Godless Lema amuomba Rais Mpya Samia Suluhu kuchunguza ofisi ya DPP na BoT

Godless Lema amuomba Rais Mpya Samia Suluhu kuchunguza ofisi ya DPP na BoT

Ameomba BOT ifanyiwe uchunguzi Maalum kutokana na dhuluma kwa wenye maduka ya kubadilisha fedha za kigeni , huku akiomba Ofisi ya DPP imulikwe kutokana na kashfa ya Muda mrefu ya kubambikia watu kesi

View attachment 1736882
Sawa mkimbizi, naona Wana saccos mnamwona mh rais Samia Kama rais wa ukawa. Mnamfundisha kazi Kama vile kawaomba mumsaidie.
 
Ameomba BOT ifanyiwe uchunguzi Maalum kutokana na dhuluma kwa wenye maduka ya kubadilisha fedha za kigeni , huku akiomba Ofisi ya DPP imulikwe kutokana na kashfa ya Muda mrefu ya kubambikia watu kesi

View attachment 1736882
Anajaribu kutetea wizi aliokuwa anafanya kupitia Bureau De Change fake yake ya Arusha. Mwambieni arudi alipe madeni aache kukimbia madeni.
 
Angalia content za hayo maombi.Hii inadhihirisha kwamba watu wengi waliumizwa sana na utawala wa Jiwe kwa kubambikiwa kodi,kunyang'anywa fedha za kigeni,kuporwa fedha benki,utekaji na kupokea Ransom kiserikali(Mo Dewji,Roma) na wengine wengi.
Yaani wapinzani wa nchi hii ni bure kabisa mnategemea Rais Samia atawasikiliza akina Lema kweli? Kweli hamjitambui kabisa.
 
Magufuli alikuwa zao la mfumo ambao baada ya upinzani kutukana sna Kikwete mfumo ukaona nyie siio wa kuwachekea

Kikwete aliwachekea hadi akawahonga chai ikulu muache wala hamkuacha

Msidhani Mama Samia atarudia kosa la Kikwete aliyewachekea hadi mkaitisha migomo ya madaktari kupitia akina Ulimboka na Mashinji wengi wakapoteza maisha ikiwemo shangazi yangu kwa kukosa huduma

Raisi Mama Samia atajijua akiwachekea nyie shukrani hamna nyie
Hata Samia asipokuwa kama JK nakuahidi hawezi kuwa na roho mbaya kama marehemu.
 
Nitakua na imani walau na huyu Mama endapo

Ataitisha mchakato wa kupata katiba mpya..na ikapatikana

Kuwepo kwa tume huru ya uchaguzi..

Akiweza hivyo atakua amekua mwanaccm wa tofauti sababu naamimi siku zote CCM ni ile ile mbwembwe kibao ila hakuna jipya!

Ila itapendeza sana mama akiwanyoosha wale wapambe wa jiwe sijui matokeo chanya,Tanzania mpya,MATAGA , na matarumbeta mengineyo hatuwezi kua na mambo ya kusifia hata ujinga hii haikubaliki !
 
Rudi uongelee Tanzania Chadema tuliwaonya ongeleeni sera na vitu vyenye maslahi kwa taifa nyie mkajikita kuhangaika na Ind7ividual Magufuli mkakimbia hadi nchi mnakimbia mtu!!! sabanu hamkuwa politically strategic kuwa na hoja endelevu za kisiasa !!

Lisu kaja kugombea kutwa kutukana Magufuli tu kisha huyo katimka na mitusi yake katukana weeee na wewe Lema ukatukana weee mwisho mkatimka kwenda kulala kanada na ubelgiji

Chama ni sera na hoja sio individual attacks vipi duka lako bubu la fedha za kigeni lilifanyiziwa na Bot au ? si useme tu
Lazma tutumie dola kubaki madarakani!
 
Lema bana anafikiri Kimei atakuwa Gavana BOT awaite wamzunguke. Ajira CRDB wakati ule itufundishe kitu.
 
Utawala wa Magufuli ulikuwa kama wa majambazi. Asante Mungu kwa kutuepushia kikombe hicho kilichokuwa kimejaa kila aina ya uovu kwa watanzania
MwenyeziMungu sio mjinga, alijuwa, anajuwa na atajuwa tunachokihitaji na tusichokihitaji, tusiwe hata na mashaka yoyote kama watu tusio na matumaini. Hata SSH asipoenenda kwa mujibu w mpango wa mungu kuna namna atakavyomwambia unakosea. Sina mashaka na Wazanzibar kwakuwa na wacha mungu kwelikweli wa kweli
 
Ndugu yangu, nashukuru kwa mawazo yako mazuri ila naomba umuulize Askofu wa Ngara Diocese kama alisharudishiwa hati yake. Kosa ni kuulizia watu waliopotea na maiti zilizookotwa kwenye viroba plus katiba huru.

Rais wetu mpendwa alikataa kutoa ruhusa mshtakiwa kumzika mama yake wakati yeye mama yake amemuuguza hapo kwake Chato kitandani.
Watu walikufa kwa shinikizo la damu baada ya baba na mwana kumfukuza kazi mbele ya kadamnasi pale kwenye daraja la kigamboni.
Je sera ipi ya chama chochote inayoruhusu watu kupotea, watu kupigwa risasi na kunyang'anywa uraia bila kesi yoyote kufunguliwa?

Wote tunaishi na kufariki mara moja hivyo hakuna atakayerudi kurekebisha ya nyuma. Sera zinatungwa na binadamu na huyo binadamu anaamua afuate sera ipi na akandamize ipi.

Kumbe Rais ndio hutoa ruhusa kwa mahabusu kuzika wapendwa wao? Hebu tukumbushe sheria ziinasemaje kuhusu mahabusu kuzika wapendwa wao?
 
Raisi Mama Samia
Ili twende vizuri, tunaomba clearance ya maana haswa kwenye baraza la mawaziri clear appointees wote wa hayati, uanze na kikosi kazi chako.

Unaenenda kwa hekima huwezi kufanya kazi na wakurupukaji.

Amteue nani sasa Mkuu, chama chetu unakijua! Wafia chama waliwekwa kando muda! Wahamiaji ndio wako front line...
 
Back
Top Bottom