Hali ya maisha ya Mtanzania ni ngumu sana. Rais asipochukua hatua sasa hali itaendelea kuwa mbaya zaidi

Hali ya maisha ya Mtanzania ni ngumu sana. Rais asipochukua hatua sasa hali itaendelea kuwa mbaya zaidi

Mapori still yapo mengi tza hatuna tatizo la overpopulation,watu waendelee kuzaa tu.ukitoka tu kibaha kilometer 3 nje ni mapori tupu.
Tuache kukaa mijini,fursa zipo maporini huko
Wewe upo huko maporini au wote tumebanana hapa hapa Dar?
 
Nilimsikia akisema anakopa ili afanye kitu cha kuacha alama, hivi legacy inajengwa kwa kuacha daraja kubwa au flyover!? Nyerere aliacha legacy dunia nzima kwa aina ya uongozi, fikra na falsafa zake, leo legacy imekuwa kuacha miradi mikubwa mikubwa kwa gharama ya kuacha nchi kwenye madeni yasiyotamanika.

Hivi kweli hii ndiyo namna ya ku-manage uchumi kwenye nchi maskini kama Tanzania! badala ya kuwekeza kwenye maendeleo ya wananchi walio wengi unaenda kuwekeza kwenye mamiradi yasiyo na kichwa wala miguu yanayotumia pesa nyingi, kununua ndege kwa cash, bila kusahau matumizi ya anasa ya serikali maviieite huku ukikamua hata savings ndogo za watu kwa njia ya tozo.

Ajira hazitolewi, mishahara haieleweki......pesa zinaenda kulipa mikopo iliyochukuliwa kwa pupa.​
Unapigia mbuzi gitaa tu. Nafikiri kenge hasikii mpaka atoke damu sikioni baada ya kupigwa hasa.
 
Lini ushawahi kuskia mtanzania anasema maisha mazuri? Mwanadamu haridhiki hata umpe nini, hizi kelele za kawaida tu
Kweli kabisa, kila awamu ilikuwa na itaendelea kuwa na walalamikaji.

La muhimu mtu afanye kazi ajitahidi kujikwamua kwa mipango yake mwenyewe
 
Viongozi wa juu Serikalini wananufaika na Ugumu wa maisha wa Raia.

1. Unapolipa vat kwenye bidhaa madukani, Serikali inapata pesa za kununua mafuta kwenye V8 za viongozi.

2. Unaponunua Mchele 3,500 Kwa kilo, jua Basha anatunisha mfuko kwenye Kampuni zake za kuuza nafaka Kenya na somalia.

3. Unapolipa 55,000 nauli ya Dar Mwanza, Kuna kampuni ya mwigu na wenzie kupitia Mama Esther wanatajirika kupindukia.

4. Unaponunua maji 500 Kwa ndoo moja, uwe na HAKIKA Wizara ya maji wanatumia mwanya huo kuomba pesa hazina kutatua changamoto hiyo, na pesa zikitoka ZINAPIGWA.

5. Unaponunua bundle la internate Bei juu, Pena anapata posho Kutoka makampuni hayo, ananufaika na Bei ya vifurushi kuwa juu.

6. Unaponunua mafuta ya kupikia Lita Tano Kwa 30,000 uwe na HAKIKA Kuna TOZO na Kodi zaidi ya 5000 Kwa Kila dumu imeingia Serikalini na inatoka Kwa matumizi ya kawaida ya viongozi.

Serikali haiwezi kupunguza mzigo wanaoubeba raia, sababu kwao sisi ni chanzo Cha mapato Yao.

Tuungane kudai KATIBA mpya itokanayo na Rasimu alosimamia Judge WARIOBA Ili kuondoa mifumo kandamizi inayoumiza wengi kuhudumia Wachache.

Amen
Maneno bora kabisa. Tumeongea sana na sasa kilichobaki ni actions.
 
Hivi tunavyoongea maandamano yameanza kiripotiwa mataifa mbalimbali,

Endeleeni kupuuza sauti za Raia, itawatokea puani,

Mnapandisha Bei ya mbolea, na mbolea wanauziwa madalali Si wakulima halafu mnawambia wakalime,

Wakivuna mazao mnawalangua Kwa Bei chini na mnaweka Kwa maghala na kuuza nje ya nchi,

Hii ni 2023, mtatoka mapangoni mlikojificha. Hali inayoendelea haitapita hivi hivi,

HUKUMU juu ya viongozi waovu imeamriwa.

Tusubiri.
Hatutaki tena maneno tunataka actions
 
Hatutaki tena maneno tunataka actions
Ktk suala la KATIBA mpya, tutatoka wengi mno makundi mbalimbali.

Hamasa na Elimu iendelee bila kuchoka.

Watu waelimishwe Kwa staha na upole jinsi Gani Katiba mbovu iliyopo inavyohusika kuwabebesha mzigo mzito wananchi Ili kuwanufaisha kundi dogo.

Tutashinda. Amen
 
Ee Mungu nipe hekima yako niweze kuandika kitu kitakacho weza kuwapa uwelewa viongozi wenu juu ya Hali ilivyo mbaya kwa wananchi wake [emoji120][emoji120][emoji120][emoji120]

Awali ya yote Samia mama naomba elewa Hali za Watanzania ni mbaya Sana na inatisha kweli kweli [emoji24][emoji24][emoji24]

Tujiulize sisi kama taifa tumemkosea wapi Mungu na je viongozi wetu hamuoni jinsi wananchi wanavyo teseka

Ukitaka kujuwa udhaifu wa mtu mtese usimpe chakula nyie kama viongozi juu ya hili mmeliweza wananchi hawana chakula kabisa

Swali la kujiuliza mama hivi kweli shilling 10000 haitoshi kabisa Kwa bajeti ya siku kwa familia mfano mdogo tuu nikuonyeshe mama

Familia yenye watu 5 tu baba mama na watoto 3

Asubuhi baba aache 10000

Asubuhi wanunue vitafungwa tu 2000
Watoto wapewe nauli za shule 1000×3=3000 hii ni nauli pamoja na hela ya kula shuleni
Mchana mama haha chochote labla mama amejikaza kanunuwa mihogo ya 1000 na bibi nyingi Akala

Mfukoni imebaki 4000 je hii hela itatosha kwa chochote kile ila waweze kula jioni

Mchele kilo ni 3500
Mafutaa pishi ni 500
Mkaa 2000
Mboga za majani 1000
Nyanya +karoti + kitunguu 2000

Je swali kwenye Ile 10000 baba alio acha asubuhi imebaki shingapi

Naomba ujue kitu kimoja mama watu wanao umia juu ya huu mfumuko wa bei ya chakula ni wananchi wa chini sio wa juu [emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]

Je wewe kama RAIS una waza juu ya hili just imagine wewe unatumia shingapi kwa siku juu ya chakula jaribu kuchukuwa 10000 alafu ujaribu kuibajetia kama itatosha kwa chochote kwanzia asubuhi Hadi jioni

Ushauri wangu huu ni Muda muafaka wa serikali kusitisha kuuza nafaka nje mama naomba achana na Bashe kabisa huyu ni mfanyabishara mkubwa wa mahindi Kenya na wewe unalijuwa Hilo

Tueni Yale mazao yaliyopo kwenye ghala la taifa yauzeni kwa bei nafuu maana Hali ni mbaya mtaani huku

Wekeni mikakati ya kuboresha sekta ya kilimo kwa kuwapa vijana mikopo wakalime ili kukabiliana na hili tatizo la njaa siku za mbeleni huko

Ukiendele kufubaza shingo juu ya hili nililo kuambia tutakumbana na baa la njaa ifikapo mwezi wa 6 mwaka huu

Pia angalia mishahara ya watanzania sio rafiki kabisa na Hali ya uchumi ilivyo

Una mlipa mtu 300000 kwa mwezi huyu mtu kulingana na hesabu ya siku anapokea 10000 hapo bado hajalipa Kodi, NSSF anabakiwa na shingapi hapo lakimbili na nusu je hiyo laki mbili na nusu itatosha kumwendesha maisha kwa mwezi mzima embu fikirieni juu ya hili

Boresheni mishahara kwa sector zote private sector hawajaongezewa hela Hadi saa hizi Ina maana Hawa sio Watanzania je gharama za maisha zimepanda kwa wafanyakazi wa serikali tuu

Mnakwenda kutengeneza kizazi ambacho ni hatari sana Kwa hili taifa

Hakuna ajira Kwa vijana na wanao hitumu ni wengi je Nini kinaenda kutokea Hadi ifikapo 2035

Sina mengi ya kuyasema zaidi ya hayo kwa unyenyekevu mkubwa na shukuru mwenyezi Mungu kwa kunifungulia haya na kuyaona na kukueleza mama nimekuwa mnyenyekevu kwako kwaajili ya watanzania wote [emoji120][emoji120][emoji120][emoji120][emoji120]

Kingine japo sio Cha mwisho angalia mama swala la vifurushi vimekuwa ni hatari sana

Shilingi elfu Moja unapata MB 490 mama hii sio Haki kabisa nape ni kidonda katika hii wizara haiwezeka kuwa hivi mnawanyosha Sana wananchi wa chini SEMA neno Moja juu ya hili swala na hakika utarejesha matumaini kwa wananchi wa Hali ya chini

[emoji120][emoji120][emoji120]
Hivi Kuna yule Mama Mkurugenzi Mkuu wa NBS,kile cheo ni cha Ki-Chief?
Yule mama takwimu zake zimejaa uwongo mwingi sana,hivi ni kweli kwa mfumuko huu wa bei za bidhaa,ni 4.9% kweli [emoji1787].
Mimi naona mfumuko wetu wa bei upo kati ya 10% na kuendelea.
 
Nadhani auwajui Watanzania, hii inabaki tu kama hadithi uliyoisimulia siku ya leo.

Na bi samia na ccm yake wala hawajali na hawana hofu kwani wanatujua hatuna mpango wa kudai haki zetu dhidi ya haya maumivu.

Umeibaini standard ya hiyo elimu watoto wanayoifuata?? Ni uchafu mtupu, ndio huo unaotupa div4 na zero kwa 80%, na km hatuko tayari kutoka nje kuwaeleza watawala juu ya matendo na uovu wao dhidi yetu basi tutulie makalio yakiwa juu ili sindano zituingie haswaaa.

Overrr
Mama anapambana na Gridi ya taifa ya umeme chini Engineer Kipara Makamba kwa gharama ya Bilioni 500 badala ya kupambana na inflation!!
 
Gharama za maisha zimepanda ni matarajio yangu serikali ingekua imeshapeleka muswada wa kuongeza mishahara ya wafanyakazi. Na ni mategemeo yangu bajeti mpya itakwenda kuongeza mishahara na kima cha chini
Subirini Mama afumue Gridi ya taifa ya umeme,bei zitashuka tu!
Leo yupo Ikulu ya Magogoni anasainisha mikataba ya Bilioni 500 na Wakandarasi!
 
Aliyeshiba hamjui mwenye njaa, wahenga walisema. Tuombe tu Mungu, mvua za masika zinyeshe maskini tuweze kujipatia chakula chetu.

Pia kumbuka damu ni nzito kuliko maji, huyo bwashee hawezi kufunga mipaka wakati ndugu zake hawana chakula. Sana Sana atawahimiza waje wakati wa mavuno, waingie mpaka huko vijijini ndani ndani wakusanye shehena ya kutosha na wasafirishe makwao.
Hizi mvua tu zikikata kabla ya swala hata la chakula kuwa ghali, mabwana TANESCO watawaletea story kwamba maji yameisha hivyo watakata umeme siku nzima.

Wenye wanauza vitu vya kuhifadhiwa kwenye friji wakatafute kaz nyingine
 
Haya uliyoandika hapa yangekuwa yamekamilika kama ungeonesha role ya serikali, na vipi serikali imetimiza wajibu wake kufanikisha hilo. Nakuona unaendelea kuficha madhaifu ya serikali kwenye hili suala, naamini sababu inayokufanya uwe hivyo ni ile ile asali.

Kuwaambia watu waache kukimbilia kazi nyepesi za kubangaiza, wakati ndizo zilizopo, kwasababu serikali imeshindwa kuwapa wahitimu wa vyuo kazi nzito unazotaka wafanye, ni kuwaonea wapambanaji, show some respect!.

Serikali inayojielewa, ikishatambua changamoto wanazopitia raia wake, lazima itafute namna ya kuwapunguzia maumivu, mfano, serikali ikishajua raia wake wengi wanafanya kazi nyepesi, zinazowapa kipato kidogo, ni lazima ifanye iwezalo kupunguza mfumuko wa bei, hawa wapambanaji hawawezi control hilo.

Zaidi, unaposema watu watazame family planning, hapa napo unatengeneza tatizo jingine mbele ya safari, tunaona kwenye baadhi ya nchi zilizoendelea, hata kama teknolojia inayowarahisishia kufanya kazi zao, usiyatazame haya mambo kwa jicho la upande mmoja.
Kama umezoea sijui asali, kuhongwa, kusaidiwa, usidhani ni wote. Sisi wengine tumefika tulipo kwa kupambana hasa, kwa kutambua thamani ya muda, kuyatafuta maarifa kila yalipo, na kuhakikisha wakati unatafuta the highest productivity katika kila unachofanya.

Ndiyo maana nyakati zote, hata uje utawala gani, hutasikia nalalamika eti nimeshindwa kuyapata mahitaji ya muhimu ya familia.

Sina ubia ndani ya Serikali, sina wa kumtetea kulinda udhaifu wake ndani ya Serikali ila nautambua wajibu wangu kama myu binafsi kwa nafsi yangu, familia yangu na jamii. Wajibu wa Serikali unafuata baadaya wajibu wangu.

Nimeishi katika nchi 8 za Afrika, 2 za Ulaya, 1 ya America ya Kaskazini, 2 America ya Kusini, na 2 za Asia. Kote huko, ukiondoa Australia, usipopambana, maisha mazuri utakuwa unayasikia tu kwa wengine. Mishahara ipo juu lakini bei za vitu zipo juu sana. Australia, maji ya kunywa yanauzwa kwenye chupa kama za soda, bei unaambiwa ni dola 3 za Australia, karibia dola 2.5 za Marekani. Hiyo ni zaidi ya sh 5,000 za Tanzania. Ukiwa wa kulalamika tu, unadhani utaweza kuyanywa hata hayo maji? Japan, kuna watu wanafanya kazi mpaka kwa waajiriwa wawili ili apate pesa ya kutosheleza mahitaji yake.

Anayejua mahitaji yake ni wewe mwenyewe, siyo Serikali. Ujiwekee msimamo wa kuhakikisha maisha yanaenda hata pale ambapo ulichokitegemea toka Serikalini hukipati.
 
Ktk suala la KATIBA mpya, tutatoka wengi mno makundi mbalimbali.

Hamasa na Elimu iendelee bila kuchoka.

Watu waelimishwe Kwa staha na upole jinsi Gani Katiba mbovu iliyopo inavyohusika kuwabebesha mzigo mzito wananchi Ili kuwanufaisha kundi dogo.

Tutashinda. Amen
Kuwa na katiba mpya siyo dili sana, issue ni je, itafuatwa? Inaweza ikawepo na watu wakaendelea kuisigina tu. Hii tu inasiginwa sembuse katiba mpya? Kuna muarobaini upo mahali ila si katiba mpya.
 
Kuwa na katiba mpya siyo dili sana, issue ni je, itafuatwa? Inaweza ikawepo na watu wakaendelea kuisigina tu. Hii tu inasiginwa sembuse katiba mpya? Kuna muarobaini upo mahali ila si katiba mpya.
Mamlaka makubwa ya Rais ndo mzizi wa fitna, mengine yafuata.
 
Brother tafuta shamba Lima mandindi hekari 1 utapata gunia 30
Lima mpunga utapata gunia 40
Lima maharage utapata gunia 9

Mungu katupa mvua na ardhi
Wewe umekaa kulia lia ujinga ujinga
 
Ukiona hali inazidi kuwa mbaya, tazama mahitaji ya familia yako, ili uone yale yasiyoyalazima uyaondoe.

Mahitaji mengine huwa tunayaendekeza kwa sababu za kimazoea tu, kama vitafunwa asubuhi, muhimu washibe asubuhi, watashiba nini na vipi, jiongeze baba wa familia kwa kushirikiana mawazo na mama yao, wanawake wengi huwa wako vizuri kwenye budget.

Muache Samia apambane kwenye ngazi ya taifa, wewe pambana na mwenzio kwenye ngazi ya familia.
Ushauri mzuri
Yeye apambane ngazi ya familia
Kulalamika ni ujinga tuu kichwani
 
Back
Top Bottom