Hali ni mbaya, Watanzania wengi wamekuwa masikini zaidi awamu hii ya sita

Hali ni mbaya, Watanzania wengi wamekuwa masikini zaidi awamu hii ya sita

Mzalendo Uchwara

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2020
Posts
4,437
Reaction score
13,836
Ukweli tuuseme tu, jahazi limeanza kumshinda mama. Sio kwa ugumu wa maisha huu!

Yaani Watanzania wanatozwa tozo ambazo hata mkoloni na roho yake mbaya asingethubutu kuwatendea namna hiyo.

Wengi wetu vipato vyetu ni vilevile, lakini gharama za maisha zimepata mara dufu! Kwa lugha rahisi tumekuwa masikini zaidi.

Ni tozo tozo tozo kila kona, wakati huohuo kila kitu kimepanda bei, uwezo wa kufikiri wa mheshimiwa waziri wetu wa fedha umegota kwenye tozo tu. Yeye na timu yake kila wakiumiza vichwa bado jibu lao ni tozo zaidi!

Ni nani anayenufaika na hali hii? Au ndio wale wafanyabishara walioitia 'sirikali' mfukoni wa awamu ilee wamerudi kukusanya vyote walivyopoteza wakati wa JPM?

RIP JPM.
 
Uchumi ni namba sio blaa blaa..

Sasa kama wamezidi kuwa maskini inakuaje kila Taasisi mapato yameongezeka na kila Wizara sasa Kazi zinafanyika na Serikali inazidi kutoa ajira..

Serikali haipati pesa kutoka hewani bali kutoka kwenye shughuli zako.Mwisho ukitaka kujua kama wamekuwa maskini au Matajiri angalia sekta ya Ujenziatumizi ya saruji na mikopo huko banks ..

Mengine ni porojo za kijinga tuu 😜😜
 

Attachments

  • Screenshot_20220817-174037.png
    Screenshot_20220817-174037.png
    89.4 KB · Views: 10
Tozo zipi hizo ambazo zinakufanya kuwa maskini?

Bora hata ulivyosema kupanda Kwa Bei,hata hivyo kupanda bei Kwa vitu ni faida kwa wauzaji lakini huwa shida ikiwa watu hawana uwezo wa kununua..

Mwisho kama bia zinazidi kuuzika na watu wanajaa Bar,kumbe maisha sio magumu kwa kiasi hicho.
 
Tuwe wawazi shida ilianzia awamu ya 5 na pia kwa sasa kuna matatizo chungu nzima yameiangukia Dunia hata kama lingekuwepo lile dubwana la Chato bado hali isingekuwa nzuri kwani budget yote ingeelekezwa kwenye machuma chuma plus mahelicopter ya ulinzi plus msako wa mtu anayeitwa Kigogo aishiye Twitter
 
Umesoma hiyo reply ya Stephen K. Membe kwa Moo na kuilewa kweli wewe!!!
Pole sana mpiga zumari.
Mapovu ni ya nini sasa..Miaka yote huwa maneno ni hayo tuu kwamba ooh uchumi unakua ila haugusi watu wa chini, something which is wrong..

Swala la msingi ni kwamba Ili uchumi uweze kuwapunguza kwa kiasi kikubwa watu wa chini lazima ukuaji uanzie 10% and above..

Point ni kwamba uchumi umeanza kukua baada ya kuvurugwa so usitegemee kila kitu kuwa sawa overnight
 
Watanzania kulilia inatusumbua sana badala ya kukaza buti. Sasa tozo gani inayokatwa hata kulalamikia mamlaka ya rais kiwango hiki. Tembea uone nchi zanazokata tozo ndio utaelewa, kuhusu maisha kuwa magumu asilimia kubwa ya watanzania tumezowea kuletewa samaki nyumbani na sio kwenda kuvua baharini. Tukazeni mikanda tuvuke mto
 
Hata enzi za Magufuli namba zilikua hivi hivi mkasema anapika data, sasa nyie hizi hamjakaanga kweli?
Enzi za Mwendazake namba hazijawahi kuwa hivi bali zilikuwa zinapikwa na walitunga sheria ya kuzuia ku challenge Takwimu zao unlike kwa sasa..

So namba hizo za Sasa zinaakisi mambo haya hapa 👇
 

Attachments

  • Screenshot_20220817-170713.png
    Screenshot_20220817-170713.png
    50.6 KB · Views: 7
  • Screenshot_20220816-203211.png
    Screenshot_20220816-203211.png
    87.3 KB · Views: 9
  • Screenshot_20220813-183141.png
    Screenshot_20220813-183141.png
    139.3 KB · Views: 5
  • Screenshot_20220814-111008.png
    Screenshot_20220814-111008.png
    180 KB · Views: 6
WaTanzania wamekutwa hivyo kutokana na viongozi wabovu hasa kwenye hii chama ya Wezi watupu! Hawana wanalowasaidia wananchi wao! Sio Kielimu Wala kimaendeleo.

Mfumonwetu wa Elimu ni mbovu kiasi kuwa mwanafunzi anamaliza masomi hajielewi na hawezi kutambua upinmwelekeo wa maisha anawaza kuiba na kufuja mali! Hata kama mwajiriwa akili iko kwenye kupata sio kuwajibika!

Vijana wengi wako hawana mwelekeo wa kesho yake!

Viongozi kuanzia chini hadi juu ni waongo asb hadi usiku. Walitaka kuabudiwa na kutoa amri! Mbunge unapewa pesa ya kufanya Maendeleo lakini zote unameza. Vijijini kwenye moto kunatakiwa madaraja wananchi wanabuka kwenye maji! Yakijaa hawana pa kuvukia. Hii ni hatari Kwa jamii!!
 
Umasikini wa nchi umeanza toka wakati wa Nyerere alipoanza kutaifisha mali za watu baadaye akaja na opareshini vijiji na mwisho alipojiingiza kwenye vita na Uganda kwa ajili ya kumpigania rafiki yake Obote kurudi madarakani na alipoona kashalikoroga akaachia ngazi na sasa tumebaki kulaumu kila kiongozi anayejaribu kusawazisha mambo.
 
Acha kuwa kama mwimba taarabu wewe# lete ushahidi
Ukweli tuuseme tu, jahazi limeanza kumshinda mama. Sio kwa ugumu wa maisha huu!

Yaani watanzania wanatozwa tozo ambazo hata mkoloni na roho yake mbaya asingethubutu kuwatendea namna hiyo.

Wengi wetu vipato vyetu ni vilevile, lakini gharama za maisha zimepata mara dufu! Kwa lugha rahisi tumekuwa masikini zaidi.

Ni tozo tozo tozo kila kona, wakati huohuo kila kitu kimepanda bei, uwezo wa kufikiri wa mheshimiwa waziri wetu wa fedha umegota kwenye tozo tu. Yeye na timu yake kila wakiumiza vichwa bado jibu lao ni tozo zaidi!

Ni nani anayenufaika na hali hii? Au ndio wale wafanyabishara walioitia 'sirikali' mfukoni wa awamu ilee wamerudi kukusanya vyote walivyopoteza wakati wa JPM?


Eeh hayati JPM rais wa wanyonge, utusamehe siye wakosefu tuliokukosea adabu na kukusemasema vibaya wakati ule, sasa yametukuta, hatujui kama kuna tumaini au hali ndio hii hadi 2030. Anyway, pumzika kwa amani, kwa maana wewe haukutuangusha ila sisi tulikuangusha.
 
Back
Top Bottom