DOKEZO Habari hii ikufikie Waziri wa Afya, ubabe wa Hospitali ya Muhimbili utaniua

DOKEZO Habari hii ikufikie Waziri wa Afya, ubabe wa Hospitali ya Muhimbili utaniua

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Hismastersvoice

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2013
Posts
21,741
Reaction score
26,735
Waziri wa Afya ninaandika hili kwa uchungu mkubwa na majuto ya kujitawala, mimi ninaumwa nilikwenda hosipitali ya mkoa nikafanya X-Ray na Ct-Scan, kisha nikapewa rufaa kwenda Muhimbili.

Nimeenda Muhimbili tarehe 9/11/2023 nikiwa na CD ya Ct-Scan ili daktari aicheze kuona tatizo langu, daktari hawezi kuicheza mpaka niipeleke ICT eti waikopi waiweke kwenye mfumo wa Muhimbili!

Na ili waikopi ninatakiwa nilipe sh 86,000/=? Bila hivyo nikae na CD yangu nikafilie mbali, sina hela hiyo na pia sioni uhalali wa malipo hayo kwani hiyo CD ukiweka kwenye kompyuta inafunguka haihitaji uchawi wowote ule.

Mhe. Waziri walionipa CD hiyo ni hospitali ya Serikali na niligharamia hiyo Ct- Scan kwa ajili ya madaktari wajue tatizo langu na si kwa ajili yangu binafsi ya kutengeneza Bongo muvi, hiyo CD kwangu mimi ni nyangarakasha kwani sina utaalamu wa kuisoma na nimeingia hasara ya kufanya Ct- Scan.

Kwaheri kuonana ni majaliwa.
 
Kitengo cha ICT naona wana watu wendawazimu.

Kufanya Uploading ya data za kwenye CD kuziingiza kwenye mfumo ni kuijaza DATABASE bila sababu ya msingi. Kwanini Daktari asiwe na files zake yeye mwenyewe bila kuwa redirected na watu wengine? Kingine faragha ya Mgonjwa ipo wapi hapo? Maana IT anaona kila kitu.

Kwa upande wa pili, kwanini hizo Hospital za rufaa zisiwe na portal ya kutuma hizo data moja kwa moja kwa daktari wa Muhimbili? Dunia inatoka ktk physical devices hasa hzi storage devices kama vile CD.

Inatakiwa Ubunifu wa hali ya juu ktk hii ishu mifumo isomane.
 
Kitengo cha ICT naona wana watu wendawazimu.

Kufanya Uploading ya data za kwenye CD kuziingiza kwenye mfumo ni kuijaza DATABASE bila sababu ya msingi. Kwanini Daktari asiwe na files zake yeye mwenyewe bila kuwa redirected na watu wengine? Kingine faragha ya Mgonjwa ipo wapi hapo? Maana IT anaona kila kitu.


Kwa upande wa pili, kwanini hizo Hospital za rufaa zisiwe na portal ya kutuma hizo data moja kwa moja kwa daktari wa Muhimbili? Dunia inatoka ktk physical devices hasa hzi storage devices kama vile CD.

Inatakiwa Ubunifu wa hali ya juu ktk hii ishu mifumo isomane.
Tatizo hospital za umma zinapewa target ya kukusanya mapato kama Halmashauri na TRA, utashangaa unapiga X-ray Hosp A ukienda Hosp B wanataka upige tena na hiyo hawaitambui na wakati umetoka Government Hosp. Ni mambo ya kijinga sn
 
Muhimbili muhimbili muhimbili.nimewaita mara tatu.
Niliwahi pewa stori za umafia unaofanyika muhimbili na sijajifikiria kuamini habari za mtoa mada.
Siku nikilewa nitawaanika wote wanaofanya michezo michafu muhimbili.
 
Kwa upande wa pili, kwanini hizo Hospital za rufaa zisiwe na portal ya kutuma hizo data moja kwa moja kwa daktari wa Muhimbili? Dunia inatoka ktk physical devices hasa hzi storage devices kama vile CD.

Inatakiwa Ubunifu wa hali ya juu ktk hii ishu mifumo isomane.
Hii post ione mganga mkuu wa serikali na mkurugenzi wa hospitali ya taifa muhimbili.

Huwezi kuwa na kitu kinaitwa hospital ya taifa wakati hakiwezi kusoma taarifa kutoka hospitali za mkoa. sasa huo utaifa wamejivika wa nini?
 
Back
Top Bottom