DOKEZO Habari hii ikufikie Waziri wa Afya, ubabe wa Hospitali ya Muhimbili utaniua

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Yeah na hiyo ufanywa kwa usalama wa Server 👏👏👏👏
 
Na ili waikopi ninatakiwa nilipe sh 86,000/=? Bila hivyo nikae na CD yangu nikafilie mbali, sina hela hiyo na pia sioni uhalali wa malipo hayo kwani hiyo CD ukiweka kwenye kompyuta inafunguka haihitaji uchawi wowote ule.[emoji3064][emoji3064][emoji3064]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole ndugu yetu.Hiyo ndio Tz.Mabazazi,madhalimu na walafi wapo kila mahali.Na kwa kweli mlilie Muumbaji tu.Hao wengine hawawezi kukusaidia
 
Kwa nchi yangu Tanzania bado sana. Viongozi wanajali matumbo yao kwanza. Madaktari hawezi kubali hilo litokee kwani itapunguzia njia haramu ya kupata pesa kwa wagonjwa.

Tanzania ni nchi ya kitapeli kila mtu tapeli. Inaumiza sana.
 
mkuu kuna mtu kakuuliza unayo report ya hyo ct scan kutoka kwa mtaalamu aliyefanya hyo ct scan kutoka hospital A? mbali na hyo cd, maana radiologist ndo mwenye utaalamu mkubwa wa kutafsiri hzo picha mkuu wangu.
 
Tatizo siyo kutibiwa tatizo kwanini dakitari asiisome hiyo CD na kisha anitibu bila ya kutaka picha yangu iingizwe kwenye seva za Muhimbili, ili iweje.
sasa mkuu taarifa zako si zinatakiwa ziwe kwenye database for future reference mkuu, cd si inaweza haribika au kupotea mkuu, halafu si wanasema kila kitu kinatakiwa kiwe kwenye mfumo boss.
 
Ripoti imeambatanishwa na DVD, aliyeisoma ni mtaalamu wa hispitali ya serikali.
Mimi bado sijapata mtu akithibitisha uhalali wa hiyo gharama ys shs. 86,000/= kwa ajili ya DVD kuingizwa kwenye mfumo wa Muhimbili, ili iweje!
Ndugu heshim taratibu za hospital uliopo,
 
Da. Watanzania tuna matatizo makubwa. Hili unalosema hata Ulaya hawezi kufanya hivyo. Yaani hospital ijivike jukumu la kuwasiliana na ulikotoka ili wapate records zako? Ni hivi: tatizo letu kubwa ni kuwa wananchi wengi hawajui tatizo letu hasa ni nini! Tatizo ni uongozi wa CCM uliofeli kwa namna zote uliofanya wananchi wawe maskini wa kutupwa na kutokujiweza kiuchumi. Kama tunataka mabadiliko basi tuiondoe CCM na siyo kulalamika kusiko na maana.
 
sasa mkuu taarifa zako si zinatakiwa ziwe kwenye database for future reference mkuu, cd si inaweza haribika au kupotea mkuu, halafu si wanasema kila kitu kinatakiwa kiwe kwenye mfumo boss.
Sihitaji future reference ninahitaji tiba ya sasa hivi kwanza, nimeingia gharama za vipimo vinne vikiwemo X Ray na CT Scan si kwa ajili ya hospitali iweke kumbukumbu yangu bali ni kwa ajili ya tiba ya sasa na si kwa mwaka keshokutwa.
 
Unajua maana ya synchronization? Yaani taarifa zote za mgonjwa zinakuwa online line in confidential form. Kama ikihitajika zinapatikana, mbona taarifa za NIDA zipo kwenye mfumo zinasomwa na mamlaka zingine kama Uhamiaji?
 
Binafsi nadhani umetoa maelezo ya kutosha kabisa ya kimfumo, mpo sawa kabisa kwa kufanya hivyo. Hapo utata unakuja kwenye gharama, uploading file lwenye systems za MNH kwa 86,000 mbona ni pesa nyingi sana mkuu? Otherwise maelezo yako mimi nakubaliana nayo.
 
Sihitaji future reference ninahitaji tiba ya sasa hivi kwanza, nimeingia gharama za vipimo vinne vikiwemo X Ray na CT Scan si kwa ajili ya hospitali iweke kumbukumbu yangu bali ni kwa ajili ya tiba ya sasa na si kwa mwaka keshokutwa.
Mkuu,
Future reference kwa taasisi kubwa kama MNH ni muhimu, lazima rekodi zako zihifadhiwe kwa ajili ya matumizi ya baadae, nimekuwa na wagonjwa kadhaa wamepitia MNH, muhimu sana kuweka rekodi.

Nisichoelewa, scan uliyofanya hospitali ya mkoa iligharimu kiasi gani? Na kingine ambacho nashindwa kuuelewa uongozi wa hospitali, gharama ya kufanya uploading ya hilo file, kwa nini iwe kubwa kiasi hicho?

Binafsi naamini ni lazima files ziwe uploaded ili kuweza kufanya follow up na kuweka data zako kwenye mifumo yao.
 
Unajua maana ya synchronization? Yaani taarifa zote za mgonjwa zinakuwa online line in confidential form. Kama ikihitajika zinapatikana, mbona taarifa za NIDA zipo kwenye mfumo zinasomwa na mamlaka zingine kama Uhamiaji?
Umesoma nilichoandika? Wachana na hiyo ya NIDA, mimi nimeishi kwenye nchi zenye application ya synchronization in real life. Unakwenda kumwona Dr akishaandika vipimo na dawa taarifa zako unazikuta tayari kule unakokwenda kufanya vipimo au pharmacy yoyote mjini. Ukienda hospital nyingine, nako dr anakuomba idhini kama utakubali a-retrieve data zako kutoka hospital uliyotibiwa mwanzo. Back to the topic: Rudi usome kwa ufahamu nilichoandika ili uelewe!
 
Bahati mbaya mlalamikaji hajaongea ukweli either kwa makusudi au hakumuelewa daktari. Issue kama hiyo iliwahi kunitokea . Maelezo niliyopewa ni kua mgonjwa wangu amekuja na CD yenye picha za CT scan kutoka hospitali nyingine,bila kua na report yake. Kusoma picha za CT scan ni taaluma inayosomewa,si Kila daktari atakua na uwezo wa kusoma hizo picha na kuona tatizo. usipokuja na report, unaweza shauriwa ufuate system ya muhimbili ambapo wanatoa hiyo huduma ya kuzisoma hizo picha na pia hiyo report itakua posted Kwenye system. Nilielekezwa na nikaelewa ni kwa nia njema ili daktari aweze kujua shida ya mgonjwa na mgonjwa apate matibabu sahihi. Shida tu ni gharama zinaongezeka,but alternative inaweza kumgharimu mgonjwa maisha yake.
 
Pole sana Mkuu, njoo inbox
 
Sihitaji future reference ninahitaji tiba ya sasa hivi kwanza, nimeingia gharama za vipimo vinne vikiwemo X Ray na CT Scan si kwa ajili ya hospitali iweke kumbukumbu yangu bali ni kwa ajili ya tiba ya sasa na si kwa mwaka keshokutwa.
sawa mkuu we endelea kukomaa nao watakutibu tu hawana namna.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…