Gerald Hando: Mbowe aachie ngazi, amekaa sana CHADEMA

Gerald Hando: Mbowe aachie ngazi, amekaa sana CHADEMA

CDM wengi tunaipenda lakini ukweli usemwe, Mbowe kukaa madarakani muda mrefu ni picha mbaya kwa chama.
Mtu mwenye akili timamu lazima upate maswali, kwa mwenendo huo chama kikipewa madaraka ya nchi itakuwaje?
Kwani anachichagua?....au anachaguliwa?
 

Gerald Hando akiwa katika kipindi cha Good Morning cha Wasafi FM leo Machi 7, 2024 ametoa hoja ya kumtaka Mwenyekiti wa CHADEMA kuachia ngazi ya Uenyekiti wa chama hicho kwa kile alichodai amekaa sana, tazama video hapo juu.

Hoja hii inakuja siku chache baada ya kumshuhudia Zitto Kabwe akiachia nafasi ya Uongozi kwenye chama chake Cha ACT Wazalendo.

Upi mtazamo wako kuhusu hoja hii ya Hando?
Huyu mpuuzi ni mwana ccm ya chadema yanamhusu nn..wanataka aachie Ili waweke mtu wao...na sisi hatumtoi...akamwambie na cheyo aachie..
...
 
Mkapa = Mbowe
JK = Mbowe
JPM = Mbowe
Samia = Mbowe

Bob Makani alirithi chama kwa Edwin Mtei, Makani kaoa dada wa Mtei(SHEMEJI). Freeman Mbowe karithi kwa Makani, Mbowe kaoa mtoto wa Mtei (mkwe).

Hicho ni chama cha FAMILIA, mkitaka Mbowe atoke anzisheni chama chenu
Mtaumia sana
 

Gerald Hando akiwa katika kipindi cha Good Morning cha Wasafi FM leo Machi 7, 2024 ametoa hoja ya kumtaka Mwenyekiti wa CHADEMA kuachia ngazi ya Uenyekiti wa chama hicho kwa kile alichodai amekaa sana, tazama video hapo juu.

Hoja hii inakuja siku chache baada ya kumshuhudia Zitto Kabwe akiachia nafasi ya Uongozi kwenye chama chake Cha ACT Wazalendo.

Upi mtazamo wako kuhusu hoja hii ya Hando?
Wapi na wapi,Mugabe wa 1980 na Paulo Bia wa 1959 Hadi Leo yupo na wanampenda
 
Naye amekaa muda mrefu sana hapo Wasafi, inatakiwa aachie ngazi.
 
Naona leo hando kaongea wasiyoyapenda Makamanda.

Hando akiongea wanayoyapenda makamanda utaona anavyosifiwa na kuvikwa ukamanda.
 
Sisi wanachadema ndo wenye maamuzi juu ya mbowe, hatuwezi kushauriwa au kulazimishwa na kenge yyte kuhusu nani awe mkiti wa chadema Taifa...kwa sasa mbowe ataendelea kuiongoza chadema mpk pale na ccm nayo itakaposema imechoka kuongoza nchi hii
 
CDM wengi tunaipenda lakini ukweli usemwe, Mbowe kukaa madarakani muda mrefu ni picha mbaya kwa chama.
Mtu mwenye akili timamu lazima upate maswali, kwa mwenendo huo chama kikipewa madaraka ya nchi itakuwaje?
Mbowe hakai madarakani kimabavu, isipokuwa sisi wanachadema wa chunya na majimbo mengine ndo tunamtaka mbowe aendelee kuwepo kwenye hicho kiti...siku ccm ikiondoka madarakani ndo siku ambayo tutampumzisha mbowe...kwa sasa hatuwezi kulazimishwa na bata yyte kuhusu mstakabari wa chama chetu
 
"Mbowe aachie ngazi amekaa sana Chadema"

Nimeitazama hiyo kauli nimeiona imekaa kidikteta, na sio hiyo kauli ya Hando pekee, wote wanaomtaka Mbowe aachie ngazi nao wamekaa kidikteta hurudia kauli hiyo hiyo wakijidai kutaka demokrasia ifuatwe, hii demokrasia yao ni ya ajabu sana.

Hawa viumbe wanajiona wao ndio wapo juu ya maamuzi ya wengine, hawajui demokrasia inasema wengi wape wachache wasikilizwe, sasa kama wengi wameamua kumpa Mbowe, hawa viumbe wengine wachache kwanini wanateseka?!

Halafu wanaposhangaza zaidi, wanamtaka Mbowe afuate mfano wa Zitto, ni kama vile wanataka kulazimisha Zitto aondoke na Mbowe, sijui wanataka iwe hivyo kwa lengo gani..

Hawajui hata huyo Zitto wanaemuona ameondoka uongozini ACT, anaenda kuwa "mshauri mkuu wa chama" chake kulingana na Katiba yao, hawajui huyu ni sawa na ametoka kwa mlango wa mbele, lakini anarudi ndani kwa mlango wa nyuma, sijui huu ujinga ndio wanataka Mbowe nae aufuate?!.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Zitto hana cha kupoteza kwenye siasa, Mbowe ana vingi vya kupoteza kwenye siasa.

Wanataka atoke ili wapate ahueni tu.
 

Gerald Hando akiwa katika kipindi cha Good Morning cha Wasafi FM leo Machi 7, 2024 ametoa hoja ya kumtaka Mwenyekiti wa CHADEMA kuachia ngazi ya Uenyekiti wa chama hicho kwa kile alichodai amekaa sana, tazama video hapo juu.

Hoja hii inakuja siku chache baada ya kumshuhudia Zitto Kabwe akiachia nafasi ya Uongozi kwenye chama chake Cha ACT Wazalendo.

Upi mtazamo wako kuhusu hoja hii ya Hando?
Shida ya Hando nn?Aseme.Kama tatizo ni muda mrefu mbona tuna vyama vina muda mrefu vinaongoza lakini Bado wananchi wanavitaka.Kama chama Kina muhitaji basi Kuna shida gani.Kuna kiongoz fulan WA michezob kasema atagombea tena mbona hasemi?
 
Pumbavu zake, mbona yeye hajastaafu utangazaji? Ni mwaka wa ngapi anatangaza?
Jinga punga hili bila kutaja mbowe mimba yake inamsumbua,pia yupo dada mmoja clauds 360 aitwa kija sijui anakichwa Cha boxsi kama mabasi ya mwendokasi wanamponda mbowe kwa kutafuta teuzi kwenye lichama lao zee kwanza hajui hata kuvaa sijui anafundishwa na bibi wa nachingwea kuvaa
 

Gerald Hando akiwa katika kipindi cha Good Morning cha Wasafi FM leo Machi 7, 2024 ametoa hoja ya kumtaka Mwenyekiti wa CHADEMA kuachia ngazi ya Uenyekiti wa chama hicho kwa kile alichodai amekaa sana, tazama video hapo juu.

Hoja hii inakuja siku chache baada ya kumshuhudia Zitto Kabwe akiachia nafasi ya Uongozi kwenye chama chake Cha ACT Wazalendo.

Upi mtazamo wako kuhusu hoja hii ya Hando?
Umekosa adabu sana kwa WaTZ
 

Gerald Hando akiwa katika kipindi cha Good Morning cha Wasafi FM leo Machi 7, 2024 ametoa hoja ya kumtaka Mwenyekiti wa CHADEMA kuachia ngazi ya Uenyekiti wa chama hicho kwa kile alichodai amekaa sana, tazama video hapo juu.

Hoja hii inakuja siku chache baada ya kumshuhudia Zitto Kabwe akiachia nafasi ya Uongozi kwenye chama chake Cha ACT Wazalendo.

Upi mtazamo wako kuhusu hoja hii ya Hando?
Hando, demokrasia siyo kitendo cha mtu kukaa muda mfupi madarakani, bali ni kitendo cha kumchaguwa yule wanaemuona ni sahihi. Wanachama wanaona Mbowe bado ni mtu sahihi kuingoza Chadema. Ni kwann husiilaumu CCM kung'ang'ania madaraka ya kuongoza nchi kwa kipindi chote kwa wizi wa kura, rushwa na mabavu?
 

Gerald Hando akiwa katika kipindi cha Good Morning cha Wasafi FM leo Machi 7, 2024 ametoa hoja ya kumtaka Mwenyekiti wa CHADEMA kuachia ngazi ya Uenyekiti wa chama hicho kwa kile alichodai amekaa sana, tazama video hapo juu.

Hoja hii inakuja siku chache baada ya kumshuhudia Zitto Kabwe akiachia nafasi ya Uongozi kwenye chama chake Cha ACT Wazalendo.

Upi mtazamo wako kuhusu hoja hii ya Hando?
Huu woga wa CCM kwa Mbowe, unatoka wapi?
Mara Kesi ya Ugaidi, mara aachie ngazi, woga wa nini?
Mwalimu Julius Nyerere aliongoza TANU na CCM kwa miaka 36.
Matokeo yake, TANU/CCM bado ipo ipo mpaka leo.
Mwacheni Freeman Mbowe achuane na Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere
 
Mkapa = Mbowe
JK = Mbowe
JPM = Mbowe
Samia = Mbowe

Bob Makani alirithi chama kwa Edwin Mtei, Makani kaoa dada wa Mtei(SHEMEJI). Freeman Mbowe karithi kwa Makani, Mbowe kaoa mtoto wa Mtei (mkwe).

Hicho ni chama cha FAMILIA, mkitaka Mbowe atoke anzisheni chama chenu
Mmmh
 
Wananicheka kwanini? Kwa akili yako ndogo unaamini kuwa hao uliwataja watakuja kuwa ma Rais wa Tanzania?

Basi wewe Dr Matola PhD ni mgeni wa siasa za Tanzania.
Soma ulichoandika ukielewe ndipo uhusianishe na majibu ya aliyekujibu. Kichwa panzi nn?
 
CCM mna vichekesho Sana, sasa Zitto si anapewa ubunge Kigoma na wapemba wanachukuwa Chama chao?

Hivi unaamini Wapemba wanaoweza kuongozwa na Zitto?

Hujui kwamba ACT ni kimvuli cha CUF? Base ya ACT ni Zanzibar na lazima Chama kiwe chini ya Wazanzibar na ndicho kilichofanyika, huyo dada atakuwa kiongozi ceremonial tu kama Rais wa Ujerumani na Rais wa Israel, hapo wenye nguvu ni mwenyekiti na makamu wake Jusa.

Hayo ni maigizo ya kisiasa Zitto anarudishiwa Jimbo la Ujiji Kigoma.
Nadhani ni vyema watu wajifunze kujibu hoja kwa hoja.

Mbowe kukaa miaka nenda rudi ni kushindwa katika uongozi hata kama katiba haijatoa ukomo huo na huenda katiba imewekwa hivyo maksudi kabisa.

Kiongozi mzuri ni yule anayeandaa viongozi wengine na kuwaachia nafasi ili wew ubaki kwenye nafasi ya mshauri.

Hongera Zitto kwa kuongoza kwa mfano. Inaonyesha una imani na wanachama wenzako.
 
Back
Top Bottom