Gold Mafia: Huduma ya utakatishaji fedha – Uchunguzi Uliofanywa na Al Jazeera

Gold Mafia: Huduma ya utakatishaji fedha – Uchunguzi Uliofanywa na Al Jazeera

Episode 2 - Sehemu ya 4

Daudi Khan anaendelea kueleza jinsi kaka yake anavyotakatisha fedha, kuna duka linalouza bidhaa za kidini ambalo ni moja ya kampuni ya Mo Dollars Johannesburg, ambayo inatumika katika kuonesha malipo ya awali yamefanyika. Kampuni hiyo inajulikana vizuri tu katika jiji hilo, inaendeshwa na baba pamoja na mtoto wake.

Invoice ya dola 167700 inaonyesha malipo ya awali yamefanyika katika kampuni ya china Changshu City China kwaajili ya kununua mavazi ya kiislamu, bidhaa ambazo zitapelekwa kwa tarehe ya mbele iliyopangwa, lakini hakuna pesa imetumwa kwenye kampuni hiyo. Malipo haya yanayofanyika yanakuwa makubwa sana kwa kununua mzigo, yaani kwa pesa hiyo unapata nguo nyingi mno kiasi utakosa pa kuziweka na hutakuwa na watu wa kutosha kuwauzia nguo hizo, hiki ni moja ya kiashiria kinachoonesha invoice hiyo ni fake (mkikutana na malipo kama haya sehemu mtaweza kutambua hapa kuna shida pahala[emoji2]).

Picha ya invoice

View attachment 2752832
Invoice ikionesha malipo ya awali kufanyika kwaajili ya mavazi ya kiislamu

Invoice inayotumwa na msambazaji ili Mo Dollars alipie bidhaa kwa pesa zake chafu nayo ni feki, account zote mbili zinazotuma pesa pamoja na kupokea (duka la kuuza bidhaa za kiislamu na msambazaji) ni za Mo Dollars! Hakuna bidhaa zinazotoka China kwenda Johannesburg lakini pesa chafu za Mo Dollars zinakuwa zimesafishwa kupitia account hiyo ya nje. Huku kwenye benk kuu kila kitu kinaonekana kipo shwari, muamala halali umepita, hakuna magendo yoyote yanafanyika.

Kutuma pesa kama malipo ya awali ni mbinu inayotumiwa sana na watakatishaji pesa, hii ni kwasababu unaweza kuhamisha pesa kirahisi nje bila kupokea mzigo kama malipo ya awalai na unakuwa na muda wa kutengeza documents za muamala huo kufanyika baadae.


Katika mazunguzo (kutoka kwenye kikao kilichofanyika kwa njia ya mtandao) yaliyorekodiwa, Mo Dollars alisikika akimtahadharisha mshirika mwenzake asifanye biashara na hasimu wao katika utakatishaji pesa, akielezea mbinu yake ya utakatishaji pesa kama biashara, na inatakiwa kuendelea kujulikana hivyo, akisema kwamba uliahidi kufanya biashara hii na sisi tu, ukianza kufanya 'biashara' hiyo na watu wengine wawili, watatu inatoa ishara mbaya.


Daud Khan ndio alikuwa mwandishi wa invoice feki, akielezea ofisini kwao kuna 'strong room', chumba kinachotimiwa kuhifadhia vitu vyenye thamani, na chumba hiko kinakuwa na ulinzi mkubwa. Daud anaelezea kwenye chumba hiko walikuwa na maboksi mengi sana yaliyojaa stempu za benki, passport pamoja na nyaraka za vitambulisho. Daudi pia ndio alikuwa anatengeneza logo, kuweka kiasi cha pesa na kila kitu kwenye invoice hizo, ambapo kwa kukadiria 90% ya rekodi kwenye kitabu cha kampuni ya Salt Management hazikuwa za kweli (halisi).

Makala inaturudisha kwa bwana Pattni, ambaye nae anaujua mchezo huu vizuri. Pattni anasema; huwezi ukaweka mayai yako yote sehemu moja, inabidi utawanyishe kwenye mafungu madogo madogo, na yeye hutawanyisha kwenye makundi madogo madogo kama 20 hivi. Wakati akiwa anaendelea kuongea na bwana Stanley, Pattni anasema yuko na network kubwa. Kwa upande wa UK ana duka la kuiza vito, group ya hotel, kampuni za bidhaa mbalimbali, kwahivyo wana uthibitisho wa sababu pindi wakituma pesa chafu nje ya nchi kama malipo ya bidhaa.

Hela zinatumwa kutoka kwenye kampuni zake za Dubai kwenda kwenye biashara zake za London na wana vitabu vyote vya rekodi hizo, hivyo ni rahisi kuthibitisha sababu ya kufanya malipo kwenye account ya nje katika mchakato wa kutakatisha pesa.


Si unakumbuka bwana Pattni ana utambulisho mwingine kama mtu wa dini anaependa kusaidia masikini, ambapo kwenye upande huu anajulikana kama brother Paul? Timu ya Al-Jazeera inafanikiwa kumpata mhasibu wa zamani wa brother Paul, Bwana Raj. Raj anasema wakati anajiunga na bwana Pattni (brother Paul) alikuwa anamuona kama mtu mwema sana, anaefanya kazi ya Mungu, lakini kituo cha msaada cha Bwana Pattni kinachoitwa Land of Hope ndio kimekuwa kikitumika kama sehemu muhimu ya kutakatishia pesa.

Raj anasema Pattini akaanza kutoa misaada na kwa watu rasmi, akificha rushwa kwenye jina la msaada, Raj ana kitabu kinachoonesha rushwa zilizofanywa na Pattini, kinaonesha malipo ya ada kwenye chuo kwaajili ya watoto wa mtu muhimu kutoka katika tawi la Benki Kuu ya Zimbabwe. Baba mwenye Watoto hao anaitwa David Chirozvi.

View attachment 2752836
David Chirozvi

David anafanya kazi kwenye duka la vito la Aurex Jewellery, ambako wanatengeneza vito, lakini pia duka hilo ni sehemu ya Benki Kuu, David hapo ni Mkuu wa Kitengo cha Uhasibu. Kampuni ya Pattini ya Suzan ina leseni iliyotoka Aurex, ambayo inawapa kibali cha kusafirisha vito vya dhahabu na almasi, ambapo pia kibali hicho kinajumuisha malipo ya ziada ya 18% ya mauzo kwa kampuni Suzan kutoka serikalini (si unakumbuka kuhusu malipo ya serikali kwa akina Pattini kwa kuwasaidia upatikanaji wa dola na kuruka/kukwepa vikwazo walivyowekewa na mataifa ya nje?). Kampuni ya Pattini ina leseni pia inayowawezesha kununua dhahabu kutoka wachimbaji kwa niaba ya Fidelity Printers. Mhasibu Raj anasema, kila siku Pattni anaingiza 80kg – 100kg za dhahabu.

View attachment 2752839View attachment 2752840

Lengo la Leseni hizo kutolewa kwa bwana Pattni ni kwaajili ya kuhakikisha uzalishaji na mauzo ya dhahabu yanaongezeka Zimbabwe, lakini uhalisia ni kwamba wananufaika akina Pattni na maafisa waliohusika kuthibitisha mauzo ya dhahabu hizo. Jamaa ambae anasimamia kitengo cha mauzo ya dhahabu, bwana Dube, anapokea kiasi cha Dola za Kimarekani 3000 kwa mwezi kutoka kwa Pattni. Mehluleli Dube alikuwa Mkuu wa Kitego kwenye masuala ya dhahabu kutoka Fidelity Printers, na yeye ndio alikuwa na mamlaka ya kusaini ili kupata leseni kwaajili ya kuuza na kununua dhahabu.

View attachment 2752842
Mehluleli Dube

Jina jingine katika kitabu cha mahesabu alichonacho Raj kinaonesha nguvu ya Bwana Pattni dhidi ya Fidelity Printers, F.Kun. Bwana huyu anapokea Dola za Kimarekani 30,000 kila mwezi kutoka kwa Pattni.

F.Kun ni nani? Tukutane katika muendelezo
[emoji91][emoji91][emoji91]mkuu endelea
 
Mkuu Rare Sapphire hatimae yule mwanamama amekamatwa
IMG-20231102-WA0030.jpg
 
Episode 2 - Sehemu ya 5

Screenshot 2023-11-03 020644.png

Fradreck Kunaka (FKUN) alikuwa Meneja Mkuu kwenye kampuni ya Fidelity, yeye alikuwa analipwa kiasi cha dola za kimarekani 30,000 kwa mwezi. Pattni anaendesha biashara zake katika sehemu ya mji wanaoishi wadosi ambapo kuna mjengo wa maana uliozungushiwa uzio, sehemu hiyo inaitwa Borodare, Harare-Zimbabwe.

FKUN alikuwa anaonekena kwenye ofisini hiyo ya bwana Pattni mara nyingi tu, na saini yake inaonekana kwenye leseni zote za Pattni zinazohusu biashara ya dhahabu. FKUN ndio alikuwa muhusika mkuu wa kutoa leseni za kuuza na kununua dhahabu pamoja na leseni zote zinazohusisha Fidelity Refiner. Kwa hivyo Mr Dube alikuwa analamba dola elf 3 na FKUN alikuwa akilamba dola elfu 30 kila mwezi kutokana na huduma waliyokuwa wanatoa kufanikisha bishara haramu zinaenda bila shida.

Ili kutakatisha pesa za bwana Stanley, Pattni anachaji dola milioni 10 ambazo pia zinahusisha pesa ya kutoa rushwa ili kufanikisha kazi hiyo, ukishatoa kiasi hicho cha pesa wewe unastarehe tu kusubiri kazi yako ifanikishwe, kila kitu wanakuwa wakishughulikia.

*****

Kazi za Mo Dollars Afrika Kusini kama ilivyokuwa kwa Pattni pia zinafanikishwa kwa kutumia rushwa, yeye anawalenga wafanyakazi wa Benki ya Sasfin, benki nchini Afrika Kusini inayowahudumia wafanyabiashara wadogo. Baada ya kutengeneza konekshen na watu hawa wa benk, akina Mo Dollars alikuwa anakutana nao ili kuwajua vizuri ni watu wa aina gani, wana tabia gani, kama wana famila, mke na watoto ambao ukiangalia mishahara wanayopokea haiwatoshi kabisa kuinjoy maisha, nk.

Baada ya kupata taarifa zote wanaambiwa sasa sikia, wewe unakuwa mtu wetu kuhakikisha dili zetu zinaenda vizuri unapitisha malipo yetu yote bila kuuliza uliza maswali utakapoona tu jina la kampuni yetu na sisi tutahakikisha mnakula bata vilivyo, mnaishi kama wadosi. Yaani walikuwa wanachunguza maisha yao vizuri mpaka wahakikishe wanapata kitu cha kuweza kutumia dhidi yao ili wafanikishe dili zao.

Mo Dollars anamwagiza Daud kutoa ombi la malipo kufanyika endapo tu mfanyakazi fulani akiwa ofisini, ambako kwenye ujumbe jamaa huyo anatajwa kama “H”. H inasimama badala ya Hussein Shanara, yeye alikuwa anahusika na kitengo cha kubalisha fedha katika benki ya Safsin.

Screenshot 2023-11-03 025159.png

Screenshot 2023-11-03 025737.png

Hussein Shanara

Hussein na kina Daud Khan na kaka yeake Mo Dollars walikuwa na uhusiano mzuri wa kibiashara, jamaa alikuwa anahakikisha kazi aliyopewa anaifanya vizuri, anahakikisha wafanyakazi wenzake wanapiga mzigo bila kuuliza swali lolote, kwahivyo alikuwa mtu muhimu sana kwao katika kuhakikisha utakatishaji fedha unakamilika vizuri kila mara.

Hussein anatuma ujumbe kwa bosi wake akitoa hitaji la mtu mwingine kuajiriwa, Mo Dollars watakuwa wanamcontrol mtu huyo kwa 100%. Japokuwa alikuwa hana vigezo vyovyote kufanya kazi kwenye benki, jamaa huyo anapata kazi katika benki ya Safsin.

Screenshot 2023-11-03 031445.png


Ili kuhakikisha miamala ya akina Mo Dollars haipati kashkash yoyote, Hussein Shanara alikuwa akilipwa kiasi cha kama dola 1600 kila mwezi. Pia walikuwa wanalipa kiasi cha kama dola 2000 kwa mtu mwingine kwenye benki ya Safsini, Hussein alikuwa ametambulishwa kupitia mtu mwingine aliyekuwa anaitwa Brandon Marshall.

Screenshot 2023-11-03 031959.png

Brandon

Brandon, alikuwa kwenye biashara mpya ya kuleta wateja mpya, kulikuwa na mtu mwingine pia ambaye aliwasumbua mwanzoni ila alikuja kulainika baadae, huyu alikuwa anaitwa Sheral yeye alikuwa compliance manager (mtu anayehakikisha kanuni na sheria zinafatwa kazini), yeye alikuwa anapokea dola 800 kwa mwezi.

Screenshot 2023-11-03 032331.png

Sheral

Pesa ilikuwa inaongea kufanya kila kitu, walikuwa wameikamata benki kiganjani, ni kama vile Mo Dollars alikuwa CEO wa benki hiyo bila ya wao kujua. Vitabu vya mahesabu vya Mo Dollars vinaonesha malipo ya rushwa kwa wafanyakazi wa benki nyingine pia, walikuwa na jamaa anaitwa Videsh Seeripat kutoka benki ya Absa, yeye alikuwa anafungua account za benki hewa.

Videsh alikuwa anasimamaia kitengo ya Uhusiano kwenye benki ya Absa, huyu naye alikuwa akilipwa kiasi cha dola 800 kwa mwezi. Watu wote hawa walikuwa wanahakikisha nyaraka zote zote muhimu zinapitishwa bila kukutwa na makosa au mapungufu yoyote ya sheria, na kuweka chochote wanachoambiwa kuweka kwenye nyaraka hizo bila kuuliza maswali. Mbali na watumishi hao, akina Mo Dollars wana watu wengine kwenye orodha yao ya malipo kutoka Benki ya Standard; Viviyan ambaye nae anapokea kiasi cha dola 800

Screenshot 2023-11-04 231108.png

Viviyan

Viviyan alikuwa Msimamizi Mkuu wa idara ya inayosimamia mambo sheria na taratibu za ya Benki ya Standard pamoja na miamala inayohusha nchi za nje na yeye ni mtu muhimu linapokuja suala la kufanya mawasiliano na benki kuu ya Afrika Kusini. Viviyan akitumia jina la uongo kama Vic Grimes, anahakikisha kampuni ya Mo Dollars inasajiliwa na inapata idhini kutoka benki ya Standard. Mo Dollars anampatia nyaraka muhimu zinazohitajika, halafu yeye anakamilisha sehemu iliyobaki kwa kujaza fomu zote zinazohitaka, halafu anapeleka Benki Kuu na kupata kibali kitakachowawezesha akina Mo Dollars kufanya malipo bila ukaguzi wowote kupitia benki yoyote.

*****

Tukirudi kwa Mtume Angel, yeye anamwambia Mr. Stanley pesa yake inaweza kufanya makubwa zaidi ya kununua tu dhahabu, anamwambia ukijenga hoteli utamfurahisha Rais Mnangagwa, akimaanisha kwamba amtengezee Rais kumbukumbu ya kukumbukwa na watu wake kuwa alifanikisha huduma fulani kupatikana Zimbabwe, amtengenezee historia/ legacy, kwa kufanya hivyo mambo yake takuwa yanaenda vizuri zaidi bila usumbufu wowote. Mtume Angel yuko tayari kabisa na eneo la kufanikisha hilo, mji wa maporoko ya Victoria, kwamba akikamilisha hilo watakuwa na moja ya maajabu ya dunia na wageni watafurika kama nyuki kwenda kuangalia.

Mtume Angel anamwambia kinachohitajika hapo ni eneo tu la kujenga, na hilo tukikutana na Mnangagwa unapata dk sifuri tu. Anamwambi hili ni jambo rahisi sana, tulishawahi kuuza ardhi kwa wawekezaji wa kigeni, hii sio mara ya kwanza hivyo usiwe na wasiwasi. Akisema alishafanya dili na familia ya kifalme ya Sharjah, wao walikuwa wanahitaji heka 30,000. Anasema alipomwambia Rais alisema waambie waje chap, ardhi yao ipo tayari.

Msaidizi wa Stanley akataka wapate wasaa wa kuonana na Rais Mnangagwa, Rikki, mshirika wa Mtume Angle, akamwambia kwa sasa Rais yuko bize sana, ila usijali hilo linaweza kupangwa, kwakuwa muda wa Rais una thamani sana, mtatakiwa kulipa pesa ya kufanya mkutano huo kufanikiwa, gharama yake ni dola 200,000.

Itaendelea…
 
Episode 2 - Sehemu ya 5


Fradreck Kunaka (FKUN) alikuwa Meneja Mkuu kwenye kampuni ya Fidelity, yeye alikuwa analipwa kiasi cha dola za kimarekani 30,000 kwa mwezi. Pattni anaendesha biashara zake katika sehemu ya mji wanaoishi wadosi ambapo kuna mjengo wa maana uliozungushiwa uzio, sehemu hiyo inaitwa Borodare, Harare-Zimbabwe.

FKUN alikuwa anaonekena kwenye ofisini hiyo ya bwana Pattni mara nyingi tu, na saini yake inaonekana kwenye leseni zote za Pattni zinazohusu biashara ya dhahabu. FKUN ndio alikuwa muhusika mkuu wa kutoa leseni za kuuza na kununua dhahabu pamoja na leseni zote zinazohusisha Fidelity Refiner. Kwa hivyo Mr Dube alikuwa analamba dola elf 3 na FKUN alikuwa akilamba dola elfu 30 kila mwezi kutokana na huduma waliyokuwa wanatoa kufanikisha bishara haramu zinaenda bila shida.

Ili kutakatisha pesa za bwana Stanley, Pattni anachaji dola milioni 10 ambazo pia zinahusisha pesa ya kutoa rushwa ili kufanikisha kazi hiyo, ukishatoa kiasi hicho cha pesa wewe unastarehe tu kusubiri kazi yako ifanikishwe, kila kitu wanakuwa wakishughulikia.

*****

Kazi za Mo Dollars Afrika Kusini kama ilivyokuwa kwa Pattni pia zinafanikishwa kwa kutumia rushwa, yeye anawalenga wafanyakazi wa Benki ya Sasfin, benki nchini Afrika Kusini inayowahudumia wafanyabiashara wadogo. Baada ya kutengeneza konekshen na watu hawa wa benk, akina Mo Dollars alikuwa anakutana nao ili kuwajua vizuri ni watu wa aina gani, wana tabia gani, kama wana famila, mke na watoto ambao ukiangalia mishahara wanayopokea haiwatoshi kabisa kuinjoy maisha, nk.

Baada ya kupata taarifa zote wanaambiwa sasa sikia, wewe unakuwa mtu wetu kuhakikisha dili zetu zinaenda vizuri unapitisha malipo yetu yote bila kuuliza uliza maswali utakapoona tu jina la kampuni yetu na sisi tutahakikisha mnakula bata vilivyo, mnaishi kama wadosi. Yaani walikuwa wanachunguza maisha yao vizuri mpaka wahakikishe wanapata kitu cha kuweza kutumia dhidi yao ili wafanikishe dili zao.

Mo Dollars anamwagiza Daud kutoa ombi la malipo kufanyika endapo tu mfanyakazi fulani akiwa ofisini, ambako kwenye ujumbe jamaa huyo anatajwa kama “H”. H inasimama badala ya Hussein Shanara, yeye alikuwa anahusika na kitengo cha kubalisha fedha katika benki ya Safsin.


Hussein na kina Daud Khan na kaka yeake Mo Dollars walikuwa na uhusiano mzuri wa kibiashara, jamaa alikuwa anahakikisha kazi aliyopewa anaifanya vizuri, anahakikisha wafanyakazi wenzake wanapiga mzigo bila kuuliza swali lolote, kwahivyo alikuwa mtu muhimu sana kwao katika kuhakikisha utakatishaji fedha unakamilika vizuri kila mara.

Hussein anatuma ujumbe kwa bosi wake akitoa hitaji la mtu mwingine kuajiriwa, Mo Dollars watakuwa wanamcontrol mtu huyo kwa 100%. Japokuwa alikuwa hana vigezo vyovyote kufanya kazi kwenye benki, jamaa huyo anapata kazi katika benki ya Safsin.

View attachment 2804067

Ili kuhakikisha miamala ya akina Mo Dollars haipati kashkash yoyote, Hussein Shanara alikuwa akilipwa kiasi cha kama dola 1600 kila mwezi. Pia walikuwa wanalipa kiasi cha kama dola 2000 kwa mtu mwingine kwenye benki ya Safsini, Hussein alikuwa ametambulishwa kupitia mtu mwingine aliyekuwa anaitwa Brandon Marshall.


Brandon, alikuwa kwenye biashara mpya ya kuleta wateja mpya, kulikuwa na mtu mwingine pia ambaye aliwasumbua mwanzoni ila alikuja kulainika baadae, huyu alikuwa anaitwa Sheral yeye alikuwa compliance manager (mtu anayehakikisha kanuni na sheria zinafatwa kazini), yeye alikuwa anapokea dola 800 kwa mwezi.


Pesa ilikuwa inaongea kufanya kila kitu, walikuwa wameikamata benki kiganjani, ni kama vile Mo Dollars alikuwa CEO wa benki hiyo bila ya wao kujua. Vitabu vya mahesabu vya Mo Dollars vinaonesha malipo ya rushwa kwa wafanyakazi wa benki nyingine pia, walikuwa na jamaa anaitwa Videsh Seeripat kutoka benki ya Absa, yeye alikuwa anafungua account za benki hewa.

Videsh alikuwa anasimamaia kitengo ya Uhusiano kwenye benki ya Absa, huyu naye alikuwa akilipwa kiasi cha dola 800 kwa mwezi. Watu wote hawa walikuwa wanahakikisha nyaraka zote zote muhimu zinapitishwa bila kukutwa na makosa au mapungufu yoyote ya sheria, na kuweka chochote wanachoambiwa kuweka kwenye nyaraka hizo bila kuuliza maswali. Mbali na watumishi hao, akina Mo Dollars wana watu wengine kwenye orodha yao ya malipo kutoka Benki ya Standard; Viviyan ambaye nae anapokea kiasi cha dola 800


Viviyan alikuwa Msimamizi Mkuu wa idara ya inayosimamia mambo sheria na taratibu za ya Benki ya Standard pamoja na miamala inayohusha nchi za nje na yeye ni mtu muhimu linapokuja suala la kufanya mawasiliano na benki kuu ya Afrika Kusini. Viviyan akitumia jina la uongo kama Vic Grimes, anahakikisha kampuni ya Mo Dollars inasajiliwa na inapata idhini kutoka benki ya Standard. Mo Dollars anampatia nyaraka muhimu zinazohitajika, halafu yeye anakamilisha sehemu iliyobaki kwa kujaza fomu zote zinazohitaka, halafu anapeleka Benki Kuu na kupata kibali kitakachowawezesha akina Mo Dollars kufanya malipo bila ukaguzi wowote kupitia benki yoyote.

*****

Tukirudi kwa Mtume Angel, yeye anamwambia Mr. Stanley pesa yake inaweza kufanya makubwa zaidi ya kununua tu dhahabu, anamwambia ukijenga hoteli utamfurahisha Rais Mnangagwa, akimaanisha kwamba amtengezee Rais kumbukumbu ya kukumbukwa na watu wake kuwa alifanikisha huduma fulani kupatikana Zimbabwe, amtengenezee historia/ legacy, kwa kufanya hivyo mambo yake takuwa yanaenda vizuri zaidi bila usumbufu wowote. Mtume Angel yuko tayari kabisa na eneo la kufanikisha hilo, mji wa maporoko ya Victoria, kwamba akikamilisha hilo watakuwa na moja ya maajabu ya dunia na wageni watafurika kama nyuki kwenda kuangalia.

Mtume Angel anamwambia kinachohitajika hapo ni eneo tu la kujenga, na hilo tukikutana na Mnangagwa unapata dk sifuri tu. Anamwambi hili ni jambo rahisi sana, tulishawahi kuuza ardhi kwa wawekezaji wa kigeni, hii sio mara ya kwanza hivyo usiwe na wasiwasi. Akisema alishafanya dili na familia ya kifalme ya Sharjah, wao walikuwa wanahitaji heka 30,000. Anasema alipomwambia Rais alisema waambie waje chap, ardhi yao ipo tayari.

Msaidizi wa Stanley akataka wapate wasaa wa kuonana na Rais Mnangagwa, Rikki, mshirika wa Mtume Angle, akamwambia kwa sasa Rais yuko bize sana, ila usijali hilo linaweza kupangwa, kwakuwa muda wa Rais una thamani sana, mtatakiwa kulipa pesa ya kufanya mkutano huo kufanikiwa, gharama yake ni dola 200,000.

Itaendelea…
Endeleo mkuuu
 
Episode 2 - Sehemu ya 5


Fradreck Kunaka (FKUN) alikuwa Meneja Mkuu kwenye kampuni ya Fidelity, yeye alikuwa analipwa kiasi cha dola za kimarekani 30,000 kwa mwezi. Pattni anaendesha biashara zake katika sehemu ya mji wanaoishi wadosi ambapo kuna mjengo wa maana uliozungushiwa uzio, sehemu hiyo inaitwa Borodare, Harare-Zimbabwe.

FKUN alikuwa anaonekena kwenye ofisini hiyo ya bwana Pattni mara nyingi tu, na saini yake inaonekana kwenye leseni zote za Pattni zinazohusu biashara ya dhahabu. FKUN ndio alikuwa muhusika mkuu wa kutoa leseni za kuuza na kununua dhahabu pamoja na leseni zote zinazohusisha Fidelity Refiner. Kwa hivyo Mr Dube alikuwa analamba dola elf 3 na FKUN alikuwa akilamba dola elfu 30 kila mwezi kutokana na huduma waliyokuwa wanatoa kufanikisha bishara haramu zinaenda bila shida.

Ili kutakatisha pesa za bwana Stanley, Pattni anachaji dola milioni 10 ambazo pia zinahusisha pesa ya kutoa rushwa ili kufanikisha kazi hiyo, ukishatoa kiasi hicho cha pesa wewe unastarehe tu kusubiri kazi yako ifanikishwe, kila kitu wanakuwa wakishughulikia.

*****

Kazi za Mo Dollars Afrika Kusini kama ilivyokuwa kwa Pattni pia zinafanikishwa kwa kutumia rushwa, yeye anawalenga wafanyakazi wa Benki ya Sasfin, benki nchini Afrika Kusini inayowahudumia wafanyabiashara wadogo. Baada ya kutengeneza konekshen na watu hawa wa benk, akina Mo Dollars alikuwa anakutana nao ili kuwajua vizuri ni watu wa aina gani, wana tabia gani, kama wana famila, mke na watoto ambao ukiangalia mishahara wanayopokea haiwatoshi kabisa kuinjoy maisha, nk.

Baada ya kupata taarifa zote wanaambiwa sasa sikia, wewe unakuwa mtu wetu kuhakikisha dili zetu zinaenda vizuri unapitisha malipo yetu yote bila kuuliza uliza maswali utakapoona tu jina la kampuni yetu na sisi tutahakikisha mnakula bata vilivyo, mnaishi kama wadosi. Yaani walikuwa wanachunguza maisha yao vizuri mpaka wahakikishe wanapata kitu cha kuweza kutumia dhidi yao ili wafanikishe dili zao.

Mo Dollars anamwagiza Daud kutoa ombi la malipo kufanyika endapo tu mfanyakazi fulani akiwa ofisini, ambako kwenye ujumbe jamaa huyo anatajwa kama “H”. H inasimama badala ya Hussein Shanara, yeye alikuwa anahusika na kitengo cha kubalisha fedha katika benki ya Safsin.


Hussein na kina Daud Khan na kaka yeake Mo Dollars walikuwa na uhusiano mzuri wa kibiashara, jamaa alikuwa anahakikisha kazi aliyopewa anaifanya vizuri, anahakikisha wafanyakazi wenzake wanapiga mzigo bila kuuliza swali lolote, kwahivyo alikuwa mtu muhimu sana kwao katika kuhakikisha utakatishaji fedha unakamilika vizuri kila mara.

Hussein anatuma ujumbe kwa bosi wake akitoa hitaji la mtu mwingine kuajiriwa, Mo Dollars watakuwa wanamcontrol mtu huyo kwa 100%. Japokuwa alikuwa hana vigezo vyovyote kufanya kazi kwenye benki, jamaa huyo anapata kazi katika benki ya Safsin.

View attachment 2804067

Ili kuhakikisha miamala ya akina Mo Dollars haipati kashkash yoyote, Hussein Shanara alikuwa akilipwa kiasi cha kama dola 1600 kila mwezi. Pia walikuwa wanalipa kiasi cha kama dola 2000 kwa mtu mwingine kwenye benki ya Safsini, Hussein alikuwa ametambulishwa kupitia mtu mwingine aliyekuwa anaitwa Brandon Marshall.


Brandon, alikuwa kwenye biashara mpya ya kuleta wateja mpya, kulikuwa na mtu mwingine pia ambaye aliwasumbua mwanzoni ila alikuja kulainika baadae, huyu alikuwa anaitwa Sheral yeye alikuwa compliance manager (mtu anayehakikisha kanuni na sheria zinafatwa kazini), yeye alikuwa anapokea dola 800 kwa mwezi.


Pesa ilikuwa inaongea kufanya kila kitu, walikuwa wameikamata benki kiganjani, ni kama vile Mo Dollars alikuwa CEO wa benki hiyo bila ya wao kujua. Vitabu vya mahesabu vya Mo Dollars vinaonesha malipo ya rushwa kwa wafanyakazi wa benki nyingine pia, walikuwa na jamaa anaitwa Videsh Seeripat kutoka benki ya Absa, yeye alikuwa anafungua account za benki hewa.

Videsh alikuwa anasimamaia kitengo ya Uhusiano kwenye benki ya Absa, huyu naye alikuwa akilipwa kiasi cha dola 800 kwa mwezi. Watu wote hawa walikuwa wanahakikisha nyaraka zote zote muhimu zinapitishwa bila kukutwa na makosa au mapungufu yoyote ya sheria, na kuweka chochote wanachoambiwa kuweka kwenye nyaraka hizo bila kuuliza maswali. Mbali na watumishi hao, akina Mo Dollars wana watu wengine kwenye orodha yao ya malipo kutoka Benki ya Standard; Viviyan ambaye nae anapokea kiasi cha dola 800


Viviyan alikuwa Msimamizi Mkuu wa idara ya inayosimamia mambo sheria na taratibu za ya Benki ya Standard pamoja na miamala inayohusha nchi za nje na yeye ni mtu muhimu linapokuja suala la kufanya mawasiliano na benki kuu ya Afrika Kusini. Viviyan akitumia jina la uongo kama Vic Grimes, anahakikisha kampuni ya Mo Dollars inasajiliwa na inapata idhini kutoka benki ya Standard. Mo Dollars anampatia nyaraka muhimu zinazohitajika, halafu yeye anakamilisha sehemu iliyobaki kwa kujaza fomu zote zinazohitaka, halafu anapeleka Benki Kuu na kupata kibali kitakachowawezesha akina Mo Dollars kufanya malipo bila ukaguzi wowote kupitia benki yoyote.

*****

Tukirudi kwa Mtume Angel, yeye anamwambia Mr. Stanley pesa yake inaweza kufanya makubwa zaidi ya kununua tu dhahabu, anamwambia ukijenga hoteli utamfurahisha Rais Mnangagwa, akimaanisha kwamba amtengezee Rais kumbukumbu ya kukumbukwa na watu wake kuwa alifanikisha huduma fulani kupatikana Zimbabwe, amtengenezee historia/ legacy, kwa kufanya hivyo mambo yake takuwa yanaenda vizuri zaidi bila usumbufu wowote. Mtume Angel yuko tayari kabisa na eneo la kufanikisha hilo, mji wa maporoko ya Victoria, kwamba akikamilisha hilo watakuwa na moja ya maajabu ya dunia na wageni watafurika kama nyuki kwenda kuangalia.

Mtume Angel anamwambia kinachohitajika hapo ni eneo tu la kujenga, na hilo tukikutana na Mnangagwa unapata dk sifuri tu. Anamwambi hili ni jambo rahisi sana, tulishawahi kuuza ardhi kwa wawekezaji wa kigeni, hii sio mara ya kwanza hivyo usiwe na wasiwasi. Akisema alishafanya dili na familia ya kifalme ya Sharjah, wao walikuwa wanahitaji heka 30,000. Anasema alipomwambia Rais alisema waambie waje chap, ardhi yao ipo tayari.

Msaidizi wa Stanley akataka wapate wasaa wa kuonana na Rais Mnangagwa, Rikki, mshirika wa Mtume Angle, akamwambia kwa sasa Rais yuko bize sana, ila usijali hilo linaweza kupangwa, kwakuwa muda wa Rais una thamani sana, mtatakiwa kulipa pesa ya kufanya mkutano huo kufanikiwa, gharama yake ni dola 200,000.

Itaendelea…
Tuendelee Rare Sapphire
 
Aya ya nne ya huu Uzi na comment namba 11 ya chotera ndio maisha halisi ya mafia a.k.a mafioso. Ukibahatika kusoma riwaya ya Mario puzo ya the godfather utagundua kwamba mafia Wana play role kubwa katika ku support project kadhaa za serikali na pia kupenyeza rupia Ili mambo Yao na biashara zao Haramu ziende. Na amini usiamini hata bills zinazokuwa proposed bungeni haswa mabunge yetu haya ya kiafrika muda mwingine zinakuwa ni kwa ajili ya kuwa favor Hawa THE MEN OF HONOR au mafia. Hawa mafia ndio hutoa chochote kitu ku fund kampeni za wanasiasa Ili kulainisha mambo Yao na wapo kila sekta kila idara za serikali na pia ni miongoni mwa DEEPSTATE.
 
Back
Top Bottom