Uchaguzi 2020 Hali si shwari ndani ya CCM, Katibu Mkuu wa CCM Ndg. Bashiru Ally amekemea vikali baadhi ya wanachama wanaopanga kukisaliti chama

Uchaguzi 2020 Hali si shwari ndani ya CCM, Katibu Mkuu wa CCM Ndg. Bashiru Ally amekemea vikali baadhi ya wanachama wanaopanga kukisaliti chama

Bashiru aongee na mwenyekiti wake awe na adabu kwa wanachama na wananchi waliomchagua; hakujifanya yeye kuwa mwenyekiti/rais
Inawezekana "wanasiasa" kuwa wamewekwa pembeni na nafasi zao kujazwa na "wasomi" kukakigharimu chama hicho.
 
Kufikia hapo wacha na mimi niwe msaliti tu, Bashiru nakusubiri baada ya tarehe 28 October
 
Nimesoma mahali Bashiru kawa mkaki, anasema watawashughulikia wasaliti wote baada ya uchaguzi, yani hawa jamaa wanawaona wanachama wa CCM ni kama mbuzi tu, wawekee majani hapo watakula, wanasahau wale ni wanadamu wana utashi wao na maamuzi yao, ubabe wa kina Bashiru lazima utawa-cost dearly kwenye sanduku la kura.
Kwasababu hawatashinda, ndio chama chao kitasambaratika chote. Ndio utajua waTanzania walikuwa wanavumilia tu na uvumilivu unao mwisho wake.
 
Ulishasikia wakatoliki wangapi wamekufa kwa kuichagua Democrat.
Mkatoliki anayeshabikia utoaji wa mimba na akashindwa kupinga hadharani anakufuru na ana hatari ya kupoteza roho yake. Na hatakiwi kupokea ekaristi. Hapo sikusema kufa ila maana ya kupoteza roho yake.
 
Mkatoliki anayeshabikia utoaji wa mimba na akashindwa kupinga hadharani anakufuru na ana hatari ya kupoteza roho yake. Na hatakiwi kupokea ekaristi. Hapo sikusema kufa ila maana ya kupoteza roho yake.
"Based solely on the party platform, no Catholic may vote for any Democrat without danger to their immortal soul" Fr. Jeffrey Keyes.
 
Mama Samia suluhu kachokoza nyuki tunduni...kapokea waunga juhudi wapya ...kituko ni pale hao wanachama wapya waliovutiwa sana na sera na ilani ya ccm wote wanatoka CHADEMA. Mama Samia tunakupenda sana lakini epuka hizi ghiliba hazikisaidii chama bali zinazidi kukiangamiza

TAL ni game changer...atafanya yake kuelekea count down ya uchaguzi mkuu October...atafanya zoazoa mpaka wale wa majalalani
Ulishawahi kuona mbusi mee anakula makaratasi? Tena anayanyofoa toka yalipobandikwa? Mfahamuni mnyama mbuzi beberu kiroho ni nani..Mbuzi kachana tangazo la kampeni la kiongozi anayejifanya ni mtu wa Mungu sana.

Ulishawahi kuona mtu anasema MUNGU OYEE...!? Mungu si mwanasiasa ! Mungu si binadamu... Huku ni kuchanganyikiwa.....kadiri joto la uchaguzi linavyozidi kupanda nyoka wanatoka pangoni mmoja baada ya mwingine ..mwishowe watatoka kwa makundi

Makinikeni enyi chama cha majalala...MATAGA wengi wameshaanza kujivua gamba. Yale ya BBC yanatisha..yanakarahisha...yamefunua nyeti za mtu mbele ya wageni na wakati mbaya mno...kama mnadhani TAL ni EL fikirieni tena mara 7....BBC KASEMA WAZI..TUMEPIGWA!!!! Hakuna majigambo tena hapa!

Fukuto la uchaguzi linavyozidi kupanda...nyumba ya MATAGA innazidi kupata joto.

Yajayo ni historia ya kimbunga
 
Wee naye eti mchambuzi wa siasa, bure kabisa wewe kijana,huna ulijualo kuhusu hii nchi ,wewe endelea kuwa punda wa lissu lakini kwa CCM umeula wa chuya
 
IMG-20200919-WA0086.jpg
 
Unapoteza werevu tuluokuwa tunaofahamu. Umeandika kitaarabu sana mzee samahani kama takuwa nimekuudhi
 
Back
Top Bottom