Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mimi nime - subscribe kabisa mapemaHii thread ni nzito, naihifadhi nitaamka nayo with fresh mind.
Shida yenu mnaishi kwa kukariri maisha yaani mpaka muda huu hujaelewa unapoambiwa kuna elites na hao ndiyo waasisi wa vyama unavyoshabikia.Hakuna cha kitabu wala nini. Waweke tume huru na kubadili katiba ndiyo utaijua hiyo nguvu ya hicho kijitabu.
Kwani mimi nilikua nimeandikaje mkuu?Maalimu akiugua anatibiwa kama wanavyotibiwa viongozi wengine maalim alishawahi kuwa makamu wa rais incase hujui
Mkuu Nyerere alitawala tukiwa na mfumo wa vyama vingi.Yeye ndio alileta mfumo wa Chama kimmoja.
Lakini alipo ngatuka akataka mfumo wa vyama vingi.
Chadema si majengo,chadema ni utayari wa wanachama kuchukuwa dola.Kwani hayo majengo ,viwanja vya michezo na miradi inayomiliki CCM ni nguvu ya wananchi wote wakati ws chama kimmoja.
Hata Mwalimu wa Propaganda zenu naona anapwaya.
Mkuu hapa ni mada juu ya mada. Akili yangu ni kama yako.Akili yangu imegoma kuamini ulichoandika mkuu..
Ikiwa mambo hupangwa na kuratibiwa na hao ' Elites ' , kwanini tunaona matumiz ya nguvu kupita kiasi.
Magereza
Police
Mahakama
Uvccm
Jeh ThinkTank wameishiwa maarifa.
Kwanini waruhusu wakosoaji kupotezwa.
Kwanini image ya Rais Maghufuli ichafuliwe na wasiojulikana..
Kwanini wabariki sheria za kioga oga
Na kandamiz ikiwa wao ndio wapishi wa kila ktu. Sheria za sijui takwimu. Huduma za vyombo vya habari. Kinga ya kutoshtakiwa.. nk
Wewe hujui tokea TANU hadi CCM mali zote za chama zililiwa na vigogo wa chama?Hakuna taasisi isiyo na Ofisi ,inayoelea angani itakayoweza kuchukua dola.Chadema inaongozwa na Mtu mbinafsi kubali usikubali,mtu mwenye Malengo binafsi ya kupata manufaa ya kibinafsi na watu wachache na sio umma anaouongoza.
Ndani ya Chadema ya Mhuni na Tapeli Mbowe ,Watu wanapiga hela za manunuzi ya bendera,T-shirt, vipeperushi,kofia, Magari, na Kupangishia chama majengo binafsi kwa gharama kubwa. Hivi kwa akili yako unaona ni sawa kuendelea kuacha Chama chenye Wanachama zaidi ya mil. 6 kipangishe Ofisi kwenye majengo ya watu binafsi hulo Uchochoroni na kulipa Pango la nyumba ?? Mnaakili za kichwani kweli au mnashikiliwa na Ubinafsi uliowajaa mioyoni mwenu. Siasa haziendeshwi na uroho Bali na roho za watu wenye nia Njema zikiongozwa na Roho wa Mungu.
Hujiulizi imekuaje Chadema ilikua inawatu wengi wa hali ya chini lakini ghafla upepo umebadilika wanyonge hawataki hata kumsikia Mbowe zaidi ya mabwanyenye ndani ya Chadema . Yote ni kwa sababu ya kumkumbatia mtu mwenye nia Ovu kuongoza chama.
CCM ilipoteza sifa za kushika dola ilipojichanganya na kufuata Njia Mbaya kama anayoifuata Mbowe kwa sasa.
Nani alikua kuwa Chama cha ACT kingeibuka ghafla na sasa kinajiandaa kuingia madarakani kule Zanzibar na kuitoa CCM jasho huku Bara mwaka huu?? Jibu ni kuwa nia ya dhati ya Zito ndiyo nguvu ya kiroho inayowabadili watu na kukiona hicho chama kama chama Mbadala. Sababu ya kuibuka kwa ACT ni upofu wa mtu mmoja mbinafsi anayetaka kukihodhi chama kama Mali yake binafsi huku akiwatumia vijana wa makabila mengine kama Makaratasi ya kuchambia. Huyo Mbowe Hata fanikiwa milele kukiingiza hicho chama Madarakani kwa ubinafsi alionao kwa sababu watanzania wa hali ya chini wameshamshtukiza kuwa sio mtu mzuri kabisa kabisa.
Ndio maana nasema kamwe Chadema haitaingia Ikulu kwa nguvu ya wajinga. Ni bora kuwafagilia mbali wajinga wote wabaki watu wenye akili na nia njema wajenge nchi. Tanzania sio kama unavyoiona kwa nje na kusikiliza mawazo uchwara ya kina Mbowe na wapuuzi wenzake.
Hii nchi ina misingi yake iliyowekwa na waasisi wa Taifa hili. Mbowe asiporudi kwenye misingi ya Ujamaa na kujitegemea asahau kuingia madarakani na hicho Chama chake kinachokaa kwenye Ofisi ambazo ni nyumba za watu binafsi huku akidanganya wajinga kuwa Ofisi hazina umuhimu wowote. Wanapanga hayo majengo kwa nini sasa kama Ofisi hazina umuhimu. Si wangekaa nje mitaani kama ilivyo kwa wamachinga wasio na maeneo rasmi ya biashara. Nyerere hakuwa mjinga alipowaunganisha watanzania kujenga Ofisi za chama nchi nzima kwa nguvu zao. Tulichanga sh.1 enzi hizo tukiwa shule ya msingi kujenga Ofisi za Chama za Wilaya mpaka Leo zipo na zimekua ni mradi wa chama. Ilikua ni kazi ya Baba wa Taifa asiyekuwa na ubinafsi kama Mlevi Mbowe.
Nakukumbusha tu kuwa Mtu yeyote hataweza kuingia madarakani kama etaenda kinyume na Misingi hiyo iliyojengwa kwa nia njema . Na hata akiingia atatolewa mchana kweupe endapo ataenda kinyume na misingi hiyo.
Chadema ilipata umaarufu mkubwa na kujenga imani kwa Wananchi kwa sababu ya CCM kupoteza misingi hiyo.
Leo hii Magufuli amejitahidi kuirudisha nyie ndio mnataka kuturudisha kwenye Uhuni wa watawala waliokua wamepoteza misingi ya Taifa letu.
Mbowe anatumiwa na Mabeberu kuihujumu nchi kwa tamaa yake ya kuingia madarakani ili achote fedha zote za hazina akijifanya ni fidia ya kupigania Chama . Kama anaona biashara ya siasa hailipi aachane nayo lakini asitumie umma kujinufsisha.
Mwakani tutahakikisha ruzuku zote zinafutwa kwenye vyama vyote . Miaka 28 sasa inatosha kwa wapinzani kujiendesha vyenyewe ,sio kutumia pesa za umma kuwanufaisha wanasiasa wanaopinga maendeleo na kujaza chuki kwa watananzani kwa Malengo yao binafsi wakiongozwa na Muovu na Kafiri mmoja anayeitwa Mbowe. Kama kazi ya Mbowe na Chadema yake ni kuandaa umma ufanye uasi na sio Chama cha kufanya siasa za hoja na kusapoti maendeleo ya wanyonge kwa Hoja basi nakuambia Hatupo tayari kuona nchi hii inachukuliwa na Chadema chini ya Wakala wa Mabeberu na mabwanyenye, Mwizi ,mhuni Kabisa Mbowe. Tutaipigania nchi hii kwa nguvu zote amini usiamini. Hiyo nguvu ya umma mnayoisema haipo kwa sasa imebaki nguvu ya wahuni ,Malaya Malaya, wasaliti wa nchi hii, walevi ,wavuta bangi, na watu wabinafsi,wezi wa mali za umma, mercenaries wa Mabeberu ; tutawasaka popote walipo na kuwatia kizuizini nchi irudi kwa wananchi wa kawaida ambao ni zaidi ya 85%.
Najua Mbowe ni Mlevi wa kupindukia bado yupo kwenye Baa anavizia Mlupo wa kuondoka nao japo bado ni majeruhi.
Muongezee Mbowe Konyagi Moja!!
Sasa mbona mnamkumbatia?.Yule ni kama kawa ni agent,tatizo atakalolipata sasa hivi ni kwamba huku mtaani wajuba wote wamemshtukia kwamba yeye ni pandikizi tu.
Kumbe yale ya 2015 yalikuwa makosa?Waling'atwa na nyoka awarudii kosa,naona mazungumzo yake na CDM yaligonga mwamba anajaribu ACT.Ila ACT wakirudia kosa la cdm 2015 kuyapa mapandikizi leseni za udereva watavunja mioyo ya wanachama wao.
Hadi matokeo yatokee ndipo unakuwa tomaso,Safari mbobezi amelamba garasa.Hii mbinu chakavu waliitumia 2015,ACT wakimeza tu ndoano watazigawa kura za CDM na kuipalilia ccm iendelee kutusomesha namba againKumbe yale ya 2015 yalikuwa makosa?
Mbona tuliwaambia moashupaza shingo mpaka zilipovunjika ndio mnagutuka?
Ngoja amnukie Zitto huko.Sasa mbona mnamkumbatia?.
By the Way, si ni jasusi wenu mbobevu huyo? Na akiguswa ananuka?
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
Ujinga katika hii post ni Kuamini na kuaminisha wengine wote kuwa mpinzani wa kweli nchini ni Mbowe na ujinga zaidi ni kuamini Zitto alianzisha chama ili aimalize ChademaWanabodi,
Kwanza hakuna kitu kinatokea kwenye siasa kwa bahati mbaya. Kila kitu hupanga na wenye akili "Elites" ambao wengi wao hawapo kabisa kwenye siasa ila ndio wanaamua siasa.
Ukiona siasa ya Mkapa,Kikwete na leo JPM ujue wao wenye siasa yao wameamua kuifinyanga iwe hivyo unavyoiona leo.
Siasa ya ni kama mchezo wa kuigiza "Tamthilia" inayoigizwa jukwaani. Kuna wanaoangalia na kuisgabikia tamthilia ambao ndio sisi wananchi tunaokaa mbele ya jukwaa na mchezo unatuhusu sisi,na waigizaji "stunts" ambao ndio wanasiasa wenyewe wanaoigiza na nyuma ya jukwaa kuna pazia ambako huko ndiko mambo na mipango yote ya tamthilia inakopangwa. Huko nyuma ya pazia ndiko wanapambwa na kufanya mazoezi ya kuigiza na huko ndiko hao "Elites" wapo na ndio wanaamua mchezo uweje huku kila Muigizaji akipewa kipande aigize vipi na kwa namna gani na ili iweje,huku lengo kuu ni kuendelea kubaki milele katika dora huku waigizaji lengo lao ni kuishi kupitia mchezo huo unaolipa vizuri sana.
Na huko nyuma ya pazia ndio wapo "craftsmen" ambao ndio waandishi na waongozaji "masterminds" wa mpango mzima wa igizo.
Tuangazie ishu moja tuu ya vyama vingi msingi wake ambao mpaka leo tunateseka nao sababu bado "Elites" wameushikilia mpango wao huku "stunts" wengi wamezeeka japo wanaendelea kucheza tamthilia huku kazi kubwa ikiwa ni kuwaandaa wachezaji wengine wachanga.
Ndio maana leo utaona mtu kama Cheyo anaomba apewe viti vya ubunge free na ukimuona unaona wazi amechoka kimwili na fikra ila ni mchezaji wa siku nyingi sana na ana ukwasi anajiita "bwana mapesa".
Bosi wa TLP ambaye amewahi kuwa "Naibu Waziri Mkuu". Jamaa ambaye enzi hizo mimi napata akili aliwahi hamasisha tuandamane na mwishoni tukapigwa sisi na kwa macho yangu nikamuona anapanda gari ya RPC kwa kupigiwa saluti. Huyu jamaa yupo kwenye "payroll" nyingi za nchi hii na ni tajiri sema afya tuu mzee wetu huyu.
Vijana wengi "smart" wa walitolewa katika nafasi zao nyeti na kupewa mpunga na kuanzishwa vyama vyao huku wakipewa ruzuku na hao hao wanaowapinga. Yaani unampinga na kumtukana mtu,huyo huyo mtu ndiye anasaini malipo yenu kulipa chama chenu ruzuku kupitia msajiri wa hazina. Huku ujira wa hao "stunts" ukiwa ni ruzuku. Hawa hawana nia ya kushika dora,wao wananufaika na ruzuku na tips za hapa na pale kutoka kwa wale wanaowapinga.
Kwanza ieleweke mchakato wa vyama vingi haukuwa msukumo wetu wa ndani, ulikuwa ni msukumo wa nje maana sisi tuliukataa. Ila wakati huo ili kuendana na masharti ya mabeberu kutoka Bretton Woods ikiwemo WB na IMF chini ya mfumo wa SAP's "Elites" au "think tankers" walifikiri na kuja na mkakati wa siku nyingi wa kuleta vyama na namna ya kuvidhibiti.
Waliandaliwa watu "smart" kutoka vitengo wakapewa "mchanga" kwa lengo la kuanzisha vyama hiyo 1992.
Mtei na Makani ni miongoni mwa watu hao. Mbowe amechukua chama hicho 2000 hakuwahi jua waanzishaji wa chama hicho wana ajenda zao na wana mkono mrefu. Yeye akaja serious akakikuza chama hicho,"Elites" wakaona kijana anavuka grafu wakamchezea shere,wakawavuta vijana wake aliowapika akiwemo Boss wa ACT,alipolambishwa chambi ishu ya Buzwagi akawa hana namna akawa mtumwa wa "Elites". Elites wakawa wakaanza mtumia na wakampa mpunga aanzishe chama chama ndani ya chama. Huyo bosi ACT ana ukwasi wa kuweza kuendesha chama kichanga kusimamamisha mgombea uraisi na kumzungusha nchi kubwa kila kijiji. Hela hiyo aliotoa wapi?.
Mwaka 2015 "Elites" wakapika mpango washindane wao kwa wao. Wakafanikiwa kuwaingiza kingi CDM wakamletea EL. 2015 hapakuwa na upinzani,Chama dora kilikuwa peke yake,walishindana wale wale. 2015 mchawi "CDM" alipewa mwana amlee na akakubali. Mtoto kakua kanyea kambi na karudi kwa baba yake.
EL alikuwa na malengo mawili kwanza ajisafishe na pili alitimiza lengo la chama dora kushindana wenyewe. EL kwa sasa ni "msafi" na hafuatwi na nzi tena na unaishi "uzee mwema".
Tragedy of miscalculation inabaki kuitafuna CDM. Wakati kamati kuu inampitisha EL kuwa mgombea wao "mzee ruksa" alisema "wamekwisha" lakini sikio la kufa wakakomaa kumpiga jiki EL huku wakifurahia bilioni tisa alizokuja nazo wakijua ni zake,kumbe mwenzao alipewa huo "mpunga" na "Elites" na yeye hakuweka hata mia mbovu ya kwake.
2020 kuendelea...
Huyo dogo wa visiwani alianza kuandaliwa muda ni mpango wa muda mrefu toka enzi za Ben.
Ishu ya BM kufukuzwa na yenyewe ni trap ni mpango kama ulivyokuwa wa EL mwaka 2015.
Mtoto wa kigoma Mwandiga na yeye anadeni lile lile la kuwamaliza hawa CDM huku yeye akiwa hana mpango wa kushika dora ila kupiga ruzuku. Kazi hiyo bado hajatimiza na ndio maana Maalim amenyakwa visiwani na huku anampanga BM agombee bara.
Lengo lao ni kuwapoka CDM na CUF kitumbua "ruzuku" na kuimaliza CDM.
NATABIRI HAYA BAADA YA OKTOBA
BM ataenda ACT atapunguza kura za CDM. ACT watapewa majimbo na watapata asilimia nyingi za kura kupata ruzuku kutoka visiwani.
BM akimaliza uchaguzi chama chake watamsamehe na watamrudushia uanachama.
ZZK hatagombea uraisi mwaka huu,mpango wake ni 2025 ambapo atakuwa ametimiza lengo la kuiondoa CDM katika "key opposition" ya nchi.
Maalim mwaka huu atapata kura kiduchu sana maana CUF nao wataweka mtu kugawana kura na Huseni atapeta.
Bado tunasafari ndefu sana ya "upinzani" bongo. Aliyebuni mpango wa mwaka 1992 wa namna ya kuendesha siasa ya vyama vingi akili yake itaishi kwa siku nyingi na kwa vizazi vingi. Mpaka pale ambapo tutakuja kufahamu tunataka nini na tukafanya kazi kubwa ya kupata tunachokitaka ndipo tutapata jibu.
Wasaalam.
"Upepo ukipuliza sana uchi wa kuku huonekana"
"Ukiwa na subra utaona mwisho wa kila kitu"
Kuna mambo mawili au matatu amboyo ni msingi wa kudumu kwa vyama dola vyenye mlengo kijamaa.Sawa. Umepatia kiasi fulani ingawa humo humo yapo yanayotokea bila kutarajiwa (by chance). Kwa mfano, haikutarajiwa Freeman atakuja kuibadilisha CHADEMA toka chama cha washua (gentlemen’s party) hadi kuwa movement ya kupika vijana machachari kisiasa kiasi cha kutoa changamoto kali sana kwa CCM. Hakika sura ya CCM ya leo ni zao la kashkash za CHADEMA. Na ajabu ni chama kinachopata misukosuko ya kufisha lakini hakikati roho - kama paka mwenye roho saba vile.
Labda kama utasema Mbowe naye kapangwa na Elites kuhakikisha CHADEMA inatisha tu lakini haishindi uchaguzi. Kwamba vipigo anavyopata ni geresha tu. Aidha, tuone kama roba iliyopangwa 2020 kuikaba CHADEMA itafanikiwa kutoa uhai wote wa chama hicho.
eti ndugu zito na chama chake kichanga alitoa wapi pesa 2015 yaku mzungusha mgombea urais tanzania nzima? labda unajuaUjinga katika hii post ni Kuamini na kuaminisha wengine wote kuwa mpinzani wa kweli nchini ni Mbowe na ujinga zaidi ni kuamini Zitto alianzisha chama ili aimalize Chadema
Lakini ujinga wa mwisho katika post hii ni kushindwa kutambua mchango wa Zitto kuisimamisha upinzani uliopo nchini na kuifanya serikali isipumue
NdotoNaunga mkono hoja. Ukifikiri kwa undani kikao cha Maalim Seif na Magufuli ikulu Dar es Salaam na haya yanayotokea kwa Membe kujiunga Act utagundua kuwa ACT ni mpango maalum wa kuua nguvu ya CHADEMA.
CHADEMA kuweni makini sana Mie Nina uhakika mkimsimamisha LISSU na mkienda na agenda ya nguvu ya umma mwaka huu huu ushenzi wote uliosukwa na CCM toka miaka ya nyuma unaenda kufa na kuisha rasmi