Haji Manara ni nani hapa Tanzania hadi kuwadhalilisha Askari Magereza na wafungwa bila kuchukuliwa hatua?

Haji Manara ni nani hapa Tanzania hadi kuwadhalilisha Askari Magereza na wafungwa bila kuchukuliwa hatua?

Kwa 90% Haji Manara yuko sahihi kabisa. Inaonekana anajua sheria na akaamua kusimama katika sheria.
Askari Magereza hana mamlaka yoyote ya kumkata au kumuamuru raia, mamlaka yake yapo gerezani kwa wafungwa na mahabusu.

Tz tunahitaji wakina Haji Manara wengine kama 100 hivi.
Kumbe na wewe ni kizibo tu, hujui mengi kuhusu mamlaka ya askari magereza
 
Hawa machawa wa viongozi na Lumumba + pale makumbusho kwasababu ya kutumika kwao kukisaidia chama chetu basi nao hujiona wanahati mmiliki ya kufanya lolote lile.

Tuweke mipaka na kuchora mstari kwenye suala zima la discipline kwa jamii bila kujali cheo au dhamana uliyonayo.
Too late
 
Huyu haji manara mdomo wake ni mchafu anajikuta ana mamlaka ya kumtusi na kumdhalilisha yeyote kama kesi ilikuwa na magereza wafungwa wamefuata nini anasahau naye kesho anaweza kuwa mfungwa.

Na hao kituo cha sheria za haki za binadamu hatusikii wakikemea kitu wafungwa wapo kutumikia makosa yao sasa kama haji kakoromewa na magereza ya nini awadhalilishe na wafungwa

Mtu huyu hastahili huruma kwa ule ulemavu wake achukuliwe hatua tu!

Haji Manara ni nani katika nchi hii!
CCM wamemfuga
 
Hilo Sope linajivunia ulemavu wake, ndo maana haliogopi mamlaka.

Mxxxxiiiiieeeew zake.
Huo ni UNYANYAPAA LIVE kwa sababu alichosema au kufanya Manara kinaweza kusemwa au kufanywa hata na mtu asiye na ulemavu kwa sababu issue hapo ni attitude!! Sasa nini kimekufanya uone Manara kafanya hayo kwa sababu ya ulemavu wake na sio attitude yake?!
 
Huko mbona mbali sana hao hao aliowatusi kuna namba humo na bila shaka unazipata green beret..
Mkuu acha kabisa si wale KMGM? hahahahaaa nimecheka kwa uchungu kidogo chukua hii,

Kipindi kile Amboni Tanga kulitokea visa vya ugaidi si unakumbuka? Basi bwana baadhi ya washukiwa walipelekwa pale gereza kuu la Tanga liitwalo Maweni,

Sasa bwana kulikua na vinjia wachunga ng'ombe au watu wa vijiji vya mbele wanapita ila vinaelekea karibu na gereza kisha vinapitiliza vijijini ,

Basi mjomba wangu mtata mtata hakujua kuwa vile vinjia vilipigwa marufuku kupita na doria ilishikwa na wale KMGM wale buubaaaa Anko anamaliza kichaka tu alistukia kofi la uso pwaaaaaah , anakwambia nguvu ya lile kofi alitoa kubwa pale pale, ile kutahamaki anakutana na majamaa marefu meusi tiii wawili tu ndio mahojiano kuanza na vipigo vya chombeza,

Basi tangu hapo Anko anadai wale KMGM sio binadamu wa kawaida ,

Wakimkamata Manara wapige fimbo nyingi sana za mdomo ule
 
Jana wakati wa mchezo Kati ya Yanga na Prisons, Haji Manara alifanya kitendo kisicho cha kingwana na udhalilishaji kwa jeshi la Magereza kwa kuwaita askari ni wafungwa.

Manara ambae alikuwa anahojiwa na waandishi wa habari huku akiwa amepark gari lake njiani na kuziba njia hiyo magari mengine yasipite, alipotakiwa kulitoa gari lake ili gari la Magereza lipite alimtukana askari huyo na kumuita ni mfungwa hivyo askari wote wa magereza ni wafungwa.

Kitendo hiki kilikuwa cha kidhalilishaji haswa kwani wote tunatambua kuwa kuna utofauti mkubwa Kati ya askari magereza na wafungwa, askari ni muajiriwa wa serikali ambae analinda na kurekebisha wafungwa wakati mfungwa ni mtu aliyepatikana na hatia na kuhukumiwa adhabu na mahakama.

Jeshi la Magereza linatakiwa kumchukulia hatua Haji ili iwe fundisho kwa watu wengine, kama jeshi litaruhusu udhalilishaji wa namna hii na wakakaa kimya basi ipo siku tutashuhudia udhalilishaji zaidi ukifanywa kwa askari.

Mbona hatuoni askari wa jeshi la polisi, Jwtz wakidhalilishwa Kwanini iwe kwa magereza.

Huyu mtu anapaswa kukamatwa ikiwezekana apelekwe gerezani akaone utofauti wa askari magereza na mfungwa.

View: https://youtu.be/F93mZI980ZU?si=sShG-Fz-jyypfYKV
 
Acha ujuha, Magereza haina uwezo wa kumchukulia hata raia wa kawaida kwa kitendo kama hicho, hata hivyo Manara ni chawa wa serikali tegemea atajitokeza muda wowote kutubu na kuomba msamaha kwa magereza na serikali.
 
Jana wakati wa mchezo Kati ya Yanga na Prisons, Haji Manara alifanya kitendo kisicho cha kingwana na udhalilishaji kwa jeshi la Magereza kwa kuwaita askari ni wafungwa.

Manara ambae alikuwa anahojiwa na waandishi wa habari huku akiwa amepark gari lake njiani na kuziba njia hiyo magari mengine yasipite, alipotakiwa kulitoa gari lake ili gari la Magereza lipite alimtukana askari huyo na kumuita ni mfungwa hivyo askari wote wa magereza ni wafungwa.

Kitendo hiki kilikuwa cha kidhalilishaji haswa kwani wote tunatambua kuwa kuna utofauti mkubwa Kati ya askari magereza na wafungwa, askari ni muajiriwa wa serikali ambae analinda na kurekebisha wafungwa wakati mfungwa ni mtu aliyepatikana na hatia na kuhukumiwa adhabu na mahakama.

Jeshi la Magereza linatakiwa kumchukulia hatua Haji ili iwe fundisho kwa watu wengine, kama jeshi litaruhusu udhalilishaji wa namna hii na wakakaa kimya basi ipo siku tutashuhudia udhalilishaji zaidi ukifanywa kwa askari.

Mbona hatuoni askari wa jeshi la polisi, Jwtz wakidhalilishwa Kwanini iwe kwa magereza.

Huyu mtu anapaswa kukamatwa ikiwezekana apelekwe gerezani akaone utofauti wa askari magereza na mfungwa.

View: https://youtu.be/F93mZI980ZU?si=sShG-Fz-jyypfYKV

nadhani ni lugha ya kimichezo hiyo haina ukakasi 🐒
 
Back
Top Bottom