GEITA: Wananchi wavamia kituo Cha Polisi, wawili wauawa

GEITA: Wananchi wavamia kituo Cha Polisi, wawili wauawa

Nmecheka kwenye msiba
Aisee mpaka wazo langu la kuishi vijijini limenikata.. kuna matukio ma3 yamenichosha 1. Yule mganga alokua anaua watu na wenzie wanawazika wamekaa
2. Mauaji mauaji tu yasioeleweka na uvamizi
3. La leo hili wamefata mkumbo matokeo ndo hayaa
Aisee 🤣🤣 nmecheka kama mazuri
Hahaha ujinga jumuishi ni mbaya sana
 
Na wewe ungekuwa makini kichwani ungeichukua hii hadithi ya Afande with a grain of salt.

Mabomu ya machozi na maji ya kuwasha siku hizi hayawashi enough ?

Hakunaga reinforcement za askari zinazoweza kuja kutuliza ghasia bila ku shuti point blank ?

Watoto walikuwa wanatoka kwa wifi yake, walikuwa wanae, hamjasikia mjomba kabaka mtoto mpaka kaua, baba mtu kauza mtoto, hakunaga ? Ilikuwaje kuwaje kama watoto ni wao wananchi wakakataa na ikafika vurugu ?


Unabugiaje nzima nzima taarifa ya mtu ambae yeye siku zote ndie prime suspect wa majority ya vifo tata ?
Mtoto ambaye huna uhusiano naye mbona inajulika tu chap.
 
Vijana wawili wamefariki dunia hii leo Septemba 11, 2024 baada ya wananchi 800 kuvamia na kufanya vurugu katika kituo cha polisi Lulembela wilayani Mbogwe mkoani Geita vurugu zilizoanzia katika eneo la mnada wa Lulembela baada ya watu wawili kuonekana wakiwa wamebeba watoto wawili na wananchi waliokuwa katika mnada huo kuwahisi kuwa ni wezi wa watoto na kuanza kuwashambuilia, ndipo akatokea Mtendaji wa Kata akawabeba kwenye pikipiki na kuwakimbiza katika kituo cha Polisi Lulembela.

Ambapo baada ya watu hao kufikishwa katika kituo cha polisi, wananchi hao walifika katika kituo hicho na kuwataka askari polisi wawakabidhi watuhumiwa hao ili wawaue na Askari walijaribu kuwaelimisha na kuwaeleza ni kosa na si vizuri kujichukulia sheria mkononi lakini walikaidi na baada ya askari kuona hali hiyo ya kuhatarisha maisha ya watu na mali za serikali walitumia mabomu ya machozi ili kuwatawanya watu hao na iliposhindikana walitumia silaha za moto kwa kupiga risasi juu ili watu hao watawanyike

"Mbali na kushambulia kituo hicho kwa mawe na kutaka kuingia kwa nguvu ndani ya kituo hicho, wananchi hao walichoma moto gari moja lenye namba za usajili T.440 ATW aina ya Toyota Cardina lililokuwa limeegeshwa nje ya kituo hicho na katika vurugu hizo watu wawili wamepoteza maisha, mmoja ni mwanaume anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 18 hadi 20 na wa pili ni msichana aitwaye Teresia John mwenye umri wa miaka 18, mwanafunzi wa kidato cha nne Shule ya Sekondari Lulembela ambaye nyumba yao inatazamana na kituo hicho cha Polisi," imeeleza taarifa ya Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini

Aidha taarifa hiyo imeongeza kuwa, "Hata hivyo, ilibainika kuwa watu waliokuwa wamebeba watoto hao ni Emanuel John (33) mkazi wa Kigamboni Lulembela ambaye alikuwa amembeba mtoto wake aitwaye Ikram Emanuel mwenye umri wa mwaka mmoja na miezi kumi na moja na wa pili anaitwa Ng'amba Leonard (24) ambaye alikuwa amembeba mtoto aitwaye John Emanuel mwenye umri wa miaka miwili na miezi nane, Mama wa watoto hao aitwaye Rachel Luhende (22) amethibitisha kuwa watoto hao ni wakwake na walikuwa kwa wifi yake ambapo baba yao mzazi na mjomba wao walikwenda kuwachukua,".

#EastAfricaRadio

View attachment 3093573
CCM wanatupeleka wapi?
 
Vijana wawili wamefariki dunia hii leo Septemba 11, 2024 baada ya wananchi 800 kuvamia na kufanya vurugu katika kituo cha polisi Lulembela wilayani Mbogwe mkoani Geita vurugu zilizoanzia katika eneo la mnada wa Lulembela baada ya watu wawili kuonekana wakiwa wamebeba watoto wawili na wananchi waliokuwa katika mnada huo kuwahisi kuwa ni wezi wa watoto na kuanza kuwashambuilia, ndipo akatokea Mtendaji wa Kata akawabeba kwenye pikipiki na kuwakimbiza katika kituo cha Polisi Lulembela.

Ambapo baada ya watu hao kufikishwa katika kituo cha polisi, wananchi hao walifika katika kituo hicho na kuwataka askari polisi wawakabidhi watuhumiwa hao ili wawaue na Askari walijaribu kuwaelimisha na kuwaeleza ni kosa na si vizuri kujichukulia sheria mkononi lakini walikaidi na baada ya askari kuona hali hiyo ya kuhatarisha maisha ya watu na mali za serikali walitumia mabomu ya machozi ili kuwatawanya watu hao na iliposhindikana walitumia silaha za moto kwa kupiga risasi juu ili watu hao watawanyike

"Mbali na kushambulia kituo hicho kwa mawe na kutaka kuingia kwa nguvu ndani ya kituo hicho, wananchi hao walichoma moto gari moja lenye namba za usajili T.440 ATW aina ya Toyota Cardina lililokuwa limeegeshwa nje ya kituo hicho na katika vurugu hizo watu wawili wamepoteza maisha, mmoja ni mwanaume anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 18 hadi 20 na wa pili ni msichana aitwaye Teresia John mwenye umri wa miaka 18, mwanafunzi wa kidato cha nne Shule ya Sekondari Lulembela ambaye nyumba yao inatazamana na kituo hicho cha Polisi," imeeleza taarifa ya Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini

Aidha taarifa hiyo imeongeza kuwa, "Hata hivyo, ilibainika kuwa watu waliokuwa wamebeba watoto hao ni Emanuel John (33) mkazi wa Kigamboni Lulembela ambaye alikuwa amembeba mtoto wake aitwaye Ikram Emanuel mwenye umri wa mwaka mmoja na miezi kumi na moja na wa pili anaitwa Ng'amba Leonard (24) ambaye alikuwa amembeba mtoto aitwaye John Emanuel mwenye umri wa miaka miwili na miezi nane, Mama wa watoto hao aitwaye Rachel Luhende (22) amethibitisha kuwa watoto hao ni wakwake na walikuwa kwa wifi yake ambapo baba yao mzazi na mjomba wao walikwenda kuwachukua,".

#EastAfricaRadio

View attachment 3093573
Ndo tunachotengeneza hapa
 
Imefika hatua Sasa ukiwa mkoani ukikshika katoto ka ndugu yako kakilia na kukukataa tu tayari unauliwa
 
Hii kwa mazingira ya sasa ya viongozi wenye viburi, dharau,ujuaji na wizi wa mali za taifa ni jambo zuri na inaweza kuwa mwanzo wa kuwawajibisha kama raia wataendelea na misimamo.
Kwa upande mwingine huu ndio mwanzo wa Civil disobedience to the law and order kama matokeo ya wao kutosikilizwa na kutendewa haki kwa mujibu wa sheria na katiba ya taifa letu.

Ushauri kwa ng'ombe zinazoleta shida huko serikalini na kuwa kisababishi cha machungu kwa raia ja kuwanyima amani ni kutojiamini kiasi hicho sababu ipo siku hamtaamini kitakachowakuta. Hawa hawa raia wapole wasio na makuu watakuwa adhabu yenu hapa ardhini na hamtaamini kitachowakuta.
 
Hii kwa mazingira ya sasa ya viongozi wenye viburi, dharau,ujuaji na wizi wa mali za taifa ni jambo zuri na inaweza kuwa mwanzo wa kuwawajibisha kama raia wataendelea na misimamo.
Kwa upande mwingine huu ndio mwanzo wa Civil disobedience to the law and order kama matokeo ya wao kutosikilizwa na kutendewa haki kwa mujibu wa sheria na katiba ya taifa letu.

Ushauri kwa ng'ombe zinazoleta shida huko serikalini na kuwa kisababishi cha machungu kwa raia ja kuwanyima amani ni kutojiamini kiasi hicho sababu ipo siku hamtaamini kitakachowakuta. Hawa hawa raia wapole wasio na makuu watakuwa adhabu yenu hapa ardhini na hamtaamini kitachowakuta.
Haya mambo hayajaanza Leo Toka miaka ya 90
 
Mob justice ipo sana Tanzania, lakini unakuta wengi waliouawa hawana hatia , ni mihemuko tu. Mfano kwa mwaka jana zaidi ya watu 500 wameuwawa sababu hiyo (LHRC report). Watanzania hawawezi kuandamana hata bei ya mafuta au sukari au wizi wa mabilioni inayofanywa na baadhi ya watumishi wa serikali ambavyo kwa asilimia kubwa vinaathiri maisha yao na kupelekea mwananchi kuwa maskini na kuendelea kuwa wajinga.
Yaah wengi hawana hatia aisee, wanaacha kupambana na wanasiasa wanao order hayo mambo kwa ajili ya makafara wanachagua watu wanaowamudu na wasio na hatia..
 
Polisisiemu waache uongo ,watu 800 wavamie kituo cha polisi halafu polisisiemu watoke salama hata kama wana silaha?
 
Tunakoelekea wananachi wameanza kuona kumbe yawezekana kumalizana na mapolice.

Wananchi ni kama wameanza kuwa sugu, ilikuwa Simiyu sasa Geita.

Mambo yanachangamka.
 
Ww bado Hujielewi, kilichotokea sio kigeni huko kanda ya ziwa na wala hakihusiani na siasa. Sasa inakuaje unaongea upuuzi.
wewe ndio hujaelewa ama unaogopa ulichokielewa.
Kinachoongelewa hapo ni nguvu ya umma, upo sawa kwa mantiki hapo haijatumika kisiasa, bsli hujaelewa anachokiongelea mwenzio kuwa, nguvu hiyo ikiingia siasani hapo ndipo ukombozi utapatikana na hicho ndicho ukiogopacho na kukiita upuuzi.
 
Vyombo vya usalama Hali hii mnaistawisha kwa kas nyie wenyewe
Ndich nilitaka kusema, akili ya binadam akijiona hayuko salama anaishi kwa hofu anakuwa anaongozwa na mihemuko.. anakuwa anachukua maamuzi kwa kukurupuka n

Kitendo cha wimbi la utekaji watoto na watu wazima na kuuawa .. huku Vyombo vya usalama vikionekana kama havilivalii njuga hili swala matokeo yake ndo haya .. watu wanatoana uhai kwa mihemuko

Ni kama yale ya wezi kuchomwa moto..
 
Ndich nilitaka kusema, akili ya binadam akijiona hayuko salama anaishi kwa hofu anakuwa anaongozwa na mihemuko.. anakuwa anachukua maamuzi kwa kukurupuka n

Kitendo cha wimbi la utekaji watoto na watu wazima na kuuawa .. huku Vyombo vya usalama vikionekana kama havilivalii njuga hili swala matokeo yake ndo haya .. watu wanatoana uhai kwa mihemuko

Ni kama yale ya wezi kuchomwa moto..
MAANA YAKE UMMA UNAHISI JESHI LA POLISI LIMEPIGWA GANZI, Linasubiri kupata maagizo ya kuishughurikia CDM viongozi wake wapande cheo
 
Back
Top Bottom