Halima Mdee: Serikali iache kukimbilia kukopa inadumaza akili

Halima Mdee: Serikali iache kukimbilia kukopa inadumaza akili

Halima ana haki ya kuongea lakini ukweli ni kwamba Yeye yuko vizuri anafaidi keki ya Taifa.

Leo hii ukitaka kupeleka miradi kwa haraka Ili iwe na tija lazima ukope,na uzuri wa Kukopa unalipa taratibu bila maumivu na Kwa mda mrefu na pia inaweza wewe usilipe wakaja kulipa wengine.

Hii ya eti inalemaza ni kitu kigumu kuelewa inalemazaje wakati unakopa na kulipa.Unaweza kudunduliza kiasi gani hadi ulete maendeleo kwenye Nchi?

Halima anaweza nitajia Nchi yeyote anayoijua yeye ambayo imeendelea bila mikopo? Kama mikopo inalemaza vipi Kuhusu misaada? Bora angesema misaada angeeleweka.

Mwisho ni kwamba Halima anataka Rais asikope Ili alete Kodi za kumwaga kwa wananchi? Kuna uchumi unaweza kujua kwa kuua purchasing power?

Jamani sio kila kenge ni WA kumsikiliza,Rais asiwasikilize Hawa wapuuzi ambao Wanafaidi kodi za maskini,Rais wasikilize wachumi na sio Hawa washenzi.
Halima amesema siyo kila changamoto ni ya kutatua kwa mikopo...Labda kamaanisha mikopo ile ya kujengea madarasa,kwa hakika madarasa tungeweza kujenga kwa pesa za kodi zetu tu.
Halima anaweza kuwa amekosea kwenye maoni yake kimtazamo na ya kwako,ila abadani hajafikia hatua ya kuwa kenge kama unavotaka tuamini
 
Halima amesema siyo kila changamoto ni ya kutatua kwa mikopo...Labda kamaanisha mikopo ile ya kujengea madarasa,kwa hakika madarasa tungeweza kujenga kwa pesa za kodi zetu tu.
Halima anaweza kuwa amekosea kwenye maoni yake kimtazamo na ya kwako,ila abadani hajafikia hatua ya kuwa kenge kama unavotaka tuamini
Miaka yote mliweza kujenga hayo madarasa kwa pesa zenu? Unajua kwa nini serikali iliamua kujenga kwa pesa za mkopo?

Sio swala la kuamini bali ni swala la facts,nimekuuliza nitajie Nchi ambayo inategemea kudunduliza ndani ndio ifanye maendeleo.

Kwanza lazima mjue Tzn haiendelei kwa sababu ya ujinga wa watu,core issue ni kukosa maarifa na ujuzi na Wala sio madaraja sijui maji na upuuzi kama huo.

Ndio maana wakina Lowassa walisema elimu elimu elimu.
 
Katika Matatizo yote ya kukimbilia Kukopa pamoja na Kudumuza Akili ni MALIPO....

Kukopa Harusi kulipa Matanga.....
 
Mdee anajielewa kuliko wewe na hayuko tayari kusujudu udikteta wa Lisu na Mbowe
Tumia akili hata kama conscience yako imekufa kabisa. Hili suala la mikopo na serikali za CCM limejaa unafiki mwingi.

Halafu Mdee ali-surrender kwa Magufuli baada ya kuaminishwa kuwa CHADEMA itauawa na dola na Magufuli ataitawala Tanzania milele kwa mkono wa chuma na hakuna mtu wa kufanya kitu. Mbowe, mentor wake hajawahi kuwa tishio kwake. I believe she's experiencing a sense of remorse on the bizarre transaction that saw her and her BAWACHA colleagues fall into Ndugai's arms.

Wote tulishuhudia jinsi ushindi wa Halima Jimbo la Kawe ulivyoporwa kinguvu na vyombo vya dola kwa maagizo ya Magufuli. Tuliona jinsi Halima alivyohangaika kufuatilia kura hadi kutoa chozi. Mwishowe alifuatwa na kuaminishwa kuwa hakuna namna zaidi ya kuunga mkono juhudi au asubiri aende na hatma ya kifo cha CHADEMA. Katika maajabu ya karne, uwepo wa Magufuli ukakomeshwa ghafla na ndoto zote haramu za wafuasi wake juu ya Tanzania zikafa papo hapo.

Hatuhitaji kurejeshwa kwenye scenario ya kishetani ya awamu ya tano. Nyuzi za aina hii hazitusaidii kabisa.
 
Nadhani watoto wa kisiasa wa Mbowe wana maumivu makali sana baba yao kuendelea kukaa jela, bila kujali rangi zao za vyama' Madee ni miongoni mwao
 
Yeye pia amesabibishia kukopa kwa ajili ya kulipwa mahela uku hana chama
 
Moja ya sababu zilizopelekea JoBO Ndungai afukuzwe usipika ni kumkemea hadharani mama wa Taifa Ili ahaache kukopa maana kukopa kunadumaza Akili na kutapelekea nchi kupigwa mnada.

Baada ya kauli hii yalitofatia kwa jobo ndungah ni kufukuzwa usipika kwa kigezo Cha kujiuzulu,weeeee hacha mvua inyeshe hakuna aliyejiuzulu usipika Bali ile barua iliandikwa na wanaume wasio chezewa dadeki na yule mwamba mara ya mwisho kuonekana alionekana amepiga PC na Mh Raisi geti la Ikulu dadeki.mpaka leo hajulikani aliko wapo wa naosema kawekwa MWALI. baada ya kukatwa bira ganzi.

Swali fikirishi kwa nini MDEE mbunge hasiye na Baraka za chama alimsema live kuwa serikali ipunguze kukopa Ili iweze kufikiria vyanzo vya mapatocya ndani mbona kaachwa na Huyu ni mwepesi maana ni mbunge wa Ndugu jobo na mwendazake.?Sasa mwendazake yupo aela na Jobo hajulikani haliko sijui ni mbinguni au Tanzania haijulikani.
 
Yeye nawenzie walokimbilia bungeni wamejidumaza akili na kajiheshma kadogo walikokuwa nako...shwain!!
 
Moja ya sababu zilizopelekea JoBO Ndungai afukuzwe usipika ni kumkemea hadharani mama wa Taifa Ili ahaache kukopa maana kukopa kunadumaza Akili na kutapelekea nchi kupigwa mnada...
Ndugai ni spika ambaye ni kiongozi wa mhimili na Halima ni mbunge wa kawaida.
 
Halima James Mdee hana madhara karopoka tu!
Aisee. SIku hizi baada ya kumhamishia kwenu mnamdharau sana. Ingekuwa enzi zile, leo mngemuanzishia nyuzi kibao za kumlaani kwa kupuuza juhudi za mama serikalini. Hata bungeni kungekuwa moto. Leo mdee anaongea anafananishwa na kina mwanyika.
 
Aliyekuwa spika, Bwana Ndugai; Chagueni moja kati ya Tozo ama mikopo

Rais Samia: Mimi nimechagua Mikopo, kwani Mimi ndiye wa kwanza kukopa? Waliopita hamkuwaona wakikopa?? Tena Bwana Ndugai unikome
Hahahaha,kichambo hichooo.wenye stress zenu njoeni jf mziondoe
 
Hivi kuna nchi isiyo kopa kweli, jambo la msingi ni kuona namna bora ya matumizi ya fedha za mikopo ni namna gani zinatumika kama zinafanikisha ujenzi wa miradi na utoaji wa huduma za kumnufaisha mwananchi kuna shida gani au ni mradi tu mbunge wa upinzani uonekane umeongea bungeni.
NI MBUNGE WA UPINZANI UPI YUPO CHAMA GANI?
 
Mkipo ni mizuri sana ila tusiiendee pupa. Unapokopa unaona raha lakini wakati wa malipo ni matanga. Hayati Mhe. Mkapa alikuwa mwangalifu sana katika kusimamia suala mikopo.

Mikopo tumayopata sharti ipate ridhaa ya Bunge na isiye ya kifichoficho. Nakubaliana na Mhe. Halima Mdee kuhusu mchango wake kuhusu suala la mikopo.

Watanzania tunatakiwa tufanye kazi na mikopo iwe ni kitu cha mwisho. Mfano hai ni nchi mbalimbali zinazosumbuliwa na mikopo mfano Zambia, Kenya etc. Tuwe waangalifu sana kuhusu mikopo.
 
Hii ni Mara ya pili Serikali ya Mama kuambiwa huu ujumbe huwezi jua labda ni ujumbe kutoka deep state.Mama asipuuze utamng'oa.
 
Back
Top Bottom