MamaSamia2025
JF-Expert Member
- Mar 29, 2012
- 14,588
- 32,361
Maskini na wapumbavu 800 wakijikusanya na kuamua lazima walete uharibifu. Katika hao washenzi 800 walioleta vurugu kuna ambao watakiona cha moto.Watu 800 hawawezi kukosea
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Maskini na wapumbavu 800 wakijikusanya na kuamua lazima walete uharibifu. Katika hao washenzi 800 walioleta vurugu kuna ambao watakiona cha moto.Watu 800 hawawezi kukosea
Haohao masikini na wapumbavu,kwa kadiri ya ufinyu wa akili zako,wakiamua ulale umevaa kama unaenda kusali hawashindwi.Kama unabisha,waulize wanajeshi hodari wa Misri kilichowakuta hadi wakakimbia na kuvua magwanda huku wanapiga yowe.🤔Maskini na wapumbavu 800 wakijikusanya na kuamua lazima walete uharibifu. Katika hao washenzi 800 walioleta vurugu kuna ambao watakiona cha moto.
Kwahiyo hao watu 800 ndio wanawajua zaidi hao watoto kuliko wazazi wao ambao wamethibitisha kua hao watoto ni wao? punguza mihemko mkuu,just use a simple logic to understand it,Hapa Kuna maswali mengi kuliko majibu!! Watu 800+ wasingizie watu wawili kweli?
Hamia MisriHaohao masikini na wapumbavu,kwa kadiri ya ufinyu wa akili zako,wakiamua ulale umevaa kama unaenda kusali hawashindwi.Kama unabisha,waulize wanajeshi hodari wa Misri kilichowakuta hadi wakakimbia na kuvua magwanda huku wanapiga yowe.🤔
Kwahiyo hawakutakiwa kua na watoto wao hapo mnadani kisa tu kwavile hakuna watu wengine wenye watoto wao hapo Mnadani?Ina maana hapo mnadan ni wao tuu ndio walikuwa na watt
Nahamia Mbogwe si muda mrefu nikitokea Ibadakuli.Karibu ule michembe na nswalu.Hamia Misri
Acheni kulishana ujinga mtaendela kuliwa kama kuku.Hizi ni salamu kuwa inawezekana.
Heshima itakuwepo na ujingaujinga utatokomea maporini.Duh,Watu wamechafukwa kweli kweli.Sipati picha kama hali ikiwa hivyo kwenye kila eneo ambalo inaonekana haki haitendeki
Acha akili zako za ajabu.Watauawa wote?Unawajua waru wakichukia na kuhamasishana wafanye jambo?Wewe baki nyumbani tu unachambua maharage mabovu.Acheni kulishana ujinga mtaendela kuliwa kama kuku.
Si ni juzi tu apa aliuliwa raia ktk mazingira kama ayo ya kituo cha polisi?
Ni hatua gani raia mlichukua baada ya polisi kukatisha maisha ya hao raia ?
Si kila mmoja yupo kwake ameufyata mkia kmya huku mkiaziacha familia za wafiwa na majonzi ya kuondokewa na mpendwa wao ?
Ni afadhali mgekinukisha basi kuwa hatua zichukuliwe kwa hao askar
ila ivo mnavyofanya vurugu mkiuliwa wawili watatu mnaishia kuufyata mkia sio poa.
Wengine wamejiunga tu bila hata kujua kunaniniKwann? Una uhakika Gani watu 800 wote waseme uongo?
Mob justice.Watu wakichukia na kuhamasishana kufanya lolote,hakuna wa kukinga ugoko wala bunduki vitafaa kuwatuliza.Haki itawale.Wengine wamejiunga tu bila hata kujua kunanini
Mshangazi 😛Kokorikooooo ..!
Hawauwawi wote ila ni faida gani wamepta baada ya kufanya izo vurugu zao apo kituo cha polisi?Acha akili zako za ajabu.Watauawa wote?Unawajua waru wakichukia na kuhamasishana wafanye jambo?Wewe baki nyumbani tu unachambua maharage mabovu.
Faida utaiona tukio lingine likitokea.Hawauwawi wote ila ni faida gani wamepta baada ya kufanya izo vurugu zao apo kituo cha polisi?
Ukombozi utoke kwa watu wajinga wanaojichukulia maamuzi bila hta kujiridhishaUkombozi wa Nchi hii utatoka Kanda ya Ziwa. Hizi ni salaam kuelekea uchaguzi mkuu 2025 hawataogopa Cha police Wala mabomu
Mambo haya yamelelewa na serikali ya Chifu Hangaya hadi imefika wakati sasa binadamu hatuaminiani. Mtendaji wa Kata ashukuriwe sana kwa kuokoa roho za wananchi hawa, vinginevyo wangeuawa.Vijana wawili wamefariki dunia hii leo Septemba 11, 2024 baada ya wananchi 800 kuvamia na kufanya vurugu katika kituo cha polisi Lulembela wilayani Mbogwe mkoani Geita vurugu zilizoanzia katika eneo la mnada wa Lulembela baada ya watu wawili kuonekana wakiwa wamebeba watoto wawili na wananchi waliokuwa katika mnada huo kuwahisi kuwa ni wezi wa watoto na kuanza kuwashambuilia, ndipo akatokea Mtendaji wa Kata akawabeba kwenye pikipiki na kuwakimbiza katika kituo cha Polisi Lulembela.
Ambapo baada ya watu hao kufikishwa katika kituo cha polisi, wananchi hao walifika katika kituo hicho na kuwataka askari polisi wawakabidhi watuhumiwa hao ili wawaue na Askari walijaribu kuwaelimisha na kuwaeleza ni kosa na si vizuri kujichukulia sheria mkononi lakini walikaidi na baada ya askari kuona hali hiyo ya kuhatarisha maisha ya watu na mali za serikali walitumia mabomu ya machozi ili kuwatawanya watu hao na iliposhindikana walitumia silaha za moto kwa kupiga risasi juu ili watu hao watawanyike
"Mbali na kushambulia kituo hicho kwa mawe na kutaka kuingia kwa nguvu ndani ya kituo hicho, wananchi hao walichoma moto gari moja lenye namba za usajili T.440 ATW aina ya Toyota Cardina lililokuwa limeegeshwa nje ya kituo hicho na katika vurugu hizo watu wawili wamepoteza maisha, mmoja ni mwanaume anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 18 hadi 20 na wa pili ni msichana aitwaye Teresia John mwenye umri wa miaka 18, mwanafunzi wa kidato cha nne Shule ya Sekondari Lulembela ambaye nyumba yao inatazamana na kituo hicho cha Polisi," imeeleza taarifa ya Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini
Aidha taarifa hiyo imeongeza kuwa, "Hata hivyo, ilibainika kuwa watu waliokuwa wamebeba watoto hao ni Emanuel John (33) mkazi wa Kigamboni Lulembela ambaye alikuwa amembeba mtoto wake aitwaye Ikram Emanuel mwenye umri wa mwaka mmoja na miezi kumi na moja na wa pili anaitwa Ng'amba Leonard (24) ambaye alikuwa amembeba mtoto aitwaye John Emanuel mwenye umri wa miaka miwili na miezi nane, Mama wa watoto hao aitwaye Rachel Luhende (22) amethibitisha kuwa watoto hao ni wakwake na walikuwa kwa wifi yake ambapo baba yao mzazi na mjomba wao walikwenda kuwachukua,".
#EastAfricaRadio
View attachment 3093573
Aiseeee dooooh!Kuna wapuuzi walichoma moto vijana wa watu kisa ishu hizi hizi za kukurupuka. Wabongo kuna muda kama makondoo yakiona mwenzao kaanzisha yanafata tu bila kuhoji.
Dodoma: Wanakijiji Mvumi - Chamwino wachoma moto gari na kuuwa maafisa wa Taasisi ya Kilimo
. Wakuu kuna habari zinasambaa mitandaoni kuwa kuna Maafisa wa Taasisi ya Kilimo ya Seliani iliyopo Mkoani Arusha wameuawa na wanakijiji wa Mvumi. Kukatokea kutokuelewana kati ya maafisa hao na wanakijiji,kiasi cha maafisa hao kuchomwa moto wao na gari lao. Picha zinatisha. Wanakijiji wa Mvumi...www.jamiiforums.com