GSM: Kila bao atakalolifunga Yanga dhidi ya Mamelodi Sundowns nitalinunia kwa Tsh. 100M

Uzee sio miaka! Kikwete ana uzee gani bado analipa kabisa
Ukiacha mwili uwe na likitambi lazima uwahi kuzeeka
Sasa wewe na kitambi chako hiko soon utazeeka😄
Ahahahah..katika vitu sina na sijawah kuwa navyo na as long as nitaendelea kuishi hapa mjini sitakuwa nacho ni kitambi 😂😂. Huo uzito tu sijawah fikisha 75kg, kitambi kitatoka wapi?.
Najali sana afya, maana nikiumwa kila kitu kitaumwa 😂
 
Image inayokujaga kichwani kwangu ni mtu mmoja mnene kiasi mrefu😂 kilogram za kutoshaaaaaaa....... kitambi kama chote
 
Dah..ramadhani hii watu wanatoa swadaka wengine wanafanya haya.
 
Picha iko hivi; Yanga wamewaahidi mastaa wao Tsh. 100Mil kila bao watakalofunga dhidi ya Mamelodi. Kumbuka, Simba na Yanga mpaka sasa zina uhakika wa Tsh. 2.3Bil kama zawadi kwa kucheza hatua ya robo fainali lakini yoyote atakayefuzu nusu tu mkwanja unaongezeka kufikia Tsh. 3Bil kwahiyo hata wakichomoa kwenye hiyo bado klabu zitabaki na cha juu.

Yanga wakati wanacheza mechi yao ya kwanza nyumbani dhidi ya Mamelodi Sundowns vigogo wao waliwawekea mezani kiasi cha Sh 300Mil endapo itafanikiwa kushinda matajiri hao wa madini lakini mechi hiyo ikamalizika kwa Suluhu.

Kuhakikisha matokeo ya sare yoyote ya mabao au ushindi yanayohitajika na Yanga ili ifuzu nusu fainali yanapatikana kwenye mchezo wa ugenini utakaopigwa Ijumaa saa 3:00 usiku, Kigogo wa Yanga, GSM ameongeza dau zaidi akiwaambia mastaa wao kuwa kila bao la mchezo huo litakuwa na thamani ya Sh 100Mil.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…