Habari Njema; Nimeidhinishwa na Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Kutoa Elimu ya Fedha

Habari Njema; Nimeidhinishwa na Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Kutoa Elimu ya Fedha

Mkuu,
Nafikiri maelekezo niliyotoa yanaeleweka.
Sasa kama huwezi kufuata hata maelekezo, unataka tujadili nini hapa?
Au ndiyo kutafuta attention tu humu?
Useme una milioni 700 kwa mdomo halafu ue ndiyo ukweli?
Mnaonaga watu ni misukule au?
Haaha, Wewe sema tu, akaunti yako ina kiasi gani? Tuone kama una credibility ya kufundisha mtu, halafu mi sisemi tu.., ipo kweli hiyo 700 😁

Hata ingekuwa wewe, ungekubali kufundishwa kuhusu pesa na mtu ambae hata maandazi asubuhi yanampiga chenga?
 
Hongera sana Bwana Makirita. Hii ni habari njema sana. Nimekuwa pia mwanachama mwaminifu wa UTT na faida yake naendelea kuiona. Asante kwa kuendelea kutuelimisha kupitia experience yako pia. Naomba ushauri mmoja.

Nami pia nipo kwenye safari ya kuusaka utajiri na uhuru wa kifedha. Nina uwezo wa kusave 4,200,000 kila mwezi kwenye mfuko wa UTT na nimekuwa nikifanya hivyo. Nataka nifikie uhuru wa kifedha haraka iwezekanavyo ndani ya miaka 7 mpaka 8 ijayo. Unanishauri nijikite katika uwekezaji upi hasa ili niweze kufikia malengo yangu kwa haraka zaidi?

NB: Sina muda wa kusimamia biashara kabisa
 
Ila huruhusiwi kuchukua hadi miaka 25?
Unaweza kuchukua, unauza bond yako kwenye soko la hisa na kuchukua chako.
Ila hapo itategemea na hali ya soko.
Baada ya bond kuuzwa kwenye soko la awali (IPO) huwa zinaingia kwenye soko la upili kwenye soko la hisa. Kwenye soko la hisa watu wanaweza kuuziana kama wanavyouziana bidhaa nyingine.
 
Bosi unamiini Forbes? Hujui kuwa iko manipulated kuwezesha watu am nchi kupata loans au financial status for lobbing?
😀 😀
Kwa hiyo tusiamini forbes ila tukuamini wewe?
Hizi conspiracy za kimasikini huwa zinashangaza sana.
Maana huwa hata haziendani na logic.
Watu wote wanaokuwa featured kwenye forbes utajiri wao ni wa vyanzo vilivyo wazi.
Sasa unasemaje inakuwa manipulated?
 
Nakupongeza kwa hatua.
Pia, naomba muongozo unawafanya watu wathibitishwe na BOT kutoa elimu ya fedha yaani ada ya seminar na process nzima. Shukrani.
Karibu Mkuu,
Wanatoa hii programu kwa batches na wanatoa matangazo kabla ya programu.
Kwa batch niliyofanya programu ilikuwa ya wiki mbili na ada ilikuwa Tsh laki 5.
Sijajua kama batch ijayo kutakuwa na mabadiliko.
Fuatilia taarifa zao na kwenye majukwaa ninayoshirikisha maarifa, watakapotangaza batch nyingine nitawajulisha watu kwenye majukwaa hayo.
Karibu.
 
Unajua kwa nini madaktari hawatakiwi kujisifia?
We nakupuuza kwa sababu naona unataka tu attention.
Pata elimu ya usimamizi wa fedha binafsi na ujijenge vizuri kifedha, utaacha kuhangaika na haya mambo yako yasiyokuwa na tija.
Kila la kheri.
 
Hahaha, tit for tat sio! Sasa utapata wateja vinywa ngumu kweli
Mkuu, nipo humu JF tangu 2012, hawa wanacoment hasi kwenye maudhui ya aina hii huwaga siyo wateja, hivyo nachangamsha nao genge tu mada iende.
Wateja huwa wanakuja inbox na tunafanya kazi.
Mwaka 2014 niliandika humu humu kuhusu kuwekeza kwa kuanza na buku, nilipingwa kama hivi lakini miaka 10 imepita, mimi nimewekeza na kunufaika na wengi hawajawekeza.
Njia maana siwaachagi wanaokuja kwenye hizi mada kizembe.
Makala ya kuwekeza kwa kuanza na buku niliyoandika 2014 hii hapa; Hivi Ndivyo Unavyoweza Kutajirika Kwa Kuanza Na Shilingi Elfu Moja
 
Haaha, Wewe sema tu, akaunti yako ina kiasi gani? Tuone kama una credibility ya kufundisha mtu, halafu mi sisemi tu.., ipo kweli hiyo 700 😁

Hata ingekuwa wewe, ungekubali kufundishwa kuhusu pesa na mtu ambae hata maandazi asubuhi yanampiga chenga?
Wewe pia nakupuuza kwa sababu naona unataka tu attention.
Pata elimu ya usimamizi wa fedha binafsi na ujijenge vizuri kifedha, utaacha kuhangaika na haya mambo yako yasiyokuwa na tija.
Kila la kheri.
 
Hongera sana Bwana Makirita. Hii ni habari njema sana. Nimekuwa pia mwanachama mwaminifu wa UTT na faida yake naendelea kuiona. Asante kwa kuendelea kutuelimisha kupitia experience yako pia. Naomba ushauri mmoja.

Nami pia nipo kwenye safari ya kuusaka utajiri na uhuru wa kifedha. Nina uwezo wa kusave 4,200,000 kila mwezi kwenye mfuko wa UTT na nimekuwa nikifanya hivyo. Nataka nifikie uhuru wa kifedha haraka iwezekanavyo ndani ya miaka 7 mpaka 8 ijayo. Unanishauri nijikite katika uwekezaji upi hasa ili niweze kufikia malengo yangu kwa haraka zaidi?

NB: Sina muda wa kusimamia biashara kabisa
Hongera sana mkuu kwa kuwa mwekezaji, hasa kupitia UTT ambayo ni fursa nzuri sana kwa hapa nchini kwetu.
Kuhusu kufikia uhuru wa kifedha ndani ya huo muda na kwa kiasi unachowekeza, inategemea zaidi matumizi yako ya kila mwezi.
Hiyo ni kwa sababu UHURU WA KIFEDHA ni pale uwekezaji wako unapoweza kukuingizia fedha ya kuendesha maisha yako bila ya kulazimika kufanya kazi moja kwa moja.
Huwa nina miongozo mbalimbali ya kukokotoa kiasi cha kuwekeza na muda ili mtu kufikia uhuru wa kifedha, kama utahitaji tutawasiliana tufanyie kazi.
Ila kwa jibu la haraka na ambalo kila mtu anaweza kufanyia kazi ni kuchukua wastani wa matumizi yako ya mwezi na kuzidisha mara 100. Kisha kuwa na uwekezaji wenye hiyo thamani, kwenye UTT au BONDS.
Kwa mfano kama matumizi yako ya mwezi ni TSH 5,000,000/= (milioni 5) unahitaji kuwa na uwekezaji wenye thamani ya Tsh 500,000,000/= (milioni 500).
Ukiweza kuwa na uwekezaji huo kwenye Mfuko wa UMOJA, UKWASI au BOND wa UTT au ukawa na bonds za serikali kwa thamani hiyo, au mchanganyiko wa aina hiyo, utafikia uhuru wa kifedha.
Hivyo anza na matumizi yako ya mwezi kwa kipindi hicho utakachokuwa umestaafu na zidisha mara 100 kisha kokotoa itakuchukua muda gani.
MUHIMU; Hii niliyotoa ni rough calculation, kama unataka ukokotozi sahihi na wa kina zaidi, tuwasiliane kwa wasap 0678 977 007. Karibu sana.
 
Na pesa ikija bila elimu sahihi, unaishia kutenganishwa nazo na wajanja kama DECI, Mr. Kuku, na wengine kama hao.
Kwa hiyo hakikisha unapata elimu ya fedha kwanza, ili ukizipata ziweze kudumu.
Hakuna.pesa.inayodumu pesa.zote.zinatumika kwenye mzunguko wa matumizi hata akiba hutolewa pale unapohitajika so kusema.za kudumu nakataa .
 
Unaweza kuchukua, unauza bond yako kwenye soko la hisa na kuchukua chako.
Ila hapo itategemea na hali ya soko.
Baada ya bond kuuzwa kwenye soko la awali (IPO) huwa zinaingia kwenye soko la upili kwenye soko la hisa. Kwenye soko la hisa watu wanaweza kuuziana kama wanavyouziana bidhaa nyingine.
Asante kwa maelezo.
 
Nimeingia kwenye website yako mkuu.. Kuna mafunzo mazuri sana ya pesa..
Hongera sanaa.. mimi nitakua mdau wako kukufuatilia. Pia niwashauri wanajf wajifunze kupitia kwako.
 
Na pesa ikija bila elimu sahihi, unaishia kutenganishwa nazo na wajanja kama DECI, Mr. Kuku, na wengine kama hao.
Kwa hiyo hakikisha unapata elimu ya fedha kwanza, ili ukizipata ziweze kudumu.
Exactly Fact
 
Unaweza kuchukua, unauza bond yako kwenye soko la hisa na kuchukua chako.
Ila hapo itategemea na hali ya soko.
Baada ya bond kuuzwa kwenye soko la awali (IPO) huwa zinaingia kwenye soko la upili kwenye soko la hisa. Kwenye soko la hisa watu wanaweza kuuziana kama wanavyouziana bidhaa nyingine.
Mkuu Makirita,nifanyeje na mimi niweze kupata cheti kama hiko?
 
😀 😀
Kwa hiyo tusiamini forbes ila tukuamini wewe?
Hizi conspiracy za kimasikini huwa zinashangaza sana.
Maana huwa hata haziendani na logic.
Watu wote wanaokuwa featured kwenye forbes utajiri wao ni wa vyanzo vilivyo wazi.
Sasa unasemaje inakuwa manipulated?
Huwa siamini sana taarifa zao maana kuna kipindi waliiweka Nigeria na Rwanda ktk nchi zenye uchumi mkubwa Africa. Sasa ukiangalia Rwanda Ina asilimali gani au biashara gani za kuiweka ktk list hiyo? Kuna Uzi humu tulishawahi kujadili hilo suala.
Fatilia manipulation za Forbes utagundua hizi habari. Wapi matajiri wengi wanachekechewa hizo list ili wapate favor fulani za kimikopo. Fatilia hata inshu ya Trump was of the same nature
 
Wewe pia nakupuuza kwa sababu naona unataka tu attention.
Pata elimu ya usimamizi wa fedha binafsi na ujijenge vizuri kifedha, utaacha kuhangaika na haya mambo yako yasiyokuwa na tija.
Kila la kheri.
Kunipuuuza ni kutojibu comment yangu. Una kiasi gani kwenye akaunti, 😁
 
Back
Top Bottom