Gold Mafia: Huduma ya utakatishaji fedha – Uchunguzi Uliofanywa na Al Jazeera

Gold Mafia: Huduma ya utakatishaji fedha – Uchunguzi Uliofanywa na Al Jazeera

Mambo ni mengi haya makanisa ya manabii matajiri yanamambo mengi
FB_IMG_1686767697950.jpg
 
Episode 1 Sehemu ya 3

Usafirishaji wa dhahabu wa Zimbabwe una thamani ya hadi dola bilioni mbili kwa mwaka, ni biashara yenye pesa ndefu. Sehemu ya tatu inatukutanisha na mshindani wa bwana Patni, wa pili kwenye biashara hii ya kuuza dhahabu kwa magendo, wa kwanza akiwa kubwa lao Patni, huyu ni bwana Ewan MacMillan.

ewan.jpeg

Mara ya kwanza MacMillan alikuwa akifanya biashara hii mwenyewe na kumiliki kila kitu, baadaye akaanza kushirikiana na wadogo zake wawili. MacMillan alienda jela kwa mara ya kwanza akiwa na umri wa miaka 21 kwa kosa la kumiliki dhahabu yenye kiasi cha kg 1.2 kimagendo, pia alifungwa sana miaka ya 90 kwa makosa yanayohusisha kufanya biashara ya dhahabu kwa magendo.

MacMillan anafanya biashara ya kubadili kilo 200 za dhahabu kuwa pesa kila wiki. MacMillan anakutana pia na undercover, wanampa mchongo wa kutakatisha pesa zao kutoka china, Ewan anaingia kingi, anawaambia mmefika kwa mtu sahihi, hilo limeisha.

Awaambia sikia kama unataka dola za Kimarekani katika akaunti ya benki, basi unatakiwa kuwa na akaunti ya dola kwenye benki ya Dubai. Kule Dubai Ewan ana mshirika, ambaye yeye ndio mtaalamu wa kutakatisha pesa za watu, jamaa huwa anatakatisha mpaka pesa za Warusi. Mtu anayetaka kutakatisha pesa anampatia pesa hizo Ewan, ambapo yeye anazibadilisha kuwa dhahabu anamtumia huyo mshirika wake wa Dubai ambaye naye anafanya manuva ya kubadili dhahabu mpaka kwenye pesa, kutoka hapo unaweza kuipata pesa yako popote ulimwenguni. Mshirika wa Ewan si mwingine, bali ni bwana Alistair Mathias.

alistair.jpg

Mathias pia ni mfanyabiashara wa dhahabu, yeye ni mtaalamu wa mambo ya fedha, anayepanga mikakati ya kutakatisha fedha za wanasiasa mafisadi, amekuwa kwenye biashara hii kwa takribani miaka 14. Mathias anakubali dili la kutakatisha fedha za bwana Stanley kupitia connections zake alizokuwa nazo kwenye biashara hii Afrika, ambapo kwa mwezi huwa anatakatisha kiasi cha dola za Kimarekani milioni 70 - 80. Mathias pamoja na watu wengine waliokuwa kwenye biashara hii kama vile bwana Patni wanafanya biashara kwenye nchi nyingi Afrika kama vile Zimbabwe, Ghana, Zambia, Angola, Afrika Kusini, Mozambique, Malawi, DRC Congo, Uganda, Kenya, Tanzania, yaani mtandao ni mkubwa.

Patni pia anafanyakazi kutoka Dubai. Dubai ni kama makao makuu ya biashara na huduma za kifedha kwa Waafrika, hakuna kodi za ajabu ajabu, huna haja ya kuwa na nyaraka zote, ni rahisi kufanya mambo yao. Hawa mabwana huko Dubai wana sehemu yao kwenye uwanja wa ndege wa Dubai ya kuhakikisha leseni zao za kusafirisha dhahabu hazisumbuliwi, wana idhini ya Benki Kuu ya Dubai, wana vyeti vya ukaguzi wa kutakatisha pesa, yaani wamejipanga kwelikweli kuhakikisha biashara zao haramu hazikwami. Ili kukuhakishia mchakato huu uko salama na uelewe zaidi, unapelekwa kabisa katika ofisi zao Dubai uone jinsi mambo yanavyofanyika, ukitoka hapo wewe mwenyewe unakubali hawa watu wamejipanga kwenye hili.

Screenshot 2023-06-25 030259.png

Patni akionesha mchakato wa kubadili dhahabu kwenda kwenye pesa unavyofanyika
Je, ilikuaje mpaka Benki Kuu ya Zimbabwe ikaanza kufanya kazi na akina Patni? Tukutane kwenye muendelezo...

Muendelezo soma - Episode 1 - Sehemu ya 4
 
Ufaransa walifanikiwa baada ya wanainchi kuchukua maamuzi mazito kwa kumtoa kafara mfalme, familia yake na ukoo wake pamoja na wote waliomsapoti na ndipo ufaransa ikayaona maendeleo iliyonayo leo na serikali ikawa kwa wanainchi badala ya watu wachache.


China leo wamempita marekani kasi ya maendeleo sababu walishakubaliana fisadi, na wabadhirifu na wahujumu uchumi hawatakiwi kuwa hai mara tu ukweli wa madhira yao utakapogundulika.

Tanzania kama tunataka kusafisha na kuendesha inchi na siasa safi na watu safi huu ni wakati muafaka sasa wa kuweka sheria ambayo haitaangalia nyuma.
 
Episode 1 Sehemu ya 4

Kutokana na maelezo ya Waziri wa Fedha Zimbabwe Bwana Tendai Biti (2009 - 2013) Zimbabwe kuna sheria ya dhahabu ambayo inafanya Benki Kuu kuwa msimamizi na mdhibiti na muuzaji mkuu wa dhahabu nchini Zimbabwe. Benki Kuu ilipewa jukumu hilo kwa sababu kihistoria sarafu yote imekuwa ikitegenezwa na madini ya dhahabu. Akiongeza kuwa anafikiri takribani 80% ya dhahabu inayochimbwa nchini Zimbabwe inasafirishwa kwa njia haramu.

MacMillan na mpinzani wake Patni, wanafanya kazi kwaajili ya Benki Kuu ya Zimbabwe. Wachimbaji wadogo wanazalisha nusu ya dhahabu ya nchi hiyo, lakini benki kuu ya Zimbabwe haina pesa za kutosha kununua dhahabu kutoka kwao. Patni na MacMillan hununua dhahabu kwa niaba ya benki kuu. Wakati mtu anaenda kumuuzia dhahabu Patni au MacMillan hana haja ya kuandikisha popote, haitaji kueleza jina lake au taarifa zozote kuhusu yeye, wala kueleza dhahabu aliyokuwanayo kaipataje pataje. Yeye anatoa dhahabu na kupewa pesa, biashara imeisha, kila mtu anaendelea na mambo yake, na serikali wala haihoji chochote Patni na mwenzake wakienda kukabidhi.

Dhahabu inayopelekwa na akina Patni hupewa kampuni inayomilikiwa na Benki Kuu ya Zimbabwe, Fidelity Printers and Refiners, ambayo inawajibika kuchapisha vitu vya serikali na huduma yao kuu ni kuchakata dhahabu. Kama malipo ama fidia kwa huduma wanayotoa Patni na MacMillan, hupewa leseni za kuuza dhahabu nje ya nchi!

Wakiwa na leseni tayari Patni na mwenzake hupeleka dhahabu hiyo hadi Dubai na kuiuza huko, kisha wanarudisha mapato hayo Zimbabwe kwa njia ya dola za Kimarekani sababu Serikali inahitaji Dola hizo kutokana na kuwa fedha ya Zimbawe haina thamani kimataifa. Dola hizo zinanunua dhahabu zaidi kutoka kwa wachimbaji na kusaidia kufanya biashara zaidi ya nje. Magenge hayo ya dhahabu hutumia mpango huu kutakatisha pesa, na ndio njia ambayo Bwana Stanley anapewa kutakatisha pesa zake.

Kumbuka bwana Stanley anakutana na magenge haya kwa wakati tofauti. Kwa upande wa MacMillan, Bwana Stanley anaelekezwa njia nyingine ya kuanzisha kampuni ya biashara ya dhahabu (dhahabu atakazokuwa ananunua kwa MacMillan) na akaunti ya benki huko Dubai ili sasa aweze kupata leseni ya kuagiza dhahabu katika Falme za Kiarabu.

Akishauza dhahabu anapata pesa safi ambazo zinaingia kwenye account yake, halafu zile pesa zake chafu kutoka China zitapelekwa na wakala wa MacMillan Zimbabwe na kama mapato yaliyotokana na kuuza dhahabu Dubai, na zikishawekewa muhuri uwanja wa ndege wa Harare kuwa ni pesa safi na documents zikiwa mahala pake kazi inakuwa imeisha. Kwahivyo mapato hayo ya dhahabu kutokana na pesa chafu yanahalalishwa kama pesa safi mara mbili, kwanza Dubai kama pesa za mauzo, lakini pia zikiwa zinaingizwa Zimbabwe. Na hivyo mzunguko unakuwa hivyo tena na tena bwana Stanley akitaka kutakatisha pesa zake.

Upande wa pili Patni naye anatoa njia nyingine ya kusafirisha pesa chafu za Bwana Stanley kutoka China kwenda Dubai. Njia hizo ni kwa kutumia wakala wa usafirishaji na njia ya pili ni kupitia Hawala.


Tukutane kwa muendelezo kesho kufahamu zaidi njia zinazotumiwa na bwana Patni na kujua Hawala ndio kitu gani.

Muendelezo soma - Episode 1 - Sehemu ya 5
 
Back
Top Bottom