DOKEZO Habari hii ikufikie Waziri wa Afya, ubabe wa Hospitali ya Muhimbili utaniua

DOKEZO Habari hii ikufikie Waziri wa Afya, ubabe wa Hospitali ya Muhimbili utaniua

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Hii post ione mganga mkuu wa serikali na mkurugenzi wa hospitali ya taifa muhimbili.

Huwezi kuwa na kitu kinaitwa hospital ya taifa wakati hakiwezi kusoma taarifa kutoka hospitali za mkoa. sasa huo utaifa wamejivika wa nini?
Taarifa nimewapelekea lakini na wao wanataka chochote wapate ndipo waipokee!
 
Tatizo hospital za umma zinapewa target ya kukusanya mapato kama Halmashauri na TRA, utashangaa unapiga X-ray Hosp A ukienda Hosp B wanataka upige tena na hiyo hawaitambui na wakati umetoka Government Hosp. Ni mambo ya kijinga sn
Sasa hizi ndio sehemu za kufanyia overhaul.. Huduma ya Afya sio chanzo cha Mapato.

Waache upumbavu kuna namna nyingi za kuchukua hela za Wananchi kwa hiari yao bila wao kuumia ni swala la ubunifu tu.
 
Hii post ione mganga mkuu wa serikali na mkurugenzi wa hospitali ya taifa muhimbili.

Huwezi kuwa na kitu kinaitwa hospital ya taifa wakati hakiwezi kusoma taarifa kutoka hospitali za mkoa. sasa huo utaifa wamejivika wa nini?
Ni shida sana.. na huenda hata Hapo Muhimbil na kule Mloganzila taarifa hazisomani.
 
Sasa hzi ndio sehem za kufanyia overhaul.. Huduma ya Afya sio chanzo cha Mapato.

Waache upumbavu kuna namna nyingi za kuchukua hela za Wananchi kwa hiari yao bila wao kuumia ni swala la ubunifu tu.
Mkuu wasipofikia target 90% ya makusanyo wanaitwa kwenda kujieleza ama Mkurugenzi/MOi uteuzi wake unatenguliwa na KM, ni mambo ya kijinga sn kugeuza huduma ya Afya kuwa chanzo cha mapato.
 
Kitengo cha ICT naona wana watu wendawazimu.

Kufanya Uploading ya data za kwenye CD kuziingiza kwenye mfumo ni kuijaza DATABASE bila sababu ya msingi. Kwanini Daktari asiwe na files zake yeye mwenyewe bila kuwa redirected na watu wengine? Kingine faragha ya Mgonjwa ipo wapi hapo? Maana IT anaona kila kitu.


Kwa upande wa pili, kwanini hizo Hospital za rufaa zisiwe na portal ya kutuma hizo data moja kwa moja kwa daktari wa Muhimbili? Dunia inatoka ktk physical devices hasa hzi storage devices kama vile CD.

Inatakiwa Ubunifu wa hali ya juu ktk hii ishu mifumo isomane.
Wao wanatumia kigezo kuwa sisi hatujui kompyuta zinavyofanya kazi, tuione kompyuta kama dubwasha kuubwa la ajabu.
 
Mkuu wasipofikia target 90% ya makusanyo wanaitwa kwenda kujieleza ama Mkurugenzi/MOi uteuzi wake unatenguliwa na KM, ni mambo ya kijinga sn kugeuza huduma ya Afya kuwa chanzo cha mapato.
Kama ni hivi basi hata huduma hupewi kwa asilimia 100. Maana ukipona hautarudi.. utatibiwa kwa kupapasa juu juu tu. Ilimradi usife ila usipone. Ili kesho urudi tena.
 
Wao wanatumia kigezo kuwa sisi hatujui kompyuta zinavyofanya kazi, tuione kompyuta kama dubwasha kuubwa la ajabu.
Ni mambo ya ajabu sana kwa kweli.. au kwanini kusiwe na User portal ya Mgonjwa? Anaingia anaweka taarifa zake na kila kitu kumhusu kinabaki humo. Akienda ktk hosp nyingine wanalogin na kutrack historia ya matibabu yake.? Kuna mambo mengi ya kimfumo yanatakiwa yawe implemented
 
Waziri wa Afya ninaandika hili kwa uchungu mkubwa na majuto ya kujitawala, mimi ninaumwa nilikwenda hosipitali ya mkoa nikafanya X-Ray na Ct-Scan, kisha nikapewa rufaa kwenda Muhimbili.

Nimeenda Muhimbili tarehe 9/11/2023 nikiwa na CD ya Ct-Scan ili daktari aicheze kuona tatizo langu, daktari hawezi kuicheza mpaka niipeleke ICT eti waikopi waiweke kwenye mfumo wa Muhimbili!

Na ili waikopi ninatakiwa nilipe sh 86,000/=? Bila hivyo nikae na CD yangu nikafilie mbali, sina hela hiyo na pia sioni uhalali wa malipo hayo kwani hiyo CD ukiweka kwenye kompyuta inafunguka haihitaji uchawi wowote ule.

Mhe. Waziri walionipa CD hiyo ni hospitali ya Serikali na niligharamia hiyo Ct- Scan kwa ajili ya madaktari wajue tatizo langu na si kwa ajili yangu binafsi ya kutengeneza Bongo muvi, hiyo CD kwangu mimi ni nyangarakasha kwani sina utaalamu wa kuisoma na nimeingia hasara ya kufanya Ct- Scan.

Kwaheri kuonana ni majaliwa.
Nijuavyo mimi lazima waiingize kwenye mfumo wa Muhimbili , ili iwe kwenye systems zao, Hospitali nyingine wanamfumo wao na Muhimbili wanamfumo wao. kwanini hospital X wa Kucharge CT scan hali hawana utaalamu wa kusoma? Wakikuoa rufaa Muhimbili kisheria wanahitaji wakupime upya
 
Nijuavyo mimi lazima waiingize kwenye mfumo wa Muhimbili , ili iwe kwenye systems zao, Hospitali nyingine wanamfumo wao na Muhimbili wanamfumo wao. kwanini hospital X wa Kucharge CT scan hali hawana utaalamu wa kusoma? Wakikuoa rufaa Muhimbili kisheria wanahitaji wakupime upya
Kwahiyo nako nifanye Ct-scan upya! Bora nife tu.
 
Mkuu,
Kwanza pole sana kwa changamoto unazozipitia. Nakuelewa mimi. Kikawaida,japo maelezo hapa ni kama hayajitoshelezi,ila kuna haya:

1. Kiukweli mpaka CT-Scan, ni kwamba kuna tatizo.

2. Ili ifanyike hiyo CT-Scan au vipimo vya mashine hizo, lazima kuna daktari aliyekuandikia kufanya hivyo vipimo.

Mara zote iwe hiyo X-ray, Iwe CT-Scan, iwe MRI, Cd zinazotolewa huambatana na karatasi inayoripoti waliokupima wameona nini.

Hawa watu wanaokupima, ni watumiaji tu wa mashine hizo,hawawezi kamwe kuintapreti walichokiona na kumwambia mgonjwa. Wanaheshimu sana maagizo. Hivyo,unapopewa majibu,yanakuwa yamefungwa na hurudishwa kwa daktari alieomba vipimo hivyo tu.

Ikitokea hayupo karibu,huomba anaemfahamu mwenye uwezo wa kusoma na kuelewa.

Nadhani kutoka huko ulikozipata,iwe praiveti au hospitali ya serikali kwenda Muhimbili, ulipewa referal na ulitakiwa umuone either doctor fulani au uende kitengo furani na majibu yako,wakutengee doctor wa kuyasoma na kukusaidia.

Kama uliondoka na CD tu,bado unakosa ripoti inayoelezea ugonjwa wako,kwa sababu wengine akishasoma ile ripoti ataelewa tatizo lako hata asipocheza hiyo CD.

Kingine nachokiona hapa,hutaki kukili lakini ulikosea. Na kamwe usirudie au na mwingine asijaribu.
Wewe umesema kwamba hiyo CD kwenye computer inacheza. Ni kweli.
Ulijuaje inacheza?

Kwa sababu inapotoka sehemu kwenda sehemu nyingine,licha ya kuwa labda aliyekuandikia mara ya kwanza aliitazama,hawezi kukupa wazi wazi kuipeleka bila kufungwa,hiyo ni siri ya mgonjwa na ajuae ni daktari tu.

Labda yeye akwambie mwenyewe. Sasa,kuna uwezekano pia wa wao kuisusia baada ya kuona imeletwa katika mazingira yasiyo salama. Kama ulifungua,ulitakiwa uombe radhi na uahidi kutorudia.
Maana akisema ulipewa uwaletee,ukapeleka kwingine,ana point.

Harafu,kwa jazba ulonayo hapa,inaoekana huenda ulifika ukawagombeza. Na wale jamaa wana akili mbovu asikwambie mtu. Japo hupaswi kubembeleza tiba,inapobidi huna namna.

Mi nahisi haya makosa mawili ulifanya.
Japo sikumbuki vizuri,si lazima watu wa ICT waupload ndo aicheze,kama ana computer inayoisoma ni rahisi.
Changamoto ipo tu kwenye hizo gharama.

Nadhani ungeweka wazi kitengo,na waliotakiwa wafanye hivyo.

JF ina kila aina ya watu na si kwamba hili hawalioni. We elezea shida bila kupindisha maneno,nakuhakikishia utapata msaada tena haraka sana. Na kama ni kosa ulifanya,we jishushe uwe mkweli,wengine ni watu wazima wanaelewa ujana na maumivu,utasaidiwa
 
Back
Top Bottom