wawe makini wasipoteze pesa zao...

Hii ina maana FDI zitazidi kupungua na ajira kuota mbawa

Sent using Jamii Forums mobile app
Kifupi CIA ya Sasa Ni wapumbavu wakumbwa wanategemea oppsisdition iwape information bila ku cross check aurhenicity ya hizo information from realiable independent party!!!!!!! President Trump tumbua CIA leaders they are feeding you craps.Ulisema wazi kuwa Marekani ilikosea kuua Gaddafi na Saddam Hussein.You were Right .The Current CIA leadersb are hooligans who
Doesn't know their works .Trump.make changes Quickly
 
Kwahiyo nawe umekubaliana na hili gazeti kwamba serikali ya Meko INA uwezo mdogo kifedha?

Mwenyewe (Meko) si ndiye amekuwa akituaminisha kwamba serikali yake ni ya kitajiri na kwamba nchi hii ina uwezo hata wa kutoa misaada kwa nchi nyingine!

Tukisema Meko kaharibu uchumi wetu mnapinga.
Hii nchi uchumi uko hoi tofauti na ilivyokuwa enzi za Kikwete na Mkapa.

Standard ya maisha ya watu inazidi kushuka kila iitwapo leo. Watanzania hawana uhakika hata wa milo miwili kwa kutwa.

Si watumishi wa umma, wafanyabiashara, wakulima, wamachinga na hata wavuvi wanaofurahia maisha, wote wamepigika. Leo nyanya moja inauzwa kwa sh. 500 lakini bado Meko na serikali yake ya kidhalimu wanataka kutuaminisha kwamba maisha ya watanzania ni mazuri.

Nakuhakikishia kwamba CCM na huyo dikteta wenu mtapata taabu sana kwenye kampeni za uchaguzi 2020. Sijui mtawaambia mini wananchi hawa waliopigika.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu;
Umeandika, ''Nakuhakikishia kwamba CCM na huyo dikteta wenu mtapata taabu sana kwenye kampeni za uchaguzi 2020. Sijui mtawaambia mini wananchi hawa waliopigika''.

Wakati wewe unawaza kuhusu CCM na unayemuita dikteta kupata taabu wakati wa kampeni, gazeti la The Economist wanasema, ‘’Under the leadership of John Magufuli, the long-standing ruling party, the CCM, will retain a firm grip on power’’
 
Magazeti mengine yanaharibu tu fursa za kupiga pesa hasa ukizingatia huu ni mwaka wa mavuno kwa wapinzani kutoka kwa watoa misaada wetu wa nje.
Duh!
Niliposoma maoni yako imenibidi nicheke tu!
 
Hilo gazeti lilichokifanya pamoja na kuwa halimpendi Magufuli LINALENGA kuwaonya wafadhili wa nchi zao kuwa wasiingie mkenge kuwachangia pesa upinzani walioanza kujipitisha pitisha huko nje ya nchi kwenye nchi zao kuwa ni matapeli wala hawana nia ya kushinda wanawinda pesa tu dakika hizi za majeruhi wazitafune kuelekea uchaguzi mkuu

LInatoa warning signals
Sio kwamba wanajaribu kubalance mambo ili Kabendara aachiwe?!?
 
MsemajiUkweli,

Swala la idadi ndogo ya wabunge wa upinzani me sitaki kuamini Coz kila uchaguzi huwa tunahisi hivyo na matokeo yake ndio kwanza wanajaa,

Me nadhani watanzania wanawaamini sana upinzani kwenye ubunge kuliko kwenye urais

Na la urais linakuwa gumu sana hasa kwenye kuunda serikali bcoz upinzani hawana watu ambao wanaweza kusema wanaunda serikali

..kwani ccm iliajiri watumishi.wapya serikalini?

..huwezi kusema kwamba ktk Tz hii hakuna watu wa kutosha wa kuteuliwa ikiwa wapinzani watachukua dola.

..kama ulimaanisha mawaziri, siyo lazima mawaziri wote watoke chama kilichoshinda nafasi ya Uraisi.

..Vilevile usisahau kipengele cha katiba kinachosema Waziri Mkuu atatokana na chama chenye wabunge wengi bungeni au anayeungwa mkono na wabunge wengi. Katiba yetu imeona uwezekano wa vyama tofauti kushinda Uraisi na majority bungeni.
 
I believe wewe ndie mjinga namba moja kuleta vitu visivyo na sababu halafu unataka werevu wajadili, considering ulivyoisifia hiyo Intelligence Unit ya hao jamaa zako.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu;
Hakuna yeyote aliyelazimishwa kujadili thread yangu!

Wewe kama ni mwerevu na unadhani hii thread haina sababu basi nenda kwenye thread zenye sababu ya kujadili!

Kumbuka gazeti la The Economist limeandika, "Under the leadership of John Magufuli, the long-standing ruling party, the CCM, will retain a firm grip on power".
 
Hebu kiruhusu kichwa chako kitafakari basi Bingwa. 2010 Dr. Slaa alimshinda a serving Preaident? Halafu 2015 CDM ikiwa ina nguvu na maarufu mara dufu ya 2010 na DR. Slaa akiwa maarufu mara dufu ya 2010, CCM wakiwa wamemuweka mgombea asiye maarufu na kukiwa na mpasuko mkubwa. CDM ikamwacha Dr.Slaa aliyekuwa ametoka kumshinda Rais aliyeko madarakani 2010 na kumuweka Lowassa aliyekuwa ana siku tatu amehama toka CCM na nembo ya ufisadi Tanzania kwa mujibu wa CDM yenyewe. Kama unachosema ni kweli basi inawezekana CDM 2015 mmeweka record na waliochukua maamuzi hayo ni mbumbumbumbu kweli kweli!
Mkuu;
Nimeyapenda maoni yako!

Unajua kuna baadhi ya watu wanaandika tu bila kujua mantiki ya kile wanachokiandika!

Yaani eti aliyeshinda Uchaguzi Mkuu 2010 anawekwa kando kwenye Uchaguzi wa 2015 ili kumpisha mgombea ambaye amehamia ndani ya chama siku tatu zilizopita!

Halafu huyo mgombea anayedaiwa mwaka 2015 alishinda anaamua pia kukiacha chama ambacho wanachama wake mpaka sasa wanapiga kelele wakidai alishinda uchaguzi mkuu 2015!

Hivi vituko utavikuta tu kwa watu ambao hawajui kwa nini wanashindwa katika chaguzi kuu!
 
Back
Top Bottom