Hali ya kiuchumi Arusha inazidi kushuka kila uchwao

Moshi naku-support ndio maana ule mji umedoda una wakazi 221,000 mpk leo ukiziwa na miji ya juzi tu km Geita n.k. Wachaga ni wabinafsi mno na wabaguzi. Arusha hawana ubavu ndio maana uongozi wa kisiasa kuupata ni vigumu.
Sio wabinafsi wala wabaguzi hawa ni watu walioleta biashara na maendeleo kila kona ya nchi wangekuwa wabinafsi na wabaguzi wangefanya maendeleo yote kule Moshi na mji huu ungekuwa mkubwa kuliko Dar! Unapaswa kutambua kuwa mahali walipokimbia watu hawa hakuna mwingine anaweza kustawi pale!
 
KWA KUMBU KUMBU ZANGU,
WALIONDOLEWA WABUNGE WA UPINZANI KWA NGUVU, YA HILA NA POLISI.
YOTE HII NI KULETA MAENDELEO KWA WANANCHI
NI NINI TENA KIMETOKEA?

NA BADO MNA UJASIRI WA KUIMBA NYIMBO ZA KUSIFU NA KUMTUKUZA MAMA!!!
 
Uyo chizi anasema ukikaa mwaka mmoja unawajua wakazi woteπŸ˜€πŸ˜€
Ni muongo, labda uwe kizurule 24/7 hutulii kwako na huna kazi za kufanya
 
Tuache ubishi, kesho tukutane Florida saa tano ukanioneshe hiyo nyumba ya vyumba vitatu ya 150k, mimi nitakupa 200k. Njoo inbox nikupe namba ya simu tuwasiliane.
Na kwanini ukae florida? πŸ˜‚ ukae unashindana na honi asbh za kina BM!!
 
Kilicho kutoa kwako ukaenda Arusha nini?
Rudi kwenu au nenda mji/jiji unalopenda kwan umeshikiwa kisu kubak Arusha??

Njoo namanyere kuna fursa nyingi sana
Kazi kutupigia kelele mara dar kuchafu mara Arusha hakuna hela pumbavu mkubwa wewe

Njoo huku ulambe asali laiyoni wewe

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Kodi ya laki na nusu kwa nyumba ya self contained kwa Arusha pale city centre tena nyumba ya vyumba vitatu kwakweli mleta mada unadanganya.

Halafu wali kuku wa buku, hiyo bei naamini wahenga wenzangu watakubaliana nami ni ya mwaka 1990 kurudi nyuma.

Ni kweli hali ya uchumi ni mbaya ila sio kwa kiwango hicho mkuu.
 
Endelea kujidanganya, kinachosemwa watu wamekipitia, kwaiyo usilazimishe mtazamo wako ndio uwe uhalisia, halafu swala la walipopakimbia wachaga mwengine hawez huo ni uwongo, saiz kriakoo mkinga na mbena wanawakimbiza wachaga, na kule kwao nyanda za juu kusini(iringa, mbeya, njombe, sumbawangq, songea, tunduma) ndio kabisaaa wanatawala kila kitu.
 
Hali ya mzunguko wa fedha imeshuka. Sio Arusha tu Tz nzima. Watu badala ya kujadili mada husika wanaanza ushabiki kama kawaida.
 
Acheni Uchawi na Wivu ...mawazo ya Kimaskini na roho mbaya....niko hapa Picnic nazimuwa vumbi la Serengeti
 
ppf kuna nyumba ya laki tatuπŸ˜ƒπŸ˜ƒπŸ˜ƒπŸ˜ƒπŸ˜ƒπŸ˜ƒπŸ˜ƒπŸ˜ƒ
 
Ni wivu tu mnaionea Arusha
Licha ya serikali kuutelekeza huu mji kutokana na siasa za upinzani
Bado Arusha ndio the best place in Tz weather + hakuna misongamano
Ndio mji kinara kwa kupokea watalii na kuingiza fedha za kigeni
Leo hii mji kama mpanda na sumbawanga kuna stendi za kisasa Arusha ni jiji lakini hakuna kitu sad
Ipo siku tu na sisi tutapata hiyo miundombinu na sisi
Maana halisi #genevaofAfrica

View: https://youtu.be/eoO1KzFNE4s?si=Z0NEZBTyvkdadM8V
 
Baada ya dar na dodoma, Arusha ndio mji unaobebwa na serikali, nenda mbeya ukapate picha ya miji iliyotengwa na serikali
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…