Hakuna kitu kinatokea kwa bahati mbaya katika siasa ya Bongo

Hakuna kitu kinatokea kwa bahati mbaya katika siasa ya Bongo

Ujinga katika hii post ni Kuamini na kuaminisha wengine wote kuwa mpinzani wa kweli nchini ni Mbowe na ujinga zaidi ni kuamini Zitto alianzisha chama ili aimalize Chadema

Lakini ujinga wa mwisho katika post hii ni kushindwa kutambua mchango wa Zitto kuisimamisha upinzani uliopo nchini na kuifanya serikali isipumue
Mkalamo
Sijui kwanini unatumia neno ujinga. Nimeeleza jinsi Mbowe alivyochezewa "shere" hiyo haimananishi yeye ni mpinzani wa kweli. Kuhusu kuifanya "serikali isipumue" watu wengi wamewahi fanya hivyo na sio wapinzani wa kweli. Kuna wabunge wa CCM wamewahi ilaza macho hii selikali bungeni na mabaraza ya mawaziri yalivunjwa mara kibao.
Hoja ya msingi ni je,kuna dhamira ya kweli kuelekea kushika dola katika harakati zao.
Kuna mtu amewahi "ilaza macho" selikali kama Mrema wa NCCR Mageuzi? Au ulikuwa mdogo?
 
Wanabodi,

Kwanza hakuna kitu kinatokea kwenye siasa kwa bahati mbaya. Kila kitu hupanga na wenye akili "Elites" ambao wengi wao hawapo kabisa kwenye siasa ila ndio wanaamua siasa.

Ukiona siasa ya Mkapa,Kikwete na leo JPM ujue wao wenye siasa yao wameamua kuifinyanga iwe hivyo unavyoiona leo.
Siasa ya ni kama mchezo wa kuigiza "Tamthilia" inayoigizwa jukwaani. Kuna wanaoangalia na kuisgabikia tamthilia ambao ndio sisi wananchi tunaokaa mbele ya jukwaa na mchezo unatuhusu sisi,na waigizaji "stunts" ambao ndio wanasiasa wenyewe wanaoigiza na nyuma ya jukwaa kuna pazia ambako huko ndiko mambo na mipango yote ya tamthilia inakopangwa. Huko nyuma ya pazia ndiko wanapambwa na kufanya mazoezi ya kuigiza na huko ndiko hao "Elites" wapo na ndio wanaamua mchezo uweje huku kila Muigizaji akipewa kipande aigize vipi na kwa namna gani na ili iweje,huku lengo kuu ni kuendelea kubaki milele katika dora huku waigizaji lengo lao ni kuishi kupitia mchezo huo unaolipa vizuri sana.

Na huko nyuma ya pazia ndio wapo "craftsmen" ambao ndio waandishi na waongozaji "masterminds" wa mpango mzima wa igizo.

Tuangazie ishu moja tuu ya vyama vingi msingi wake ambao mpaka leo tunateseka nao sababu bado "Elites" wameushikilia mpango wao huku "stunts" wengi wamezeeka japo wanaendelea kucheza tamthilia huku kazi kubwa ikiwa ni kuwaandaa wachezaji wengine wachanga.

Ndio maana leo utaona mtu kama Cheyo anaomba apewe viti vya ubunge free na ukimuona unaona wazi amechoka kimwili na fikra ila ni mchezaji wa siku nyingi sana na ana ukwasi anajiita "bwana mapesa".

Bosi wa TLP ambaye amewahi kuwa "Naibu Waziri Mkuu". Jamaa ambaye enzi hizo mimi napata akili aliwahi hamasisha tuandamane na mwishoni tukapigwa sisi na kwa macho yangu nikamuona anapanda gari ya RPC kwa kupigiwa saluti. Huyu jamaa yupo kwenye "payroll" nyingi za nchi hii na ni tajiri sema afya tuu mzee wetu huyu.

Vijana wengi "smart" wa walitolewa katika nafasi zao nyeti na kupewa mpunga na kuanzishwa vyama vyao huku wakipewa ruzuku na hao hao wanaowapinga. Yaani unampinga na kumtukana mtu,huyo huyo mtu ndiye anasaini malipo yenu kulipa chama chenu ruzuku kupitia msajiri wa hazina. Huku ujira wa hao "stunts" ukiwa ni ruzuku. Hawa hawana nia ya kushika dora,wao wananufaika na ruzuku na tips za hapa na pale kutoka kwa wale wanaowapinga.

Kwanza ieleweke mchakato wa vyama vingi haukuwa msukumo wetu wa ndani, ulikuwa ni msukumo wa nje maana sisi tuliukataa. Ila wakati huo ili kuendana na masharti ya mabeberu kutoka Bretton Woods ikiwemo WB na IMF chini ya mfumo wa SAP's "Elites" au "think tankers" walifikiri na kuja na mkakati wa siku nyingi wa kuleta vyama na namna ya kuvidhibiti.

Waliandaliwa watu "smart" kutoka vitengo wakapewa "mchanga" kwa lengo la kuanzisha vyama hiyo 1992.

Mtei na Makani ni miongoni mwa watu hao. Mbowe amechukua chama hicho 2000 hakuwahi jua waanzishaji wa chama hicho wana ajenda zao na wana mkono mrefu. Yeye akaja serious akakikuza chama hicho,"Elites" wakaona kijana anavuka grafu wakamchezea shere,wakawavuta vijana wake aliowapika akiwemo Boss wa ACT,alipolambishwa chambi ishu ya Buzwagi akawa hana namna akawa mtumwa wa "Elites". Elites wakawa wakaanza mtumia na wakampa mpunga aanzishe chama chama ndani ya chama. Huyo bosi ACT ana ukwasi wa kuweza kuendesha chama kichanga kusimamamisha mgombea uraisi na kumzungusha nchi kubwa kila kijiji. Hela hiyo aliotoa wapi?.

Mwaka 2015 "Elites" wakapika mpango washindane wao kwa wao. Wakafanikiwa kuwaingiza kingi CDM wakamletea EL. 2015 hapakuwa na upinzani,Chama dora kilikuwa peke yake,walishindana wale wale. 2015 mchawi "CDM" alipewa mwana amlee na akakubali. Mtoto kakua kanyea kambi na karudi kwa baba yake.

EL alikuwa na malengo mawili kwanza ajisafishe na pili alitimiza lengo la chama dora kushindana wenyewe. EL kwa sasa ni "msafi" na hafuatwi na nzi tena na unaishi "uzee mwema".
Tragedy of miscalculation inabaki kuitafuna CDM. Wakati kamati kuu inampitisha EL kuwa mgombea wao "mzee ruksa" alisema "wamekwisha" lakini sikio la kufa wakakomaa kumpiga jiki EL huku wakifurahia bilioni tisa alizokuja nazo wakijua ni zake,kumbe mwenzao alipewa huo "mpunga" na "Elites" na yeye hakuweka hata mia mbovu ya kwake.

2020 kuendelea...
Huyo dogo wa visiwani alianza kuandaliwa muda ni mpango wa muda mrefu toka enzi za Ben.

Ishu ya BM kufukuzwa na yenyewe ni trap ni mpango kama ulivyokuwa wa EL mwaka 2015.
Mtoto wa kigoma Mwandiga na yeye anadeni lile lile la kuwamaliza hawa CDM huku yeye akiwa hana mpango wa kushika dora ila kupiga ruzuku. Kazi hiyo bado hajatimiza na ndio maana Maalim amenyakwa visiwani na huku anampanga BM agombee bara.
Lengo lao ni kuwapoka CDM na CUF kitumbua "ruzuku" na kuimaliza CDM.

NATABIRI HAYA BAADA YA OKTOBA
BM ataenda ACT atapunguza kura za CDM. ACT watapewa majimbo na watapata asilimia nyingi za kura kupata ruzuku kutoka visiwani.
BM akimaliza uchaguzi chama chake watamsamehe na watamrudushia uanachama.

ZZK hatagombea uraisi mwaka huu,mpango wake ni 2025 ambapo atakuwa ametimiza lengo la kuiondoa CDM katika "key opposition" ya nchi.

Maalim mwaka huu atapata kura kiduchu sana maana CUF nao wataweka mtu kugawana kura na Huseni atapeta.

Bado tunasafari ndefu sana ya "upinzani" bongo. Aliyebuni mpango wa mwaka 1992 wa namna ya kuendesha siasa ya vyama vingi akili yake itaishi kwa siku nyingi na kwa vizazi vingi. Mpaka pale ambapo tutakuja kufahamu tunataka nini na tukafanya kazi kubwa ya kupata tunachokitaka ndipo tutapata jibu.

Wasaalam.
"Upepo ukipuliza sana uchi wa kuku huonekana"
"Ukiwa na subra utaona mwisho wa kila kitu"
Nishawahi kusema hapa JF kuwa ktk nchi zisizo za kibepari sanduku la kura haliwezi kukiondoa chama tawala madarakani na ikiwezekana basi nyuma yake kuna influences za mabeberu.
 
mwayena.
Kumwamini mtu hutegemea namna unavyotazama mambo na uelewa.
Siasa ina mengi kuielewa inahitaji usiwe kuku uwe tai.
Hapo Kenya Raisi ajaye 2022 ni Gideon Moi. Usishangae Ridhiwani Kikwete akapata wizara 2020 na akawa bosi wetu 2025.
Nimekuelewa Mkuu, hivyo katika siasa tunajifunza kwamba kile unachotegemea kinaeza Kisiwe na kinyume chake ni sawa.
 
Ujinga katika hii post ni Kuamini na kuaminisha wengine wote kuwa mpinzani wa kweli nchini ni Mbowe na ujinga zaidi ni kuamini Zitto alianzisha chama ili aimalize Chadema

Lakini ujinga wa mwisho katika post hii ni kushindwa kutambua mchango wa Zitto kuisimamisha upinzani uliopo nchini na kuifanya serikali isipumue

Umeandika kinyume kabisa cha ukweli bila shaka ukitarajia bado nchi ina wajinga wengi wa kuaminishwa chochote.

Yaani umeshindwa hata kuona jinsi dola ilivyompuuza Zitto hata atoe kauli ya kuudhi kiasi gani kumhusu JPM wakati Mbowe na makada wengine wa CHADEMA wanavamiwa na polisi kila kukicha hata kwa kuhisiwa tu kuwa wanatarajiwa kutoa kauli za “kichochezi”.
 
Shida yenu mnaishi kwa kukariri maisha yaani mpaka muda huu hujaelewa unapoambiwa kuna elites na hao ndiyo waasisi wa vyama unavyoshabikia.
Pangusa macho yako kisha soma tena. Sina sehemu nimeandika chama chochote.
 
Utabiri wangu sasa umetimia. BM yupo ACT wazalendo atagombea uraisi wa Bongo. Bravo
 
Maalimu kua kitengo hilo sijui lkn akiumwa ni lazima agharamiwe na SMZ sababu yeye alikua ni makamu wa raisi huko Zenji(kipindi cha Shein) na matibabu ni sehemu ya stahiki yake kama makamu wa rais mstaafu.
Mng'ato
Naomba kukuhabarisha.
Ni rasmi sasa BM anagombea kupitia ACT na Maalim anagombea visiwani. Nafikiri sasa umefahamu mpango wa "Elites".
Wasaalam
 
Mng'ato
Naomba kukuhabarisha.
Ni rasmi sasa BM anagombea kupitia ACT na Maalim anagombea visiwani. Nafikiri sasa umefahamu mpango wa "Elites".
Wasaalam
Mkuu Membe hajawahi kunipa tabu,najua atafanya kazi kama ile ya Lowassa akimaliza atarudi zake kwao CCM.

Hio ya Maalim kua eagle ndio sikua na uhakika nayo na sijabisha kwamba ni mwenzao,lolote linawezekana tu.
 
Mkuu Membe hajawahi kunipa tabu,najua atafanya kazi kama ile ya Lowassa akimaliza atarudi zake kwao CCM.

Hio ya Maalim kua eagle ndio sikua na uhakika nayo na sijabisha kwamba ni mwenzao,lolote linawezekana tu.

Mng'ato
Ndio ujue sasa kuhusu Maalim. Sasa ni wazi wataenda tumia ilani "manifesto" moja kuomba kura za watanzania. Na watatumia hela za "elites" kuendesha siasa zao.
Watakaa kamati moja kujadili mambo yao na watashare mikakati yao.
Wasaalam
 
Mng'ato
Ndio ujue sasa kuhusu Maalim. Sasa ni wazi wataenda tumia ilani "manifesto" moja kuomba kura za watanzania. Na watatumia hela za "elites" kuendesha siasa zao.
Watakaa kamati moja kujadili mambo yao na watashare mikakati yao.
Wasaalam
Kiongozi hao hawanipi shida kabisa,maana kwa mfano huyo Membe kila mtu anajua kabisa motives behind yeye kugombea.

Maalim huyo atapambana na wazenji wenzake wakina Jussa.
 
eti ndugu zito na chama chake kichanga alitoa wapi pesa 2015 yaku mzungusha mgombea urais tanzania nzima? labda unajua
Mwalisi.
Pia muulize mgombea wa ACT Anna baada ya kugombea uraisi alienda wapi?
Je,alikuwa akimfahamu Mghwira kabla ya ACT? Au anafikiri Mghwira walimkuta tuu mtaani wakamwambia njoo ugombee uraisi wa ACT?
Mmewahi kujihangaisha kumjua Mghwira ni nani? Au alikuja kuja tuu kugombea.
 
Mwalisi.
Pia muulize mgombea wa ACT Anna baada ya kugombea uraisi alienda wapi?
Je,alikuwa akimfahamu Mghwira kabla ya ACT? Au anafikiri Mghwira walimkuta tuu mtaani wakamwambia njoo ugombee uraisi wa ACT?
Mmewahi kujihangaisha kumjua Mghwira ni nani? Au alikuja kuja tuu kugombea.
kuna maswali mawili magumu wakinijibu ntashukulu
 
Ni Mungu tu ndio anayeweza kuvuruga mbinu za wenye mbinu safi na chafu .

Kila jambo na majira yake,
Bado inawezekana sana tu ukurasa mpya kutoka kitabu kipya chenye kusomeka TANZANIA MPYA yenye kuongozwa na CHAMA CHA UPINZANI.

Namwomba Mungu mabadiliko hayo yakitokea,YATOKEE KWA AMANI,KUSIWE NA UMWAGAJI WA DAMU KWA TAIFA LETU HILI ZURI.
 
Kuna msemo ulivuma sana mwaka 2015 kwamba "CCM ina kitabu kikubwa cha MBINU ZA KUSHINDA UCHAGUZI na mpaka mwaka 2015 walikua ndo kwanza wako kurasa ya 3" kwahiyo bado kurasa kibao yaan Wapinzani wa nchi hii wajipange😢😢
Kaandika uongo na wewe hutumii ubongo Hata kidogo? ENL aliondoka Kwa hasira na alirudi Kwa vitisho, huyo mwandishi ni conspiracy theories zisizo na akili.

Unawaamini CCM wana thinktank mujarabu, Hata T-shirt wanaiga CHADEMA? Ningemuelewa angeongelea tume na Vyombo vya dola lakini si vinginevyo, and, Tume na Vyombo vya dola sio permanent solution maana tuneona 2010 hawakuwa pro CCM unless wewe ni kinda ulikuwa huna akili 2010!
 
Wanabodi,

Kwanza hakuna kitu kinatokea kwenye siasa kwa bahati mbaya. Kila kitu hupanga na wenye akili "Elites" ambao wengi wao hawapo kabisa kwenye siasa ila ndio wanaamua siasa.

Ukiona siasa ya Mkapa,Kikwete na leo JPM ujue wao wenye siasa yao wameamua kuifinyanga iwe hivyo unavyoiona leo.
Siasa ya ni kama mchezo wa kuigiza "Tamthilia" inayoigizwa jukwaani. Kuna wanaoangalia na kuisgabikia tamthilia ambao ndio sisi wananchi tunaokaa mbele ya jukwaa na mchezo unatuhusu sisi,na waigizaji "stunts" ambao ndio wanasiasa wenyewe wanaoigiza na nyuma ya jukwaa kuna pazia ambako huko ndiko mambo na mipango yote ya tamthilia inakopangwa. Huko nyuma ya pazia ndiko wanapambwa na kufanya mazoezi ya kuigiza na huko ndiko hao "Elites" wapo na ndio wanaamua mchezo uweje huku kila Muigizaji akipewa kipande aigize vipi na kwa namna gani na ili iweje,huku lengo kuu ni kuendelea kubaki milele katika dora huku waigizaji lengo lao ni kuishi kupitia mchezo huo unaolipa vizuri sana.

Na huko nyuma ya pazia ndio wapo "craftsmen" ambao ndio waandishi na waongozaji "masterminds" wa mpango mzima wa igizo.

Tuangazie ishu moja tuu ya vyama vingi msingi wake ambao mpaka leo tunateseka nao sababu bado "Elites" wameushikilia mpango wao huku "stunts" wengi wamezeeka japo wanaendelea kucheza tamthilia huku kazi kubwa ikiwa ni kuwaandaa wachezaji wengine wachanga.

Ndio maana leo utaona mtu kama Cheyo anaomba apewe viti vya ubunge free na ukimuona unaona wazi amechoka kimwili na fikra ila ni mchezaji wa siku nyingi sana na ana ukwasi anajiita "bwana mapesa".

Bosi wa TLP ambaye amewahi kuwa "Naibu Waziri Mkuu". Jamaa ambaye enzi hizo mimi napata akili aliwahi hamasisha tuandamane na mwishoni tukapigwa sisi na kwa macho yangu nikamuona anapanda gari ya RPC kwa kupigiwa saluti. Huyu jamaa yupo kwenye "payroll" nyingi za nchi hii na ni tajiri sema afya tuu mzee wetu huyu.

Vijana wengi "smart" wa walitolewa katika nafasi zao nyeti na kupewa mpunga na kuanzishwa vyama vyao huku wakipewa ruzuku na hao hao wanaowapinga. Yaani unampinga na kumtukana mtu,huyo huyo mtu ndiye anasaini malipo yenu kulipa chama chenu ruzuku kupitia msajiri wa hazina. Huku ujira wa hao "stunts" ukiwa ni ruzuku. Hawa hawana nia ya kushika dora,wao wananufaika na ruzuku na tips za hapa na pale kutoka kwa wale wanaowapinga.

Kwanza ieleweke mchakato wa vyama vingi haukuwa msukumo wetu wa ndani, ulikuwa ni msukumo wa nje maana sisi tuliukataa. Ila wakati huo ili kuendana na masharti ya mabeberu kutoka Bretton Woods ikiwemo WB na IMF chini ya mfumo wa SAP's "Elites" au "think tankers" walifikiri na kuja na mkakati wa siku nyingi wa kuleta vyama na namna ya kuvidhibiti.

Waliandaliwa watu "smart" kutoka vitengo wakapewa "mchanga" kwa lengo la kuanzisha vyama hiyo 1992.

Mtei na Makani ni miongoni mwa watu hao. Mbowe amechukua chama hicho 2000 hakuwahi jua waanzishaji wa chama hicho wana ajenda zao na wana mkono mrefu. Yeye akaja serious akakikuza chama hicho,"Elites" wakaona kijana anavuka grafu wakamchezea shere,wakawavuta vijana wake aliowapika akiwemo Boss wa ACT,alipolambishwa chambi ishu ya Buzwagi akawa hana namna akawa mtumwa wa "Elites". Elites wakawa wakaanza mtumia na wakampa mpunga aanzishe chama chama ndani ya chama. Huyo bosi ACT ana ukwasi wa kuweza kuendesha chama kichanga kusimamamisha mgombea uraisi na kumzungusha nchi kubwa kila kijiji. Hela hiyo aliotoa wapi?.

Mwaka 2015 "Elites" wakapika mpango washindane wao kwa wao. Wakafanikiwa kuwaingiza kingi CDM wakamletea EL. 2015 hapakuwa na upinzani,Chama dora kilikuwa peke yake,walishindana wale wale. 2015 mchawi "CDM" alipewa mwana amlee na akakubali. Mtoto kakua kanyea kambi na karudi kwa baba yake.

EL alikuwa na malengo mawili kwanza ajisafishe na pili alitimiza lengo la chama dora kushindana wenyewe. EL kwa sasa ni "msafi" na hafuatwi na nzi tena na unaishi "uzee mwema".
Tragedy of miscalculation inabaki kuitafuna CDM. Wakati kamati kuu inampitisha EL kuwa mgombea wao "mzee ruksa" alisema "wamekwisha" lakini sikio la kufa wakakomaa kumpiga jiki EL huku wakifurahia bilioni tisa alizokuja nazo wakijua ni zake,kumbe mwenzao alipewa huo "mpunga" na "Elites" na yeye hakuweka hata mia mbovu ya kwake.

2020 kuendelea...
Huyo dogo wa visiwani alianza kuandaliwa muda ni mpango wa muda mrefu toka enzi za Ben.

Ishu ya BM kufukuzwa na yenyewe ni trap ni mpango kama ulivyokuwa wa EL mwaka 2015.
Mtoto wa kigoma Mwandiga na yeye anadeni lile lile la kuwamaliza hawa CDM huku yeye akiwa hana mpango wa kushika dora ila kupiga ruzuku. Kazi hiyo bado hajatimiza na ndio maana Maalim amenyakwa visiwani na huku anampanga BM agombee bara.
Lengo lao ni kuwapoka CDM na CUF kitumbua "ruzuku" na kuimaliza CDM.

NATABIRI HAYA BAADA YA OKTOBA
BM ataenda ACT atapunguza kura za CDM. ACT watapewa majimbo na watapata asilimia nyingi za kura kupata ruzuku kutoka visiwani.
BM akimaliza uchaguzi chama chake watamsamehe na watamrudushia uanachama.

ZZK hatagombea uraisi mwaka huu,mpango wake ni 2025 ambapo atakuwa ametimiza lengo la kuiondoa CDM katika "key opposition" ya nchi.

Maalim mwaka huu atapata kura kiduchu sana maana CUF nao wataweka mtu kugawana kura na Huseni atapeta.

Bado tunasafari ndefu sana ya "upinzani" bongo. Aliyebuni mpango wa mwaka 1992 wa namna ya kuendesha siasa ya vyama vingi akili yake itaishi kwa siku nyingi na kwa vizazi vingi. Mpaka pale ambapo tutakuja kufahamu tunataka nini na tukafanya kazi kubwa ya kupata tunachokitaka ndipo tutapata jibu.

Wasaalam.
"Upepo ukipuliza sana uchi wa kuku huonekana"
"Ukiwa na subra utaona mwisho wa kila kitu"
Naona umeungaunga ili uwe mtumwa wa hisia zako!
 
Adui wa Demokrasia ya nchi hii ni Mbowe .

Mbowe hakuikuza Chadema Bali Mbowe alisafiria nyota za makada wenzake waliotoka CCM.
Mbowe angemkosa Slaa ni kama mkulima mwenye mpini tu usio na jembe.
Mbowe angemkosa Zito miaka ya 2010-2015 vyuo vikuu na waislam kuiamini Chadema ni kama mkulima mwenye Jembe bila mpini wake.
Mbowe angemkosa Lowasa 2015 ni kama mkulima mwenye Jembe bila kuwa na shamba la kulima.

Sasa Mbowe Mwaka huu anataka kusafiria nyota ya Lisu na Nyarandu yupo kama mkulima mwenye Shamba bila kuwa na Jembe la kulimia .
Baada ya Uchaguzi huu Mlevi huyo unayetaka kuwaaminisha wahuni kuwa ndiye aliyeijenga Chadema atabaki kama mkulima asiye na shamba wala Jembe.

Siasa sio mchezo kama kama mpira. Siasa zinahitaji ushawishi na hoja zenye misimamo imara kiroho na kijamii.
Mbowe hana mvuto wa kiroho wala kijamii .
Mbowe ni mjasiriamali mwenye haiba na hulka ya tamaa ya fedha ,wizi, ubinafsi, na mtu asiye na huruma anaposikia harufu ya madaka na fedha.
Ni kosa kubwa sana kumwamini tajiri Mbowe apiganie haki za maskini 80% wa nchi hii. Ni kujilisha upepo kumtegemea Tajiri atangulie mbele ya vitani wakati anawaza Mali zake na starehe na mademu wake.
Kujitoa muhanga kunaendana na kujaa imani kiroho ili mtu aweze kuipigania jamii bila kujali maslahi au kupoteza.
Mbowe ni muoga kuliko kunguru. Ndio maana mpaka kijijini kwake Chadema imefyata mkia kwa kumwogopa kijana Machachari na Kada wa CCM DC .Sabaya.

Kumlinganisha Zito Msomi na mwanasiasa aliyeanzisha Chama wakati mgumu kabisa huku akitukana na CCM na Chadema ni sawa na kumlinganisha Faru (Zito) na Ngiri (Mlevi Mbowe).
Mbowe amerithishwa chama kwa sababu ya ukabila tu na ukaribu wake na Mtei lakini Mbowe hana uwezo wa kuanzisha chama cha siasa duniani na hata kuzimu achilia mbali Mbinguni Patakatifu pasipohitaji walevi na wazinzi na wezi.

Siasa ni kazi na vipaji vya baadhi ya watu kama ilivyopira na michezo mingine na hata biashara na kazi nyingine.
Wanasiasa ni watu kwenye jamii wasiopenda kuongozwa wala kupangiwa jambo na wengine bila wao kushiriki. Hata mkikaa kwenye kikao cha harusi kama kuna mwanasiasa atakua msemaji sana na kutoka kuona mawazo yake ndiyo yanasikilozwa. Hata kwenye msiba wanasiasa watakuwa mstari wa mbele kuonekana.
Kwenye familia pia wanasiasa watajitokeza mbele kutaka wasikilizwe wao.
Kwa hiyo hakuna namna ya kuwazuie eti wasitoke CCM na kwenda Chadema au kutoka chadema kurudi CCM.

Dunia ndivyo ilivyo. Hakuna namana ya kuwatenganisha wanasiasa wa upande mmoja tuu wasiunge mkono upande mwingine kwenye baadhi ya mambo.
Ni vijana wachache walevi tu ndani ya Chadema wanaowaita watu wa vyama vingine wanaojiunga na chama hicho au wanaohama kuunga mkono baadhi ya utendaji wa wapinzani wao kuwa ni wasaliti. Ingekua hivyo Marekani chama kimoja kingetawala milele. Lakini kule watu wanamkataa hata kama ni MTU wa Chama chake lakini anafanya mambo ya hovyo anapingwa na ananyimwa kura na wanachama wa chama chake wanapunguza kura zake zinahamia kwa mpinzani wake.

Tanzania katika Uchanga wake imefanikiwa kuwa na siasa nzuri za ushindani wa hoja ndani ya CCM na nje ya CCM. Nchi hii ilikua ya Chama kimoja chenye upinzani mkubwa sana wa ndani hivyo usione ajabu watu kutoka nje ya CCM na kumpinga mtu waliyekua wanaimba pamoja CCM yajenga nchi.

Kumbuka Bado Afrika tunatambuana kwa makabila na dini na asili zetu.
Hata kwenye taarifa zetu kwenye fomu mbali mbali zinaeneo la kujaza Kabila lako,dini yako n.k.
Dini ,kabila na ukanda unaathiri sana siasa za Tanzania . Jambo ambalo Chama la Chama la kupindua wanafanikiwa kudumu milele madarakani kwa kutumia hayo mambo matatu.
Akiwa wa dini Fulani basi dini ile wote wataapena ishara ya kumuunga mkono hata kama atakosea watajitokeza kumuunga mkono kwa nguvu zote.
Wakiona dini haimuungi mkono huyo basi wanahamia kwenye ukanda au kabila . Yote hayo ni tatizo la woga wa mwanasiasa waliozoea kukaa madarakani na wakajiwekea marupurupu makubwa na Kuweka katiba inayowapa madaraka makubwa.

Hapo ishu sio kikundi cha watu nyuma ya pazia kupanga nani awe wapi . Huo ni uongo mkubwa. Siasa za Kiafrika zinaathiriwa na Umaskini na Katiba zinazotoa madaraka makubwa kwa watawala.
Mtawala akishika madaraka anakua ni zaidi ya mungu juu ya wanadamu wenzake mana anashila mpaka nafasi ya kupanga nani ashibe na nani aishi kama malaika na nani aishi kama shetani.
Hii hali inawafanya wanasiasa wakose misimamo zaidi ya kubaki wakiwa wanajipendekeza ili waishi kama malaika muda wote.

Hivi Mbowe na Tundu Lisu nani ni mpinzani toka Rohoni bila kujali Umaarufu, madaraka, Dhiki, kupoteza uhai, kupoteza fedha na kudai Mali za chama kama fidia ya muda na fedha zake n.k????
Bila shaka Lisu ndiye mpinzani wa kweli .
Mbowe ni Magumashi ndio maana alibadili katiba ya Chama ili afie kwenye Uenyekiti wa Chadema.
Mkitaka Mbowe arudi CCM kesho asubuhi mtoeni kwenye Uenyekiti halafu aone Mali zake zinafilisiwa na hana uwezo wa kukwapua Ruzuku kufidia mali anazopoteza .
Atakimbilia ikulu asubuhi kabisa kupiga magoti.

Nisipomtaja Mbowe kwa mabaya yake ni sawa na Mchungaji asipomtaja Shetani kwa kumlaani kuwa ashindwe.

Mlevi na Mzinzi Mbowe Shindwa na Ulegee! !!
Nchi yetu ipone kwa kuwa na siasa safi na za kidemokrasia kuanzia ndani ya vyama.
Acha ulevi, nani hajui kama Zitto alipewa chama na serikali kwa kumtumia msajili kumpora Limbu? Miaka yote mnapambana Mbowe aachie uenyekiti CDM...Sabaya amefanya nini Hai? ulitaka wamfanyie nini labda ndio uelewe kuwa kila walichopanga kinafeli!
 
Nilikuwa nimeamua kusoma comments tu lakini nilipokutana na hii ya kwako nikasema nije kukupigia salute Mkuu.

I salute you Mkuu.

Hakuna cha kitabu wala nini. Waweke tume huru na kubadili katiba ndiyo utaijua hiyo nguvu ya hicho kijitabu.
 
Naam Mkuu kabla ya saa tano asubuhi watakuwa wameshaachia dola na majimbo mengi kwenda upinzani ndiyo utakuwa mwisho wa hili genge la wahuni.

Na wao wanajua wakiruhusu tume huru asubuhi tu watakua wameaga pale magogoni.
 
👏🏽👏🏽👏🏽👏🏽👏🏽👏🏽👊🏽 Hakuna Elites wala mama yake Elites bali kuna UHUNI wa hali ya juu na UBABE kupitia vyombo vya dola.

Kama si vyombo vya dola kuibeba ccm naamini uchaguzi wa 2010 Chadema ingechukua Nchi.

Mkapa katoa wito wa kutaka Tume Huru lakini humsikii yoyote yule ndani ya ccm au Serikali kutia neno ama kuunga mkono hoja ya Mkapa au kuipinga bali wameamua kupiga kimya kwa kujua fika Tume Huru ndiyo KIAMA cha maccm.

Akili yangu imegoma kuamini ulichoandika mkuu..

Ikiwa mambo hupangwa na kuratibiwa na hao ' Elites ' , kwanini tunaona matumiz ya nguvu kupita kiasi.
Magereza
Police
Mahakama
Uvccm

Jeh ThinkTank wameishiwa maarifa.
Kwanini waruhusu wakosoaji kupotezwa.

Kwanini image ya Rais Maghufuli ichafuliwe na wasiojulikana..

Kwanini wabariki sheria za kioga oga
Na kandamiz ikiwa wao ndio wapishi wa kila ktu. Sheria za sijui takwimu. Huduma za vyombo vya habari. Kinga ya kutoshtakiwa.. nk
 
Back
Top Bottom