Hali si shwari kati ya Hussein Mwinyi na Othman Masoud. Hawaelewani kuhusu suala la Muungano

Hali si shwari kati ya Hussein Mwinyi na Othman Masoud. Hawaelewani kuhusu suala la Muungano

Jamaa is very radical.

Nakumbuka kipindi kile cha kesi ya mashekhe wa uamsho alikua anawahamasisha wananchi kuwachangia mawakili wa mashehe wa uamsho.

Inashangaza mtu kuchukua upande wa mtuhumiwa wazi wazi wakati upo ndani ya serikali inayowashitaki hao mashehe.
 
Huyu jamaa nimemfuatulia vizuri sana muda mrefu tangu akiwa CCM tena kwa cheo cha mwanasheria mkuu wa SMZ.

Kama kwenye bunge la katiba aliamua kusimama na Wazanzibar na kukubali kupoteza nafasi ya AG wa SMZ ni lazima mjue huyu ni zaidi ya Maalim Seif, Maalim Seif anamzidi huyu jamaa umri tu, historia na kuwa ndio icon ya upinzani Zanzibar, sikushangaa hata kidogo baada ya kifo cha Maalim Seif ni yeye ndio akateuliwa kuziba nafasi ya Maalim ya VP.

Na kwakuwa Rais wa JMT ni Mzanzibar huyu jamaa hakuna wa kumnyamazisha, awamu ya sita ndio ya kuclear dhuluma zote walizofanyiwa Wazanzibar.

Mkuu Maalim Seif alipoteza cheo cha Uwaziri Kiongozi ambacho ni kikubwa zaidi kuliko alichopoteza huyo jamaa. NA akakaa ndani miaka miwili 2 .
Maalim Seif ni habari nyengine kabisa.
 
Huyu Othman anajua idadi ya wazanzibari walioko huku Tanganyika na biashara zao?
Muungano ukivunjika hawa wote watalipa vibali vya ajira.
 
Kwahiyo unataka tuwaache ili waikaloe zenji..muungano unamapungufu yake sana..ila kuipa uhuru kamili zenji ni kuhatarisha maisha ya watanganyika.

Tunazijua itikadi hizo zikikita mizizi..

#MaendeleoHayanaChama

Halafu nawewe unajiita mwana mabadiliko. Dah kwa kweli Tanzania kukomboka bado sana.
 
Tatizo wanzanzibar mnajikaanga wenyewe kwa wenyewe. Bara kazi yao ni kuwaletea kuni na kuwaacha nyie mkoke moto, muinjike sufuria, muweke mafuta na kujikaanga wenyewe. Sasa hivi rais ni kutoka Zanzibar, kwa nini asikubali mabadiliko ya katiba yatakayozingatia maslahi ya wazanzibar wanayodai? Bungeni Dodoma mnaenda kufanya nini kama mnaona muungano haufai? Nachelea kusema malalamiko yenu ni visingizio baada ya uongozi wenu kushindwa kuwaletea wananchi wake maendeleo. Punguzeni kula urojo na viongozi wenu waache kutumikia serikali ya muungano na mjiongoze wenyewe kama mnadhani mambo ni rahisi sana.

Kuwa Raisi sio hoja toshelezi, tatizo ni mfumo na sio Raisi. Hata yeye Raisi akiamua, Kuna TISS, JWTZ na Baba yao CCM wote watamshuhulikia mapema sana. Hivo vyombo vitatu ndivyo vinavyoulinda huu Muungano uchwara kwa hali yoyote. Sababu kuu ya katiba ya Warioba kukwama ilikua ni suala hili hili la Muungano.

Suala la muungano litatuliwa na wananchi wenyewe kwa umoja wetu tukiamua kutumia People's Power. Hakuna option nyengine.
 
Wazenji wengi hawana fahamu kuwa Muungano huu ni "iron-clad" yaani hauvunjiki sababu waliouanzisha ni marehemu kwasasa.

Wapiga kelele kama hao kina Othman ni kuwatumia "watu wasiojulikana" tu wapelekwe chocho na kutulizwa!
Ukiwatumia "wasiojulikana" ili wapelekwe "chocho", basi nyie wapeleka watu chocho ndiyo mnakuwa mmeshindwa na sio wakweli. Kuua/kupoteza watu sio suluhisho, bali ni ushenzi na uwendawazimu kwa wafanyao hayo...!!

Permanent Solution ya hii kitu inayoitwa "muungano wa Tanganyika & Zanzibar" ni kuipeleka kwa wananchi kwa njia ya "referendum" na swali liwe moja tu tena liulizwe kwa uwazi "unataka muungano au la" basi

Kabla ya watu kuamua, kampeni za wazi zifanyike na kila upande utetee NDIYO au HAPANA kwa kutoa sbb za kushawishi wananchi ili waamue ..
 
Ni ngumu sana kuvunja muungano huu, ni ngumu sana tena sana tu.

Familia karibu zote za Wazanzibar wana ndugu Bara, tumechanganyika sana.

Nimeishi Zanzibar kwa miaka 2 hivi, wenye shida kubwa ni Wapemba, ila hawa wa kutoka unguja hawana tofauti sana na wa Tanzania Bara, ni kama watu wa Kilwa tu. Kule Pemba ndio wao hujiona kama wanaonewa na hawaoni umuhimu wa Muungano.

Hizi chokochoko zina nguvu zaidi PEMBA na si UNGUJA.
 
Huyu Othman anajua idadi ya wazanzibari walioko huku Tanganyika na biashara zao?
Muungano ukivunjika hawa wote watalipa vibali vya ajira.

Mkuu unajua kuna watanganyika wangapi walioko Zanzibar?
 
Wazanzibar wanaotaka kujitenga ni wahuni tu Kwa Sababu kihalali Watanganyika ndo wanaunizwa na huu muungano Watu wanamiliki uchumi wa Tanganyika halafu Leo wanajiona wanjanja na kuanzia kulia eti wanaonewa huu ni ujinga tu .
 
Chuki zenu haziwez kufichika kamwe
Jamaa is very radical.

Nakumbuka kipindi kile cha kesi ya mashekhe wa uamsho alikua anawahamasisha wananchi kuwachangia mawakili wa mashehe wa uamsho.

Inashangaza mtu kuchukua upande wa mtuhumiwa wazi wazi wakati upo ndani ya serikali inayowashitaki hao mashehe.
 
Hakika ujinga wa uzeen lazma utakufa nao tu
Wazanzibar wanaotaka kujitenga ni wahuni tu Kwa Sababu kihalali Watanganyika ndo wanaunizwa na huu muungano Watu wanamiliki uchumi wa Tanganyika halafu Leo wanajiona wanjanja na kuanzia kulia eti wanaonewa huu ni ujinga tu .
 
Wazenji wengi hawana fahamu kuwa Muungano huu ni "iron-clad" yaani hauvunjiki sababu waliouanzisha ni marehemu kwasasa.

Wapiga kelele kama hao kina Othman ni kuwatumia "watu wasiojulikana" tu wapelekwe chocho na kutulizwa!
Ndio mnaloweza tu hilo lá wasiojulikana washenzi wakubwa.

Hakuna mzanzibar anaehitaji muungano isipokuwa hão mliowaeka ili kutimiza matakwa yenu ya kiunyonyaji na kwanini mng'ang'anie wakati hampati faida mnayoipata huko znz.

Sent from my SM-N9150 using JamiiForums mobile app
 
Kwa maoni yangu, huyu mtu anatakiwa awekwe pembeni, apate muda wa kutosha ajishughulishe na siasa, kwasababu ACT ndani ya GNU wanatakiwa kutekeleza Ilani na sera za CCM!.

Ushauri kama huu kumhusu mtu huyu huyu niliwahi kuutoa kule nyuma na ukatekelezwa, Dr. Shein Mfute Kazi Haraka, Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Kabla Hajamwaga Sumu Hii

P
Hayo ndio mawazo mgando mtu akiwa tofauti ya maono na nyinyi hafai. Nanllomo.

Sent from my SM-N9150 using JamiiForums mobile app
 
Ndio mnaloweza tu hilo lá wasiojulikana washenzi wakubwa.

Hakuna mzanzibar anaehitaji muungano isipokuwa hão mliowaeka ili kutimiza matakwa yenu ya kiunyonyaji na kwanini mng'ang'anie wakati hampati faida mnayoipata huko znz.

Sent from my SM-N9150 using JamiiForums mobile app
Wewe huoni faida ya umoja amani na undugu..kingine bahari na vilivyomo.

Muungano unafaida nyingi..mpungufu yaliyopo yalekebishwe tuwe na serikali moja ama tatu.

#MaendeleoHayanaChama
 
Na kwakuwa Rais wa JMT ni Mzanzibar huyu jamaa hakuna wa kumnyamazisha, awamu ya sita ndio ya kuclear dhuluma zote walizofanyiwa Wazanzibar.
Huyu atawasumbua sana CCM kwa ujinga wao tu, wa kuamini kwamba njia nzuri ya kunyamazisha upinzani ni ku'appease', kama kutoa hongo za nafasi za uongozi.

Njia hiyo ilikuwa ikisaidia wakati wa Maalim, lakini siyo kwa huyu Othman.

Njia nzuri ya kushughulika na huyu ni kumkabili na kupambana naye moja kwa moja bila ya kupepesa macho mbele za wananchi kwa kueleza manufaa yanayotokana na muungano. Ni kupambana naye kwa hoja wananchi waamue wenyewe. Wakishaelewa vyema, watampuuza. Akikosa 'platiform' amekwisha kazi.
 
Huyu si hardliner ni kwamba hautaki muungano. Ukisikia kauli zake utashangaa sana

Rejea clip ya pili ya bandiko#6 anatukana na kusema Tanganyika ni wagonjwa wameziba njia za Zanzibar
OMO hajui gharama za ving'ora anavyozunguka navyo, usalama wa nchi wa mipaka na ndani n.k.

Wachina hawataki kuipa Zanzibar kwa kuchelea kuwa haidhaminiki kwa uchumi wake.
Yeye anasema Tanganyika inawazibia, akili za jabu sana, kwamba izibe Zanzibar isikope kwa faida gani.
Kauli zote hizo ni kuchochoea kwamba Zanzibar inapunjwa ingawa haelezi kwa lipi bali lalama tu

Kuna watu waliojificha lakini hawataki muungano. VP OMO, Ali Salehe na yule wa London Rajabu
Jitokezeni mpige chapuo kura ya maoni. OMO katoa mfano wa Scotland katika jitihada za kuwaambia Wazaznibar wadai kura ya maoni. Tatizo lake hasemi wazi anatumia code na kuzua uongo dhidi ya Tanganyika

OMO waambie ACT wasidai tume ya uchaguzi au katiba mpya, Wazanzibar wadai kura ya moni tutawaunga mkono 100%
Anatumia udhaifu wa CCM kujibaraguza hivi.

Huu muungano ulipoanzishwa, ile ilikuwa ni hatua ya mwanzo tu. Lengo lilikuwa ni kuendelea kuuimarisha kadri watu wa pande mbili walivyoweza kushirikiana na kuelewana.
Badala ya kufanya juhudi kuuimarisha muungano, CCM wakazembea, na kundi lililokuwa halitaki muungano huko visiwani likapamba moto na kuanza kulegeza/kudhoofisha badala ya kuimarisha muungano.

CCM wakadhani njia bora ya kuwatuliza hawa ni kuwakubalia mambo waliyodai. Kila walipowapa jambo moja, wanaanza kudai la pili. Sasa wamefikia hatua ya kudai uhuru kamili, yaani kuvunja muungano.

Sioni kiongozi mwenye uwezo wa kuwakabili hawa kwa wakati huu, na kelele zitakuwa kubwa sana, hasa wakati huu wa Samia.
 
Huyu ni katika wanafunzi wa Siasa Maalim Seif kama ulikua hulifahamu. Hapo akiwa na Ismail Jussa wakiwa wadogo sana.
View attachment 2280695
EeeeenHeeee!

Ahsante kwa taarifa, na hasa hiyo picha.

Lakini si mwanafunzi hutokea akamzidi mwalimu wake? Ni nadra sana kumpata mwanafunzi akawa 'replica' wa mwalimu aliyemfundisha.
 
Kwahiyo unataka tuwaache ili waikaloe zenji..muungano unamapungufu yake sana..ila kuipa uhuru kamili zenji ni kuhatarisha maisha ya watanganyika.

Tunazijua itikadi hizo zikikita mizizi..

#MaendeleoHayanaChama
Fear of the unknown...

Ndio nyie mnaogopa kuiondoa Ccm madarakani kwa kuinyima kura mkiogopa upinzani kushika dola.
 
Back
Top Bottom