Raia mdogo
JF-Expert Member
- Jan 5, 2018
- 1,387
- 1,518
Tatizo connectionHizi ndio dili
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Tatizo connectionHizi ndio dili
Kusoma na kuelewa ni vitu viwili tofauti,umesoma hujaelewa kilichoandikwaMleta mada kwenye hiyo.documentaey sijaona Mwizi au aliyeibiwa hata mmoja kama yupo tuambie wewe Kamwibia nani kwenye hicho kinaitwa Gold Mafia? Rudia tena kuiangalia mimi binafsi sijaona aliyeibiwa hapo nani Tusaidie wewe kwenye hiyo Gold Mafia Documentary nani kaibiwa chochote kwa wahusika wote Sababu hakuna Mlalamikaji kwenye hiyo Documentary sio serikali ya Dubai wala ya Zimbabwe wala wafanyabiashara wakubwa na wadogo wa dhahabu.Kila mmoja kalipwa chake kwenye chain .
Aljazeera hopeless kabisa.Kwa hiyo Aljazeera ndie Mlalamikaji au?
Kilichoandikwa wala hakina weledi wowote wa maana kama ambavyo hiyo Gold Mafia Documentary yenyewe.isivyokuwa na weledi wa maana wenye hitimisho la.maana la mwizi nani na aliyeibiwa naniKusoma na kuelewa ni vitu viwili tofauti,umesoma hujaelewa kilichoandikwa
Kaa kimya kuficha Upumbavu wako
"ba welding" ndio nini?Kilichoandikwa wala hakina weledi wowote wa maana kama ambavyo hiyo Gold Mafia Documentary yenyewe.isivyokuwa ba welding wa maana wenye hitimisho la.maana la mwizi nani na aliyeibiwa nani
Achana na shoga Hilo linatafuta bwana"ba welding" ndio nini?
Yani wana sisiem mnachekesha sana! Kwahiyo wewe hapo huoni kilichoibiwa kwa sababu nyie mmezoea wizi mnaona sawa tu au sio?Mleta mada kwenye hiyo.documentaey sijaona Mwizi au aliyeibiwa hata mmoja kama yupo tuambie wewe Kamwibia nani kwenye hicho kinaitwa Gold Mafia? Rudia tena kuiangalia mimi binafsi sijaona aliyeibiwa hapo nani Tusaidie wewe kwenye hiyo Gold Mafia Documentary nani kaibiwa chochote kwa wahusika wote Sababu hakuna Mlalamikaji kwenye hiyo Documentary sio serikali ya Dubai wala ya Zimbabwe wala wafanyabiashara wakubwa na wadogo wa dhahabu.Kila mmoja kalipwa chake kwenye chain .
Aljazeera hopeless kabisa.Kwa hiyo Aljazeera ndie Mlalamikaji au?
Achana nae mwana sisiem huyo! Wamezoea wizi ndio maana anakushangaa eti wizi uko wapi?Ipi definition yako ya 'kuibiwa' tuanzie hapo....
Anaetumia mali ya umma kwa manufaa yake ni mwizi usifukie mashimo... Na mifano kwa waliolalamika...part ya Kenya umepitia? Hujaona chochote kuhusu hilo? Waziri wa Fedha Zimbabwe kuongelea magendo yanayofanywa kutorosha dhahabu hiyo ambayo ingetumiwa accordingly kwa manufaa ya nchi ingewasogeza pakubwa...unaona ninsawa kwakuwa kila mtu "Anapewa chake"?
1 + 1 = 11Ikiendelea mnitag wakuu
Uebert Angel na pastor kapola walikuwa na mkutano wa injili wiki jana,je Kuna muunganiko wowote hapa?
Ngumu ila km unazipata ,uhakikaTatizo connection
Nimetoa huko Instagram....Episode 1 - Sehemu ya 5
Tulipoishia Bwana pili Patni naye kwa upande wake alitoa njia nyingine ya kusafirisha pesa chafu za Bwana Stanley kutoka China kwenda Dubai. Njia hizo ni kwa kutumia wakala wa usafirishaji na njia ya pili ni kupitia Hawala.
Tuendelee...
Hawala ni kama neno la kitamaduni linalomaanisha njia isiyo rasmi ya kuhamisha fedha nje ya njia za benki kutoka nchi A kwenda nchi B. Kawaida, hawala hujumuisha watu wenye uhusiano wa karibu unaoweza kuwa wa kindugu (familia) au wanaojuana kwa njia nyingine ambao hubadilishana fedha na kuweka rekodi katika vitabu vya hesabu. Mfano unataka kutuma dola mia katika jambo letu, wakala wa Hawala wa Patni huko Hong Kong angechukua noti ya dola mia chafu kutoka kwa Bwana Stanley, kisha wataandika katika kitabu chao cha hesabu kwamba wamepokea pesa, halafu watatuma ujumbe kwa mshirika wao Dubai ukiwaambia tumepokea pesa kiasi kadhaa, tafadhali mlipeni pesa sawa kama iliyolipwa huku.
Mtu mwingine wa operesheni hii ya hawala anayefanya kazi na Pattni huko Dubai atamlipa Stanley dola mia. Kwa hivyo, dola mia hazitumwi kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine, ila ni kanjia ka kufanya account zisome bila shida. Mawakala hawa wa Hawala wanahakikisha vitabu vyao viko sawa kwa pande zote mbili kadri wateja wanavotuma pesa. Kwa upande mmoja, njia hii ni halali, mara nyingi ndio njia pekee kwa wahamiaji wa kiuchumi (wahamiaji wanaohama nchi moja moja kwenda nyingine kwaajili ya fursa za kiuchumi) kuhamisha pesa, lakini pia inaweza kutumiwa kama njia ya wahalifu na magenge ya uhalifu kuepuka kugundulika kupitia mfumo wa benki, na akina Pattni na wahalifu wenzake wanaitumia njii hii vizuri kwenye biashara zao za kutakatisha pesa.
***
Unamkumbuka Nabii Angel? Makala hii inaturudisha kwake kutuonesha jinsi naye alivyoingia mkenge kwa Bwana Stanley akidhani ni mteja kweli anayetaka kutakatishiwa pesa zake. Nabii Angel anamwambia Stanley kama unataka dhahabu hilo halina shida ninaweza kumpigia Rais wa Chama cha Wachimbani wa Madini nchini, ukamsikiliza mwenyewe anavyoelezea mlolongo huu tukafanya biashara.
View attachment 2673703
Nabii Angel akiwa anaongea na Rais wa Chama cha Wachimba Madini akiwa kwenye loud speaker
Rais wa Chama cha Wachimba Madini anavutiwa waya chaap, huyu si mwingine bali ni bibie Henrietta Rushwaya, mpwa wa Rais Manangagwa. Nabii Angel anamuleza dili lililopo mezani na kumwabia bibie Rushwaya kuwa jamaa wanataka kuwekeza pia kununua na kuwekeza kwenye dhahabu, Rushwaya anasema hamna tatizo, hilo jambo dogo sana sana, limeisha.
Rushwaya anaanza kuelezea mchakato wa jinsi wanavyofanya biashara, kwa kila kilo 100 za dhahabu wanapata punguzo la 4% katika bei soko ya dunia, mpango wa Rushawa utakuwa unatakatisha dola milioni 5 kila wiki kwa njia ya mzunguko. Mchakato unaanza na malipo ya fedha chafu kiasi cha dola milioni 10 kwa wenye jukumu la kuchakata dhahabu Zimbabwe, Fidelity Printers. Wakipeleka kiasi cha milioni 10 kwa mfano, milioni 5 zitawekwa Fidelity Printers kwa kipindi cha uhusiano wao na watakuwa wanapata dhahabu yenye thamani ya milioni 5 kila wiki, wakitakata tena huduma hiyo mzunguko unakuwa huohuo wataacha dola milioni 5 na kila wiki watakuwa wanapata dhahabu yenye thamani wa dola milioni 5. Mchakato huu unaendelea mpaka hela zote zisafishwe.
Mfumo wa Rushwaya unaweza kusafisha pesa nyingi zaidi za Bwana Stanley. Ikiwa atapeleka fedha chafu milioni 20, utaratibu ni ule ule nusu ya fedha hizo zitawekwa (zitabaki) Fidelity Printers, dola milioni tano zitasafishwa kila wiki kwa wao kupewa dhahabu zenye thamani sawa na kiasi hicho na dola milioni 5 nyingine zilizoongezeka zitasafishwa kupita moja ya connection za Rushwaya. Hivyo kwa mpango huo bwana Stanley ataweza kusafisha dola milioni 10 kila wiki. Rushwaya anamaliza kutoa maelezo yake na wanaahidiana kutafutana baadae Nabii Angel akishawekana sawa na Stanley. Wakati wanaendelea na mazunguzo, Nabii Angel anamtambulisha mtu anayefanya naye kazi (wa kushoto kwenye picha inayoonekana hapo chini) kwenye kampuni yake inayoitwa Billion Group iliyoko Zimbabwe na inafanya shughuli zake zote Zimbabwe, ambaye anaweza kuwa mshirika wa bwana Stanley kila atakapokuwa anashughuli Zimbabwe, ili awe na mtu anayemfamu akitata kufanya biashara wakati mwingine.
Wakati hayo yanaendelea Nabii Angel yuko Glasgow na Rais Manangagwa kwenye mkutano wa mabadiliko ya hali ya hewa wa Umoja wa Mataifa ambako anadai kuwa vikwazo walivyowekewa vinaizuia Zimbabwe kutekeleza ahadi zake kwenye uchumi endelevu. Angel anamwambia Bwana Stanley kwamba anaweza kukutana na Rais.
Vikwazo vilivyowekwa na mataifa ya nje vinazuia uwezo wa wanasiasa na taasisi za serikali za Zimbabwe kufanya biashara, hivyo wanatumia watu (binafsi) wengine kufanya biashara kwa niaba yao kwakuwa mtu mmoja mmoja haguswi na vikwazo hivyo vilivyoikusudia Zimbabwe kama nchi. MacMilan ana uhusiano wa kifamilia na mfanyabiashara mwingine anayesaidia serikali kukiuka vikwazo ama tuseme kupigana na vikwazo hivyo. MacMillan anamuelezea jamaa huyu kama baba lao, yaani ana pesa za kutosha yeye na Pattni wanakaa, na hela zake ndio zinatumika kufadhili benki zote Zimbabwe. Jamaa anaweza kumpigia simu Gavana wa Benki kuu muda wowote na kupanga mkutano. Yeye ni mmiliki wa kampuni kubwa ya sigara nchini Afrika Kusini, chapa ya bidhaa zake ni jina lake, huyo si mwingine bali ni Bwana Simon Rudland.
Wakuu tukutane siku nyingine kwaajili ya muendelezo na kumfahamu zaidi kubwa lao Bwana Simon Rudland
Muendelezo soma - Episode 1 - Sehemu ya 6
IN ONE NIGHTNimetoa huko Instagram....
Hao mafia wanapiga hela hatariNgumu ila km unazipata ,uhakika
Leo ntaweka muendelezo tumalize kabisa Episode 1Mkuu Rare Sapphire tunaomba muendelezo tafadhali
Sawa mkuu! Ikiwezekana weka episodes za kutosha mkuu Rare SapphireLeo ntaweka muendelezo tumalize kabisa Episode 1