Hakuna kitu kinatokea kwa bahati mbaya katika siasa ya Bongo

Hakuna kitu kinatokea kwa bahati mbaya katika siasa ya Bongo

Adui wa Demokrasia ya nchi hii ni Mbowe .

Mbowe hakuikuza Chadema Bali Mbowe alisafiria nyota za makada wenzake waliotoka CCM.
Mbowe angemkosa Slaa ni kama mkulima mwenye mpini tu usio na jembe.
Mbowe angemkosa Zito miaka ya 2010-2015 vyuo vikuu na waislam kuiamini Chadema ni kama mkulima mwenye Jembe bila mpini wake.
Mbowe angemkosa Lowasa 2015 ni kama mkulima mwenye Jembe bila kuwa na shamba la kulima.

Sasa Mbowe Mwaka huu anataka kusafiria nyota ya Lisu na Nyarandu yupo kama mkulima mwenye Shamba bila kuwa na Jembe la kulimia .
Baada ya Uchaguzi huu Mlevi huyo unayetaka kuwaaminisha wahuni kuwa ndiye aliyeijenga Chadema atabaki kama mkulima asiye na shamba wala Jembe.

Siasa sio mchezo kama kama mpira. Siasa zinahitaji ushawishi na hoja zenye misimamo imara kiroho na kijamii.
Mbowe hana mvuto wa kiroho wala kijamii .
Mbowe ni mjasiriamali mwenye haiba na hulka ya tamaa ya fedha ,wizi, ubinafsi, na mtu asiye na huruma anaposikia harufu ya madaka na fedha.
Ni kosa kubwa sana kumwamini tajiri Mbowe apiganie haki za maskini 80% wa nchi hii. Ni kujilisha upepo kumtegemea Tajiri atangulie mbele ya vitani wakati anawaza Mali zake na starehe na mademu wake.
Kujitoa muhanga kunaendana na kujaa imani kiroho ili mtu aweze kuipigania jamii bila kujali maslahi au kupoteza.
Mbowe ni muoga kuliko kunguru. Ndio maana mpaka kijijini kwake Chadema imefyata mkia kwa kumwogopa kijana Machachari na Kada wa CCM DC .Sabaya.

Kumlinganisha Zito Msomi na mwanasiasa aliyeanzisha Chama wakati mgumu kabisa huku akitukana na CCM na Chadema ni sawa na kumlinganisha Faru (Zito) na Ngiri (Mlevi Mbowe).
Mbowe amerithishwa chama kwa sababu ya ukabila tu na ukaribu wake na Mtei lakini Mbowe hana uwezo wa kuanzisha chama cha siasa duniani na hata kuzimu achilia mbali Mbinguni Patakatifu pasipohitaji walevi na wazinzi na wezi.

Siasa ni kazi na vipaji vya baadhi ya watu kama ilivyopira na michezo mingine na hata biashara na kazi nyingine.
Wanasiasa ni watu kwenye jamii wasiopenda kuongozwa wala kupangiwa jambo na wengine bila wao kushiriki. Hata mkikaa kwenye kikao cha harusi kama kuna mwanasiasa atakua msemaji sana na kutoka kuona mawazo yake ndiyo yanasikilozwa. Hata kwenye msiba wanasiasa watakuwa mstari wa mbele kuonekana.
Kwenye familia pia wanasiasa watajitokeza mbele kutaka wasikilizwe wao.
Kwa hiyo hakuna namna ya kuwazuie eti wasitoke CCM na kwenda Chadema au kutoka chadema kurudi CCM.

Dunia ndivyo ilivyo. Hakuna namana ya kuwatenganisha wanasiasa wa upande mmoja tuu wasiunge mkono upande mwingine kwenye baadhi ya mambo.
Ni vijana wachache walevi tu ndani ya Chadema wanaowaita watu wa vyama vingine wanaojiunga na chama hicho au wanaohama kuunga mkono baadhi ya utendaji wa wapinzani wao kuwa ni wasaliti. Ingekua hivyo Marekani chama kimoja kingetawala milele. Lakini kule watu wanamkataa hata kama ni MTU wa Chama chake lakini anafanya mambo ya hovyo anapingwa na ananyimwa kura na wanachama wa chama chake wanapunguza kura zake zinahamia kwa mpinzani wake.

Tanzania katika Uchanga wake imefanikiwa kuwa na siasa nzuri za ushindani wa hoja ndani ya CCM na nje ya CCM. Nchi hii ilikua ya Chama kimoja chenye upinzani mkubwa sana wa ndani hivyo usione ajabu watu kutoka nje ya CCM na kumpinga mtu waliyekua wanaimba pamoja CCM yajenga nchi.

Kumbuka Bado Afrika tunatambuana kwa makabila na dini na asili zetu.
Hata kwenye taarifa zetu kwenye fomu mbali mbali zinaeneo la kujaza Kabila lako,dini yako n.k.
Dini ,kabila na ukanda unaathiri sana siasa za Tanzania . Jambo ambalo Chama la Chama la kupindua wanafanikiwa kudumu milele madarakani kwa kutumia hayo mambo matatu.
Akiwa wa dini Fulani basi dini ile wote wataapena ishara ya kumuunga mkono hata kama atakosea watajitokeza kumuunga mkono kwa nguvu zote.
Wakiona dini haimuungi mkono huyo basi wanahamia kwenye ukanda au kabila . Yote hayo ni tatizo la woga wa mwanasiasa waliozoea kukaa madarakani na wakajiwekea marupurupu makubwa na Kuweka katiba inayowapa madaraka makubwa.

Hapo ishu sio kikundi cha watu nyuma ya pazia kupanga nani awe wapi . Huo ni uongo mkubwa. Siasa za Kiafrika zinaathiriwa na Umaskini na Katiba zinazotoa madaraka makubwa kwa watawala.
Mtawala akishika madaraka anakua ni zaidi ya mungu juu ya wanadamu wenzake mana anashila mpaka nafasi ya kupanga nani ashibe na nani aishi kama malaika na nani aishi kama shetani.
Hii hali inawafanya wanasiasa wakose misimamo zaidi ya kubaki wakiwa wanajipendekeza ili waishi kama malaika muda wote.

Hivi Mbowe na Tundu Lisu nani ni mpinzani toka Rohoni bila kujali Umaarufu, madaraka, Dhiki, kupoteza uhai, kupoteza fedha na kudai Mali za chama kama fidia ya muda na fedha zake n.k????
Bila shaka Lisu ndiye mpinzani wa kweli .
Mbowe ni Magumashi ndio maana alibadili katiba ya Chama ili afie kwenye Uenyekiti wa Chadema.
Mkitaka Mbowe arudi CCM kesho asubuhi mtoeni kwenye Uenyekiti halafu aone Mali zake zinafilisiwa na hana uwezo wa kukwapua Ruzuku kufidia mali anazopoteza .
Atakimbilia ikulu asubuhi kabisa kupiga magoti.

Nisipomtaja Mbowe kwa mabaya yake ni sawa na Mchungaji asipomtaja Shetani kwa kumlaani kuwa ashindwe.

Mlevi na Mzinzi Mbowe Shindwa na Ulegee! !!
Nchi yetu ipone kwa kuwa na siasa safi na za kidemokrasia kuanzia ndani ya vyama.

Mbowe is a total man one and half.
Mbowe hanunuliki ni kamanda si kwa magwanda bali rohoni.A freedom fighter kama jina lake Freeman.
Husweka Lupango mara kwa mara lakini akitoka ni yule yule Mbowe wa jana na leo.
Raisi Magufuli katumia mkono wa chuma kumpelekesha kama ataunga tela wapi.

Vibaraka na vikaragosi wametumiwa kumkatisha tamaa lakini wakasahau ana roho ngumu kama Senator John McCain alipotekwa na kuteswa na KGB,huko Vietnam,wakimwahidi kumuachia huru akikili upumbavu waliokuwa wamemwandikia asome,akakataa kata kata.
 
Hahahaa... Alipigiwa saluti na wala siyo mabomu!
Bosi wa TLP ambaye amewahi kuwa "Naibu Waziri Mkuu". Jamaa ambaye enzi hizo mimi napata akili aliwahi hamasisha tuandamane na mwishoni tukapigwa sisi na kwa macho yangu nikamuona anapanda gari ya RPC kwa kupigiwa saluti.
 
Maalimu kua kitengo hilo sijui lkn akiumwa ni lazima agharamiwe na SMZ sababu yeye alikua ni makamu wa raisi huko Zenji(kipindi cha Shein) na matibabu ni sehemu ya stahiki yake kama makamu wa rais mstaafu.


Maalimu akiugua anatibiwa kama wanavyotibiwa viongozi wengine maalim alishawahi kuwa makamu wa rais incase hujui
 
Mbowe is a total man one and half.
Mbowe hanunuliki ni kamanda si kwa magwanda bali rohoni.A freedom fighter kama jina lake Freeman.
Husweka Lupango mara kwa mara lakini akitoka ni yule yule Mbowe wa jana na leo.
Raisi Magufuli katumia mkono wa chuma kumpelekesha kama ataunga tela wapi.

Vibaraka na vikaragosi wametumiwa kumkatisha tamaa lakini wakasahau ana roho ngumu kama Senator John McCain alipotekwa na kuteswa na KGB,huko Vietnam,wakimwahidi kumuachia huru akikili upumbavu waliokuwa wamemwandikia asome,akakataa kata kata.
Mtu imara hanganganii Madaraka.
Angekua tishio wangeanza naye kabla ya Lisu.

Mbowe ingia hata kwenye Tweets zake au Kurasa zake za FB au hata hapa JF kama kuna jambo lolote la maana analoandika ukimlinganisha na Zito, au Lisu.
Hakuna kitu anachoandika chenya hamasa.

Mbowe hawezi kununulika kwa sababu anakula mil.300 kila Mwezi za ruzuku na michango mingine bila kufungwa au hata kunyongwa kwa kuhujumu pesa za walipa kodi.
Ukitaka ujue kuwa Mbowe anipigania chadema basi hata Lipumba anaipigania CUF mana naye hataki kung'atuka.Au Mrema na Cheyo . Hao wote wanapigiwa kura za kuendelea kuongoza vyama vyao.
Hakuna Mwenyekiti wa Chama chenye ruzuku anayeweza kukiuza wakati yeye ni Mbunge pia. Auze ili iweje wakati yeye ndiye kidume ndani ya chama.

Mnakosea sana kuwadanganya watu kuwa Chadema ni Mbowe ,bila mbowe Hakuna chadema. Mnakiua chama mana watu wasiompenda Mbowe wanakichukia mpaka Chama.
Ma ukweli ni kwamba Mbowe hakubaliki kabisa huko mitaani mana wanamuona kama MTU anayengangania Madaraka.
 
Maalimu akiugua anatibiwa kama wanavyotibiwa viongozi wengine maalim alishawahi kuwa makamu wa rais incase hujui

Miss Madeko
Nilikuwa sijui,nashukuru kwa kunifahamisha. Asante sana.
 
Kuna msemo ulivuma sana mwaka 2015 kwamba "CCM ina kitabu kikubwa cha MBINU ZA KUSHINDA UCHAGUZI na mpaka mwaka 2015 walikua ndo kwanza wako kurasa ya 3" kwahiyo bado kurasa kibao yaan Wapinzani wa nchi hii wajipange[emoji22][emoji22]
Mbinu za CCM ni tatu tu:

Polisi+TISS

TUME YA UCHAGUZI

MAHAKAMA TU.

Hivi vyombo vikiwa huru hata waweke mamluki laki moja wanaondoka madarakani.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Wanabodi,

Kwanza hakuna kitu kinatokea kwenye siasa kwa bahati mbaya. Kila kitu hupanga na wenye akili "Elites" ambao wengi wao hawapo kabisa kwenye siasa ila ndio wanaamua siasa.

Ukiona siasa ya Mkapa,Kikwete na leo JPM ujue wao wenye siasa yao wameamua kuifinyanga iwe hivyo unavyoiona leo.
Siasa ya ni kama mchezo wa kuigiza "Tamthilia" inayoigizwa jukwaani. Kuna wanaoangalia na kuisgabikia tamthilia ambao ndio sisi wananchi tunaokaa mbele ya jukwaa na mchezo unatuhusu sisi,na waigizaji "stunts" ambao ndio wanasiasa wenyewe wanaoigiza na nyuma ya jukwaa kuna pazia ambako huko ndiko mambo na mipango yote ya tamthilia inakopangwa. Huko nyuma ya pazia ndiko wanapambwa na kufanya mazoezi ya kuigiza na huko ndiko hao "Elites" wapo na ndio wanaamua mchezo uweje huku kila Muigizaji akipewa kipande aigize vipi na kwa namna gani na ili iweje,huku lengo kuu ni kuendelea kubaki milele katika dora huku waigizaji lengo lao ni kuishi kupitia mchezo huo unaolipa vizuri sana.

Na huko nyuma ya pazia ndio wapo "craftsmen" ambao ndio waandishi na waongozaji "masterminds" wa mpango mzima wa igizo.

Tuangazie ishu moja tuu ya vyama vingi msingi wake ambao mpaka leo tunateseka nao sababu bado "Elites" wameushikilia mpango wao huku "stunts" wengi wamezeeka japo wanaendelea kucheza tamthilia huku kazi kubwa ikiwa ni kuwaandaa wachezaji wengine wachanga.

Ndio maana leo utaona mtu kama Cheyo anaomba apewe viti vya ubunge free na ukimuona unaona wazi amechoka kimwili na fikra ila ni mchezaji wa siku nyingi sana na ana ukwasi anajiita "bwana mapesa".

Bosi wa TLP ambaye amewahi kuwa "Naibu Waziri Mkuu". Jamaa ambaye enzi hizo mimi napata akili aliwahi hamasisha tuandamane na mwishoni tukapigwa sisi na kwa macho yangu nikamuona anapanda gari ya RPC kwa kupigiwa saluti. Huyu jamaa yupo kwenye "payroll" nyingi za nchi hii na ni tajiri sema afya tuu mzee wetu huyu.

Vijana wengi "smart" wa walitolewa katika nafasi zao nyeti na kupewa mpunga na kuanzishwa vyama vyao huku wakipewa ruzuku na hao hao wanaowapinga. Yaani unampinga na kumtukana mtu,huyo huyo mtu ndiye anasaini malipo yenu kulipa chama chenu ruzuku kupitia msajiri wa hazina. Huku ujira wa hao "stunts" ukiwa ni ruzuku. Hawa hawana nia ya kushika dora,wao wananufaika na ruzuku na tips za hapa na pale kutoka kwa wale wanaowapinga.

Kwanza ieleweke mchakato wa vyama vingi haukuwa msukumo wetu wa ndani, ulikuwa ni msukumo wa nje maana sisi tuliukataa. Ila wakati huo ili kuendana na masharti ya mabeberu kutoka Bretton Woods ikiwemo WB na IMF chini ya mfumo wa SAP's "Elites" au "think tankers" walifikiri na kuja na mkakati wa siku nyingi wa kuleta vyama na namna ya kuvidhibiti.

Waliandaliwa watu "smart" kutoka vitengo wakapewa "mchanga" kwa lengo la kuanzisha vyama hiyo 1992.

Mtei na Makani ni miongoni mwa watu hao. Mbowe amechukua chama hicho 2000 hakuwahi jua waanzishaji wa chama hicho wana ajenda zao na wana mkono mrefu. Yeye akaja serious akakikuza chama hicho,"Elites" wakaona kijana anavuka grafu wakamchezea shere,wakawavuta vijana wake aliowapika akiwemo Boss wa ACT,alipolambishwa chambi ishu ya Buzwagi akawa hana namna akawa mtumwa wa "Elites". Elites wakawa wakaanza mtumia na wakampa mpunga aanzishe chama chama ndani ya chama. Huyo bosi ACT ana ukwasi wa kuweza kuendesha chama kichanga kusimamamisha mgombea uraisi na kumzungusha nchi kubwa kila kijiji. Hela hiyo aliotoa wapi?.

Mwaka 2015 "Elites" wakapika mpango washindane wao kwa wao. Wakafanikiwa kuwaingiza kingi CDM wakamletea EL. 2015 hapakuwa na upinzani,Chama dora kilikuwa peke yake,walishindana wale wale. 2015 mchawi "CDM" alipewa mwana amlee na akakubali. Mtoto kakua kanyea kambi na karudi kwa baba yake.

EL alikuw na malengo mawili kwanza ajisafishe na pili alitimiza lengo la chama dora kushindana wenyewe.

2020 kuendelea...
Huyo dogo wa visiwani alianza kuandaliwa muda ni mpango wa muda mrefu.
Ishu ya BM kufukuzwa na yenyewe ni trap ni mpango kama ulivyokuwa wa EL mwaka 2015.
Mtoto wa kigoma Mwandiga na yeye anadeni lile lile la kuwamaliza hawa CDM huku yeye akiwa hana mpango wa kushika dora ila kupiga ruzuku. Kazi hiyo bado hajatimiza na ndio maana Maalim amenyakwa visiwani na huku anampanga BM agombee bara.
Lengo lao ni kuwapoka CDM na CUF kitumbua "ruzuku" na kuimaliza CDM.

NATABIRI HAYA BAADA YA OKTOBA
BM ataenda ACT atapunguza kura za CDM. ACT watapewa majimbo na watapata asilimia nyingi za kura kupata ruzuku kutoka visiwani.
BM akimaliza uchaguzi chama chake watamsamehe na watamrudushia uanachama.

ZZK hatagombea uraisi mwaka huu,mpango wake ni 2025 ambapo atakuwa ametimiza lengo la kuiondoa CDM katika "key opposition" ya nchi.

Maalim mwaka huu atapata kura kiduchu sana maana CUF nao wataweka mtu kugawana kura na Huseni atapeta.

Bado tunasafari ndefu sana ya "upinzani" bongo. Aliyebuni mpango wa mwaka 1992 wa namna ya kuendesha siasa ya vyama vingi akili yake itaishi kwa siku nyingi na kwa vizazi vingi. Mpaka pale ambapo tutakuja kufahamu tunataka nini na tukafanya kazi kubwa ya kupata tunachokitaka ndipo tutapata jibu.

Wasaalam.
"Upepo ukipuliza sana uchi wa kuku huonekana"
"Ukiwa na subra utaona mwisho wa kila kitu"
Kwa hiyo mbowe na lissu wamekuwa serious kiasi kwamba wanawaudhi Elite,

Mipango ya Elites inavurugwa na Akina mbowe, au wakaidi maelekezo ya Elites hivyo elites wameamua kuwaadhibu,

Mbowe anatembelea magongo
Na Lisu anachechemea
 
Mtu imara hanganganii Madaraka.
Angekua tishio wangeanza naye kabla ya Lisu.

Mbowe ingia hata kwenye Tweets zake au Kurasa zake za FB au hata hapa JF kama kuna jambo lolote la maana analoandika ukimlinganisha na Zito, au Lisu.
Hakuna kitu anachoandika chenya hamasa.

Mbowe hawezi kununulika kwa sababu anakula mil.300 kila Mwezi za ruzuku na michango mingine bila kufungwa au hata kunyongwa kwa kuhujumu pesa za walipa kodi.
Ukitaka ujue kuwa Mbowe anipigania chadema basi hata Lipumba anaipigania CUF mana naye hataki kung'atuka.Au Mrema na Cheyo . Hao wote wanapigiwa kura za kuendelea kuongoza vyama vyao.
Hakuna Mwenyekiti wa Chama chenye ruzuku anayeweza kukiuza wakati yeye ni Mbunge pia. Auze ili iweje wakati yeye ndiye kidume ndani ya chama.

Mnakosea sana kuwadanganya watu kuwa Chadema ni Mbowe ,bila mbowe Hakuna chadema. Mnakiua chama mana watu wasiompenda Mbowe wanakichukia mpaka Chama.
Ma ukweli ni kwamba Mbowe hakubaliki kabisa huko mitaani mana wanamuona kama MTU anayengangania Madaraka.
Wewe kama huna chuki binafsi labda una lako jambo.
CCM imetumia mabavu na pesa yetu kununua wabunge na viongozi wa CHADEMA tena kwa vitisho,bila aibu.
Hata siasa ya maelewano imewashinda,yaani mmefirizika kiasi mmegeuka mabubu wa hoja?
Hivi Mwl.Nyerere ndio shule ya siasa aliowafundisha ?

Juzi Mjumbe wa Halmashauri kuu kauliza Mwenyekiti wenu kwanini wazamiaji wanapewa vyeo kuliko CCM damu damu?Akajibiwa tena bila wasiwasi kwamba CCM damu damu hamna kitu ndio maanake anasajiri kutoka nje.Kwa majibu hayo bado unaona kuna kitu au mmegeuzwa fidodido?

Mbowe ana jenga chama hadi atakapomaliza kazi ya kuondoa mbegu mbovu na pandikizi.
Wewe unalia na Mbowe Mbowe kuwa Mwenyekiti wa Chadema. Kutoka 1954 Nyrere ni mwenyekiti,hadi 1987 miaka 34 ni mwenyekiti,na hata baada ya kustaafu alikuwa na nguvu ndani ya chama kuliko mwenyekiti hadi kifo chake.
Au Historia ya Chama chenu imekupita kando?
 
Wewe kama huna chuki binafsi labda una lako jambo.
CCM imetumia mabavu na pesa yetu kununua wabunge na viongozi wa CHADEMA tena kwa vitisho,bila aibu.
Hata siasa ya maelewano imewashinda,yaani mmefirizika kiasi mmegeuka mabubu wa hoja?
Hivi Mwl.Nyerere ndio shule ya siasa aliowafundisha ?

Juzi Mjumbe wa Halmashauri kuu kauliza Mwenyekiti wenu kwanini wazamiaji wanapewa vyeo kuliko CCM damu damu?Akajibiwa tena bila wasiwasi kwamba CCM damu damu hamna kitu ndio maanake anasajiri kutoka nje.Kwa majibu hayo bado unaona kuna kitu au mmegeuzwa fidodido?

Mbowe ana jenga chama hadi atakapomaliza kazi ya kuondoa mbegu mbovu na pandikizi.
Wewe unalia na Mbowe Mbowe kuwa Mwenyekiti wa Chadema. HIvi kutoka 1954 Nyrere ni mwenyekiti,hadi 1987 miaka 34 ni mwenyekiti,na hata baada ya kustaafu alikuwa na nguvu ndani ya chama kuliko mwenyekiti hadi kifo chake.
Au Historia ya Chama chenu imekupita kando?
Nyerere hakutawala wakati wa Mfumo wa vyama Vingi .
Pia Nyerere aliingia kwenye uenyekiti akiwa Mdogo sana.
Miaka 32 alikua mwenyekiti wa TANU. Lakini pia alikua na Mbinu kama alivuo Zito.
Alihamasisha vijana wakawa Jeuri kwa kua alikua anakubalika.

Mbowe nakuambia hata kijijini kwake hana ushawishi . Yani jimboni kweke anashindwa kufanya hata mikutano kama Mbunge. Amekaa Gerezani karibu miezi sita Hakuna hata kifaranga kilichoandamana kupinga uonevu. Na wakati alipokua Gerezani Chama kilitulia na hakuna hata MTU mmoja aliyakihama Chama.
Watu wanakihama Chama sio kwa sababu ya kununuliwa lakini watu wenye upeo mkubwa hawampendi Mbowe kabisa.
Wanaompenda Mbowe ni ama watu wachache sana wa kabila lake au wale wenye maslahi na Chama na wanaoona kuwa Mbowe ndiye Chama na akiondoka wataondoka naye mana ni wazi kuwa akitokea Mwenyekiti Mpya atakisafisha chama na kuwaacha pembeni wahuni na walevi wote wanaokitumia chama kwa manufaa yao.

Kweli unaona kuwa Mbowe yupo sirious na Chama wakati ameshindwa kuwahamasisha wanachama mamilioni wanopenda Mageuzi kujenga Ofisi za Kanda na za MAKAO MAKUU.
HIVI HUONI KUWA CHAKA KIKIWA NA Majengo yake ni rasilimali kubwa sana za Chama na ni sehemu ya kuwaunganisha watu pia. Hamasa ya ujenzi wa Chama ingewaleta watu pamoja na kukifanya Chama kuwa na Pamanent Address kila Jimbo na baadae Kila Kata na hata vijijini kote tena ni nafasi ya kupima uimara na Utayari wa wanachama katika kukijenga chama chao.

Chadema kinakosa mipango ya kukabiliana na CCM ya Magufuli kwa sababu ya akili ndogo ya Mbowe. Hivi kweli unaweza kusema kuwa Unaeneza dini kama ya Uislam au Ukristo halafu hujengi Msikiti wa kuswalia Kanisa !! Utakua Kichaa kama utakubaliana na Imamu au Mchungaji au Padri atakayewaambia waumini kuwa hakuna haja ya kujenga nyumba ya ibada kwa sababu waumini wanahitaji neno la Mungu tuu!!!

Mbowe hataki Kujenga na kuwekeza rasilimali za Chama kwa sababu ya roho Mbaya na kuona kuwa watakaonufaika ni wengine watakaoshika Chama. Miaka mitano bila harakati za Kisiasa fedha zimetumika kwenye mambo ya Hovyo badala ya kujenga miundo Mbinu ya Chama. Mbowe alikua haguswi na mfumo kwa sababu ni mmoja wapo wa watu waliotumiwa na kuhujumu watu ndani ya CCM kwa manufaa ya CCM. Mbowe kwa sasa anabanwa sio kwa sababu eti mpinzani wa kweli Bali ni kwa sababu Magufuli hataki mitandao ndani ya CCM ndio maana Mbowe anakosa kazi. Kazi ilikua kutumika kuwachafua watu. Kama unabisha angalia muda wote Mbowe anamwandama Magufuli tuu wakati walikua wanamsifia wakati akiwa Waziri na kumuona ndiye waziri mchapa Kazi.
Vipi Leo aonekane Mbaya wakati anafanya Yale Yale waliyokuwa wanayapigania.?jibu ni kwamba walikua wanatumika kuwachafua watu ndio maana walikua hawaguswi. Wakati Ule Mbowe alikua hakamati wala kukaa Gerezani. Slaa ndio alivunjwa mpaka mkono.
Mbowe anatamani awe na umaarufu wa Lisu lakini anaogopa risasi.Mwishowe imebidi ajiangushe kwenye ngazi baada ya kulewa Chakari. Dili lake la kujitangaza kuwa amevamiwa likabumburuka. Hapo eti ndiyo mikakati ya Mbowe ya kujijenga kisiasa!! Khatari ksana!
 
Wanabodi,

Kwanza hakuna kitu kinatokea kwenye siasa kwa bahati mbaya. Kila kitu hupanga na wenye akili "Elites" ambao wengi wao hawapo kabisa kwenye siasa ila ndio wanaamua siasa.

Ukiona siasa ya Mkapa,Kikwete na leo JPM ujue wao wenye siasa yao wameamua kuifinyanga iwe hivyo unavyoiona leo.
Siasa ya ni kama mchezo wa kuigiza "Tamthilia" inayoigizwa jukwaani. Kuna wanaoangalia na kuisgabikia tamthilia ambao ndio sisi wananchi tunaokaa mbele ya jukwaa na mchezo unatuhusu sisi,na waigizaji "stunts" ambao ndio wanasiasa wenyewe wanaoigiza na nyuma ya jukwaa kuna pazia ambako huko ndiko mambo na mipango yote ya tamthilia inakopangwa. Huko nyuma ya pazia ndiko wanapambwa na kufanya mazoezi ya kuigiza na huko ndiko hao "Elites" wapo na ndio wanaamua mchezo uweje huku kila Muigizaji akipewa kipande aigize vipi na kwa namna gani na ili iweje,huku lengo kuu ni kuendelea kubaki milele katika dora huku waigizaji lengo lao ni kuishi kupitia mchezo huo unaolipa vizuri sana.

Na huko nyuma ya pazia ndio wapo "craftsmen" ambao ndio waandishi na waongozaji "masterminds" wa mpango mzima wa igizo.

Tuangazie ishu moja tuu ya vyama vingi msingi wake ambao mpaka leo tunateseka nao sababu bado "Elites" wameushikilia mpango wao huku "stunts" wengi wamezeeka japo wanaendelea kucheza tamthilia huku kazi kubwa ikiwa ni kuwaandaa wachezaji wengine wachanga.

Ndio maana leo utaona mtu kama Cheyo anaomba apewe viti vya ubunge free na ukimuona unaona wazi amechoka kimwili na fikra ila ni mchezaji wa siku nyingi sana na ana ukwasi anajiita "bwana mapesa".

Bosi wa TLP ambaye amewahi kuwa "Naibu Waziri Mkuu". Jamaa ambaye enzi hizo mimi napata akili aliwahi hamasisha tuandamane na mwishoni tukapigwa sisi na kwa macho yangu nikamuona anapanda gari ya RPC kwa kupigiwa saluti. Huyu jamaa yupo kwenye "payroll" nyingi za nchi hii na ni tajiri sema afya tuu mzee wetu huyu.

Vijana wengi "smart" wa walitolewa katika nafasi zao nyeti na kupewa mpunga na kuanzishwa vyama vyao huku wakipewa ruzuku na hao hao wanaowapinga. Yaani unampinga na kumtukana mtu,huyo huyo mtu ndiye anasaini malipo yenu kulipa chama chenu ruzuku kupitia msajiri wa hazina. Huku ujira wa hao "stunts" ukiwa ni ruzuku. Hawa hawana nia ya kushika dora,wao wananufaika na ruzuku na tips za hapa na pale kutoka kwa wale wanaowapinga.

Kwanza ieleweke mchakato wa vyama vingi haukuwa msukumo wetu wa ndani, ulikuwa ni msukumo wa nje maana sisi tuliukataa. Ila wakati huo ili kuendana na masharti ya mabeberu kutoka Bretton Woods ikiwemo WB na IMF chini ya mfumo wa SAP's "Elites" au "think tankers" walifikiri na kuja na mkakati wa siku nyingi wa kuleta vyama na namna ya kuvidhibiti.

Waliandaliwa watu "smart" kutoka vitengo wakapewa "mchanga" kwa lengo la kuanzisha vyama hiyo 1992.

Mtei na Makani ni miongoni mwa watu hao. Mbowe amechukua chama hicho 2000 hakuwahi jua waanzishaji wa chama hicho wana ajenda zao na wana mkono mrefu. Yeye akaja serious akakikuza chama hicho,"Elites" wakaona kijana anavuka grafu wakamchezea shere,wakawavuta vijana wake aliowapika akiwemo Boss wa ACT,alipolambishwa chambi ishu ya Buzwagi akawa hana namna akawa mtumwa wa "Elites". Elites wakawa wakaanza mtumia na wakampa mpunga aanzishe chama chama ndani ya chama. Huyo bosi ACT ana ukwasi wa kuweza kuendesha chama kichanga kusimamamisha mgombea uraisi na kumzungusha nchi kubwa kila kijiji. Hela hiyo aliotoa wapi?.

Mwaka 2015 "Elites" wakapika mpango washindane wao kwa wao. Wakafanikiwa kuwaingiza kingi CDM wakamletea EL. 2015 hapakuwa na upinzani,Chama dora kilikuwa peke yake,walishindana wale wale. 2015 mchawi "CDM" alipewa mwana amlee na akakubali. Mtoto kakua kanyea kambi na karudi kwa baba yake.

EL alikuw na malengo mawili kwanza ajisafishe na pili alitimiza lengo la chama dora kushindana wenyewe.

2020 kuendelea...
Huyo dogo wa visiwani alianza kuandaliwa muda ni mpango wa muda mrefu.
Ishu ya BM kufukuzwa na yenyewe ni trap ni mpango kama ulivyokuwa wa EL mwaka 2015.
Mtoto wa kigoma Mwandiga na yeye anadeni lile lile la kuwamaliza hawa CDM huku yeye akiwa hana mpango wa kushika dora ila kupiga ruzuku. Kazi hiyo bado hajatimiza na ndio maana Maalim amenyakwa visiwani na huku anampanga BM agombee bara.
Lengo lao ni kuwapoka CDM na CUF kitumbua "ruzuku" na kuimaliza CDM.

NATABIRI HAYA BAADA YA OKTOBA
BM ataenda ACT atapunguza kura za CDM. ACT watapewa majimbo na watapata asilimia nyingi za kura kupata ruzuku kutoka visiwani.
BM akimaliza uchaguzi chama chake watamsamehe na watamrudushia uanachama.

ZZK hatagombea uraisi mwaka huu,mpango wake ni 2025 ambapo atakuwa ametimiza lengo la kuiondoa CDM katika "key opposition" ya nchi.

Maalim mwaka huu atapata kura kiduchu sana maana CUF nao wataweka mtu kugawana kura na Huseni atapeta.

Bado tunasafari ndefu sana ya "upinzani" bongo. Aliyebuni mpango wa mwaka 1992 wa namna ya kuendesha siasa ya vyama vingi akili yake itaishi kwa siku nyingi na kwa vizazi vingi. Mpaka pale ambapo tutakuja kufahamu tunataka nini na tukafanya kazi kubwa ya kupata tunachokitaka ndipo tutapata jibu.

Wasaalam.
"Upepo ukipuliza sana uchi wa kuku huonekana"
"Ukiwa na subra utaona mwisho wa kila kitu"
Gud analisis
 
Ngumu sana kuwa na siasa safi na ya ushindani bila ya wananchi na wanasiasa kuacha tabia ya kutumikia tumbo. Vijana wengi wenye uwezo wa fikra mbadala hawawezi kusimamia fikra zao kwasababu ya tumbo. Tume ya uchaguzi haiwezi kusimamia haki kwasababu ya kutumikia matumbo yao. Polisi halikadhalika.utaona na wabunge nao bungeni wanaweka maslahi binafsi mbele zaidi ya fikra angavu.
Swala la kutumikia tumbo halikwepek.
 
Drifter,
Mbowe alikuwa na ajenda seriously lakini alikosa umakini. "Elites outsmarted the guy back in 2015" na hiyi ndio sifa kubwa ya "Elites". Wama "ku-outsmart".
ZZK alipoingia kingi ya kuwa family friend wa JK kupitia mama yake Shida Salum (R.I.P) ndipo "spy chief" wa enzi hizo alipoanza mtumia na ndipo ACT wazalendo ilianza kupikwa.
Mbowe alinusa hii kitu na mkakati ulikuwa mkubwa sana wa kukimaliza CDM.
Pia Mbowe na ile ya "kutokuwa na njaa tumboni" ili msaidia sana.
Njaa ikihamia tumboni nao ni mtego.
Wasalaam
J.Zoka yuko wapi siku hizi?[/QUOTE]Labda alipewa ubaloz
 
Umemjua Maalim lini?
Maalim sasa yupo kwenye 70's wewe umeanza mjua enzi zipi?
Tukianza leo kuandika kitabu cha Maalim tukianzia alipikuwa Mwanafunzi wa PSPA UDSM tutajaza page nyingi sana za kitabu.
Huwezi Muelezea Maalim kwa aya mbili tatu. Maalim ni mkakati na ni historia.
Wasalaam
Maalim tangu enzi za jumbe kwenye ubora wake
 
Nyerere hakutawala wakati wa Mfumo wa vyama Vingi .
Pia Nyerere aliingia kwenye uenyekiti akiwa Mdogo sana.
Miaka 32 alikua mwenyekiti wa TANU. Lakini pia alikua na Mbinu kama alivuo Zito.
Alihamasisha vijana wakawa Jeuri kwa kua alikua anakubalika.

Mbowe nakuambia hata kijijini kwake hana ushawishi . Yani jimboni kweke anashindwa kufanya hata mikutano kama Mbunge. Amekaa Gerezani karibu miezi sita Hakuna hata kifaranga kilichoandamana kupinga uonevu. Na wakati alipokua Gerezani Chama kilitulia na hakuna hata MTU mmoja aliyakihama Chama.
Watu wanakihama Chama sio kwa sababu ya kununuliwa lakini watu wenye upeo mkubwa hawampendi Mbowe kabisa.
Wanaompenda Mbowe ni ama watu wachache sana wa kabila lake au wale wenye maslahi na Chama na wanaoona kuwa Mbowe ndiye Chama na akiondoka wataondoka naye mana ni wazi kuwa akitokea Mwenyekiti Mpya atakisafisha chama na kuwaacha pembeni wahuni na walevi wote wanaokitumia chama kwa manufaa yao.

Kweli unaona kuwa Mbowe yupo sirious na Chama wakati ameshindwa kuwahamasisha wanachama mamilioni wanopenda Mageuzi kujenga Ofisi za Kanda na za MAKAO MAKUU.
HIVI HUONI KUWA CHAKA KIKIWA NA Majengo yake ni rasilimali kubwa sana za Chama na ni sehemu ya kuwaunganisha watu pia. Hamasa ya ujenzi wa Chama ingewaleta watu pamoja na kukifanya Chama kuwa na Pamanent Address kila Jimbo na baadae Kila Kata na hata vijijini kote tena ni nafasi ya kupima uimara na Utayari wa wanachama katika kukijenga chama chao.

Chadema kinakosa mipango ya kukabiliana na CCM ya Magufuli kwa sababu ya akili ndogo ya Mbowe. Hivi kweli unaweza kusema kuwa Unaeneza dini kama ya Uislam au Ukristo halafu hujengi Msikiti wa kuswalia Kanisa !! Utakua Kichaa kama utakubaliana na Imamu au Mchungaji au Padri atakayewaambia waumini kuwa hakuna haja ya kujenga nyumba ya ibada kwa sababu waumini wanahitaji neno la Mungu tuu!!!

Mbowe hataki Kujenga na kuwekeza rasilimali za Chama kwa sababu ya roho Mbaya na kuona kuwa watakaonufaika ni wengine watakaoshika Chama. Miaka mitano bila harakati za Kisiasa fedha zimetumika kwenye mambo ya Hovyo badala ya kujenga miundo Mbinu ya Chama. Mbowe alikua haguswi na mfumo kwa sababu ni mmoja wapo wa watu waliotumiwa na kuhujumu watu ndani ya CCM kwa manufaa ya CCM. Mbowe kwa sasa anabanwa sio kwa sababu eti mpinzani wa kweli Bali ni kwa sababu Magufuli hataki mitandao ndani ya CCM ndio maana Mbowe anakosa kazi. Kazi ilikua kutumika kuwachafua watu. Kama unabisha angalia muda wote Mbowe anamwandama Magufuli tuu wakati walikua wanamsifia wakati akiwa Waziri na kumuona ndiye waziri mchapa Kazi.
Vipi Leo aonekane Mbaya wakati anafanya Yale Yale waliyokuwa wanayapigania.?jibu ni kwamba walikua wanatumika kuwachafua watu ndio maana walikua hawaguswi. Wakati Ule Mbowe alikua hakamati wala kukaa Gerezani. Slaa ndio alivunjwa mpaka mkono.
Mbowe anatamani awe na umaarufu wa Lisu lakini anaogopa risasi.Mwishowe imebidi ajiangushe kwenye ngazi baada ya kulewa Chakari. Dili lake la kujitangaza kuwa amevamiwa likabumburuka. Hapo eti ndiyo mikakati ya Mbowe ya kujijenga kisiasa!! Khatari ksana!
Mkuu Nyerere alitawala tukiwa na mfumo wa vyama vingi.Yeye ndio alileta mfumo wa Chama kimmoja.
Lakini alipo ngatuka akataka mfumo wa vyama vingi.
Chadema si majengo,chadema ni utayari wa wanachama kuchukuwa dola.Kwani hayo majengo ,viwanja vya michezo na miradi inayomiliki CCM ni nguvu ya wananchi wote wakati ws chama kimmoja.
Hata Mwalimu wa Propaganda zenu naona anapwaya.
 
Back
Top Bottom