Rare Sapphire
JF-Expert Member
- Jul 24, 2021
- 590
- 1,648
- Thread starter
- #101
Episode 1 - Sehemu ya 7 (Mwisho wa Episode ya 1)
Pattni nae ana vijana wake special wanaofanya kazi ya kusafirisha dhahabu kwenda Dubai na kurudi na pesa Zimbabwe. Ripota Undercover anafanikiwa kukutana na mmoja wa vijana hawa. Mwamba huyu anaitwa Dmytro Abakumov.
Dmytro Abakumov
Mbali na Abakumov kufanya kazi hiyo ya kuwa msafirishaji wa Bwana Pattni, Abakumov pia ni Mkurugenzi katika moja ya kampuni za Pattni ambayo ipo Zimbabwe. Kamera ya Al-Jazeera haikumuacha salama, inamdaka jamaa akiwa katika majukumu yake ya magendo Uwanja wa Ndege wa Harare, Zimbabwe.
Abakumov akiwa amenaswa na kamera ya Al-Jazeera uwanja wa ndege wa Harare
Ili waweze kufanya biashara zao bila shida, lazima wawe na nyaraka sahihi kwa ajili ya biahsara hiyo. Bwana Pattni bila kujua kama ananaswa na kamera, anaonyesha barua kutoka Fidelity Printers kwenda Dubai inayotaja majina ya Abakumovu na ndugugu yake Pattni, Mishaal Pattni inayoidhinisha kampuni ya Pattni inayoitwa Susan General Trading kubeba dola za Kimarekani milioni 3 kila wiki kuingia Zimbabwe
Barua kutoka Fidelity Printers kwenda Dubai inayowataja Abakumovu na Mishaal Pattni kuidhinisha kampuni ya Susan General Trading kubeba dola za Kimarekani milioni 3 kila wiki kuingia Zimbabwe
Benki Kuu inatangaza kuwa biashara/kampuni ya Susan's jewelry and gold exports ndio inayoongoza kwa kuingiza dola za Marekani nchini. Kampuni hii ya Susan imejiimarisha na kukuza network yake iliyipa nguvu kifedha na kuzalisha dola za Kimarekanani milioni 168 kwa mwaka 2020. Biashara ya Susan inachukuliwa kuwa ni yenye thamani kubwa katika kuzalisha fedha taslimu kwaajili Zimbabwe, mpaka serikali imeamua kuwalipa bonasi ya thamani ya 18% ya mauzo yake. Lakini nyaraka zilizopatikana kutoka kitengo cha Al-Jazeera zinaonyesha kuwa yote ni sehemu ya himaya ya Pattni kwenye biashara zake chafu za dhahabu.
Benki Kuu inatangaza kampuni ya Susan's jewelry and gold exports kuwa kinara wa kuingiza dola za Marekani nchini
Barua inayoonesha serikali kupitisha bonasi ya thamani ya 18% ya mauzo yake kwa Suzan General Trading
Al-Jazeera walitafuta wahasabu wa zamani wa Pattni kupata taarifa zaidi na kufanikiwa kuwapata baadhi. Muhasibu Sami (utambulisho wake halisi umefichwa), akaeleza jinsi Pattni alivyokuwa akifanya kazi, akisema kuwa Pattni anauza vito na dhahabu nchini Dubai na sehemu nyingine za dunia, ambapo yeye anapaswa kupeleka fedha za kigeni Zimbabwe. Wakati hao wabeba/wasafirisha dhahabu wakifika uwanja wa ndege wa Harare baada ya safari zao za Dubai, walitakiwa kusema pesa walizorejesha Zimbabwe kwa kutumia Fomu 47 ambayo kwa kawaida huitwwa Fomu ya Bluu. Akaendelea kusema kuwa wakati mawakala wao/wasafirisha dhahabu wakitaja kiasi cha fedha walizorejesha huwa hawasemi kweli, wanadanganya! Wakati mwingine hupeleka dola elfu 50 au laki moja lakini kwenye kujaza fomu/kutaja kiasi walichopeleka huandika milioni 1 au 2.
Pattni mwenyewe siku moja anarekodiwa katika Fomu ya Bluu akiwa anarejesha pesa Zimbabwe. Pattni akajaza kuwa amepeleka dola milioni 1.2, pesa zilizopatikana baada ya kuuza vito Dubai. Lakini Patni hakupelea pesa hizo dola milioni 1.2 badala yake alipeleka hela ambayo haifiki hata dola laki moja. Pattni na wenzake wanaweza kufanikisha hilo kwa kuhonga wafanyakazi wa uhamiaji na kuwaambiwa waandike kiasi wanachotaka.
Fomu ya Bluu iliyorekodi pesa alizoingia nazo Pattni Zimbwabwe
Wakati mhasibu anarekodi kwenye vitabu vyake hakuandika dola milioni 1.2 badala yake aliandika pesa halisi bwana Patni aliyokuja nayo ambayo ilikuwa haifiki data dola laki moja.
Kitabu kikionesha kiasi halisi cha pesa alichoingianacho Bwana Patni
Patni akionesha Fomu ya Bluu ambayo wanasema kiasi cha fedha walichoingia nacho Harare kutoka mauzo ya dhahabu Dubai
Patni anaacha sehemu kubwa ya pesa za mauzo ya dhahabu Dubai, kutokana na hili sasa Bwana Pattni anakuwa hana hela za kutosha kununua dhahabu kwaajili ya roundi nyingine (kupeleka dhahabu Dubai kuuza na kurudisha fedha Zimbabwe). Ili kuendelea kuwa na leseni inayomsuhuru kwenda kuuza dhahabu nje ya nchi itabidi sasa anunue dhahabu kutoka kwa wachimbaji wadogo, anafidia kiasi cha pesa ambacho hana kutoka kwenye soko la Hawala (si unaikumbuka hii, wale wanafirisha pesa bila pesa yenyewe kutembea?) wa Zimbabwe wanaotaka kutuma pesa Dubai. Kwahiyo hela anayoipata kwa hawa watu ndio anayotumia kununua dhahabu, huku Dubai wateja wake wa Hawala wanalipwa kutokana na mauzo ya dhahabu aliyoinunua Zimbabwe na mzunguko unakuwa huo huo kila wakati huku yeye akiweka mfukoni 18% yake. Pesa inayohitajika kwa udi na uvumba haingii kwenye uchumi wa Zimbabwe haifiki kama inavyotajariwa.
Fomu inayoonesha hela zilizopokelewa na Pattni kutoka soko la Hawala
Kutokana na anachofanya, Pattni anakuwa mafia mara mbili, kwenye hizo dili zake tayari ni mhalifu tayari lakini anaongezea na kuibia na serikali ambayo imemruhusu kufanya uhalifu wake! Anajifanya kuisaidia Zimbabwe kwa kupeleka fedha za kigeni zinazohitajika sana lakini anachopeleka ni kiduchu sana ambacho ni sawa sawa na 0. Hii tunaiitaje, mbwa kala mbwa au mbuzi kafia kwa muuza supu?
Sasa hapa kila mtu amaeshaonesha uwezo wake wa kukamilisha kazi ya Bwana Stanley (kutakatisha pesa zake kutoka china), washajiuza vya kutosha na kutoa ramani yote ya jinsi mchongo unavyofanyika na mambo yatakavyoenda vizuri bila wasiwasi, sasa ni muda wa kutamba kujionesha kwamba wewe ni zaidi ya genge fulani. Nabii Angel anatamba mbele ya ripota wa undercover, anasema bwana we mimi sio mjinga, nina degree mbili za uchumi, kwahiyo ninajua vizuri nini nafanya, anasema jamani mi siongei sana CV yangu inajieleza; mbali na degree zangu mbili niliingia pia kwenye orodha ya matajiri ya Forbes kwa Afrika mwaka 2013, lakini pia ni Waziri wa Injili.
Nabii Angel akitamba kuonesha nguvu alizonazo akiwa na chawa (wasaidizi) wake
Stanley anamwambia Nabii Angel hapa tumesomana vizuri, mimi ntaleta mtaji ambao ni pesa Taslimu, nataka kuwekeza hela zangu hapa, chawa wa Bwana Stanley akaongezea maneno kumuelezea tajiri, akasema anachomaanisha bosi wangu hapa ni kuwa hela zote alizokuwanazo haziwezi kuchukuliwa/kukubaliwa au kutumika huko tulikotoka kwahivyo inabidi mzigo wote uingie kwenye uwekezaji ili tuweze kupata pesa safi na hatutaki tuje tuingie kwenye matatizo yoyote.
Nabii Angel na chawa wake wanajibu, jamani msiwe na shaka, tumeshaongea kuhusu hilo, mmeshuhudia wenyewe simu kadhaa zikipigwa kwa watu wa nguvu, yaani mambo yameshawekwa sawa, tunasubiri nyinyi tu mtie mzigo tufanye biashara, halafu Nabii Angel akauliza, kwani mnataka kuwekeza mpunga kiasi gani?
Bwana Stanley akajibu kwa kuanzia nataka niwekeze kama dola bilioni moja hivi, Nabii akajibu okaaaay (hapo anaona ameulmba), kisha anamjibu Bwana Stanley kuwa, sisi tumewahi kufanya biashara za dola milioni 200 au 300 lakini hatujawahi kufanya kwa kiasi kikubwa hivyo kama bilioni 1.
Angel na msaidizi wake wanamchukua Bwana Stanley pembeni, na kumwambia bwana sikia, mimi ndio mtu wa pili mwenye nguvu kimamlaka Zimbabwe, unajua naweza kumuweka huyu chawa wangu (akionesha upande wa msaidizi wake) kwenye mfuko na hakuna mtu ataruhusiwa kugusa wala kukagua mzigo wangu? Unajua naweza kuweka kwenye mkoba wangu dola bilioni 1.2 kwenye mkoba wangu nikazungushia utepe mwekundu wa kibalozi na kazi imeisha? Nabii Angel anajitamba jinsi anavyoweza kutumia kofia yake ya ubalozi kupiga dili zake chafu bila shida yoyote. Anamwambia Bwana Stanley usiwe na wasiwasi wowote kwani kofia ya ubalozi itaingiza hizo hela Zimbabwe fasta tu, kama nakunywa maji vile, mzigo utafika Zimbabwe hakuna mtu ataugusa mpaka utafika nyumbani kwangu (kwa Nabii Angel).
Uchunguzi kwa Episode ya 1 ukaishia hapa, matokeo ya uchuguzi huu, yaani kila kilichorekodiwa mwanzo mpaka mwisho kilipelekwa/wasilishwa kwa kila aliyohusishwa/aliyeonekana katika Makala hii, na haya ndio yalikuwa majibu yao;
Simon Rudland ~ Alisema tuhuma zote kuhusu yeye ni uongo, ni kampeni zilizofanywa dhidi yake na watu wasiojulikana kumchafua, akajielezea yeye kama mfanyabiashara imara, mwenye nguvu, anaejiweza, anaepambana na watu wenye tamaa na wivu
Gold Leaf Tobbaco ~ Walikanusha kuhusika kwao katika Sakata hili kwa nguvu zote kwenye chochote kilichofanyika kipindi cha nyuma ama sasa kuhusisha shughuli za utakatishaji fedha, biashara ya magendo ya dhahabu ama chochote kinachoendana na hayo.
Fidelity Printers and Refiners ~ Walikanusha kuwa na uhusiano wowote wa kibiashara na Bwana Simon Rudland au kumpa leseni ama kutoa upendeleo au motisha kwa yeyote aliyetajwa kwenye Makala hii. Pia Fidelity ikakanusha kuhusika kwa vyovyote vile kwenye shughuli za utakatishaji pesa, biashara za magendo au majaribio ya kukwepa/kuvunja vikwazo walivyowekewa na chi za Magharibi kupitia mlango wa nyuma.
Benki Kuu ya Zimbabwe ~ Iliwaambia Al-Jazeera kuwa inachukulia vitendo vya utakatishaji pesa na shughuli zote za biashara haramu/magendo kwa uzito mkubwa sana na kwa vyovyote vile iwe moja kwa moja wao au kupitia mtu/taasisi nyingine haiwezi kujihusisha na shughuli hizo.
Alistair Mathias ~ Alikanusha kutengeza mpango wa kutakatisha pesa na kusema hajawahi kutakatisha pesa au kufanya biashara ya dhahabu kwa magendo kwa Warusi ama kwa mtu yoyote yule, na kuongeza kuwa hajawahi kuwa na uhusiano wowote wa kibiashara na Bwana Ewan MacMillan.
Kamlesh Pattni ~ Amekanusha kufanya uhalifu wowote Kenya na kusisitiza kuwa hajawahi kukutwa na hatia kuhusiana na shughuli alizokuwa anafanya Kenya. Pia alikanusha uhusika wake kwenye utakatishaji pesa wala kuisaidia Zimbabwe kukwepa vikwazo walivyowekewa na chi za magharibi, alikanusha pia kuwahi kuajiri mtu yoyote kuingiza pesa kimagendo au kujitolea kushughulikia pesa ambazo anajua zimetokana na shughuli za uhalifu, na kwamba alipokutana na wachunguzi wa Al-Jazeera alidhani amekutana na mwekezaji aliyetaka kuuza sehemu ya biashara ya hoteli na ambaye alitaka “Kujiondoa katika mfuko wa uwekezaji nchini China ili kuwekeza katika kununua dhahabu na uchimbaji madini nchini Zimbabwe”.
Suzan General Trading ~ Walisema kwamba shughuli zao ni halali na zilizingatia sheria katika kila hali.
Dmytro Abakumov ~ Alikanusha kuajiriwa na Bwana Pattni au kujihusiha na vitendo vyovyote vya kiuhalifu, ama kupitia yeye mwenyewe au kampuni yake ya Skorus Investiments, na kwamba kila kitu yeye na kampuni yake ilifanya ilikuwa katika utekelezaji kamili wa masharti ya leseni yake na sheria zote zinazotumika.
Mishaal Pattni ~ Ndugu wa Bwana Kamlesh Pattni aliyetajwa kwenye barua kutoka Fidelity kwenda Uhamiaji Dubai pia alikanusha kuhusika na chochote na kuwaambia Al-Jazeera kuwa hajasafiri kwenda Zimbabwe toka mwaka 2017.
Aurex Jewellery ~ Walisema hawakuwa na ufahamu juu ya shughuli za utakatishaji fedha za Bwana Kamlesh Pattni wala Ewan MacMillan au kuhusu hatia (vifungo gerezani) za MacMillan kwenye usafirishaji haramu wa dhahabu na kwamba yenyewe inatoa huduma zake za utengenezaji wa mapambo ya vito kwa kampuni mbalimbali zilizosajiliwa kwenye eneo hilo baada ya kufanya uchunguzi na kufuata taratibu zote zinazostahili.
Watu/Pande nyingine zilizohusiswa kwenye Makala hii ~ Hawakujibu chochote.
Pale ambapo mtu anakuonesha vithibitisho vyote lakini unakomaa kuwa sio wewe ila ni mkono wa baunsa😂😂😂.
Katika Episode ya 2 ya Gold Mafia Simon Rudland anatafuta mtakajishaji pesa, na anamapata. Je ni nani huyo? Upande mwingine mkutano wa Bwana Stanley na Rais Manangagwa unakuja na gharama kubwa… Tukutane wakati mwingine wakuu kwa muendelezo wa makala hii.
Muendelezo Soma - Episode 2 - Sehemu ya 1
Pattni nae ana vijana wake special wanaofanya kazi ya kusafirisha dhahabu kwenda Dubai na kurudi na pesa Zimbabwe. Ripota Undercover anafanikiwa kukutana na mmoja wa vijana hawa. Mwamba huyu anaitwa Dmytro Abakumov.
Dmytro Abakumov
Mbali na Abakumov kufanya kazi hiyo ya kuwa msafirishaji wa Bwana Pattni, Abakumov pia ni Mkurugenzi katika moja ya kampuni za Pattni ambayo ipo Zimbabwe. Kamera ya Al-Jazeera haikumuacha salama, inamdaka jamaa akiwa katika majukumu yake ya magendo Uwanja wa Ndege wa Harare, Zimbabwe.
Abakumov akiwa amenaswa na kamera ya Al-Jazeera uwanja wa ndege wa Harare
Ili waweze kufanya biashara zao bila shida, lazima wawe na nyaraka sahihi kwa ajili ya biahsara hiyo. Bwana Pattni bila kujua kama ananaswa na kamera, anaonyesha barua kutoka Fidelity Printers kwenda Dubai inayotaja majina ya Abakumovu na ndugugu yake Pattni, Mishaal Pattni inayoidhinisha kampuni ya Pattni inayoitwa Susan General Trading kubeba dola za Kimarekani milioni 3 kila wiki kuingia Zimbabwe
Benki Kuu inatangaza kuwa biashara/kampuni ya Susan's jewelry and gold exports ndio inayoongoza kwa kuingiza dola za Marekani nchini. Kampuni hii ya Susan imejiimarisha na kukuza network yake iliyipa nguvu kifedha na kuzalisha dola za Kimarekanani milioni 168 kwa mwaka 2020. Biashara ya Susan inachukuliwa kuwa ni yenye thamani kubwa katika kuzalisha fedha taslimu kwaajili Zimbabwe, mpaka serikali imeamua kuwalipa bonasi ya thamani ya 18% ya mauzo yake. Lakini nyaraka zilizopatikana kutoka kitengo cha Al-Jazeera zinaonyesha kuwa yote ni sehemu ya himaya ya Pattni kwenye biashara zake chafu za dhahabu.
Benki Kuu inatangaza kampuni ya Susan's jewelry and gold exports kuwa kinara wa kuingiza dola za Marekani nchini
Barua inayoonesha serikali kupitisha bonasi ya thamani ya 18% ya mauzo yake kwa Suzan General Trading
Al-Jazeera walitafuta wahasabu wa zamani wa Pattni kupata taarifa zaidi na kufanikiwa kuwapata baadhi. Muhasibu Sami (utambulisho wake halisi umefichwa), akaeleza jinsi Pattni alivyokuwa akifanya kazi, akisema kuwa Pattni anauza vito na dhahabu nchini Dubai na sehemu nyingine za dunia, ambapo yeye anapaswa kupeleka fedha za kigeni Zimbabwe. Wakati hao wabeba/wasafirisha dhahabu wakifika uwanja wa ndege wa Harare baada ya safari zao za Dubai, walitakiwa kusema pesa walizorejesha Zimbabwe kwa kutumia Fomu 47 ambayo kwa kawaida huitwwa Fomu ya Bluu. Akaendelea kusema kuwa wakati mawakala wao/wasafirisha dhahabu wakitaja kiasi cha fedha walizorejesha huwa hawasemi kweli, wanadanganya! Wakati mwingine hupeleka dola elfu 50 au laki moja lakini kwenye kujaza fomu/kutaja kiasi walichopeleka huandika milioni 1 au 2.
Pattni mwenyewe siku moja anarekodiwa katika Fomu ya Bluu akiwa anarejesha pesa Zimbabwe. Pattni akajaza kuwa amepeleka dola milioni 1.2, pesa zilizopatikana baada ya kuuza vito Dubai. Lakini Patni hakupelea pesa hizo dola milioni 1.2 badala yake alipeleka hela ambayo haifiki hata dola laki moja. Pattni na wenzake wanaweza kufanikisha hilo kwa kuhonga wafanyakazi wa uhamiaji na kuwaambiwa waandike kiasi wanachotaka.
Fomu ya Bluu iliyorekodi pesa alizoingia nazo Pattni Zimbwabwe
Wakati mhasibu anarekodi kwenye vitabu vyake hakuandika dola milioni 1.2 badala yake aliandika pesa halisi bwana Patni aliyokuja nayo ambayo ilikuwa haifiki data dola laki moja.
Kitabu kikionesha kiasi halisi cha pesa alichoingianacho Bwana Patni
Patni akionesha Fomu ya Bluu ambayo wanasema kiasi cha fedha walichoingia nacho Harare kutoka mauzo ya dhahabu Dubai
Patni anaacha sehemu kubwa ya pesa za mauzo ya dhahabu Dubai, kutokana na hili sasa Bwana Pattni anakuwa hana hela za kutosha kununua dhahabu kwaajili ya roundi nyingine (kupeleka dhahabu Dubai kuuza na kurudisha fedha Zimbabwe). Ili kuendelea kuwa na leseni inayomsuhuru kwenda kuuza dhahabu nje ya nchi itabidi sasa anunue dhahabu kutoka kwa wachimbaji wadogo, anafidia kiasi cha pesa ambacho hana kutoka kwenye soko la Hawala (si unaikumbuka hii, wale wanafirisha pesa bila pesa yenyewe kutembea?) wa Zimbabwe wanaotaka kutuma pesa Dubai. Kwahiyo hela anayoipata kwa hawa watu ndio anayotumia kununua dhahabu, huku Dubai wateja wake wa Hawala wanalipwa kutokana na mauzo ya dhahabu aliyoinunua Zimbabwe na mzunguko unakuwa huo huo kila wakati huku yeye akiweka mfukoni 18% yake. Pesa inayohitajika kwa udi na uvumba haingii kwenye uchumi wa Zimbabwe haifiki kama inavyotajariwa.
Fomu inayoonesha hela zilizopokelewa na Pattni kutoka soko la Hawala
Kutokana na anachofanya, Pattni anakuwa mafia mara mbili, kwenye hizo dili zake tayari ni mhalifu tayari lakini anaongezea na kuibia na serikali ambayo imemruhusu kufanya uhalifu wake! Anajifanya kuisaidia Zimbabwe kwa kupeleka fedha za kigeni zinazohitajika sana lakini anachopeleka ni kiduchu sana ambacho ni sawa sawa na 0. Hii tunaiitaje, mbwa kala mbwa au mbuzi kafia kwa muuza supu?
Sasa hapa kila mtu amaeshaonesha uwezo wake wa kukamilisha kazi ya Bwana Stanley (kutakatisha pesa zake kutoka china), washajiuza vya kutosha na kutoa ramani yote ya jinsi mchongo unavyofanyika na mambo yatakavyoenda vizuri bila wasiwasi, sasa ni muda wa kutamba kujionesha kwamba wewe ni zaidi ya genge fulani. Nabii Angel anatamba mbele ya ripota wa undercover, anasema bwana we mimi sio mjinga, nina degree mbili za uchumi, kwahiyo ninajua vizuri nini nafanya, anasema jamani mi siongei sana CV yangu inajieleza; mbali na degree zangu mbili niliingia pia kwenye orodha ya matajiri ya Forbes kwa Afrika mwaka 2013, lakini pia ni Waziri wa Injili.
Nabii Angel akitamba kuonesha nguvu alizonazo akiwa na chawa (wasaidizi) wake
Nabii Angel na chawa wake wanajibu, jamani msiwe na shaka, tumeshaongea kuhusu hilo, mmeshuhudia wenyewe simu kadhaa zikipigwa kwa watu wa nguvu, yaani mambo yameshawekwa sawa, tunasubiri nyinyi tu mtie mzigo tufanye biashara, halafu Nabii Angel akauliza, kwani mnataka kuwekeza mpunga kiasi gani?
Bwana Stanley akajibu kwa kuanzia nataka niwekeze kama dola bilioni moja hivi, Nabii akajibu okaaaay (hapo anaona ameulmba), kisha anamjibu Bwana Stanley kuwa, sisi tumewahi kufanya biashara za dola milioni 200 au 300 lakini hatujawahi kufanya kwa kiasi kikubwa hivyo kama bilioni 1.
Angel na msaidizi wake wanamchukua Bwana Stanley pembeni, na kumwambia bwana sikia, mimi ndio mtu wa pili mwenye nguvu kimamlaka Zimbabwe, unajua naweza kumuweka huyu chawa wangu (akionesha upande wa msaidizi wake) kwenye mfuko na hakuna mtu ataruhusiwa kugusa wala kukagua mzigo wangu? Unajua naweza kuweka kwenye mkoba wangu dola bilioni 1.2 kwenye mkoba wangu nikazungushia utepe mwekundu wa kibalozi na kazi imeisha? Nabii Angel anajitamba jinsi anavyoweza kutumia kofia yake ya ubalozi kupiga dili zake chafu bila shida yoyote. Anamwambia Bwana Stanley usiwe na wasiwasi wowote kwani kofia ya ubalozi itaingiza hizo hela Zimbabwe fasta tu, kama nakunywa maji vile, mzigo utafika Zimbabwe hakuna mtu ataugusa mpaka utafika nyumbani kwangu (kwa Nabii Angel).
***
Uchunguzi kwa Episode ya 1 ukaishia hapa, matokeo ya uchuguzi huu, yaani kila kilichorekodiwa mwanzo mpaka mwisho kilipelekwa/wasilishwa kwa kila aliyohusishwa/aliyeonekana katika Makala hii, na haya ndio yalikuwa majibu yao;
Simon Rudland ~ Alisema tuhuma zote kuhusu yeye ni uongo, ni kampeni zilizofanywa dhidi yake na watu wasiojulikana kumchafua, akajielezea yeye kama mfanyabiashara imara, mwenye nguvu, anaejiweza, anaepambana na watu wenye tamaa na wivu
Gold Leaf Tobbaco ~ Walikanusha kuhusika kwao katika Sakata hili kwa nguvu zote kwenye chochote kilichofanyika kipindi cha nyuma ama sasa kuhusisha shughuli za utakatishaji fedha, biashara ya magendo ya dhahabu ama chochote kinachoendana na hayo.
Fidelity Printers and Refiners ~ Walikanusha kuwa na uhusiano wowote wa kibiashara na Bwana Simon Rudland au kumpa leseni ama kutoa upendeleo au motisha kwa yeyote aliyetajwa kwenye Makala hii. Pia Fidelity ikakanusha kuhusika kwa vyovyote vile kwenye shughuli za utakatishaji pesa, biashara za magendo au majaribio ya kukwepa/kuvunja vikwazo walivyowekewa na chi za Magharibi kupitia mlango wa nyuma.
Benki Kuu ya Zimbabwe ~ Iliwaambia Al-Jazeera kuwa inachukulia vitendo vya utakatishaji pesa na shughuli zote za biashara haramu/magendo kwa uzito mkubwa sana na kwa vyovyote vile iwe moja kwa moja wao au kupitia mtu/taasisi nyingine haiwezi kujihusisha na shughuli hizo.
Alistair Mathias ~ Alikanusha kutengeza mpango wa kutakatisha pesa na kusema hajawahi kutakatisha pesa au kufanya biashara ya dhahabu kwa magendo kwa Warusi ama kwa mtu yoyote yule, na kuongeza kuwa hajawahi kuwa na uhusiano wowote wa kibiashara na Bwana Ewan MacMillan.
Kamlesh Pattni ~ Amekanusha kufanya uhalifu wowote Kenya na kusisitiza kuwa hajawahi kukutwa na hatia kuhusiana na shughuli alizokuwa anafanya Kenya. Pia alikanusha uhusika wake kwenye utakatishaji pesa wala kuisaidia Zimbabwe kukwepa vikwazo walivyowekewa na chi za magharibi, alikanusha pia kuwahi kuajiri mtu yoyote kuingiza pesa kimagendo au kujitolea kushughulikia pesa ambazo anajua zimetokana na shughuli za uhalifu, na kwamba alipokutana na wachunguzi wa Al-Jazeera alidhani amekutana na mwekezaji aliyetaka kuuza sehemu ya biashara ya hoteli na ambaye alitaka “Kujiondoa katika mfuko wa uwekezaji nchini China ili kuwekeza katika kununua dhahabu na uchimbaji madini nchini Zimbabwe”.
Suzan General Trading ~ Walisema kwamba shughuli zao ni halali na zilizingatia sheria katika kila hali.
Dmytro Abakumov ~ Alikanusha kuajiriwa na Bwana Pattni au kujihusiha na vitendo vyovyote vya kiuhalifu, ama kupitia yeye mwenyewe au kampuni yake ya Skorus Investiments, na kwamba kila kitu yeye na kampuni yake ilifanya ilikuwa katika utekelezaji kamili wa masharti ya leseni yake na sheria zote zinazotumika.
Mishaal Pattni ~ Ndugu wa Bwana Kamlesh Pattni aliyetajwa kwenye barua kutoka Fidelity kwenda Uhamiaji Dubai pia alikanusha kuhusika na chochote na kuwaambia Al-Jazeera kuwa hajasafiri kwenda Zimbabwe toka mwaka 2017.
Aurex Jewellery ~ Walisema hawakuwa na ufahamu juu ya shughuli za utakatishaji fedha za Bwana Kamlesh Pattni wala Ewan MacMillan au kuhusu hatia (vifungo gerezani) za MacMillan kwenye usafirishaji haramu wa dhahabu na kwamba yenyewe inatoa huduma zake za utengenezaji wa mapambo ya vito kwa kampuni mbalimbali zilizosajiliwa kwenye eneo hilo baada ya kufanya uchunguzi na kufuata taratibu zote zinazostahili.
Watu/Pande nyingine zilizohusiswa kwenye Makala hii ~ Hawakujibu chochote.
Pale ambapo mtu anakuonesha vithibitisho vyote lakini unakomaa kuwa sio wewe ila ni mkono wa baunsa😂😂😂.
Katika Episode ya 2 ya Gold Mafia Simon Rudland anatafuta mtakajishaji pesa, na anamapata. Je ni nani huyo? Upande mwingine mkutano wa Bwana Stanley na Rais Manangagwa unakuja na gharama kubwa… Tukutane wakati mwingine wakuu kwa muendelezo wa makala hii.
Muendelezo Soma - Episode 2 - Sehemu ya 1