Hakuna utamu wa pombe tuacheni kuikuza

Hakuna utamu wa pombe tuacheni kuikuza

Hivi kwanini pombe imekuwa overrated kama wachezaji wa Uingereza!!??

Naamini wengi wameingia kwenye ulevi kwa ajili ya kufata mkumbo. Na wengine kutokana na ile mentality iliyozoeleka kuwa kunywa bia ni ujanja.

Ushauri wangu hasa kwa Vijana pombe ni ujinga na haina faida yoyote.
Labda kama hujui... BIA 10 zina madhara yanayolingana na SODA 1.
Binadamu wameanza kunywa pombe kabla hata ya kuanza kulima na kufuga—kutokana na matunda yaliyoanguka na kuvunda yenyewe. Pombe ni antidepressant, na ni kweli kuwa kila kitu kina madhara kikitumiwa bila kiasi. Lakini, ukiwa na depression, hatari ya kufa kutokana na magonjwa kama shinikizo la damu, kisukari, na saratani ni kubwa zaidi kuliko madhara ya unywaji wa pombe kwa kiasi.

Unajua kuwa dawa za hospitali ndizo chanzo kikubwa cha vifo? Lakini kila mtu anakubali kuwa dawa zina faida pale zinapotumika kwa uangalifu.

Utafiti unaonyesha yafuatayo kuhusu unywaji wa pombe:

  • Wale wanaokunywa pombe kupita kiasi wanaongoza kwa vifo vya mapema.
  • Wanaofuata kwa vifo vya mapema ni wale wasiotumia pombe kabisa.
  • Wana afya bora zaidi ni wale wanaotumia pombe kwa kiasi—yaani, bia mbili kwa siku kwa wanaume na moja kwa wanawake.

Faida za kunywa pombe kwa kiasi:

Inaimarisha mfumo wa mmeng’enyo wa chakula – Kuvunda kwa pombe husaidia kuweka bakteria rafiki kwenye utumbo.
Hupunguza kiwango cha sukari mwilini – Kwa pombe zisizo na sukari, inasaidia kongosho kutochoka, hivyo kuzuia kisukari Type 2, kiharusi, na shinikizo la damu.
Huongeza nguvu za kiume – Ingawa haiongezi moja kwa moja, pombe husaidia kupunguza msongo wa mawazo na uoga, hivyo kuimarisha homoni za kiume (testosterone) na kupunguza cortisol (homoni ya stress), jambo linaloweza kusaidia kuimarisha hamu na uwezo wa tendo la ndoa.
Hupunguza hatari ya magonjwa yasiyoambukiza na kuongeza urefu wa maisha – Iwe ni kutokana na virutubisho vilivyomo kwenye pombe, kupunguza depression, au kusaidia usambazaji wa homoni mwilini, tafiti zinaonyesha kuwa wale wanaotumia pombe kwa kiasi wana uwezekano mkubwa wa kuishi muda mrefu kuliko wale wasiokunywa kabisa au wale wanaokunywa kupita kiasi.


Onyo: Unywaji wa pombe kupita kiasi ni hatari kwa afya yako. Kunywa kwa kiasi na kwa uwajibikaji.
 
Hivi kwanini pombe imekuwa overrated kama wachezaji wa Uingereza!!??

Naamini wengi wameingia kwenye ulevi kwa ajili ya kufata mkumbo. Na wengine kutokana na ile mentality iliyozoeleka kuwa kunywa bia ni ujanja.

Ushauri wangu hasa kwa Vijana pombe ni ujinga na haina faida yoyote.
Unapo sema utamu una maana gani? Utamu kwa maana ya sweetness.

Kama sio kwa maana ya sweetness basi hapa ni sawa sawa na kusema mapenzi sio matamu. Kwasababu hayana usukari.

Yote ya yote kuna vitu Kama bado haujajipata sio vya kujaribu, maana ukijaribu tu umenasa na ukishikwa na uraibu, lazima upoteze focus (dira) na maisha(mafanikio).
 
Ni
Unaposema pombe ni ujinga unamaanisha wanywaji ni wajinga, wauzaji ni wajinga, serikali iliyoruhusu ni wajinga pia.
Kuna watu wengi sana wanaendesha maisha kupitia hizo pombe.
Me sio mnywaji lakini acha kuingilia starehe za watu kama hujawasaidia kutafuta hela. Acha kabisa!
Unaingilia uhuru wao, unaingilia pesa zao, unaingilia haki zao za msingi za kisheria na kibinadamu.
Nimekuelewa Mkuu, Acha kila mtu aishi maisha yake.

Tusiopenda kutumia pombe ngoja tuendelee kuwa washamba

Oya Weita nipe coca ya baridi.....
 
Ni

Nimekuelewa Mkuu, Acha kila mtu aishi maisha yake.

Tusiopenda kutumia pombe ngoja tuendelee kuwa washamba

Oya Weita nipe coca ya baridi.....
hahaha [emoji23]
Nikiwa na stress huwa naagiza fanta kreti zima.
 
Hivi kwanini pombe imekuwa overrated kama wachezaji wa Uingereza!!?

Naamini wengi wameingia kwenye ulevi kwa ajili ya kufata mkumbo. Na wengine kutokana na ile mentality iliyozoeleka kuwa kunywa bia ni ujanja.

Ushauri wangu hasa kwa Vijana pombe ni ujinga na haina faida yoyote.
Usikute hunywi pombe, na KONDOMU hutumii
 
Hivi kwanini pombe imekuwa overrated kama wachezaji wa Uingereza!!?

Naamini wengi wameingia kwenye ulevi kwa ajili ya kufata mkumbo. Na wengine kutokana na ile mentality iliyozoeleka kuwa kunywa bia ni ujanja.

Ushauri wangu hasa kwa Vijana pombe ni ujinga na haina faida yoyote.
Ww hunywi pombe lakini huna pesa Wala nini na mkeo anakunyima unyumba unabaki unalia Lia me nala gambe na pesa kias nashika na wife nampiga triple per round...
 
Back
Top Bottom